image

Ujuwe mlo sahihi kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo

Post hii itakwenda kuangalia mlo sahihi wa mwenye vidonda vya tumbo. Hata utajifunza ni vyakula vipi hapaswi kula na vipi ana paswa kula.

VYAKULA VYA KUVIEPUKA KWA MGONJWA WA VIDONDA VYA TUMBO

Vidonda vya tumbo ni nini?

Vidonda vya tumbo ni aina za vidonda ambavyo hutokea kwenye mfumo wa mmeng’enyo wa chakula. Vidonda vivi vinaweza kutokea kwenye tumbo ama utumbo. Hata hivyo koo la chakula linaweza kuathirika kupata vidonda, jambo hatuviiti vidonda vya tumbo. Vidonda vya tumbo vinaweza kuleta maumivu makali sana ya tumbo na mara nyingi hutokea wakati mtu ana njaa.

 

Nini husababisha vidonda vya tumbo?

Sababu kuu ya kutokea kwa vidonda vya tumbo ni mashambulizi ya bakteria wanaojulikana kama Helicobacter pylor (H.pylor). bakteria hawa wanaishi kwenye tumbo. Mtu anaweza kuishi na bakteria hawa kwa miaka kwa miaka mingi bila ya kusabbabisha madhara yeyote yale. Lakini si mara zote, bakteria hawa wanaweza kusababisha kuvimba (inflamation) kwenye kuta za tumbo, na kupelekea kutokea kwa michubuko na hatimaye vidonda vya tumbo. Vingine vinavyosababisha vidonda vya tumbo ni kama:-

  1. Misongo ya mawazo
  2. Ongezeko la uzalishwaji wa tindikali tumboni
  3. Matumizi mabaya ya dawa
  4. Saratani ya tumbo

 

Dalili za vidonda vya tumbo

Maumivu ya vidonda vya tumbo ni makali, pia mgonjwa wa vidonda vya tumbo anaweza kupatwa na changamoto nyingine ambazo ni katika dalili za vidonda vya tumbo. Kwa mfano kutapika, kiungulia cha mara kwa mara, tumbo kujaa gesi, maumivu ya kifua, kupungua kwa damu na uzito. Endapo vidonda vya tumbo vitadumu kwa muda mrefu bila ya kupatiwa matibabu afya ya mgonjwa inaweza kuwa mbaya ijapokuwa vidonda vya tumbo havisababishi kifo.

 

Vipi nitatuliza maumivu?

Unaweza kutuliza maumivu ya vidonda vya tumbo kwa kutumia dawa za hospitali. Pia kwa kutumia dawa za kienyeji pia. Lakini unaweza kutuliza maumivu haya kwa kutumia vyakula. Wapo baadhi ya wagonjwa wa vidonda vya tumbo hutumia baadhi ya vyakula kutuliza maumivu. Mfano wa vyakula hivyo ni maziwa. Endelea na makala hii hapo chini utajifunza vyakula hivi vilivyo vizuri kwa vidonda vya tumbo.

 

 

 

Nini husabaabisha maumivu?

Maumivu ya vidonda vya tumbo pia yanaweza kusababishwa na matumizi ya madawa na vyakula ama vinywaji fulani. Pia kukaa kwa njaa kwa muda mrefu kunaweza kuleta maumivu kwa mgonjwa. Hutokea pia misongo ya mawazo ikawa pia ni vichochezi vya maumivu haya. Huenda mgonjwa anatumia hivi bila ya yeye kujua ama anatumia kwa sababu hana namna nyingine ya kufanya. Kwa mfano ijapokuwa maziwa hutuliza maumivu lakini kitaalamu sio mazuri sana kwa mgonjwa. Endelea na makala hii hapo chini utajifunza vyakula hatari kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo.

 

Vyakula anavyopasa kula mgonjwa wa vidonda vya tumbo.

Ni ngumu sana hapa kuanza kukuorodheshea orodha ya vyakula vyote anavyotakiwa kula mgonjwa wa vidonda vya tumbo. Hata hivyo kila jamii ina aina ya vyakula vyao ambavyo ni ngumu kujulikana kwa watu wa jamii nyingine. Hapa nitakuletea tu kanuni ambazo utaziangatia pindi unapochaguwa chakula kwa ajili ya kutumiwa na mgonjwa wa vidonda vya tumbo. Angalia vyakula vyenye sifa hizi:-

  1. Vyakula ambavyo havina gesi
  2. Vyakula ambavyo havina uchachu sana
  3. Vyakula ambavyo havina chumvi nyingi sana
  4. Vyakula ambavyo havina mafuta mengi
  5. Pia vyema ukatumia na vyakula vifuatavyo kwa namna ambayo unaona itafaa kwa upande wako:-

 

  1. kabichi
  2. matunda aina ya maepo
  3. karoti
  4. mboga za majani za kijani
  5. asali
  6. kitunguu thaumu

Vyakula hatari kwa vidonda vya tumbo:

Kama nilivyokueleza hapo juu kuhusu kanuni za kuzishikili unapochaguwa vyakula basi hapa pia utaendelea na kanuni zile zile pindi unapotaka kuepuka vyakula ukiwa kama mgonjwa wa vidonda vya tumbo. Epuka vyakula hivi:-

  1. vyenye gesi kama maharagwe
  2. vyenye uchachu sana
  3. vyenye pilipili kwa wingi
  4. vyenye mafuta mengi
  5. vyenye chumvi nyingi

Pia punguza matumizi ya vifuatavyo ama wacha kabisa iwezekanapo:-

  1. sigara
  2. pombe
  3. kahawa
  4. maziwa unaweza kupunguza tu matumizi
  5. pilipili kwa wingi

 

Vipi nitajilinda na vidonda vya tumbo?

Ni ngumu sana kwa sababu mpaka leo bado haijajulikana sababu ya kupata bakteria wa vidonda vya tumbo. Hivyo kujikinga na vidonda vya tumbo vinavyosababishwa na mashambulizi ya bakteria ni ngumu. Ila kwa kuwa sababu za kutokea kwa vidonda vya tumbo ni nyingi, unaweza kujikinga na vidonda vya tumbo vinavyosababishwa na sababu nyingine. Njkia hizo ni kama:-

  1. Punguza misongo ya mawazo
  2. Wacha ama punguza kutumia kilevi
  3. Punguza ama wacha kabisa kuvuta sigara
  4. Wacha kutumia dawa kiholela

 

Je vidonda vya tumbo vinaweza kupona kabisa?

Tambuwa kuwa vidonda vya tumbo vinatibika bila ya wasi wowote ule. Unaweza kutibiwa na ukapona kabisa. Hakuna muda maalumu wa kupona lakini haiwezi kumaliza miezi hata sita utapona kabisa. Tukutane makala inayofata ttakapojifunza kuhusu matibabu na dawa za vidonda vya tumbo.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 3440


Sponsored links
πŸ‘‰1 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰2 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰3 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Namna ya kuzuia ugonjwa wa Homa ya inni.
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia ugonjwa wa Homa ya inni, ni njia ambazo utumiwa Ili kuepuka kusambaa kwa ugonjwa wa Homa ya inni kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine, Soma Zaidi...

Ugonjwa wa kisukari ambao husababisha kupoteza fahamu ( coma ya kisukari)..
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa kisukari unaopelekea kukosa fahamu ni tatizo linalohatarisha maisha kisukari ambalo husababisha kupoteza fahamu. Ikiwa una kisukari, sukari ya juu ya damu (hyperglycemia) au sukari iliyopungua sana (hypoglyc Soma Zaidi...

Huduma kwa wenye Maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia Watu wale ambao wana Maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo. Soma Zaidi...

Huduma kwa walio na matatizo ya asili nyingi mwilini
Posti hii inahusu zaidi huduma kwa wale ambao tayari wameshakuwa na tatizo la asidi mwilini, ni njia ambazo unaweza kuzitumia ili kuweza kupunguza tatizo hili au Mgonjwa anapoendelea kupata matibabu. Soma Zaidi...

Sababu za Kuvimba kwa kope.
Post hii inazungumzia kuhusiana na Sababu zinazopelekea kuvimba kwa kope, kawaida huhusisha sehemu ya kope ambapo kope hukua na kuathiri kope zote mbili. Pia hutokea wakati tezi ndogo za mafuta ziko karibu na msingi wa kope huziba. Hii inasababisha kuw Soma Zaidi...

Njia za kuzuia upele
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuzuia upele, ni njia ambazo utumiwa Ili kupunguza tatizo la upele kwenye jamii, kwa hiyo jamii inapaswa kutumia njia hizi Ili kuweza kupambana na ugonjwa huu ambao unatibika. Soma Zaidi...

Je fangasi ikikaa kwa muda mrefu bila kutibiwa ina madhara gani?
Je umeshawaho kujiuliza maswali mengi kihusu fangasi?. Huyu hapa ni mmoja katika waulizaji waliopata kuuliza rundo la maswali haya. Soma post hii kuona nini ameuliza Soma Zaidi...

Athari za Ugonjwa wa herpes simplex kwa wajawazito
Post inahusu zaidi athari za Ugonjwa wa herpes simplex kwa wajawazito au ugonjwa wa vipele kwenye midomo na sehemu za siri.ugonjwa huu uleta madhara kwa wajawazito kama tutakavyoona Soma Zaidi...

Dawa za kutibu kiungulia
Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya dawa za kutibu kiungulia Soma Zaidi...

Vyanzo vya magonjwa yanayotokea kwenye sehemu za siri
Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya magonjwa yanayotokea kwenye sehemu za siri,kwa sababu siku kwa siku kuna magonjwa mengi yanayotokea kwenye sehemu za siri ila kuna vyanzo mbalimbali ambavyo usababisha kuwepo kwa magonjwa kwenye sehemu mbalimbali za siri Soma Zaidi...

Ugonjwa wa Maambukizi ya mfumo wa mkojo kwa watoto chini ya miaka mitano (UTI)
posti hii inazungumzia kuhusiana na Maambukizi kwenye mfumo wa mkojo ambapo kitaalamu hujulikana Kama UTI(Urinary Tract Infection (UTI)) hufafanuliwa kuwa ni maambukizo ya mfumo wa uzazi ambayo yanahusisha urethra. UTI ni maambukizi ya mfumo wa mkojo, m Soma Zaidi...

ugonjwa wa Malaria dalili zake na chanzo chake.
Malaria ni moja ya magonjwa hatari yanayoongoza katika vifo vya watoto wengi duniani walio chni ya umri wa miaka 5. Katika post hii utakwend akujifunza kuhusuugonjwa huu jinsi unavyotokea, hatuwa zake na dalili zake. Soma Zaidi...