image

Maswali kuhusu hali ya bara arabu zama za jahiliyyah

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Zoezi la 7.

  1. (a)    Nini maana ya ‘zama za Jahiliyyah’?

(b)  Bainisha baadhi ya mambo aliyoyakuta Mtume (s.a.w) katika jamii ya waarabu wa Makkah zama za Jahiliyyah.

  1. Mji wa Makkah ni mji mkongwe na mtukufu tangu zama za Nabii Ibrahim (a.s). Thibitisha kauli hii kwa kutoa sababu ya utukufu wa mji wa Makkah.
  2. (a)  Bainisha sababu zilizopelekea Muhammad (s.a.w) alipokuwa mdogo   kwenda kulelewa nje ya mji wa Makkah.
    1.     Taja baadhi ya sifa au tabia za Mtume (s.a.w) alizokuwa nazo tangu utotoni zilizokuwa kama ishara ya kuandaliwa kuwa Mtume wa Allah.

 

  1. (a)  Bainisha maandalizi ya Mtume (s.a.w) kabla ya kupewa Utume (mafunzo ya Ki-Ilhamu).

(b)  Ni yapi mafunzo yatokanayo na Maandalizi ya Mtume (s.a.w) ya Ki-Ilhamu?

  1. Mtume (s.a.w) alianza kupewa mafunzo ya Ki-wahyi mara tu baada ya kuanza kumshukia sura tatu za mwanzo, (96:1-5), (73:1-10) na (74:1-7).

    Kutokana na aya hizi ainisha mafunzo yatokanayo.

  1. (a)  Ni sababu zipi za msingi ziliwafanya Maquraish wa Makkah kuupinga Ujumbe wa Qur’an?
    1. Ainisha njia na mbinu walizotumia Maquraish katika kuupinga na kuuzuia ujumbe wa Uislamu kuenea katika jamii na mafunzo yatokanayo.

 

  1. Changanua njia alizotumia Mtume (s.a.w) katika kuandaa ummah wa Kiislamu Makkah kwa kutumia mikataba ya ‘Aqabah.

 

  1. Katika kuendesha harakati za kuusimamisha Uislamu, hatuna budi kuwa na mikakati madhubuti. Kwa kurejea historia ya Mtume (s.a.w) onyesha jinsi alivyotumia stretejia madhubuti wakati wa kuhama kwenda Madinah.

 

  1. ‘Hijra katika Uislamu si sawa na Ukimbizi, bali na stretejia za kuunganisha nguvu ya kuusimamisha Uislamu’. 

Kwa kutumia Hijra ya Mtume (s.a.w), mambo gani waislamu wa leo tunajifunza katika hatua za kuupigania Uislamu. 

 

**********************************************

Wabillah Tawfiiq

**********************************





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1269


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Zakaria(a.s) na Yahya(a.s)
Kutokana na Historia ya Nabii Zakaria (a. Soma Zaidi...

Yunus(a.s) Kulingania Uislamu kwa Watu Wake
Nabii Yunus(a. Soma Zaidi...

Maana ya kusimamisha uislamu katika dini
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Salih(a.s)
Mafunzo tuyapatayo hayatofautiani na yale yatokanayo na Historia ya Nabii Hud(a. Soma Zaidi...

Msimamo wa Nabii Hud(a.s) Dhidi ya Makafiri wa Kaumu Yake
Pamoja na kwamba alipingwa na nguvu za Dola ya makafiri wa kaumu yake, Mtume Hud(a. Soma Zaidi...

Mafunzo yatokanayo na maandalizi haya ya ki ilhamu
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Je waislamu walishindwa vita vya Uhudi?
Katika vita vya Uhudi waislamu walikufa wengi kulinganisha na makafiri. Lakini makafiri walikimbia uwanja wa vita baada ya kuzidiwa. Je ni nanibalishindwa vita vya Uhudi kati ya waislamu na makafiri? Soma Zaidi...

Vitimbi vya Makafiri Dhidi ya Nabii Salih(a.s) na Waumini na kuangamizwa kwao
Makafiri wa Kithamud hawakuishia tu kwenye kuukataa ujumbe wa Nabii Salih(a. Soma Zaidi...

Historia ya Vijana wa Pangoni
Makafiri wa Kiquraish walikuwa na tabia ya kumghasi Mtume(s. Soma Zaidi...

Wapinzani wa Ujumbe wa Nabii Salih(a.s)
Baada ya Nabii Salih(a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII ADAM
Soma Zaidi...

fadhila za kusoma quran
Fadhila na umuhimu wa kusoma quran 1. Soma Zaidi...