Ugonjwa wa Pumu, dalili zake na njia za kujilinda dhidi ya Pumu.
Pumu ni ugonjwa ambao huathiri sehemu ya kupitisha hewa kwenda kwenye mapafu ya binadamu kitaalamu huitwa bronchioles. Mtu mwenye pumu huwa na michubuko sugu mwilini kwenye mirija yake ya kupitisha hewa. Hali ambayo husababisha kuvimba kwa kuta za mirija
Kuna makundi mawili ya pumu nayo ni:; 1.pumu ya ghafla (acute). Hii huwa ya Kawaida ambapo humfanya mgonjwa aweze kustahimili 2.pumu sugu; hii hufanya njia kuwa nyembamba zaidi kutokana na kuziba kwa kuta na Hali hii ikizidi nyia huwa nyembamba zaidi.
Sababu zinazopelekea kupata ugonjwa wa pumu;
-matatizo ya kinasaba
-maendeleo ya kiuchumi
-uvutaji wa sigara na tumbaku kipind mama akiwa mjamzito kupelekea mtoto kupata pumu.
-magonjwa ya mapafu Kama bronchitis
-vyanzo vya mzio ( allergens) Kam vile vumbi, vinyesi vya wanyama na baadhi ya vyakula.
-uchafuzi wa mazingira Kama Moshi na baadhi ya harufu Kali.
-baadhi ya kemikali kwenye maeneo ya kazi hasa kwenye viwanda Kama vya rangi chuma sementi na zege
-baadhi ya wagonjwa wanaotumia dawa za shinikizo la damu
Visababishi au uwezekano wa kupata pumu;
-kuishi sehemu yenye baridi na vumbi
-msongo wa mawazo
-kuishiwa na pumzi na kupumua kwa shida
-historia ya pumu au historia ya kurithi
-Aina ya matatizo katika njia yake ya kula
Dalili za pumu
-kuishiwa na pumzi na kupumua kwa shida
-kutoa sauti Kama mluzi wakati wa kupumua
-kifua kubana
-kushindwa kuongea endapo ugonjwa utakuwa sugu
-kukohoa Sana asa wakati wa asubuh na usiku
Vipimo madactari huangalia vitu mbalimbali ili kujiridhisha Kama mgonjwa ana pumu navyo ni;
1.kipimo Cha Cha damu
2.kipimo cha kuchunguza uwezo wa mgonjwa kutoa hewa nje Mara baada ya kuvuta.
3.x-ray ya kifua.
Mgonjwa wa pumu anashauriwa kuwa na dawa wakati wote ambayo itakuwa inamsaidia pale ambapo atakuwa anashindwa kutoa au kuvuta hewa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 web hosting 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Sababu za kumwosha Mgonjwa mwili mzima.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kumwosha Mgonjwa mwili mzima,ni sababu ambazo umsaidie mgonjwa ili aweze kupata nafuu mapema na kumsaidia kama tutakavyoona hapo chini
Soma Zaidi...Vyakula vya fati na mafuta
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu faida za vyakula vya fati na mafuta
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu kazi za ini.
Posti hii inahusu zaidi kazi za ini, kwa kawaida tunafahamu kwamba ini ni sehemu muhimu kwenye mwili wa binadamu kwa sababu ni.likikosa kufanya kazi yake maisha ya binadamu yanakuwa hatarini kwa sababu mbalimbali.
Soma Zaidi...Namna ya kumlisha Mgonjwa ambaye hawezi kujilisha mwenyewe ni
Posti hii inahusu njia za kumlisha Mgonjwa ambaye hawezi kujilisha wenyewe, hali hii uwa inawapata wagonjwa wale ambao hawawezi kujilisha wenyewe tunaweza kuwalisha kwa njia zifuatazo.
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu vitamini D na kazi zake mwilini
Hapa utajifunza kuusu vitamini D, kazi zake, upungufu wake na chanzo cha kupata vitamini D.
Soma Zaidi...Namna ya kuwasaidia wagonjwa wa vidonda vya tumbo
Post hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia wagonjwa wa vidonda vya tumbo, ni njia ya kuwasaidia wagonjwa waliopata madonda ya tumbo
Soma Zaidi...