image

Maryam Apewa Habari ya Kumzaa Isa(a.s)

Baada ya maandalizi hayo ya kimalezi pamoja na hifadhi ya Allah(s.

Maryam Apewa Habari ya Kumzaa Isa(a.s)

Maryam Apewa Habari ya Kumzaa Isa(a.s)


Baada ya maandalizi hayo ya kimalezi pamoja na hifadhi ya Allah(s.w) aliyopewa Maryam, Allah(s.w) akamtuma Malaika kumueleza Bi Maryam habari za kumzaa masihi, Isa(a.s) bila ya baba ila kwa amri ya Allah(s.w) ya “Kuwa ikawa”. Malaika akamwambia:


Ewe Maryam! Mwenyezi Mungu anakupa habari njema (za kumzaa mtoto kwa) neno litokalo kwake. Jina lake Masihi Isa bin Maryam, mwenye heshima katika dunia na akhera, na ni miongoni mwa waliotukuzwa.(3:45) Naye atazungumza na watu katika utoto na katika utu uzima wake, na ni katika watu wema (3:46)



Maryam Akasema:Mola wangu! Nitapataje Mtoto hali mtu yoyote hakunigusa? Akajibu: Ndivyo, vivyo hivyo; Mwenyezi Mungu huumba anavyopenda: anapohukumu jambo, huliambia ‘Kuwa’, likawa(3:47) Na Mwenyezi Mungu atamfunza kitabu na hekima, na kujua Taurati na
Injili. Na ni Mtume kwa wana wa Israili...................(3:48-49)



Kuzaliwa Nabii Isa(a.s)


Allah(s.w) anatueleza kuwa Nabii Isa(a.s) alizaliwa chini ya mtende, na wala hakuzaliwa kwenye zizi la ng’ombe lenye najisi kama wanavyodai katika Biblia.




Basi (Maryam)akachukua mimba yake, na akaondoka nayo mahali pa mbali. Kisha uchungu ukampeleka katika shina la mtende, akasema: “Laiti ningekufa kabla ya haya, na ningekuwa niliyesahaulika kabisa. (19:22-23)

Mara ikamfika sauti kutoka chini yake inamwambia: “Usihuzunike”. Hakika Mola wako amejaalia kijito cha maji chini yako”. Na litikise kwako shina la mtende, litakuangushia tende nzuri, zilizo mbivu. (19:24-25) Basi ule na unywe litue jicho lako.(19:26)





                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 363


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Sababu ya uislamu kuwa ndiyo dini sahihi pekee
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Imam Ibn Majah na Sunan Ibn Majah
Soma Zaidi...

tarekh11
KUKUTANA NA BAHIRA (MTAWA) WA KIYAHUDIMzee Abu talib alikuwa ni mfanya biashara, hivyoslikuwa akimchukuwa kijana wake kwenda kwenye biashara. Soma Zaidi...

HISTORIA YA KUZALIWA KWA MTUME MUHAMMAD (S.A.W) NA MAMA AMINA MKE WA ABDALLAH MTOTO WA ABDUL-AL MUTALIB
KUZALIWA KWA MTUME (S. Soma Zaidi...

Mafunzo yatokanayo na hijrah ya mtume na maswahaba wake
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Maswali kuhusu hali ya bara arabu zama za jahiliyyah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mafunzo yatokanayo na Historia ya Nabii Yunus(a.s)
(i) Allah(s. Soma Zaidi...

Mtume (s.a.w) alivyoandaa ummah wa kiislamu makkah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Ijuwe Dua ya Ayyuub(a.s)
Nabii Ayyuub(a. Soma Zaidi...

Maandalizi ya hijrah ya mtume na waislamu kuhamia madinah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ibrahiim(a.s)
Soma Zaidi...

Kuzaliwa kwa Mtume S.A.W
Sura na historia ya Mtume Muhammad s.sa. w, sehemu ya 5. Hapa utajifunza kuhusu kuzaliwa kwa Mtume. Soma Zaidi...