Siku ya sita ya wageni

Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani

SIKU YA SITA YA WAGENI

Siku ya sita walianza mapema kama siku ya nne kisha wakamueleza baba awapeleke msituni. Baba aliwapeleka msituni maeneo yenye tembo. Baba alikuwa na lengo lake, akiamini kuwa kama watauwa tembo atapewa kichwa hivyo atauza meno na kupata pesa nyingi sana. Lakini wale mabwana walisha tambua hili, mmoja wao akasema “wala usitende wema kwa kutarajia malipo kwa mema wako, bali taka malipo kwa Mwenyezi Mungu”. nafsi yangu ilinisuta sana ila sikujali sana nilitambua kuwa ni kawaida yao. Haya ni maneno aliyojisemea baba.

 

Basi baba akawapeleka kwenye msitu wenye tembo. Wale mabwana walikuwa wanatumia mikuki, michale na mmoja wao alikuwa na bunduki iliyotengenezwa India. Niliitambua kutokana na hati ya maandish yaliyoandikwa. Basi baba akawapeleka kwenye msitu wenye tembo na akawapeleka sehemu ambapo tembo huwa wanapenda kunywa maji. Wale watu wakakaa sawa kwa kujiandaa kuwinda, ngafla kundi la tembo likaja. Baba akaanza kufurahia moyoni akidhani sasa utajiri unafata. Kitu cha ajabu mmojawao akapiga bunduki juu ili kuwatisha tembo.

 

Wale tembo wakakimbia na kubakiwa vinyama vijidogo. Baba akapata hasira moyoni lakini mmoja wa wale watu akasema “wala usikodolee macho kitu kilichopo kwa mwenzio”. muda si mrefu mamba wakaanza kuja mmoja kati ya wale watu akachukuwa mkuki na kumnyatia mamba na akapiga kwa nguvu. Mamba alitapatapa sana lakini wakafanikiwa kumvua. Nilianza kuhoji maswali mengi hata nikadhani wanataka kula mamba. Haya ni maneno ambayo baba alikuwa akiwaza.

 

Wakamtoa mamba na kumuandaa vyema na kuotoa sumu yake na kuifukia. Walipomaliza wakamkata kichwa na kumpatia baba. Yule mzee sana akasema “mamba huyu amezoea kula kambare wakubwa wanaojificha kwenye matope. Kihifadhi kichwa hiki mpaka siku ya miadi”. baba anasema niliwaacha kulekule baada ya kuniambia kuwa njia wanaijuwa hivyo watarudi wenyewe. Baba hakujuwa yule mamba wamemfanya nini alipokuja kichwa chake akakiweka tena sehemu nzuri. Wageni wetu tuliwasubiri hata ikafika usiku wa manane bila kutokea.

 

Baba akaamuwa aende kuwafatilia huenda wamepotea. Aliwakuta palepale alipowaacha, na walipomuona walimshukuru sana na kumuombea dua kwa ukarimu wake na kwa kujali kwake wageni. Wageni wakamweleze kuwa watalala pale asubuhi ndio wataonana. Basi baba akarudi na ilipofika subuhi wageni wakamwita baba uwani kwetu na kumwambia ahakikishe milango amefunga na hakuna mtu atakayesikiliza mazungumzo yao.

 

Baba ananieleza kuwa wakamwambia alete vichwa vile vitatu na kuviweka mbele yao. Wakakipasua kichwa cha kambale na kukuta alimeza dini la dhahamu kubwa. Kumbe madini yalikuwa yakihuka kwenye yale maporomoko ya maji na kwa kuwa makambale wanajitafutia chakula kwenye matope kwa bahati mbaya kambale yule alimeza dini nile na likamkwama kwenye kichwa chake. Baba akaambiwa auze dini lile na ndio zawadi yeke.

 

Walachukuwa kichwa cha kunguru na kukipasua wakatoa mkufu wa dhahabu. Wakamwambia auze mkufu ule baada ya mwaka mmoja. Maana mkufu ule ulikuwa ni mali ya msafiri mmoja ambaye alishawahi kusaidia na baba. Na mkufu ule aliusahau sehemu ambayo alilala siku moja baada ya kuondoka nyumbani. Kunguru yule aliubeba mkufu ule na ukamkwama kwenye koo lake. Wakamwambia kama baada ya mwaka hajatokea mwenyewe uza na utumie thamani yake.

 

Wakachukuwa kichwa cha mamba na kukipasua wakakuta kuna matope mengi sana.katika matope yale kulikuwa na madini ya dhahabu kadhaa. Wakamkabidhi tena baba na kumwambia hii ndio zawadi yako kwetu. Kishha wageni wakakusanya kila kilichochao na kuendelea na safari yao. Hatukupatapo kujuwa hata majina yao, wapi wametoka na wapi wanakwenda. Baada ya muda wa mwaka baba aliuza mali zile na hapo ndipo utajiri wetu ulipoanzia.

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2021-11-07     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 735

Post zifazofanana:-

Funga za Sunnah na umuhimu wake
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mlo kwa wagonjwa wa figo wanaochujwa damu
Posti hii inahusu zaidi mlo kwa wagonjwa wa figo wanaochujwa damu, ni wagonjwa ambao figo zao zimeharibika na zimeshindwa kufanya kazi au pengine kuna uchafu mwingi mwilini ambao uchujwa kwa hiyo kuna vyakula muhimu ambavyo wagonjwa wa figo wanapaswa kutu Soma Zaidi...

Mafunzo yatokanayo na maandalizi ya mtume ki-wahay
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Nini chanzo cha tatizo la computer au simu yako
Posti hii inakwenda kukupa elimu kuhusu chanzo cha tatizo la computer au simu yako Soma Zaidi...

Mafidodo (mafindofindo) au tonsils kweye koo je inaweza ikawa Ni moja kati ya dalil za ukimwi
Tezi za lymph huanza kuonyesha dalili za kuwa mwili upo katika mapambano dhidi ya vijidudu vya maradhi. Ishara ni pale utakapoona tezi za lymph zina maumivu. Tezi hizi hupatikana kwenye mapaja, kwapa nashingo. Soma Zaidi...

Dalili zinazonesha kuungua kwa Mdomo (burning mouth)
Ugonjwa wa mdomo unaoungua'ni neno la kimatibabu kwa ajili ya kuungua kinywani kwa mara kwa mara (kwa muda mrefu) bila sababu dhahiri. Usumbufu huo unaweza kuathiri ulimi wako, ufizi, midomo, ndani ya mashavu yako, paa la mdomo wako au maeneo yaliyoenea Soma Zaidi...

Uvimbe wa mishipa midogo ya Damu kwenye ngozi
Posti hii inazungumzia kuhusiana na uvimbe wenye uchungu wa mishipa midogo ya damu kwenye ngozi yako ambayo hutokea kutokana na ongezeko la joto la ghafla kutokana na halijoto ya baridi. Pia inajulikana kama pernio, chilblain inaweza kusababisha kuwasha, Soma Zaidi...

Uandishi wa hadithi wakati wa tabiina (wafuasi wa maswahaba)
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Vitu vinavyochochea kuwepo kwa Ugonjwa wa ukimwi.
Posti hii inahusu zaidi vitu ambavyo vinasababisha kuongezeka kwa Ukimwi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na baada ya watu kujua Ugonjwa huu na matokeo ila bado ugonjwa unazidi kuongezeka. Soma Zaidi...

Dalili za maambukizi kwenye figo
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Maambukizi kwenye figo (pyelonephritis) ni aina mahususi ya maambukizi ya njia ya mkojo (UTI) ambayo kwa kawaida huanza kwenye urethra au kibofu chako na kusafiri hadi kwenye figo zako. Soma Zaidi...

Njia za kuondokana na fangasi
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuweza kupambana na fangasi za ukeni ili kuweza kujiepusha na madhara mbalimbali kwenye maisha ambayo ni pamoja na ugumba na Maambukizi kwenye via vya uzazi. Soma Zaidi...

Huduma kwa mtoto mdogo anayeumwa
Mtoto mdogo ni mtoto chini ya miaka mitano, yaan kuanzia pale anapozaliwa mpaka anapafikisha miaka mitano Soma Zaidi...