Menu



Historia ya Watu wa Mahandaki ya Moto.

Katika Suratul Buruj, kumetajwa kisa cha makafiri waliowatesa wafuasi wa Mitume waliotangulia kabla ya Mtume Muhammad(s.

Historia ya Watu wa Mahandaki ya Moto.

Historia ya Watu wa Mahandaki ya Moto.


Katika Suratul Buruj, kumetajwa kisa cha makafiri waliowatesa wafuasi wa Mitume waliotangulia kabla ya Mtume Muhammad(s.a.w). Makafiri hao walichimba mahandaki na ndani yake wakawasha moto mkubwa kisha wakawa wanawatosa waumini humo mmoja baada ya mwingine. Dhun-Nuwas mmoja



wa waliokuwa wafalme wa Mayahudi; aliingia Najran akiwa na jeshi kubwa ili awalazimishe watu wa Najran wasifuate mafundisho ya Mitume. Watu wa Najran walipokataa kumfuata, alichimba handaki kubwa akawasha moto akawa anamtumbukiza Muumini mmoja baada ya mwingine huku yeye na watu wake wanachekelea. Habari hii inaelezwa katika Suratul-Buruj, kama ifuatavyo:




“(Kuwa) wameangamizwa watu waliowaadhibu Waislamu katika mahandaki. Yenye moto wenye kuni (nyingi). Walipokuwa wamekaa hapo (Waliangamizwa makafiri hao pale wakati walipokuwa) wanatazama yale wanayowafanyia hao Waislamu (walipokuwa wakiwaadhibu). Nao hawajaona baya lolote kwao (Waislamu) ila kumuamini Mwenyezi Mungu Mwenye kushinda (na) Mwenye kusifiwa. Ambaye ni Mwenye Ufalme wa mbingu na ardhi; na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuona kila kitu” (85:4-9).



Kisa hiki kimesimuliwa kiwape fundisho na kuwaliwaza waumini wa zama zote; kwamba taabu iwapatayo kutoka kwa makafiri imeanza kuwafikia ndugu zao waliotangulia. Aidha, kutokana na kisa hiki Waislamu wanapata funzo kuwa kubakia na Imani Thabiti na suala la kusimamisha Uislamu katika jamii, kwahitaji juhudi na subira kubwa sana.

Mwenyezi Mungu anawaliwaza Waislamu kuwa makafiri wanaowatesa na kuwaghasi Waislamu hivi leo, atawaadhibu na kuwatesa kweli kweli kama alivyowatesa As-habul- Khudud.




“Hakika wale waliowaadhibu Waislamu wanaume na Waislamu wanawake, kisha wasitubie basi watapata adhabu ya Jahanamu na watapata adhabu ya kuungua (barabara)” (85:10). “Hakika kutesa kwa Mola wako ni kukali (sana)” (85:12).



Lakini pamoja na kuliwazwa huko; Waislamu hawatakiwi walale usingizi wasubiri nusura ya Mwenyezi Mungu. Ni wajibu wao wajiandae kwa kila mbinu kupambana na vitimvi vya maadui zao.



“Basi waandalieni (wawekeeni tayari) nguvu mziwezao (silaha), mafarasi yaliyofungwa tayari tayari ili kwazo muogopeshe maadui wa Mwenyezi Mungu na maadui zenu .................” (8:60).



                   

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 1010


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Kitau cha Fiqh     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Mbinu na njia walizotumia maadui wa uislamu dhidi ya waislamu na dola ya kiislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Maswali kuhusu Quran
Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

tarekh 07
KUPASULIWA KWA KIFUA MTUMEWAKATI AKIWA MTOTO. Soma Zaidi...

Hawa ndio waaasi wakwanza wa Dola ya kiislamu wakati wa makhalifa
Soma Zaidi...

Jifunze historia ya uislamu toka mitume na manabii, kuja kwa makhalifa na maimamu hadi leo
Soma Zaidi...

Muhutasari wa sifa za wanafiki
Kwa kuzingatia aya zote tulizozipitia juu ya wanafikitunaweza kutoa majumuisho ya sifa za wanafiki kama ifuatavyo:- (1)Hutenda kinyume cha imani wanaodai kuwa nayo. Soma Zaidi...

Kazi na wajibu wa khalifa katika dola ya kiislamu
Kazi na Wajibu wa KhalifaKhalifa katika Serikali ya Kiislamu ndiye mtendaji mkuu wa Serikali kama alivyokuwa Mtume(s. Soma Zaidi...

Historia ya Dhulqarnain
Dhulqarnain sio jina la mtu bali cheo, maana yake ikiwa: “Mwenye Pembe Mbili”. Soma Zaidi...

Kuhajiri Waislamu wa Makka Kwenda Madinah
Baada ya mikataba miwili ya ‘Aqabah na baada ya Waislamu 75 kufika Yathrib salama, Mtume(s. Soma Zaidi...

Mtume (s.a.w) alivyoandaa ummah wa kiislamu makkah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...