Ugonjwa wa Pumu, dalili zake na njia za kujilinda dhidi ya Pumu.
Pumu ni ugonjwa ambao huathiri sehemu ya kupitisha hewa kwenda kwenye mapafu ya binadamu kitaalamu huitwa bronchioles. Mtu mwenye pumu huwa na michubuko sugu mwilini kwenye mirija yake ya kupitisha hewa. Hali ambayo husababisha kuvimba kwa kuta za mirija
Kuna makundi mawili ya pumu nayo ni:; 1.pumu ya ghafla (acute). Hii huwa ya Kawaida ambapo humfanya mgonjwa aweze kustahimili 2.pumu sugu; hii hufanya njia kuwa nyembamba zaidi kutokana na kuziba kwa kuta na Hali hii ikizidi nyia huwa nyembamba zaidi.
Sababu zinazopelekea kupata ugonjwa wa pumu;
-matatizo ya kinasaba
-maendeleo ya kiuchumi
-uvutaji wa sigara na tumbaku kipind mama akiwa mjamzito kupelekea mtoto kupata pumu.
-magonjwa ya mapafu Kama bronchitis
-vyanzo vya mzio ( allergens) Kam vile vumbi, vinyesi vya wanyama na baadhi ya vyakula.
-uchafuzi wa mazingira Kama Moshi na baadhi ya harufu Kali.
-baadhi ya kemikali kwenye maeneo ya kazi hasa kwenye viwanda Kama vya rangi chuma sementi na zege
-baadhi ya wagonjwa wanaotumia dawa za shinikizo la damu
Visababishi au uwezekano wa kupata pumu;
-kuishi sehemu yenye baridi na vumbi
-msongo wa mawazo
-kuishiwa na pumzi na kupumua kwa shida
-historia ya pumu au historia ya kurithi
-Aina ya matatizo katika njia yake ya kula
Dalili za pumu
-kuishiwa na pumzi na kupumua kwa shida
-kutoa sauti Kama mluzi wakati wa kupumua
-kifua kubana
-kushindwa kuongea endapo ugonjwa utakuwa sugu
-kukohoa Sana asa wakati wa asubuh na usiku
Vipimo madactari huangalia vitu mbalimbali ili kujiridhisha Kama mgonjwa ana pumu navyo ni;
1.kipimo Cha Cha damu
2.kipimo cha kuchunguza uwezo wa mgonjwa kutoa hewa nje Mara baada ya kuvuta.
3.x-ray ya kifua.
Mgonjwa wa pumu anashauriwa kuwa na dawa wakati wote ambayo itakuwa inamsaidia pale ambapo atakuwa anashindwa kutoa au kuvuta hewa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Zijue sababu za chakula kushindwa kumengenywa kwenye tumbo.
Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali za chakula kushindwa kumengenywa kwenye tumbo,ni sababu mbalimbali hasa za kiafya kama tutakavyoona hapo mbeleni
Soma Zaidi...Mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa wagonjwa walio na majeraha ya macho.
Posti hii inaelezea kuhusiana na mbinu za kutoa huduma ya kwanza kwa walio na majeraha ya macho kutokana na aina mbalimbali ya jeraha
Soma Zaidi...Umuhimu wa asidi iliyokwenye tumbo( kwa kitaalamu huitwa HCL)
Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa asidi iliyo kwenye tumbo kwa kitaalamu huitwa HCL, ni asidi inayofanya kazi nyingi hasa wakati wa kumengenya chakula.
Soma Zaidi...Kiasi Cha mkojo kisichokuwa cha kawaida.
Hii posti inahusu zaidi sifa za mkojo usio wa kawaida,ukiona mkojo wa namna hii unapaswa kwenda hospitalini kwa matibabu au vipimo vya zaidi.
Soma Zaidi...Huduma kwa watu waliodhani wamepatwa na maambukizi.
Posti hii inahusu zaidi huduma ambazo utolewa kwa watu wanaodhani wamepatwa na maambukizi ya virus vya ukimwi.
Soma Zaidi...