Kupigwa vita Uislamu Tanganyika na Afrika Mashariki

Kupigwa vita Uislamu Tanganyika na Afrika Mashariki

Kupigwa vita Uislamu Tanganyika na Afrika Mashariki

i. Wamishionari wa kikristo waliona kuwa Uislamu ni kikwazo kwao, waliagiza machifu (viongozi wa kikabila) kuzuia Uislamu kuenea zaidi nje ya miji ya Pwani.
ii. Mkutano wa Berlin mwaka 1884, ulitoa kipaumbelea na fursa ya Ukristo kuwa na nguvu Afrika na kuweka mikakati ya kudhoofisha Uislamu na waislamu.
iii. Vyama vya Wamishionari, kikiwemo cha White Fathers chini ya Kardinali Lavingire, walianzisha mashule, vyuo na makanisa ilikueneza ukristo kupitia mbinu zifuatazo;
a. Kuficha uadui na uhasama wao dhidi ya waislamu na kujenga urafiki wa uongo na kinafiki.
b. Kujikita sana maeneo ya vijijini ndio ambapo waislamu wengi hawajui dini yao.



c. Kuanzisha makanisha na huduma za kijamii kama vile; mashule na hospitali.

iv. Wamishionari wa kikristo kupitia serikali za Kijerumani na Kiingereza, walianza mashule zilizotumia mfumo wa silabi zisizokuwa za kiarabu ili kudhoofisha utamaduni wa wenyeji wanaotumia silabi za kiarabu.


v. Wamishionari wa kikristo kutokana na ustawi wa waislamu walioukuta, walimshutumu Gavana Von Soden kuwapendelea waislamu, hivyo ikawekwa sera rasmi ya kuwabagua waislamu kielimu.


vi. Serikali ilinyima kabisa au kutoa misaada kidogo (grant in aid) shule zote za waislamu huku ikielekeza makanisani.
Mfano mwaka 1957 serikali ilitoa paundi 1,338,925 kwa mashirika yanayotoa elimu kati ya hizo, waislamu walipewa paundi 6,848 tu


vii. Masharti magumu au kupigwa marufuku waislamu kuanzisha shule zao katika misikiti (Qur’anic schools) na kutakiwa kuendesha kwa maelekezo ya serikali. viii. Serikali za kikoloni zikishirikiana na wamishionari, zilitaifisha mali zote za
waislamu ikiwemo; mashule, maduka, majumba, mashamba, n.k ili kuwadhoofisha kiuchumi kupitia sare ya ujamaa.


ix. Serikali iliwaua au kuwafunga au kuwahamisha viongozi waislamu makini ili kudhoofisha harakati zao juu ya Uislamu.kama akina Tewa Said Tewa, Suleiman Takadr, Bi Titi Mohamed, n.k.

x. Wamishionari kwa kushirikiana serikali, walianza sera ya dini mseto na taasisi za kimagharibi zinazoshughulikia miradi ya waislamu mfano; mradi wa kuritadisha waislamu wa “Islam in Africa Project” huko Nairobi.


xi. Serikali za kikoloni kwa kushirikiana na wamishionari na wenyeji wakristo, walitumia nguvu ya kuwateka na kuwaua machifu (viongozi waislamu wa kikabila) kama akina; Bushiri wa Pangani, Mkwawa wa Iringa, Isike wa Unyanyembe, Ali Songea Mbano, Suleiman Mamba, n.k ili kuvunja nguvu ya Uislamu.


xii. Chuki za serikali na mishionari dhidi ya machifu waislamu na waislamu, zilizidi na kuamua kupambana nao kivita kama vile vita vya maji maji, n.k.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1100

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Tukio la kupasuliwa kifua Mtume Muhammad S.A.W

Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W, sehemu ya 7

Soma Zaidi...
HISTORIA YA KUJENGWA UPYA KWA AL-KA'BAH (NYUMBA TUKUFU YA ALLAH)

KUJENGWA UPYA KWA AL-KA’ABAHItambulike kuwa Al-ka’abah ndio mjengo wa kwanza kujengwa duniani.

Soma Zaidi...
Je waislamu walishindwa vita vya Uhudi?

Katika vita vya Uhudi waislamu walikufa wengi kulinganisha na makafiri. Lakini makafiri walikimbia uwanja wa vita baada ya kuzidiwa. Je ni nanibalishindwa vita vya Uhudi kati ya waislamu na makafiri?

Soma Zaidi...
Ibrahiim(a.s) Aomba Kupata Kizazi Chema

Nabii Ibrahiim na mkewe Sarah walikaa mpaka wakawa wazee bila ya kupata mtoto.

Soma Zaidi...
tarekh 5

KUZALIWA KWA MTUME (S.

Soma Zaidi...