KWA NINI DIRISHA MOJA?

KWA NINI DIRISHA MOJA?

KWA NINI DIRISHA MOJA?

Download Post hii hapa

KWA NINI DIRISHA MOJA?


KWA NINI DIRISHA MOJA?



Siku hiyo Aladini aliamka mapema, na kuelekea sehemu ya kuogea. Aliridhishwa vyema na usafi wa chooni na alivyovikuta. Alifanya usafi wa mwili wake, huku akimuacha binti Sultani akiwa bado amelala kwa uchovu wa pirikapirika za jana nzima. Baadaye binti mfalme aliamka na kufanya usafi kisha wote wakaelekea kupata kifungua kinywa. Wote walikuwa wamevaa pete sawa kwa rangi. Pete zilizokuwa za dhahabu huki vichwa vya pete vilikuwa ni almasi yenye kichwa cha yule ndege wao. Mama Aladini alipowaona watoto wake machozi ya furaha yalimtoka, hata akatamani mzee Mustapha angelikuwa hai siku kama ya leo.


Kama mfalme alivyoahidi, alifunga safara wake na matarumbeta yake kwenda nyumbani kwa Aladini. Walijipanga wananchi kwa kumuheshimu mfalme wao kila alipopita. Haukuchukuwa muda mrefu saana, hatimaye msafara ukawa nje ya jumba kubwala Aladini. Halikuwa ni umba la gorofa matarumbeta yote yalinyamaza punde sauti za kasuku zilipoanza kusiika. Sauti zilizidi uzuri wa matarumbeta. Mfalme alifurahi na kutabasamu. Sharubu za mfalme zilipepea vyema kwenye upepo mwanana mbele ya miti ya mauwa na matunda nyumbani kwa Aladini.


Macho ya mfalme yakaelekea kwenye ukuta wa jumba hili, na baada ya kujidhisha kwa uzuri ulioje ghafla mfalme akakaza macho a sura. Pale alipoona dirisha moja. Mfalme alimlaumu Aladini kwenye nafsi yake. Mfalme alimlaumu na kuwaza laiti kama angeliishiwa na pesa ya wajenzi ama vifaa angelinambia tu ningemtekelezea. Wakati haya yanaendelea kutokea Aladini, mkewe na Mama yake wakaja kuwapokea. Ilikuwa ni furaha juu ya furaha. Msafara ukaingia ndani na mjakazi mukuu akaendelea kupanga kila mtu kumpa majukumu yake. Kisha mfalme akaa kupata chakula. Na mazungumzo ya hapa na pale yakaanza.


Mfalme alionyesha kuridhika sana na ubora wa nyumba na wajenzi. Wakiwa wanazungumza hapa na pale binti mfalme alikuwa anahisi kitu kwa baba yake kana kwamba ana jambo anataka kulisema. Binti akaanza kumdadisi baba. Hatimaye mfalme akafunguka. โ€œbaba umejenga jumba zuri sana ila sikuridhishwa na dirishao majo., baba uliishiwa na wajenzi ama vifaaโ€? โ€œbaba nimewacha kusudi ili na wew utie baraka zako, umalizie dirisha lile iwe sifa kuwa hata mfalme amechangia katiaka ujenziโ€ ni majibu ya Aladini. Mfalme alifurai sana na kuona kumbe mkwe wake anampenda sana. Basi mfalme akaahidi kuanza kazi kesho kuleta wajenzi.


Mazungumzo yaliendelea na baadaye mama Aladini akajiunga na mazungumzo kisha Mama Aladini akaondoka na binti mfalme. Hapo mfalme akapata fursa ya kuwa pekee na mkwewe. Wakatoka nje na kuendelea kupata upepo na kuzungumza kwa undani. Walizungumza sana hata mfalme akazungumza ya moyoni kabisa kuwa anatarajia kupata mjukuu apema. Na oia Aladini ajiandae kuwa mfalme ajae pindi atakapo fariki. Basi ilkuwa ji furaha juu ya furaha. Ilipofika jioni Mfalme akarudi kwake ikulu. Waliangana kwa ucheshi sana hasa mama Aladini na Mfalme walikuwa kama dada na kaka sasa.


Baada ya mfalme kuondoka mama Aladini naye akaaga kuondoka kurudi kwake. Aladini ijapokuwa liamsihi sana mama yake waishi wote lakini mama alikataa. Watu wote walipondoka aladini alibaki yeye na mkewe na wafanyakazi. Aladini aliuweka mshumaa wake juu ya meza na kumwambia mkewe asijeutoa mshumaa ule. Lakini hakumwambia siri hasa ya mshumaa ule. Pia Aladini alikuwa navaa pete mbili moja ile ilofanana na mkewe na nyingine ni ile pete ya ajabu. Pia hakumwambia mkewe siri ya pete ile. Hata hivyo mkewe hakuonyehsa kutaka kujuwa chochote katika vitu hivi.


Siku ilofata mfalme alileta mafundi kujenga bila mafanikio. Hawakuwa na ujuzi hata hivyo hawakuwa na vifaa pia. Nchi nzima ilitafutwa madini yaliyoweza kurekebisha dirisha bila kupatikana. Hatimaye mfalme akakiri kushndwa kazi. Basi kwa Aladini haikuwa ni kazi kubwa. Ilikuwa ni kazi ya usiku mmoja chini ya nguvu ya jini wa mshumaa. Asubuhi dirisha lkawa safi. Basi maisha yaliendelea kwenda hatimaye miezi kadhaa ikapiata. Aladinia kawa anakwenda kuwinda na mkwewe kujifurahisha.


Maendeleo ya Aladini yaliweza kushangaza uma na hayakuweza kuridiwa na watu wote. Mmoja wapo alikuwa ni waziri mkuu. Ambaye mpaka sasa alipo hakujulikani. Ukweli ni kuwa baada ya tukio la ndoa ya Aladini waziri aliondoka kwenda kutafuta siri ya aladini. Waziri alifika mbali sana mpaka nchi za Afrika huko alikutana na mchawi mkubwa sana. Mchawi huyo ndiye aliyetoa siri nzima ya Aladini na maisha yake. Waziri mkuu alimpatia mchawi hongo kubwa sana ili ahakikishe kuwa Aladini anapotea, na anapata aibu kubwa na udhalili.

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Aliflela2 Main: Burudani File: Download PDF Views 755

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Madrasa kiganjani    ๐Ÿ‘‰2 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰3 Kitau cha Fiqh    ๐Ÿ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰5 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Jaribio la kwanza la aladini
Jaribio la kwanza la aladini

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu

Soma Zaidi...
Hadithi ya mjakazi wa Mfalme
Hadithi ya mjakazi wa Mfalme

HADITHI ILIYOSIMULIWA NA MJAKAZI WA SULTANI Mtukufu sultani, nakwenda kukusimulia tukio lililotokea leo hii wakati tulipokuwa tunaburudika.

Soma Zaidi...
Nani muuaji?
Nani muuaji?

Posti hii inakwenda kukusimulia kuhusu muuaji wa mtoa burudani wa sultan

Soma Zaidi...
Ndoa ya Siri yafanyika
Ndoa ya Siri yafanyika

Posti hii inakwenda kukuendelezea hadithi kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultan

Soma Zaidi...
Deni la mapenzi
Deni la mapenzi

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani

Soma Zaidi...
Siri ya kifo yafichuka
Siri ya kifo yafichuka

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi za alifu lela ulela

Soma Zaidi...