image

Hatua ya Serikali Dhidi ya Waanzilishi wa Fitna na Farka wakati wa khalifa

Hatua ya Serikali Dhidi ya Waanzilishi wa Fitna na Farka wakati wa khalifa

Hatua ya Serikali Dhidi ya Waanzilishi wa Fitna na Farka


Hatua ya kwanza ilikuwa kuwahamishia Syria viongozi 10 wa upinzani kutoka Kufa. Wakorofi hawa walipopelekwa Syria, Amir Muawiya alizungumza nao na kusikiliza mafundisho yao lakini alipowasihi waache kupoteza watu walijifanya hawamuelewi kwa sababu hii Gavana Muawiya alimuandikia Khalifa Uthman kumuomba awarudishe walikotoka ili wasiwaharibu watu wa Syria kwa vile wanazungumza lugha ya shetani na lengo lao ni kuwagawa watu na kuunda fitna. Watu hawa walirudishwa Kufa na walipoendelea na shughuli zao walihamishiwa Hirus ambako walidhibitiwa kwa muda na gavana Abdur-Rahman mtoto wa Khalid.


Hatua ya pili iliyochukuliwa na Khalifa pamoja na Shura yake ni kutuma wajumbe wanne(4)kutembelea Dola nzima na kusikiliza malalamiko ya wananchi. Maswahaba waliotumwa ni Muhammad bin Muslimah, Usamah bin Zaid, Ammar bin Yasir na Abdullah bin Umar. Wajumbe hawa ambao walirudi watatu walitoa taarifa kuwa hakukua na malalamiko. Ammar bin Yasir alibakia Misr na kujiunga na wapinzani.


Kuwasilisha Malalamiko Kwenye Kikao cha Magavana


Kama kawaida magavana walikutana kila mwaka baada ya Hija. katika mwaka ule taarifa zilitolewa kuwa wenye malalamiko waende kuwasilisha malalamiko yao kwenye kikao hicho. Lakini hakuna aliyejitokeza. Si hivyo tu lakini Khalifa Uthman alitimiza dai la wapinzani hawa kwa kumuweka Gavana wanayemtaka Kufa. Walichokifanya wapinzani ni kuwa walikusanya kundi la watu wapatao elfu moja na kumzuia Gavana wa Kufa asirudi madarakani alipokwenda Madinah mkutanoni. Walimzuia mahali paitwapo Ajara, mtumishi wake aliuliwa na yeye akarudi Madinah. Khalifa akamthibitisha Abu Mussa kuwa gavana wa Kufa baada ya kutakiwa na wapinzani. Hapa Khalifa alionesha udhaifu, watu hawa walistahili kuadhibiwa kinyume na kukubali dai lao baada ya uhaini uliowazi.


Katika kikao cha Magavana Khalifa alitaka ushauri wa kuzima uasi nchini. Saad alishauri wapinzani wakamatwe na kuadhibiwa. Abu Sarah alishauri wasipewe posho; Ibn Aamir alitaka wapinzani wauawe; Muawiya pia alitaka zichukuliwe hatua kali. Kutokana na maoni haya Khalifa alijibu:


Ukatili sitoruhusu, kama mapinduzi yakija sitaki kulaumiwa. Ukianza hivi mwisho wake mbaya. Ingekuwa vyema pale mapema wakati uasi haujaenea. Sasa hakuna la kufanya ila kukaa kimya na kusubiri bila kumkosea mtu yeyote.


Muawiya alipokuwa anaondoka Madina alimsihi Khalifa akubali kuhama Madina lakini alikataa, na kusema hata kama ni kuokoa maisha yangu sitaondoka katika ardhi ambayo Mtume aliishi na kuzikwa.


Kisha Muawiya akamuomba akubali kuletewa jeshi lilinde mji wa Madina. Hali kadhalika Khalifa alikataa na kusema; “Sitawaweka askari wanaokaa karibu na nyumba ya Mtume”. Kwa hali hiyo Muawiya akajibu “Sioni kinachokusubiri ila umauti; “Mwenyezi Mungu ndie mlinzi wangu,” alisema Khalifa Uthman.38 ambaye alikuwa mzee wa miaka 82.


Uthman bin Affan, alijua hatari iliyokuwa inamkabili lakini hakutaka kutumia nguvu kuwaadhibu wapinzani wake kwa kuhofia kuzuka vita vya wenyewe kwa wenyewe, alihiyari afe yeye kuliko kuzusha vita ambavyo vingegharimu roho nyingi.





                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 226


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

fadhila za kusoma quran
Fadhila na umuhimu wa kusoma quran 1. Soma Zaidi...

Maadui wa uislamu na mbinu zao: wanafiki, makafiri, mayahudi, wakristo,
Upinzani dhidi ya Dola ya Kiislamu Madinah. Soma Zaidi...

Mfumo wa ulinzi na usalama katika fola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII ISHAQA NA YAQUB
Soma Zaidi...

TAREKH, HISTORIA NA SIRA YA UISLAMU NA MTUME MUHAMMAD KUTOKA KUZALIWA MPAKA KUFARIKI NA HARAKATI ZAKE
1. Soma Zaidi...

Umuhimu wa jihad katika kusimamisha uislamu katika jamii
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Shu’ayb(a.s).
Kutokana na kisa cha Nabii Shu’ayb(a. Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ismail(a.s)
Kutokana na Historia ya Nabii Ismail(a. Soma Zaidi...

Mtume Muhammad s.a.w analelewa na Babu yako ikiwa na umri wa miaka 6
Sura na historia ya Mtume Muhammad s.a. w sehemu ya 9. Soma Zaidi...

tarekh 02
FAMILIA YA MTUME (S. Soma Zaidi...

Vita vya Al Fijar na sababu zake
Historia na shida ya Mtume Muhammad S.A.W, sehemu ya 12. Hapa utajifunza kuhusu kutokea kwa vita vya al fijar. Soma Zaidi...

NINI MAANA YA SWALA (SALA AU KUSWALI), KILUGHA NA KISHERIA KATIKA UISLAMU
Maana ya Swala Maana ya Swala kilugha(a) Kilugha Katika lugha ya Kiarabu neno Swalaat lina maana ya ombi au dua. Soma Zaidi...