Baada ya maandalizi hayo ya kimalezi pamoja na hifadhi ya Allah(s.
Baada ya maandalizi hayo ya kimalezi pamoja na hifadhi ya Allah(s.w) aliyopewa Maryam, Allah(s.w) akamtuma Malaika kumueleza Bi Maryam habari za kumzaa masihi, Isa(a.s) bila ya baba ila kwa amri ya Allah(s.w) ya “Kuwa ikawa”. Malaika akamwambia:
Ewe Maryam! Mwenyezi Mungu anakupa habari njema (za kumzaa mtoto kwa) neno litokalo kwake. Jina lake Masihi Isa bin Maryam, mwenye heshima katika dunia na akhera, na ni miongoni mwa waliotukuzwa.(3:45) Naye atazungumza na watu katika utoto na katika utu uzima wake, na ni katika watu wema (3:46)
Maryam Akasema:Mola wangu! Nitapataje Mtoto hali mtu yoyote hakunigusa? Akajibu: Ndivyo, vivyo hivyo; Mwenyezi Mungu huumba anavyopenda: anapohukumu jambo, huliambia ‘Kuwa’, likawa(3:47) Na Mwenyezi Mungu atamfunza kitabu na hekima, na kujua Taurati na
Injili. Na ni Mtume kwa wana wa Israili...................(3:48-49)
Allah(s.w) anatueleza kuwa Nabii Isa(a.s) alizaliwa chini ya mtende, na wala hakuzaliwa kwenye zizi la ng’ombe lenye najisi kama wanavyodai katika Biblia.
Basi (Maryam)akachukua mimba yake, na akaondoka nayo mahali pa mbali. Kisha uchungu ukampeleka katika shina la mtende, akasema: “Laiti ningekufa kabla ya haya, na ningekuwa niliyesahaulika kabisa. (19:22-23)
Mara ikamfika sauti kutoka chini yake inamwambia: “Usihuzunike”. Hakika Mola wako amejaalia kijito cha maji chini yako”. Na litikise kwako shina la mtende, litakuangushia tende nzuri, zilizo mbivu. (19:24-25) Basi ule na unywe litue jicho lako.(19:26)
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 730
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio
👉2 Kitau cha Fiqh
👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉4 Kitabu cha Afya
👉5 Madrasa kiganjani
👉6 kitabu cha Simulizi
Uasi katika dola ya kiislamu na matokeo yake
Uasi katika dola ya kiislamu na matokeo yake. Soma Zaidi...
Historia ya Dhulqarnain
Dhulqarnain sio jina la mtu bali cheo, maana yake ikiwa: “Mwenye Pembe Mbili”. Soma Zaidi...
Kuhajiri Waislamu wa Makka Kwenda Madinah
Baada ya mikataba miwili ya ‘Aqabah na baada ya Waislamu 75 kufika Yathrib salama, Mtume(s. Soma Zaidi...
Historia ya kujengwa kwa Alkabah (Maka)
Kama tulivyoona katika maisha ya Mtume Ibrahim(a. Soma Zaidi...
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Lut (a.s)
(i) Tujitahidi kwa kadiri ya uwezo wetu kuondoa maovu katika jamii kwa mikono yetu na ikiwa hatuwezi tuyakemee kama alivyofanya Nabii Lut(a. Soma Zaidi...
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Daud(a.s)
Kutokana historia ya Nabii Daud (a. Soma Zaidi...
Mpango wa kumuuwa Khalifa ally na Gavana Muawiya
Soma Zaidi...
Mchango wa Waislamu Katika Kuleta Uhuru Tanganyika
i. Soma Zaidi...
Darsa za Sira historia ya Mtume (s.a.w) Jaribio la 02
Soma Zaidi...
Hatua mbili kuu za kushuka kwa Quran
Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
tarekh 06
MAISHA YA UTOTONI YA MTUME S. Soma Zaidi...
Mkataba wa 'Aqabah na vipiengele vyake na mafunzo tunayoyapata katika mkataba wa aqaba
Mtume (s. Soma Zaidi...