Allah(s.
Allah(s.w) alimjaalia Nabii Musa(a.s) miujiza ya kuthibitisha Utume wake. Miujiza si viinimacho kama ilivyo mazingaombwe. Muujiza ni jambo halisi lisilola kawaida ambalo hutokea kwa idhini ya Allah(s.w). Musa alipoulizwa na Allah(s.w) kuwa ameshika nini alisema:
.............Akasema: โHii ni fimbo yangu, ninaiegemea na ninaangushia majani kwa ajili ya wanyama wangu. Tena ninaitumia kwa mambo mengine.(20:18)
Inadhihirika hapa kuwa Nabii Musa alikuwa na fimbo ya kawaida kabisa, lakini Allah(as) anaigeuza kuwa muujiza.
Allah(s.w) akasema: Itupe, ewe Musaโ. Akaitupa. Mara ikawa nyoka anayekwenda mbio. Allah akasema: โIkamate wala usiogope, sasa hivi Tutairudisha hali yake ya kwanza.(20:19-21)
โNa uambatanishe mkono wako katika kwapa lako; utatoka ukiwa mweupe sana pasipo na ubaya wowote. Huu ni muujiza mwingine. Ili Tukuoneshe miujiza mingine mikubwa (20:22-23)
Inabainika wazi kuwa chanzo cha miujiza yote aliyokuwa nayo Musa na Mitume wengine, ni Allah(s.w). Hakuna Mtume au Nabii aliyefanya miujiza kwa uweza wake mwenyewe!
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
hii ni historia ya vita vya Muta. Katika makala hii utajifunza sababu ya vita hivi na yaliyojiri katika uwanja wa vita.
Soma Zaidi...Sara na historia ya Mtume Muhammad s.a.w sehemu ya 16. Hapa utajifunza maandalizi wa mjadala wa ndoa hizi.
Soma Zaidi...Mitume huzaliwa Mitume.
Soma Zaidi...