image

Uchaguzi wa Omar (Umar) kuwa khalifa wa Pili baada ya Mtume

Uchaguzi wa ‘Umar bin Khattab kuwa Khalifa wa Pili.

Uchaguzi wa Omar (Umar) kuwa khalifa wa Pili baada ya Mtume

Uchaguzi wa ‘Umar bin Khattab kuwa Khalifa wa Pili.

Mtume(s.a.w.) kumchagua Abubakar kuwa Imam wa msikiti na kutoruhusu mtu mwingine kuswalisha na aliposwalisha mtu mwingine swala ilirudiwa ni dhahiri, kwa maoni yetu, Mtume(s.a.w.) aliashiria kuwa kiongozi awe Abubakar na akawaachia Waislamu waamue kumkubali au kumkataa. Tunaamini kuwa Abubakar alimuelewa hivi Mtume(s.a.w.) ndio maana alipokuwa anakaribia kutawafu aliwaita wajumbe wa Shura na kushauri kuwa yeye anampendekeza Umar awe ndiye Khalifa baada ya kifo chake. Wajumbe wa Shura walipokubali ndipo akamwambia Ali aandike usia huo. Abubakar alifanya hivi kwa jitihadi yake ambayo inakubalika katika Uislamu na hasa akizingatia hali ilivyokuwa mara Mtume alipofariki, Waislamu walipogawanyika makundi matatu yaani ukoo wa mtume, Muhajirin na Answari.

Hivyo alitumia njia hii ambayo ni ya Kiislamu, hakuiburuza Shura na kulikuwa na mjadala kabla ya kukubalika rai hiyo. Wajumbe maarufu wa Shura walikuwa ’Umar, Uthman, Ali,Talha, Abdul Rahman bin Auf, Muadh bin Jabal, Ubay bin Kaab, Zaid bin Thabit na wajumbe wengine mashuhuri kutoka Muhajirin na Ansar. Abubakar alitoa pendekezo lake la kumteua Umar kuwa Khalifa wa pili, wote walikubali ila walieleza wasi wasi wao juu ya ukali wa Umar, hii ndio hoja pekee iliyotolewa na Ali na Talha. Abubakar aliikataa hoja hii kwa kuwafahamisha kuwa Ukhalifa utamfanya asiwe mkali. Kwa kuwa hoja dhidi ya Umar ilikuwa hii tu basi pendekezo likakubalika.

Hatua iliyofuata ambayo imeimarisha uhuru wa kuchagua viongozi ni kuwahutubia waumini katika msikiti wa Mtume, akisaidiwa na jamaa zake, alisimama kwenye mimbari, kwanza alitaka ule usia usomwe mbele ya watu wote waliokuwa msikitini na yeye azungumze nao.9 Usia wenyewe ulikuwa kama ifuatavyo:

Bismillahir Rahmanir Rahiim. Hili ni tamko linalofanywa na Abubakar bin Abi Qahafu ambaye yuko karibu ya kwenda akhera. Wakati wa kuwa katika hali ya kufa hata kafiri humuamini Mwenyezi Mungu, na hata mfanya madhambi hutubia (hurudi kwenye imani yake) na kafiri humtegemea Mwenyezi Mungu. Nimefanya kila jema kwa ajili ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake na kwa kuboresha dini yake na kwa manufaa ya Waislamu na kwa mimi mwenyewe katika kumteua Umar kuwa Khalifa. Nategemea atakuwa muaminifu na mtekelezaji haki lakini akibadilika na kuwa dhalimu mimi sina lawama kwa kuwa sina elimu ya ghaibu. Kila mmoja anawajibika kwa afanyayo.24


Baada ya usia huu kusomwa, Abubakar alipanda kwenye mimbari huku akisaidiwa na kuuhutubia umma kama ifuatavyo:-

Enyi ndugu zangu, sikumchagua kuwa Khalifa ukoo wangu au ndugu zangu. Nimemteua aliyebora miongoni mwenu mnakubaliana na uteuzi wangu? Wote waliitikia kwa kukubali.11



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 305


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

Hatua ya Serikali Dhidi ya Waanzilishi wa Fitna na Farka wakati wa khalifa
Soma Zaidi...

Kuhifadhiwa kwa Quran
Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kuangamizwa Firauni na Majeshi Yake
Soma Zaidi...

HISTORIA YA MTUME ILYASA(A.S)
Mtume Ilyasa ni mmoja wa Mitume waliotumwa kupitia kizazi cha Bani Israil. Soma Zaidi...

Kazi na wajibu wa khalifa katika dola ya kiislamu
Kazi na Wajibu wa KhalifaKhalifa katika Serikali ya Kiislamu ndiye mtendaji mkuu wa Serikali kama alivyokuwa Mtume(s. Soma Zaidi...

Njama za Kumuua Nabii Yusufu(a.s)
Kwa tabia zake njema Yusufu(a. Soma Zaidi...

Mapambano ya Mtume Muhammad dhidi ya Wanafiki na hila zao Madina
Soma Zaidi...

Imam Abu Daud na Sunan Abi Daud
Soma Zaidi...

Mafunzo yatokanayo na mkataba wa aqabah katika kuandaa ummah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mbinu za Da’wah Alizotumia Nuhu(a.s)
Katika kufikisha ujumbe huu kwa watu wake Nuhu(a. Soma Zaidi...

Vita vya Badr: Chanzo na sababu za vita vya Badr, Mafunzo ya Vita Vya Badr
Vita vya Badri. Soma Zaidi...

Waliomshambulia na kumuuwa Ali, makhawariji na si muawiya
Soma Zaidi...