Maswali kuhusu hali ya bara arabu zama za jahiliyyah

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Zoezi la 7.

  1. (a)    Nini maana ya ‘zama za Jahiliyyah’?

(b)  Bainisha baadhi ya mambo aliyoyakuta Mtume (s.a.w) katika jamii ya waarabu wa Makkah zama za Jahiliyyah.

  1. Mji wa Makkah ni mji mkongwe na mtukufu tangu zama za Nabii Ibrahim (a.s). Thibitisha kauli hii kwa kutoa sababu ya utukufu wa mji wa Makkah.
  2. (a)  Bainisha sababu zilizopelekea Muhammad (s.a.w) alipokuwa mdogo   kwenda kulelewa nje ya mji wa Makkah.
    1.     Taja baadhi ya sifa au tabia za Mtume (s.a.w) alizokuwa nazo tangu utotoni zilizokuwa kama ishara ya kuandaliwa kuwa Mtume wa Allah.

 

  1. (a)  Bainisha maandalizi ya Mtume (s.a.w) kabla ya kupewa Utume (mafunzo ya Ki-Ilhamu).

(b)  Ni yapi mafunzo yatokanayo na Maandalizi ya Mtume (s.a.w) ya Ki-Ilhamu?

  1. Mtume (s.a.w) alianza kupewa mafunzo ya Ki-wahyi mara tu baada ya kuanza kumshukia sura tatu za mwanzo, (96:1-5), (73:1-10) na (74:1-7).

    Kutokana na aya hizi ainisha mafunzo yatokanayo.

  1. (a)  Ni sababu zipi za msingi ziliwafanya Maquraish wa Makkah kuupinga Ujumbe wa Qur’an?
    1. Ainisha njia na mbinu walizotumia Maquraish katika kuupinga na kuuzuia ujumbe wa Uislamu kuenea katika jamii na mafunzo yatokanayo.

 

  1. Changanua njia alizotumia Mtume (s.a.w) katika kuandaa ummah wa Kiislamu Makkah kwa kutumia mikataba ya ‘Aqabah.

 

  1. Katika kuendesha harakati za kuusimamisha Uislamu, hatuna budi kuwa na mikakati madhubuti. Kwa kurejea historia ya Mtume (s.a.w) onyesha jinsi alivyotumia stretejia madhubuti wakati wa kuhama kwenda Madinah.

 

  1. ‘Hijra katika Uislamu si sawa na Ukimbizi, bali na stretejia za kuunganisha nguvu ya kuusimamisha Uislamu’. 

Kwa kutumia Hijra ya Mtume (s.a.w), mambo gani waislamu wa leo tunajifunza katika hatua za kuupigania Uislamu. 

 

**********************************************

Wabillah Tawfiiq

**********************************

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1627

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰2 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰3 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰4 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana: