picha

Uchaguzi wa Omar (Umar) kuwa khalifa wa Pili baada ya Mtume

Uchaguzi wa ‘Umar bin Khattab kuwa Khalifa wa Pili.

Uchaguzi wa Omar (Umar) kuwa khalifa wa Pili baada ya Mtume

Uchaguzi wa ‘Umar bin Khattab kuwa Khalifa wa Pili.

Mtume(s.a.w.) kumchagua Abubakar kuwa Imam wa msikiti na kutoruhusu mtu mwingine kuswalisha na aliposwalisha mtu mwingine swala ilirudiwa ni dhahiri, kwa maoni yetu, Mtume(s.a.w.) aliashiria kuwa kiongozi awe Abubakar na akawaachia Waislamu waamue kumkubali au kumkataa. Tunaamini kuwa Abubakar alimuelewa hivi Mtume(s.a.w.) ndio maana alipokuwa anakaribia kutawafu aliwaita wajumbe wa Shura na kushauri kuwa yeye anampendekeza Umar awe ndiye Khalifa baada ya kifo chake. Wajumbe wa Shura walipokubali ndipo akamwambia Ali aandike usia huo. Abubakar alifanya hivi kwa jitihadi yake ambayo inakubalika katika Uislamu na hasa akizingatia hali ilivyokuwa mara Mtume alipofariki, Waislamu walipogawanyika makundi matatu yaani ukoo wa mtume, Muhajirin na Answari.

Hivyo alitumia njia hii ambayo ni ya Kiislamu, hakuiburuza Shura na kulikuwa na mjadala kabla ya kukubalika rai hiyo. Wajumbe maarufu wa Shura walikuwa ’Umar, Uthman, Ali,Talha, Abdul Rahman bin Auf, Muadh bin Jabal, Ubay bin Kaab, Zaid bin Thabit na wajumbe wengine mashuhuri kutoka Muhajirin na Ansar. Abubakar alitoa pendekezo lake la kumteua Umar kuwa Khalifa wa pili, wote walikubali ila walieleza wasi wasi wao juu ya ukali wa Umar, hii ndio hoja pekee iliyotolewa na Ali na Talha. Abubakar aliikataa hoja hii kwa kuwafahamisha kuwa Ukhalifa utamfanya asiwe mkali. Kwa kuwa hoja dhidi ya Umar ilikuwa hii tu basi pendekezo likakubalika.

Hatua iliyofuata ambayo imeimarisha uhuru wa kuchagua viongozi ni kuwahutubia waumini katika msikiti wa Mtume, akisaidiwa na jamaa zake, alisimama kwenye mimbari, kwanza alitaka ule usia usomwe mbele ya watu wote waliokuwa msikitini na yeye azungumze nao.9 Usia wenyewe ulikuwa kama ifuatavyo:

Bismillahir Rahmanir Rahiim. Hili ni tamko linalofanywa na Abubakar bin Abi Qahafu ambaye yuko karibu ya kwenda akhera. Wakati wa kuwa katika hali ya kufa hata kafiri humuamini Mwenyezi Mungu, na hata mfanya madhambi hutubia (hurudi kwenye imani yake) na kafiri humtegemea Mwenyezi Mungu. Nimefanya kila jema kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake na kwa kuboresha dini yake na kwa manufaa ya Waislamu na kwa mimi mwenyewe katika kumteua Umar kuwa Khalifa. Nategemea atakuwa muaminifu na mtekelezaji haki lakini akibadilika na kuwa dhalimu mimi sina lawama kwa kuwa sina elimu ya ghaibu. Kila mmoja anawajibika kwa afanyayo.24


Baada ya usia huu kusomwa, Abubakar alipanda kwenye mimbari huku akisaidiwa na kuuhutubia umma kama ifuatavyo:-

Enyi ndugu zangu, sikumchagua kuwa Khalifa ukoo wangu au ndugu zangu. Nimemteua aliyebora miongoni mwenu mnakubaliana na uteuzi wangu? Wote waliitikia kwa kukubali.11



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1872

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 web hosting    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Nabii Isa(a.s) Azungumza Akiwa Mtoto Mchanga

Maryam akamtwaa mwanawe, akaenda naye kwa jamaa zake amembeba.

Soma Zaidi...
Vitimbi vya Makafiri Dhidi ya Nabii Salih(a.s) na Waumini na kuangamizwa kwao

Makafiri wa Kithamud hawakuishia tu kwenye kuukataa ujumbe wa Nabii Salih(a.

Soma Zaidi...
Maryam Apewa Habari ya Kumzaa Isa(a.s)

Baada ya maandalizi hayo ya kimalezi pamoja na hifadhi ya Allah(s.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya sura zilizochaguliwa

Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
tarekh 10

KULELEWA NA BABA YAKE MDOGOBaada ya kufariki kwa mzee huyu, kiongozi mkubwa wa maquraysh na makkah, kiongozi ambaye jeshi la Abrah liliangamizwa ndani ya utawala wake.

Soma Zaidi...
Mbinu za Da’wah Alizotumia Nuhu(a.s)

Katika kufikisha ujumbe huu kwa watu wake Nuhu(a.

Soma Zaidi...
Historia ya Watoto Wawili wa Nabii Adam

“Na wasomee khabari za watoto wawili wa Adam kwa kweli, walipotoa sadaka, ikakubaliwa ya mmoja wao na ya mwingine haikukubaliwa Akasema (yule asiyekubaliwa sadaka yake): “Nitakuua”.

Soma Zaidi...