Qur-an inavyogawa MirathiMgawanyo wa mirathi umebainishwa katika Qur-an kama ifuatavyo:Mwenyezi Mungu anakuusieni juu ya watoto wenu: Mwanamume apate sawa na sehemu ya wanawake wawili.
Qur-an inavyogawa Mirathi
Mgawanyo wa mirathi umebainishwa katika Qur-an kama ifuatavyo:Mwenyezi Mungu anakuusieni juu ya watoto wenu: Mwanamume apate sawa na sehemu ya wanawake wawili. Na ikiwa wanawake ni (wawili au) zaidi ya wawili, basi watapata thuluthi mbili (2/3) ya mali aliyoiacha (maiti,).
Lakini akiwa mtoto mwanamke ni mmoja, basi apewe nusu. Na wazazi wake wawili kila mmoja wao apate sudusi (1/6)ya mali aliyoiacha (maiti), akiwa maiti huyo (anaye mtoto au mjukuu). Lakini kama hana mtoto, na wazazi wake wawili wamekuwa ndio warithi wake basi mama yake atapata (1/3,)(na baba) thuluthi mbili (2/3,). Na kama (huyo maiti) anaye ndugu basi mama yake atapatya sudusi moja (1/6). Na huku kurithi kunakuwa baada ya kutoa aliyoyausia au kulipa deni. Baba zenu na watoto wenu, nyingi hamjui ni nani miongoni mwao aliye karibu zaidi kukunufaisheni. Hiyo ni sheria iliotoka kwa Mwenyezi Mungu. Bila shaka Mwenyezi Mungu ni mjuzi mwenye hikima. (4:11)
Na nyinyi mtapata nusu (1/2) ya (mali) walizoacha wake zenu, kama wao hawana watoto (wala wajukuu). Na ikiwa wana mtoto (au mjukuu), nyinyi mtapata robo (1/4) ya
walivyoviacha, baada ya kutoa walivyousia au kulipa deni. Nao (wake zenu watapata robo ya mlivyoviacha, ikiwa hamna mtoto (wala mjukuu) basi wao (hao wanawake) watapata thumni (1/s) ya vile mlivyoviacha, baada ya kutoa mlivyousia au kulipa deni. Na kama mwanamume au mwanamke ni mkiwa - hana mtoto (wala mjukuu) wala wazazi, lakini anaye kaka *('wa kwa mama) au dada (wa kwa mama pia), basi kila mmoja katika hawa atapata sudusi (sehemu ya sita). Na wakiwa zaidi kuliko hivyo basi watashirikiana katika thuluthi baada ya kutoa vilivyousiwa au kulipa deni, pasipo kuleta dhara. (Huu) ndio wasia uliotoka kwa Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi (na) Mwenye Upole. (4:12)
Wanakuuliza sema: 'Mwenyezi Mungu anakupeni hukumu juu ya mkiwa. Kama mtu amekufa, hali hana mtoto, lakini anaye dada; basi atapata (huyo dada) nusu ya yale aliyoyaacha (maiti). Na yeye (mtu huyu) atamrithi (dada yake) ikiwa hana mwana. Na kama wao ni (madada) wawili, basi watapata thuluthi mbili za yale aliyoyaacha. Na wakiwa ndugu wanaume na wanawake, basi (kila) mwanamume (mmoja) atapata sehemu iliyo sawa na ya wanawake wawili. Mwenyezi Mungu anakubainishieni iii msipotee; na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu. (4:176)
Kama ilivyosisitizwa mwishoni mwa aya hizi, huu ndio mgawanyo wa mirathi aliouweka AIah (s.w) na kugawanya mirathi kwa kufuata sheria ya kimila, sheria ya Bunge au sheria nyingine yoyote ya kitwaghuuti, ni kuchupa mipaka ya Mwenyezi Mungu. Allah (s.w) anasisitiza kufuatwa kwa sheria hii katika aya mbili zinazofuatia hizi:
Katika aya hizi zinazobainisha mgawanyo wa mirathi (4:11-12), (4:176) tunajifunza kuwa watoto wa kiume/wanaume wanapata mara mbili ya watoto wa kike/wanawake na baba anapata mara mbili zaidi kuliko mama. Je, sheria ya Allah (s.w) inapendelea wengine na kuwadhulumu wengine haki zao? Allah (s.w) ni Mkwasi, Mwenye kujitosheleza asiyehitajia chochote kutoka kwa viumbe vyake, bali viumbe ndio wanaomuhitajia. Pia Allah (s.w) ni Muadilifu na mpole mno kwa viumbe vyake. Hivyo, Allah (s.w) ametakasika na kila sifa mbaya na kila sifa za upungufu kama vile kupendelea au kudhulumu baadhi ya viumbe vyake. Kwa vyovyote vile, mgawanyo huu wa Allah (s.w) ni mgawanyo unaotoa haki kwa kila mrithi kwani ni mgawanyo wa mjuzi, mwenye hikima na mpole kwa viumbe vyake. Mwenyezi Allah (s.w) amemalizia aya hizi kwa msitizo:
"...Bila shaka Mwenyezi Mungu ni mjuzi na mwenye hi/dma." (4:11).
Huu ndio usia uliotoka kwa Mwenyezi Mungu na Mwenyezi Mungu ni mjuzi na mpole. ". (4:12).
"... Mwenyezi Mungu anakubainishieni iii msipotee; na Mwenyezi Mungu ni mjuzi wa kila kitu." (4:176).
Kwa kuzingatia majukumu ya wanaume na wanawake katika familia, kuna hekima kubwa ya kumzidishia mwanamume mara mbili ya kile anachopata mwanamke katika mafungu ya mirathi. Mwanamke amepunguziwa fungu kwa kuwa hana matumizi ya kumlazimu kama alivyo mwanamume. Halazimiki kwa matumizi ya watoto wake, na kazi yake na hata matumizi yake binafsi.
Bali matumizi yote hayo huwa juu ya mwanamume. Kwa mfano, iwapo urithi ulioachwa na baba mzazi kwa mtoto wake wa kike na wa kiume ni shilingi 3,000,0001=, kulingana na mgawanyo wa Qur-an mtoto wa kiume atapata shilingi 2,000,000/= na mtoto wa kike atapata shilingi 1,000,000.
Utakuta zile za kijana mwanamume zitakwisha kwa matumizi mbali mbali yanayomlazimu ikiwa ni pamoja na matumizi ya huyo dada yake ambaye licha ya kutowajibika kutoa matumizi kwa yeyote yeye mwenyewe anabakia kutunzwa na kulelewa na kaka yake na yuko huru kutumia urithi wake huo hata kwa kununulia mapambo ya dhahabu.
Mwanamume amezidishiwa fungu kwa sababu matumizi yake yanayomlazimu kisheria ni mengi. Ndiye mwenye jukumu Ia kugharamia gharama zote za maisha kwa mke wake/wake zake na watoto wake, wazazi wake na wale wote wanaomtegemea katika familia.
Bila shaka, wale wanaoishutumu sheria hii ya mirathi kuwa inawakandamiza wanawake, hawajaiona hekima hii au wamepata mwanya wa kuwaghilibu watu waone sheria zilizotungwa na mwanaadamu ndizo bora kuliko sheria ya Allah (s.w). Allah (s.w) anatutanabahisha:
Je, wao wanataka hukumu za kijahili? Na nani aliye mwema zaidi katika hukumu kuliko Mwenyezi Mungu, kwa watu wenye yakini? (5:50).
Aya tulizozirejea (4:11-12) na (4:176) zimetaja kwa uwazi na kwa ukamilifu watu wenye kurithi na mafungu yanayorithiwa.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Quran Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 1053
Sponsored links
👉1
Kitau cha Fiqh
👉2
Simulizi za Hadithi Audio
👉3
Kitabu cha Afya
👉4
kitabu cha Simulizi
👉5
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉6
Madrasa kiganjani
Kitabu Cha Darsa za Quran
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...
Sababu za kushuka surat Al-Kawthar
Sura hii ni miongoni mwa Sura fupi sanya huwenda ndiosura yenye aya chache kuliko sura zote katika Quran. Soma Zaidi...
Fadhila za surat al-fatiha na sababu za kushuka kwake
1. Soma Zaidi...
Sababu za kushukasurat an Nasr
Sura hii ni katika sura za mwisho kushuka, huwendakuwa ndio ya mwisho kabisa. Masahaba waliamini kuwa sura hii imetabiri kifo cha Mtume S.A.W Soma Zaidi...
fadhila za sura kwenye quran
FADHILA ZA BAADHI YA SURA Umuhimu na ubora wa baadhi ya sura na aya. Soma Zaidi...
quran na sayansi
2; mbegu ya uhai uliyo changanyikaUmbile la mwanadamu limepitia hatua nyingi sana kama tutakavyoendelea mbele kuonalakini ukiachilia mbali na hatua zote alizopitia mwanadamu wakati wa kuumbwa lakiniumbile la mwanadamu bado limebakia kuwa dhalili kama ALLA Soma Zaidi...
Historia ya kushuka kwa quran
Soma Zaidi...
Kukusanywa na kuhifadhiwa kwa quran
Quran (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
surat al mauun
SURATUL-MAM’UUN Imeteremshwa Maka, anasimulia Ibn Jurayj kuwa Abuu Sufyan ibn Harb alikuwa na kawaida ya kuchinja ngamia wawili kila wiki, hivyo siku moja yatima mmoja alikuja kwake na kumlilia shida, na hakumsaidia kwa chochote na hatimaye akampiga yat.. Soma Zaidi...
Muhammad hakufundishwa quran na padri Bahira
Soma Zaidi...