Allah(s.
Allah(s.w) alimjaalia Nabii Musa(a.s) miujiza ya kuthibitisha Utume wake. Miujiza si viinimacho kama ilivyo mazingaombwe. Muujiza ni jambo halisi lisilola kawaida ambalo hutokea kwa idhini ya Allah(s.w). Musa alipoulizwa na Allah(s.w) kuwa ameshika nini alisema:
.............Akasema: βHii ni fimbo yangu, ninaiegemea na ninaangushia majani kwa ajili ya wanyama wangu. Tena ninaitumia kwa mambo mengine.(20:18)
Inadhihirika hapa kuwa Nabii Musa alikuwa na fimbo ya kawaida kabisa, lakini Allah(as) anaigeuza kuwa muujiza.
Allah(s.w) akasema: Itupe, ewe Musaβ. Akaitupa. Mara ikawa nyoka anayekwenda mbio. Allah akasema: βIkamate wala usiogope, sasa hivi Tutairudisha hali yake ya kwanza.(20:19-21)
βNa uambatanishe mkono wako katika kwapa lako; utatoka ukiwa mweupe sana pasipo na ubaya wowote. Huu ni muujiza mwingine. Ili Tukuoneshe miujiza mingine mikubwa (20:22-23)
Inabainika wazi kuwa chanzo cha miujiza yote aliyokuwa nayo Musa na Mitume wengine, ni Allah(s.w). Hakuna Mtume au Nabii aliyefanya miujiza kwa uweza wake mwenyewe!
Umeionaje Makala hii.. ?
Nabii Ibrahiim na mkewe Sarah walikaa mpaka wakawa wazee bila ya kupata mtoto.
Soma Zaidi...Mtume Dhul-kifl ananasibishwa na Ezekiel anayetajwa ndani ya Biblia.
Soma Zaidi...Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu nani alikuwa wamwisho kufariki katika masahaba wa Mtume kwa mujibu wa historia
Soma Zaidi...Kazi na Wajibu wa KhalifaKhalifa katika Serikali ya Kiislamu ndiye mtendaji mkuu wa Serikali kama alivyokuwa Mtume(s.
Soma Zaidi...Kutokana na histoira ya Nabii Sulaiman (a.
Soma Zaidi...