Tukio la kartasiTukio la ‘kartasi’ lililonakiliwa katika vitabu vya Muslim na Bukhari kuwa siku tatu kabla ya kutawafu Mtume (s.
Tukio la kartasi
Tukio la ‘kartasi’ lililonakiliwa katika vitabu vya Muslim na Bukhari kuwa siku tatu kabla ya kutawafu Mtume (s.a.w.) alitamka: “Nipeni peni na wino ili niwaandikie maelekezo yatakayowafanya watu wasipotee”, halina ukweli. Kutokana na kauli hii inadaiwa kuwa Umar alihutubia watu na kusema “Mtume yuko katika maumivu makali, Qur’an kama muongozo unatosha kwa watu. Baadhi ya watu wakasema Mtume amepoteza fahamu. Ipo kauli pia isemayo maneno haya yamesemwa na Umar (Khalifa wa pili)!
Moja ya Hadithi hizo imo katika kitabu cha Bukhari juzuu ya Hadithi namba 114 katika ukurasa wa 86 tafsiri ya Kiarabu Kingereza isemayo hivi:
Amesimulia Ubaidullah bin Abdullah kuwa Ibn Abbas amesema: Hali ya Mtume (s.a.w.) ilipokuwa mbaya alisema: “Nileteeni
karatasi ya kuandikia, na nitawaandikia tamko litalowapelekea
kutopotea”. Lakini Umar akasema; “Mtume anaumwa sana na tuna kitabu cha Mwenyezi Mungu ambacho kinatosheleza. Lakini Maswahaba wa Mtume wakatofautiana juu ya jambo hili. Kutokana na zogo hili Mtume akawaambia; “Ondokeni (na niacheni peke yangu) sio sahihi mbishane mbele yangu. Ibn Abbas akatoka nje na kusema: Imekuwa bahati mbaya na msiba mkubwa kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu amezuiwa kuandika tamko kwa Sababu ya kutokubaliana kwao na makelele yao.
Zingatio
Kutokana na Hadithi hii ni dhahiri kuwa Ibn Abbas ameshuhudia tukio hili na akatoka nje na kusema kauli hii. “Ukweli sio huu kwa Sababu Ibn Abbas alikuwa anatamka kauli hii alipokuwa anasimulia Hadithi hii, lakini yeye binafsi hakushuhudia tukio hili. Kwa maelezo zaidi juu ya hili rejea Fat-h al-Barr juzuu ya I, ukurasa wa 220).
Pamoja na kuwepo kwa maandishi juu ya tukio hili na wanahistoria kuwa na mifano na tafsiri tofauti, hakuna ushahidi wa kutosha kama tukio hili limetokea kweli au ni maandishi tu yenyewe yaliyopachikwa ili kukidhi haja ya waliyobuni tamko hili. Tukio hili halina ukweli wa kihistoria kwa sababu zifuatazo:
Ni muhali kudhania kuwa Mtume anaweza kuzuiwa na swahaba au na yeyote asiye Allah(s.w.) kutekeleza jambo la Utume wake; inashangaza zaidi kuwataja maswahaba kuwa wanaweza kumpinga Mtume katika Utume wakati huu akiwa katika kitanda cha mauti. Linaloshangaza zaidi ni lengo la tukio hili: Kwa mujibu wa maelezo yaliyopo ni kuwa Mtume(s.a.w.) hakuandika tamko alilokusudia ingawa aliishi siku nne baada ya tukio hili akiwa katika hali isiyo mbaya sana hata Abubakar akarudi kitongojini kwake, kulipokuwa na umbali wa maili mbili hivi kutoka mjini Madina. Kama hali ilikuwa hii kwa nini basi usia huu usiandikwe?
Hivyo Mtume(s.a.w.) kwa makusudi hakuacha uteuzi wowote wa nani ashike uongozi baada ya kutawafu kwake kwa kuwa ameacha mafunzo ya kudumu ya namna ya kupata viongozi, watu wachague wenyewe kwa mujibu wa mafundisho ya Uislamu.
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 519
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi
👉2 Madrasa kiganjani
👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉4 Kitau cha Fiqh
👉5 Kitabu cha Afya
👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Kuhajiri Waislamu wa Makka Kwenda Madinah
Baada ya mikataba miwili ya ‘Aqabah na baada ya Waislamu 75 kufika Yathrib salama, Mtume(s. Soma Zaidi...
Mtume Muhammad s.a.w analelewa na Babu yako ikiwa na umri wa miaka 6
Sura na historia ya Mtume Muhammad s.a. w sehemu ya 9. Soma Zaidi...
Ugonjwa wa Mtume(s.a.w) na Kufariki kwake
Miezi miwili baada ya Hijjat-al-Wada, Mtume(s. Soma Zaidi...
Kuporomoka kwa Dola ya Kiislamu
Soma Zaidi...
Matukio mbalimbali katika historia ya uislamu kabla na baada ya Mtume (s.a.w) na makhalifa wake wanne
1. Soma Zaidi...
HISTORIA YA NABII IBRAHIM
Soma Zaidi...
Mchango wa Waislamu Katika Kuleta Uhuru Tanganyika
i. Soma Zaidi...
HISTORIA YA NABII IBRAHIIM(A.S) NA KUANDALIWA KWAKE:
Nabii Ibrahiim(a. Soma Zaidi...
Imam Ibn Majah na Sunan Ibn Majah
Soma Zaidi...
MJADALA JUU YA NDOA YA MTUME S.A.W NA BI KHADIJA (HADIJA)
LAKINI UMRI WANGU MKUBWABaada ya kuwaza na kufikiri muda mrefu, bibi Khadija (Radhiya Llahu anha) akafikia uamuzi wa kutaka kuolewa na Muhammad (Swalla Laahu alayhi wa sallam). Soma Zaidi...
Mapambano ya Dola ya kiislamu dhidi ya maadui wa kikristo (warumi) wakati wa Mtume
Soma Zaidi...
HISTORIA YA MTUME DHUL-KIFL(A.S)
Mtume Dhul-kifl ananasibishwa na Ezekiel anayetajwa ndani ya Biblia. Soma Zaidi...