Ugonjwa wa Pumu, dalili zake na njia za kujilinda dhidi ya Pumu.
Pumu ni ugonjwa ambao huathiri sehemu ya kupitisha hewa kwenda kwenye mapafu ya binadamu kitaalamu huitwa bronchioles. Mtu mwenye pumu huwa na michubuko sugu mwilini kwenye mirija yake ya kupitisha hewa. Hali ambayo husababisha kuvimba kwa kuta za mirija
Kuna makundi mawili ya pumu nayo ni:; 1.pumu ya ghafla (acute). Hii huwa ya Kawaida ambapo humfanya mgonjwa aweze kustahimili 2.pumu sugu; hii hufanya njia kuwa nyembamba zaidi kutokana na kuziba kwa kuta na Hali hii ikizidi nyia huwa nyembamba zaidi.
Sababu zinazopelekea kupata ugonjwa wa pumu;
-matatizo ya kinasaba
-maendeleo ya kiuchumi
-uvutaji wa sigara na tumbaku kipind mama akiwa mjamzito kupelekea mtoto kupata pumu.
-magonjwa ya mapafu Kama bronchitis
-vyanzo vya mzio ( allergens) Kam vile vumbi, vinyesi vya wanyama na baadhi ya vyakula.
-uchafuzi wa mazingira Kama Moshi na baadhi ya harufu Kali.
-baadhi ya kemikali kwenye maeneo ya kazi hasa kwenye viwanda Kama vya rangi chuma sementi na zege
-baadhi ya wagonjwa wanaotumia dawa za shinikizo la damu
Visababishi au uwezekano wa kupata pumu;
-kuishi sehemu yenye baridi na vumbi
-msongo wa mawazo
-kuishiwa na pumzi na kupumua kwa shida
-historia ya pumu au historia ya kurithi
-Aina ya matatizo katika njia yake ya kula
Dalili za pumu
-kuishiwa na pumzi na kupumua kwa shida
-kutoa sauti Kama mluzi wakati wa kupumua
-kifua kubana
-kushindwa kuongea endapo ugonjwa utakuwa sugu
-kukohoa Sana asa wakati wa asubuh na usiku
Vipimo madactari huangalia vitu mbalimbali ili kujiridhisha Kama mgonjwa ana pumu navyo ni;
1.kipimo Cha Cha damu
2.kipimo cha kuchunguza uwezo wa mgonjwa kutoa hewa nje Mara baada ya kuvuta.
3.x-ray ya kifua.
Mgonjwa wa pumu anashauriwa kuwa na dawa wakati wote ambayo itakuwa inamsaidia pale ambapo atakuwa anashindwa kutoa au kuvuta hewa.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitau cha Fiqh 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Imani potofu juu ya chanjo.
Post hii inahusu zaidi Imani potofu juu ya chanjo kwa watoto na akina Mama, ni baadhi ya Imani waliyonayo watu juu ya chanjo.
Soma Zaidi...Ambao hawapaswi kupata chanjo
Posti hii inahusu zaidi watu ambao hawapaswi kupewa chanjo, hawa ni wale ambao wana hali tofauti na ikitokea wakapata chanjo wanaweza kupata madhara badala ya kuwasaidia.
Soma Zaidi...Njia za kukabiliana na presha ya kupanda/hypertension
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kukabiliana na presha ya kupanda
Soma Zaidi...HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEPANDWA NA PRESHA
Presha ya kupanda hutokea pale kipimo kinaposoma zaidi ya 120/80mm Hg.
Soma Zaidi...Viwango vitatu vya kuungua.
Posti hii inahusu zaidi viwango vitatu vya kuungua. Ili tuweze kujua mtu ameunguaje Kuna viwango vitatu vya kujua kiasi na namna mtu alivyoungua
Soma Zaidi...Namna ya kumwosha Mgonjwa vidonda
Posti hii inahusu zaidi njia za kutumia unapotaka kumwosha Mgonjwa vidonda, ni njia muhimu ambazo ni lazima kuzipitia unapotaka kumwosha Mgonjwa vidonda.
Soma Zaidi...