Muawiyah Ateka Jimbo la Misri
Khalifa Ali alimteua Qais bin Sad awe gavana wa Misri. Qais alichukua ahadi ya utii kwa niaba ya watu wa Misri, lakini watu wa jimbo la Khartaban hawakutoa ahadi ya utii kwa Khalifa Ali na Qais aliwaacha kwa kuwa kulikuwa na amani.
Hali hii ya kuwaacha watu wa Khartaban iliwafanya baadhi ya watu wamuone Qais sio mtiifu kwa Khalifa. Khalifa alikusudia kumjaribu Qais kwa kumuamuru awapige vita watu wa Khartaban. Qais hakuona sababu ya kupigana na watu wa Kharaban hivyo akaondolewa kwenye ugavana na nafasi yake akateuliwa Muhammad bin Abubakar.
Muhammad alikuwa kijana hivyo aliwalazimisha watu wa Khartaban wakubali Ukhalifa wa Ali. Watu wa Khartaban hawakukubali na walisubiri hadi vita vya Siffin vilipomalizika waliamua kujilinda dhidi ya majeshi ya gavana Muhammad bin Abubakar na mapigano yakazuka. Majeshi ya gavana yakashindwa mara mbili. Khalifa aliamua kumbadilisha Muhammad na kumtuma Ushtar kuwa gavana wa Misri.
Lakini Ushtar alikufa alipofika mpakani mwa Misr hivyo Khalifa alimtaka Muhammad aendelee kushikilia ugavana wa Misri akamtumia askari 2,000 ambao aliwapata kwa taabu. Lakini kabla askari wa Khalifa hawajafika Muawiya alimtuma Amri bin al As na jeshi la kutosha, likayashinda majeshi ya gavana na yeye mwenyewe kuuliwa. Kwa ushindi huu Misri ikawa chini ya Muawiyah na Amr bin al As akawa gavana wa Muawiyah Misri. Hii ilikuwa katika mwaka wa 38 A.H.
Umeionaje Makala hii.. ?
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...βNa (kumbukeni habari hii) Mola wake alipomfanyia mtihani (Nabii) Ibrahiim kwa amri nyingi; naye akazitimiza.
Soma Zaidi...Kwanza, ili tuweze kusimamisha Uislamu katika jamii hatunabudi kuanzisha na kuendeleza vituo vya harakati, misikiti ikiwa ndio vitovu.
Soma Zaidi...KULELEWA NA BABA YAKE MDOGOBaada ya kufariki kwa mzee huyu, kiongozi mkubwa wa maquraysh na makkah, kiongozi ambaye jeshi la Abrah liliangamizwa ndani ya utawala wake.
Soma Zaidi...Sira na historia ya Mtume Muhammad s.a.w, sehemu ya 17. Historia ya Bi Khadija na familia yake.
Soma Zaidi...