Menu



HISTORIA YA NABII AYYUUB(A.S)

Ayyuub(a.

HISTORIA YA NABII AYYUUB(A.S)

HISTORIA YA NABII AYYUUB(A.S)


Ayyuub(a.s) ni katika Mitume wa Allah(s.w) waliotajwa katika Qur-an kwa umadhubuti wake katika imani juu ya Allah(s.w) na Subira.

Ayyuub(a.s) aliishi Kaskazini Mashariki ya Bara Arabu. Alikuwa tajiri sana mwenye mali nyingi, watoto wengi na watumishi wengi. Lakini hakutakabari bali alimuabudu Mola wake na kumshukuru ipasavyo

Mitihani Iliyomfika Ayyuub(a.s)


Nabii Ayyuub(a.s) alitahiniwa na Mola wake kama ifuatavyo:

(1) Mali yake, watoto wake na watumishi wake wote walipatwa na majanga wakatoweka. Akabakia yeye na mkewe ambaye naye alikuwa mcha-Mungu.

(2) Pamoja na kupotelewa na mali yake na watu wake wote, alishikwa na maradhi mabaya ya kuota vidonda mwili mzima kuanzia kichwani hadi miguuni. Alijaribu kutumia dawa zote alizoweza, lakini hakupata nafuu yoyote


Nabii Ayyuub(a.s) hakutetereka katika imani yake kutokana na majanga yaliyomfika bali alisubiri na kuwa karibu zaidi na Mola wake kuliko hata wakati alipokuwa katika hali yake ya mwanzo ya utajiri na afya nzuri. Na Allah(s.w) anamsifu mjawake, Ayyuub kama ifuatavyo:

β€œβ€¦. Bila shaka tulimkuta ni mwenye subira mja mwema; kwa hakika alikuwa mnyenyekevu sana.” (38:44)

Nabii Ayyuub(a.s) aliona kuwa aliyempa mali, watoto na wale watumishi aliokuwa nao ni Allah(s.w) kama amana. Hivyo, aliona hapakuwa na kosa lolote kwa Allah(s.w) kuchukua amana yake. Pia aliridhika na hali ya ugonjwa aliyokuwa nayo. Kwa ujumla Nabii Ayyuub (a.s) aliridhika na kusubiri juu ya matatizo yote yaliyomfika na kupata matunda ya subira kama Allah(s.w) anavyotubashiria:

Na tutakutieni katika msukosuko wa (baadhi ya mambo haya); hofu na njaa na upungufu wa mali na wa watu na wa matunda. Na wapashe habari njema wanaosubiri.(2:155) Ambao uwapatapo msiba husema: β€œHakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu, na kwake Yeye tutarejea (atatupa jaza yake).(2:156)

Hao juu yao zitakuwa baraka zitokazo kwa Mola wao na rehema; na ndio wenye kuongoka. (2:157)



                   

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 2266


Sponsored links
πŸ‘‰1 Simulizi za Hadithi Audio     πŸ‘‰2 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰4 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰5 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰6 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Mbinu na njia walizotumia maadui wa uislamu dhidi ya waislamu na dola ya kiislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Hadhi na haki za Mwanamke Ulaya Wakati wa mapinduzi ya viwnda
Soma Zaidi...

NI UPI MKATABA WA AL-FUDHUL NA ASILI YAKE, ATHARI ZAKE NA WALOHUSIKA
MKATABA WA AL-FUDHULBaada ya vita hivi viongozi wa pande mbili hizi waliamuwa wakae chini na wakubaliane kuweka kanun i na utaratibu utakaozuia kutotokea uonevu kama huuu tena. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII ISMAIL
Soma Zaidi...

Nasaha za Lut(a.s) kwa Watu Wake
Nabii Lut(a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA KUZALIWA KWA MTUME MUHAMMAD (S.A.W) NA MAMA AMINA MKE WA ABDALLAH MTOTO WA ABDUL-AL MUTALIB
KUZALIWA KWA MTUME (S. Soma Zaidi...

Mtume (s.a.w) alivyoandaa ummah wa kiislamu makkah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII YUSUFU(A.S.): Ndoto ya nabii Yusufu
Mtume Yusufu(a. Soma Zaidi...

Historia ya Al-Khidhri
Jina Al-Khidhri halikutajwa mahali popote katika Qur’an. Soma Zaidi...

Vipengele vya mkataba wa Hudaibiya na faida zake katika Ukombozi (ufunguzi) wa mji wa Makkah
Soma Zaidi...