Kupigwa vita Uislamu Tanganyika na Afrika Mashariki
i. Wamishionari wa kikristo waliona kuwa Uislamu ni kikwazo kwao, waliagiza machifu (viongozi wa kikabila) kuzuia Uislamu kuenea zaidi nje ya miji ya Pwani.
ii. Mkutano wa Berlin mwaka 1884, ulitoa kipaumbelea na fursa ya Ukristo kuwa na nguvu Afrika na kuweka mikakati ya kudhoofisha Uislamu na waislamu.
iii. Vyama vya Wamishionari, kikiwemo cha White Fathers chini ya Kardinali Lavingire, walianzisha mashule, vyuo na makanisa ilikueneza ukristo kupitia mbinu zifuatazo;
a. Kuficha uadui na uhasama wao dhidi ya waislamu na kujenga urafiki wa uongo na kinafiki.
b. Kujikita sana maeneo ya vijijini ndio ambapo waislamu wengi hawajui dini yao.
c. Kuanzisha makanisha na huduma za kijamii kama vile; mashule na hospitali.
iv. Wamishionari wa kikristo kupitia serikali za Kijerumani na Kiingereza, walianza mashule zilizotumia mfumo wa silabi zisizokuwa za kiarabu ili kudhoofisha utamaduni wa wenyeji wanaotumia silabi za kiarabu.
v. Wamishionari wa kikristo kutokana na ustawi wa waislamu walioukuta, walimshutumu Gavana Von Soden kuwapendelea waislamu, hivyo ikawekwa sera rasmi ya kuwabagua waislamu kielimu.
vi. Serikali ilinyima kabisa au kutoa misaada kidogo (grant in aid) shule zote za waislamu huku ikielekeza makanisani.
Mfano mwaka 1957 serikali ilitoa paundi 1,338,925 kwa mashirika yanayotoa elimu kati ya hizo, waislamu walipewa paundi 6,848 tu
vii. Masharti magumu au kupigwa marufuku waislamu kuanzisha shule zao katika misikiti (Qurโanic schools) na kutakiwa kuendesha kwa maelekezo ya serikali. viii. Serikali za kikoloni zikishirikiana na wamishionari, zilitaifisha mali zote za
waislamu ikiwemo; mashule, maduka, majumba, mashamba, n.k ili kuwadhoofisha kiuchumi kupitia sare ya ujamaa.
ix. Serikali iliwaua au kuwafunga au kuwahamisha viongozi waislamu makini ili kudhoofisha harakati zao juu ya Uislamu.kama akina Tewa Said Tewa, Suleiman Takadr, Bi Titi Mohamed, n.k.
x. Wamishionari kwa kushirikiana serikali, walianza sera ya dini mseto na taasisi za kimagharibi zinazoshughulikia miradi ya waislamu mfano; mradi wa kuritadisha waislamu wa โIslam in Africa Projectโ huko Nairobi.
xi. Serikali za kikoloni kwa kushirikiana na wamishionari na wenyeji wakristo, walitumia nguvu ya kuwateka na kuwaua machifu (viongozi waislamu wa kikabila) kama akina; Bushiri wa Pangani, Mkwawa wa Iringa, Isike wa Unyanyembe, Ali Songea Mbano, Suleiman Mamba, n.k ili kuvunja nguvu ya Uislamu.
xii. Chuki za serikali na mishionari dhidi ya machifu waislamu na waislamu, zilizidi na kuamua kupambana nao kivita kama vile vita vya maji maji, n.k.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 730
Sponsored links
๐1
Simulizi za Hadithi Audio
๐2
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
๐3
Kitau cha Fiqh
๐4
Madrasa kiganjani
๐5
kitabu cha Simulizi
๐6
Kitabu cha Afya
Musa(a.s) Kuwaongoza Bani Israil Hadi Palestina
Baada ya matukio haya ndipo Musa(a. Soma Zaidi...
Kulelewa kwa Mtume, maisha yake ya Utotoni na kunyonya kwake.
Historia na sura ya Mtume Muhammad S.A.W sehemu ya 06. Hapa utajifunza kuhusu historia ya Mtume akiwa mtoto. Soma Zaidi...
Kuporomoka kwa Dola ya Kiislamu
Soma Zaidi...
Uchaguzi wa Ali bin Abu Twalib kuwa Khalifa wa nne na chanzo cha Makundi katika Uislamu
Soma Zaidi...
Imam Tirmidh na Jami'u At-Tirmidh
Soma Zaidi...
tarekh 5
KUZALIWA KWA MTUME (S. Soma Zaidi...
Kuandaliwa kwa Muhammad wakati na baada ya kupewa utume
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Kuzaliwa kwa Mtume S.A.W
Sura na historia ya Mtume Muhammad s.sa. w, sehemu ya 5. Hapa utajifunza kuhusu kuzaliwa kwa Mtume. Soma Zaidi...
KAZI ALIZOFANYA MTUME MUHAMMAD (S.A.W) KABLA YA UTUME
KAZI ALIZOKUWA AKIFANYA MUHAMMAD (S. Soma Zaidi...
Kufunguliwa Yusufu(a.s) Kutoka Gerezani
Yusufu(a. Soma Zaidi...