Harusi ya aladini na binti sultani


image


Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu


HARUSI YA ALADINI NA BINTI SULTANI

Basi mambo yakawa kama hivyo kila mmoja alikuwa akiiwaza siku ya harusi, huku mfalme akiwaza nikitu gani kingine cha kushangaza atakileta Aladini. Mama aladini aliendelea kuwaza ni uzuri gani wa nyumba atakayojenga Aladini. Binti mfalme ndio hakuweza kulala kabisa kwa furaha aliyo nayo. Alitamani a,ualike Aladini kuja kufurahi lakini isingekuwa ni maadini mema kwa mujibu wa dini. Binti hakuwa na mawazo mengi juu ya maendeleo alichowaza ni afanye nini ili Aladini aweze kumpenda zaidi. Waziri akiwa na msimamo tofauti wa wengine yeye aliwaza mbinu ya kuweza kusitisha harusi. Loo! Aladini alielekea kwenye pango ili aweze kuona kama kuna chochote ataweza kufikiri.

 

Aladini hakuwa na nguvu za kuingia kwenye Pango na wala pia hakutaka kugundua zaidi kama pete aliyonayo inamuingiza ndani. Alichofanya yeye ni kukaa pale nje ya lile pango huku akiwaza mambo mablimbali. Katika mawazo Aladini aliona kama mbele yake kuna uwanja mji mzima upo mbele yake. Maeneo yote ya mjini yalikuwa mbele yake na aliweza kuyatambuwa kwa majina. Katika maono hayo Aladini alianza kuangalia maeneo mazur ya kuweka nyumba yake. Hatimaye maeneo matatu yalikuwa ni machaguzi. Katika maono hayo pia Aladini akaona ikulu mbalimbali zimewekwa mbele yake, naye akaanza kuangalia moja baada ya nyingine.

 

Aladini akiwa katika hali hiyo aliona vitanda, mabostani na thamani za ndani mbalimbali mbele yake. Aladini akaanza kuchaguwa bostani zuri, na thamani anazoona zinafaha zaidi kuwa kwake. Aladini pia akiwa katika hali hiyoa liona aina mbalimbali za mavazi na akaanza kuchaguwa mavazi kwa ajili yake, mkewe, mfalme na mama yake. Aladini aliendelea kuona vitu baada ya vitu hatimaye akasituka, kumbe alikuwa katika mawazo makubwa sana. Mawazo ambayo yalimjengea taswira ya vitu alivyovijitaji. Aladini aliamini huenda hayakuwa ni mawazo ama ndoto ila ni maono. Baada ya muda Aladini akaondoka na kuelekea nyumbani.

 

Ilipofika usiku Aladini akamuita jini wa mshumaa na kumueleza atekeleze kila ambacho alichaguwa kwenye maono yale aliyoona aiwa kule mapangoni. Ila akampa sharti ya kuwa asigunduwe mtu yeyote mjini, yaani afanye siri. Jini liliahidi kutekeleza ndani ya masiku matatu. Basi siku zikazidi kuendelea kwenda kwa upole sana kwa upande wa Aladini na binti mfalme. Mama Aladini aliona siku zinakwenda kwa kasi sana. Hatimaye siku tatu za jini kukamilisha mipango zikawadia. Aladini akaenda kuhakikisha kila kitu na akajiridhisha kwa ubora wa hali yajuu. Aladini akaagiza dirisha moja la nyumba liboolewe na libakie kama halukukamilikaa wakati wa ujenzzi.

Hatimaye alhamisi ikawadia Aladini akamuagiza jini wa mshumaa amletee baadhi ya mavazi na akamuagiza vitu vingine. Loo! Iku ya ujumaa ikaungia na muda wa harusi ukawadia. Aladini kavaa mavazi ya harusi na kuongozana na mama yke pamoja na kundi la vijana wa mtaani. Aladini akiwa amepanda farasi wa rangi nyeupe. Viatu vya farasi vilikuwa vya dhahabu vilivyowekwa malalio ya hariri laini. Kiti cha farasi kilikuwa na godoro laini la hariri, na kuwekwa vishikizo vilivyoonekana kupendeza sana kwa rangi. Kamba ya farasi ilikuwa imesokotwa vyema na kuchovywa kwenye mafuta ya miski nyekundu. Kamba ilinukia na kupendeza.

 

Aladini alivaa joho lenye ukosi uliochovywa kwnye rangi ya dhahabu na kutengeneza ukosi mgumu wa kupendeza. Michirizi ya rangi ya dhahabu ilionekana kushuka mkabala na mashepele mawili ya joho. Aladini alionekana kijana mtanashati sana siku hiyo tofauti na mazoea. Viatu alivyovaa Aladini vilikuwa na sura ya ndege kwa mbele. Huwenda alitaka kumkumbusha binti mfalme kuwa bado anaikumbuka ile siku waliokutana. Kwa hakika Aladini alipendeza sana, kofia aliyoivaa utadhani ilikuwa ni kipande cha lulu kilichowekwa kichwani mwa Aladini. Hakuwa na nywele ndevu ila zilioneana zimetengenezwa vyema na kinyozi maridadi. Aladini alitembe kwa mwendo wa furaha sana na kutabasamu kama vile anaramba asali.

 

Ugeni ukafika kwa mfalme na vijana wa mtaani wakawekwa chumba maalumu na kusubiria mari ya kuanza kula. Aladini mbele ya mfalme alipata nafasi ya kusalimiana na mfalme akiwa kama baba mkwe, salamu ya kukumbatiana. Aliwasili sheh mkubwa aliyevaa mavazi yaliyovutia sana. Ndoa ikafungwa na vifijo, nderemo na shangwe zilienea ikulu nzima. Aladini alipelekwa kwa mkewe chumba ambacho aliingizwa mama Aladini siku ile. Hakukuwa na mabadiliko sana kutokakana na maelezo ya mama. Kwa mara ya kwanza Aladini anaukamata mkono wa binti mfalme na kuomba dua kubwa.

 

Vijana wa mtaani walikula vyakula vya thamani sana wakasshiba na kusaza. Mtoto wa waziri akuweza kuhudhuri harusi hio,na hata baba yeke. Mfalme aligundua na hakuwa na kinyongo. Aladini aliendelea kufurahia siku ya kwanza ya harusi. Aladini aliishi ndani ya ikulu kwa muda wa siku tatu akifurahi yeye na binti mfalme. Mama Aladini alipata nafasi ya kumuona malkia na kuongea naye sana. Urafiki kati ya mfalme na mama aladini ulianza kukuwa kwa kasi. Huwenda ni kwa sababu mfalme alikuwa na sehemu pekee kwa ajili ya mama Aladini toka mwanzo, ila Aladini aliharibu mipango.

 

Baada ya siku tatau kuisha mfalme alishangaa kuona mjengo mrefu sana kaskazini mwa ikulu yake. Mfalme alishangaa sana ni lini mjengo ule umejengwa na ni nanai amethubutu kujenga mjengo ule. Mgalme akwa katika mawazo hayo alishtuliwa na salamu ya Aladini akiwa na mkewake. Aladini akamjulisha Mfalme kuwa nahitaji kuzungumza naye. Katika mazungumzo hayo Aladini alitaa kuhusu mjengo uleulio mbele ya macho ya mfalme. Aladini alitaka mfalme pamoja na binti yake wafahamu zaidi kuhusu mjengo ule.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    2 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    3 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    4 Download App zetu hapa ujifunze zaidi    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Mtoto wa tajiri na mtoto wa maskini ( sehemu ya nne)
Post hii inahusu zaidi watoto Hawa wawili wakiwa kwenye kituo cha mapumziko ambapo mtoto wa tajiri anabugia soda aliyopewa na yule mwalimu pia tumbo linaanza tena na anaanza kuendesha Soma Zaidi...

image Kuingia kwa wageni
Posti hii inakwenda kukuletea hadithi za alifu lela ulela Soma Zaidi...

image USALITI (sehemu ya pili)
Post hii ni mwendelzo wa hadithi ya Usaliti kati ya Rhoda na Moses ambapo Moses anampenda sana Rhoda na wakati wa kuoa umefika ila akagikilia kwamba akimuoa Rhoda inawezekana wasipate watoto kwa sababu ya mimba ambazo Rhoda alikuwa anatoa mara kwa mara. Soma Zaidi...

image Ndani ya jumba la aladini
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa hadithi ya aladini na taa ya ajabu Soma Zaidi...

image Hasara za wivu na kutokuwa wazi (sehemu ya 4)
Posti hii inaendelea kuelezea hasara za kuwepo kwa wivu na kutokuwa wazi katika, jamii inafikia wakati baba anapifahamu ukweli anawaita wazazi wawili na kuwaombeza kwa kuwa kimya baada ya kuona matatizo yaliyokuwa yanampata mtoto Lisa. Soma Zaidi...

image Kifo cha mtoa burudani wa sultani
Posti hii inakwenda kukusimulia kuhusu hadithi ya kifo cha mtoa burudani wa sultan Soma Zaidi...

image Viatu vya ajabu vyaondoka na mkono wangu
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo kuhusu kifo cha mtoa burudani wa sultani Soma Zaidi...

image Mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya Binti mfalme, baada ya kijana wa kiume wa binti mfalme kuoa yule ndugu yake baba anafanya sherehe kubwa na wake wenza wamepata habari kwamba kijana wa kiume wa mfalme ameoa ndugu yake wakaamuru kunyamaza ili waje watoe siri siku ya kuapishwa kwa mfalme. Soma Zaidi...

image Safari ya tano ya Sinbad
Posti hii inakwenda kukupa muendelezo wa safari saba za Sinbad Soma Zaidi...

image Mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili
Posti hii inahusu zaidi mwendelezo wa hadithi ya vijana wawili, hapa tunaona Jackie anajibu barua ya Julius kwa kusema yafuatayo. Soma Zaidi...