Ujuwe mlo sahihi kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo
Post hii itakwenda kuangalia mlo sahihi wa mwenye vidonda vya tumbo. Hata utajifunza ni vyakula vipi hapaswi kula na vipi ana paswa kula.
VYAKULA VYA KUVIEPUKA KWA MGONJWA WA VIDONDA VYA TUMBO
Vidonda vya tumbo ni nini?
Vidonda vya tumbo ni aina za vidonda ambavyo hutokea kwenye mfumo wa mmeng’enyo wa chakula. Vidonda vivi vinaweza kutokea kwenye tumbo ama utumbo. Hata hivyo koo la chakula linaweza kuathirika kupata vidonda, jambo hatuviiti vidonda vya tumbo. Vidonda vya tumbo vinaweza kuleta maumivu makali sana ya tumbo na mara nyingi hutokea wakati mtu ana njaa.
Nini husababisha vidonda vya tumbo?
Sababu kuu ya kutokea kwa vidonda vya tumbo ni mashambulizi ya bakteria wanaojulikana kama Helicobacter pylor (H.pylor). bakteria hawa wanaishi kwenye tumbo. Mtu anaweza kuishi na bakteria hawa kwa miaka kwa miaka mingi bila ya kusabbabisha madhara yeyote yale. Lakini si mara zote, bakteria hawa wanaweza kusababisha kuvimba (inflamation) kwenye kuta za tumbo, na kupelekea kutokea kwa michubuko na hatimaye vidonda vya tumbo. Vingine vinavyosababisha vidonda vya tumbo ni kama:-
- Misongo ya mawazo
- Ongezeko la uzalishwaji wa tindikali tumboni
- Matumizi mabaya ya dawa
- Saratani ya tumbo
Dalili za vidonda vya tumbo
Maumivu ya vidonda vya tumbo ni makali, pia mgonjwa wa vidonda vya tumbo anaweza kupatwa na changamoto nyingine ambazo ni katika dalili za vidonda vya tumbo. Kwa mfano kutapika, kiungulia cha mara kwa mara, tumbo kujaa gesi, maumivu ya kifua, kupungua kwa damu na uzito. Endapo vidonda vya tumbo vitadumu kwa muda mrefu bila ya kupatiwa matibabu afya ya mgonjwa inaweza kuwa mbaya ijapokuwa vidonda vya tumbo havisababishi kifo.
Vipi nitatuliza maumivu?
Unaweza kutuliza maumivu ya vidonda vya tumbo kwa kutumia dawa za hospitali. Pia kwa kutumia dawa za kienyeji pia. Lakini unaweza kutuliza maumivu haya kwa kutumia vyakula. Wapo baadhi ya wagonjwa wa vidonda vya tumbo hutumia baadhi ya vyakula kutuliza maumivu. Mfano wa vyakula hivyo ni maziwa. Endelea na makala hii hapo chini utajifunza vyakula hivi vilivyo vizuri kwa vidonda vya tumbo.
Nini husabaabisha maumivu?
Maumivu ya vidonda vya tumbo pia yanaweza kusababishwa na matumizi ya madawa na vyakula ama vinywaji fulani. Pia kukaa kwa njaa kwa muda mrefu kunaweza kuleta maumivu kwa mgonjwa. Hutokea pia misongo ya mawazo ikawa pia ni vichochezi vya maumivu haya. Huenda mgonjwa anatumia hivi bila ya yeye kujua ama anatumia kwa sababu hana namna nyingine ya kufanya. Kwa mfano ijapokuwa maziwa hutuliza maumivu lakini kitaalamu sio mazuri sana kwa mgonjwa. Endelea na makala hii hapo chini utajifunza vyakula hatari kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo.
Vyakula anavyopasa kula mgonjwa wa vidonda vya tumbo.
Ni ngumu sana hapa kuanza kukuorodheshea orodha ya vyakula vyote anavyotakiwa kula mgonjwa wa vidonda vya tumbo. Hata hivyo kila jamii ina aina ya vyakula vyao ambavyo ni ngumu kujulikana kwa watu wa jamii nyingine. Hapa nitakuletea tu kanuni ambazo utaziangatia pindi unapochaguwa chakula kwa ajili ya kutumiwa na mgonjwa wa vidonda vya tumbo. Angalia vyakula vyenye sifa hizi:-
- Vyakula ambavyo havina gesi
- Vyakula ambavyo havina uchachu sana
- Vyakula ambavyo havina chumvi nyingi sana
- Vyakula ambavyo havina mafuta mengi
- Pia vyema ukatumia na vyakula vifuatavyo kwa namna ambayo unaona itafaa kwa upande wako:-
- kabichi
- matunda aina ya maepo
- karoti
- mboga za majani za kijani
- asali
- kitunguu thaumu
Vyakula hatari kwa vidonda vya tumbo:
Kama nilivyokueleza hapo juu kuhusu kanuni za kuzishikili unapochaguwa vyakula basi hapa pia utaendelea na kanuni zile zile pindi unapotaka kuepuka vyakula ukiwa kama mgonjwa wa vidonda vya tumbo. Epuka vyakula hivi:-
- vyenye gesi kama maharagwe
- vyenye uchachu sana
- vyenye pilipili kwa wingi
- vyenye mafuta mengi
- vyenye chumvi nyingi
Pia punguza matumizi ya vifuatavyo ama wacha kabisa iwezekanapo:-
- sigara
- pombe
- kahawa
- maziwa unaweza kupunguza tu matumizi
- pilipili kwa wingi
Vipi nitajilinda na vidonda vya tumbo?
Ni ngumu sana kwa sababu mpaka leo bado haijajulikana sababu ya kupata bakteria wa vidonda vya tumbo. Hivyo kujikinga na vidonda vya tumbo vinavyosababishwa na mashambulizi ya bakteria ni ngumu. Ila kwa kuwa sababu za kutokea kwa vidonda vya tumbo ni nyingi, unaweza kujikinga na vidonda vya tumbo vinavyosababishwa na sababu nyingine. Njkia hizo ni kama:-
- Punguza misongo ya mawazo
- Wacha ama punguza kutumia kilevi
- Punguza ama wacha kabisa kuvuta sigara
- Wacha kutumia dawa kiholela
Je vidonda vya tumbo vinaweza kupona kabisa?
Tambuwa kuwa vidonda vya tumbo vinatibika bila ya wasi wowote ule. Unaweza kutibiwa na ukapona kabisa. Hakuna muda maalumu wa kupona lakini haiwezi kumaliza miezi hata sita utapona kabisa. Tukutane makala inayofata ttakapojifunza kuhusu matibabu na dawa za vidonda vya tumbo.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π2 Kitau cha Fiqh π3 Kitabu cha Afya π4 Dua za Mitume na Manabii π5 Madrasa kiganjani π6 ai web app
Post zinazofanana:
Madhara ya Tiba homoni kwa wagonjwa wa saratani
Posti hii inahusu zaidi madhara ya Tiba homoni, ni madhara- ambayo utokea kwa mgonjwa anayetumia homoni kama Tiba kwenye kutibu saratani.
Soma Zaidi...Vyakula vinavyosaidia afya ya mwanaume
Afya ya mwanaume inahitaji muundo wa kipekee wa virutubisho ili kulinda moyo, kuongeza nguvu za mwili, kusawazisha homoni ya testosterone, na kuzuia matatizo ya tezi dume (prostate). Makala haya yanachambua vyakula vikuu vyenye uwezo wa kuimarisha afya ya wanaume, jinsi vinavyofanya kazi, na kuondoa dhana potofu zilizopo mitaani kuhusu vyakula vya kuongeza nguvu za kiume. βUtangulizi
Soma Zaidi...Kupambana na kisukari
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kupambana na kisukari
Soma Zaidi...Madhara ya kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu
Post hii inahusu Zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea Kwa mgonjwa mweye usaha kwenye mapafu.
Soma Zaidi...Dalili za ugonjwa wa Saratani.
Saratani inahusu ugonjwa wowote kati ya idadi kubwa ya magonjwa ambayo yanaonyeshwa na ukuaji wa seli zisizo za kawaida ambazo hugawanyika bila kudhibitiwa na kuwa na uwezo wa kupenya na kuharibu tishu za kawaida za mwili. Saratani mara nyingi ina uwezo
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu Ugonjwa wa pre - eclampsia
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa pre- eclampsia ni Ugonjwa ambao uwapata wanawake wajawazito uwapata pale mimba inapofikisha umri wa wiki ishilini, utokea pale ambapo Mama mjamzito huwa na kiwango kikubwa cha shinikizo la damu na pia kuwepo kwa protini
Soma Zaidi...