Ugonjwa wa Pumu, dalili zake na njia za kujilinda dhidi ya Pumu.
Pumu ni ugonjwa ambao huathiri sehemu ya kupitisha hewa kwenda kwenye mapafu ya binadamu kitaalamu huitwa bronchioles. Mtu mwenye pumu huwa na michubuko sugu mwilini kwenye mirija yake ya kupitisha hewa. Hali ambayo husababisha kuvimba kwa kuta za mirija
Kuna makundi mawili ya pumu nayo ni:; 1.pumu ya ghafla (acute). Hii huwa ya Kawaida ambapo humfanya mgonjwa aweze kustahimili 2.pumu sugu; hii hufanya njia kuwa nyembamba zaidi kutokana na kuziba kwa kuta na Hali hii ikizidi nyia huwa nyembamba zaidi.
Sababu zinazopelekea kupata ugonjwa wa pumu;
-matatizo ya kinasaba
-maendeleo ya kiuchumi
-uvutaji wa sigara na tumbaku kipind mama akiwa mjamzito kupelekea mtoto kupata pumu.
-magonjwa ya mapafu Kama bronchitis
-vyanzo vya mzio ( allergens) Kam vile vumbi, vinyesi vya wanyama na baadhi ya vyakula.
-uchafuzi wa mazingira Kama Moshi na baadhi ya harufu Kali.
-baadhi ya kemikali kwenye maeneo ya kazi hasa kwenye viwanda Kama vya rangi chuma sementi na zege
-baadhi ya wagonjwa wanaotumia dawa za shinikizo la damu
Visababishi au uwezekano wa kupata pumu;
-kuishi sehemu yenye baridi na vumbi
-msongo wa mawazo
-kuishiwa na pumzi na kupumua kwa shida
-historia ya pumu au historia ya kurithi
-Aina ya matatizo katika njia yake ya kula
Dalili za pumu
-kuishiwa na pumzi na kupumua kwa shida
-kutoa sauti Kama mluzi wakati wa kupumua
-kifua kubana
-kushindwa kuongea endapo ugonjwa utakuwa sugu
-kukohoa Sana asa wakati wa asubuh na usiku
Vipimo madactari huangalia vitu mbalimbali ili kujiridhisha Kama mgonjwa ana pumu navyo ni;
1.kipimo Cha Cha damu
2.kipimo cha kuchunguza uwezo wa mgonjwa kutoa hewa nje Mara baada ya kuvuta.
3.x-ray ya kifua.
Mgonjwa wa pumu anashauriwa kuwa na dawa wakati wote ambayo itakuwa inamsaidia pale ambapo atakuwa anashindwa kutoa au kuvuta hewa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 web hosting 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
fahamu vitamini A na kazi zake
Je na wewe i katika wale ambaowanahitaji kujuwa kuhusu Vitamini A, kazi zake na vyakula vya vitamini A. post hii inakwenda kukujuza zaidi pamoja na historia ya vitamini A.
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu vitamini D na kazi zake mwilini
Hapa utajifunza kuusu vitamini D, kazi zake, upungufu wake na chanzo cha kupata vitamini D.
Soma Zaidi...Njia za kuzuia damu isiendelee kuvuja
Posti hii inahusu zaidi njia za kuzuia damu isiendelee kuvuja, ni njia ambazo utumika ikiwa kuna damu inavuja kwenye sehemu yoyote ya mwili,kwa hiyo tunaweza kutumia njia hizi ili kuepuka kuendelea kuvuja kwa damu.
Soma Zaidi...Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na kwikwi
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na kwikwi
Soma Zaidi...Kazi ya protin na vyakula vya protini mwilini
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya kazi ya protin na vyakula vya protini mwilini
Soma Zaidi...Ratiba ya chanjo ya polio
Posti hii inahusu zaidi namna chanjo ya polio inavyotolewa na ratiba zake yaani kuanzia siku ya kwanza mpaka pale mtoto anapomaliza chanjo hii kwa hiyo tuone ratiba ya chanjo ya polio.
Soma Zaidi...