image

Utajiri wa baba na kifo chake

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani

UTAJIRI WA BABA NA KIFO CHAKE.

Baba yangu akawa tajiri kwa ghafla. Utajiri wa baba haukumfanya abadili tabia. Siku zote aliendelea kuwa mkarimu kwa watu wote. Aliamini kuwa utajiri ule amepewa na Mwenyezi Mungu kwa sababu maalumu. Baba aliwawezesha na ndugu zake kwa kuwapatia mali alizo nazo. Jina la baba lilibadilika na kuwa muheshimiwa. Utajiri wa baba haukumfanya akose amni kama walivyo matajiri wengine.

 

Baada ya miaka kadhaa baba alifariki na mimi ndiye nikarithi mai za baba yangu. Baba zangu wadogo walikuwa ni wafanyabiashara wa kusafiri maeneo mbalimbali. Sikumoja na mimi nilivutiwa kwenda Yemeni nikiamini huenda nikakutana na wale wageni wa baba wanipe ushauri. Nilisafiri kwa muda wa masiku na hatimaye nikafika. Nikakodi nyumba ya wageni, na kulipia kodi ya miezi kama mitatu.

 

Sikuwa nikifanya bishara nilikuwa nikitumia tu pesa niliyonayo. Nyumbani biashara zangu niliachia ndugu zangu na baba zangu. Nilipokuwa nimekaa kwenye mgahawa alikuja binti mmoja hivi mrefu na mwembaba. Urefu wake haukunizidi mimi na alikuwa mweupe wa wastani. Alikuwa na nywele ndefu na nyusi nyeusi sana. Hakuwa na kope ndefu kama wahindi wa vijijini. Alivaa hijabu ndefu iliyofunika kifua chake. Miinuko miwili iliweza kuonekana kwa mbali kwenye kifua chake. Hakuwa amefunika sura yake, hivyo nikapata muda wa kumtazama vyema, midomo nywekundu, yenye kutengeneza tabasamu pana.

 

Alikuja na kunong’onezana na mama muuza mgahawa. Sikupatapo kusikia sauti yake. Alipomaliza akaondoka zake. Uwepo wake haukusumbua akili yanngu hata kidogo maana nilijisemea hapa mjini ninaweza kulizwa sasahivi. Ijapokuwa nilikuwa namkumbuka lakini wala sikuwaza hata kidogo. Sikumoja nilipokuwa nikinunua farasi kwa ajili ya kutembelea nilipungukiwa na pesa. Nikiwa naomba nipunguziwe ghafla akanieleza kuwa nimelipiwa tayari.

 

Sikuamini nikauliza nani amenilipia, nikaonyeshwa nikamuona ni yule binti wa jana. Sikutaka kujuwa mengi zaidi maana nilifikri huenda ukawa ni mtego wa mimi kuliwa pesa apa mjini. Nikatoa kiasi nilicho nacho na kilichobaki nio nikamwambia huyo aiyenilipia atamaliza. Niliamini kuwa siku yeyote akihitaji pesa yake nitaweza kuilipa. Nilijiuliza inakuweje mtu asiyekujuwa anakulipia mapesa mengi.

 

Sikumoja nikaelekea kwa kadhi wa mji kwenda kumuomba ushauri kuhusu mambo ya kishria biashara halali na haramu. Nilikuwa natamani kuanzisha biashara ya kuuza viatu vya ngozi. Nikataka kujuwa kama naweza kutumia ngozi ya wanyama wasioliwa, kama chui na viatu vile nikaruhusiwa kuingia navyo kwenye nyumba ya ibada. Nilipofika kwa kadhi nkaelezwa kuwa kadhi ana mgeni. Nikaambiwa mgeni ni meya wa mji ana mazungumzo hivyo nirudi baadaye kidogo. Nilizunguka na baadaye niliporudi nikapishana na watu wawili wanatoka kwa kadhi.

 

Mtu mmoja alikuwa ni mwanaume mzee wa makamo aliyepaka hina ndevu zake. Na mwingine alikuwa ni yule binti. Niliwasalimia wote kwa pamoja salamu alykum yaani “Amani iwe juu yenu” wakaitukia waalykum salaam yaani “Na wewe pia amani iwe juu yako”. ghafla moyo ulinidunda mara tu baada ya kusikia sauti ile. Sikujuwa maradhi gani niliyo nayo. Nilipenda sauti ile hasa kwa kuwa namfahamu kidogo mwenye sauti ile.

 

Nikafika kwa kadhi na kumueleza shida yangu. Kadhi alinijibu kuwa inawezekana na bishara hiyo ni halali kabisa. Hivyo kwa pesa niliyo nayoo nikaanza kuweka ahadi kwa wawindaji na washonaji viatu. Baada ya wiki 2 nikawa na hazina ya viatu vingi sana vya ngozi vilivyo katika maumbo mazuri sana. Nilianza kuuza mwenyewe ili kuweza kulifahamu soko. Nikaanza kutengeneza jina kwa ubora wa viatu vyangu.

 

Katika duka langu nikaweza sehemu kwa ajili ya watu waheshima. Niliamini kuwa matajiri na watoto wa mabosi hawaji kwangu kwa sababu hawataki kuchanganyika na watu wa kawaida. Nikaweka chumba ambacho bei zake zilikuwa za juu ijapokuwa bidhaa ni ile ile na ubora uleule. Niliamini kuwa sikuzote matajiri hawapendei kuwa sawa namasikini. Kitu nilichowabadilishia ni rangi na uwezo wa kuweka oda kwanzia wiki mpaka mwezi.

 

Jina langu lilikuwa na bidhaa zangu ziliendwa. Sikumoja alikuja mteja wangu, ni yule binti niliyemuonaga. Binti hakufuata viatu ila alitaka kuweka oda ya viatu kwa mtindo autakao yeye. Alitaka viatu vpea tata. Pea moja iwe na umbo la kichwa cha mamba, pea moja iwe na picha ya kichwa cha kunguru na peya nyingine iwe na umbo la kichwa cha kambale. Moyo ulinidunda na kuchanganyikiwa kwa nini anaeleza sifa zinazohusiana na wageni wa ajabu. Wageni ninaowatafuta. Nikaamini kuwa makutano yangu na binti huyu hata si ya kawaida. Bila shaka kuna jambo.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1233


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

JARIBIO LA KWANZA LA ALADINI
Soma Zaidi...

Familia mpya baada ya harusi
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...

HADITHI YA MLEVI
Soma Zaidi...

hatima ya kinyozi
Soma Zaidi...

Kifo cha mtoa burudani wa sultani
Posti hii inakwenda kukusimulia kuhusu hadithi ya kifo cha mtoa burudani wa sultan Soma Zaidi...

Mrembo mtoto wa tajiri
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

HADITHI YA TUNDA EPO
Soma Zaidi...

Kukatwa mkono na kuurithi utajiri
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

Kwanini dirisha moja?
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...

HADITHI YA CHONGO WATATU WATOTO WA WAFALME
Soma Zaidi...

MSHENGA WA ALADINI MBELE YA MFALME
Soma Zaidi...

Hadithi ya mjakazi wa Mfalme
HADITHI ILIYOSIMULIWA NA MJAKAZI WA SULTANI Mtukufu sultani, nakwenda kukusimulia tukio lililotokea leo hii wakati tulipokuwa tunaburudika. Soma Zaidi...