Ujuwe mlo sahihi kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo

Post hii itakwenda kuangalia mlo sahihi wa mwenye vidonda vya tumbo. Hata utajifunza ni vyakula vipi hapaswi kula na vipi ana paswa kula.

VYAKULA VYA KUVIEPUKA KWA MGONJWA WA VIDONDA VYA TUMBO

Vidonda vya tumbo ni nini?

Vidonda vya tumbo ni aina za vidonda ambavyo hutokea kwenye mfumo wa mmeng’enyo wa chakula. Vidonda vivi vinaweza kutokea kwenye tumbo ama utumbo. Hata hivyo koo la chakula linaweza kuathirika kupata vidonda, jambo hatuviiti vidonda vya tumbo. Vidonda vya tumbo vinaweza kuleta maumivu makali sana ya tumbo na mara nyingi hutokea wakati mtu ana njaa.

 

Nini husababisha vidonda vya tumbo?

Sababu kuu ya kutokea kwa vidonda vya tumbo ni mashambulizi ya bakteria wanaojulikana kama Helicobacter pylor (H.pylor). bakteria hawa wanaishi kwenye tumbo. Mtu anaweza kuishi na bakteria hawa kwa miaka kwa miaka mingi bila ya kusabbabisha madhara yeyote yale. Lakini si mara zote, bakteria hawa wanaweza kusababisha kuvimba (inflamation) kwenye kuta za tumbo, na kupelekea kutokea kwa michubuko na hatimaye vidonda vya tumbo. Vingine vinavyosababisha vidonda vya tumbo ni kama:-

  1. Misongo ya mawazo
  2. Ongezeko la uzalishwaji wa tindikali tumboni
  3. Matumizi mabaya ya dawa
  4. Saratani ya tumbo

 

Dalili za vidonda vya tumbo

Maumivu ya vidonda vya tumbo ni makali, pia mgonjwa wa vidonda vya tumbo anaweza kupatwa na changamoto nyingine ambazo ni katika dalili za vidonda vya tumbo. Kwa mfano kutapika, kiungulia cha mara kwa mara, tumbo kujaa gesi, maumivu ya kifua, kupungua kwa damu na uzito. Endapo vidonda vya tumbo vitadumu kwa muda mrefu bila ya kupatiwa matibabu afya ya mgonjwa inaweza kuwa mbaya ijapokuwa vidonda vya tumbo havisababishi kifo.

 

Vipi nitatuliza maumivu?

Unaweza kutuliza maumivu ya vidonda vya tumbo kwa kutumia dawa za hospitali. Pia kwa kutumia dawa za kienyeji pia. Lakini unaweza kutuliza maumivu haya kwa kutumia vyakula. Wapo baadhi ya wagonjwa wa vidonda vya tumbo hutumia baadhi ya vyakula kutuliza maumivu. Mfano wa vyakula hivyo ni maziwa. Endelea na makala hii hapo chini utajifunza vyakula hivi vilivyo vizuri kwa vidonda vya tumbo.

 

 

 

Nini husabaabisha maumivu?

Maumivu ya vidonda vya tumbo pia yanaweza kusababishwa na matumizi ya madawa na vyakula ama vinywaji fulani. Pia kukaa kwa njaa kwa muda mrefu kunaweza kuleta maumivu kwa mgonjwa. Hutokea pia misongo ya mawazo ikawa pia ni vichochezi vya maumivu haya. Huenda mgonjwa anatumia hivi bila ya yeye kujua ama anatumia kwa sababu hana namna nyingine ya kufanya. Kwa mfano ijapokuwa maziwa hutuliza maumivu lakini kitaalamu sio mazuri sana kwa mgonjwa. Endelea na makala hii hapo chini utajifunza vyakula hatari kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo.

 

Vyakula anavyopasa kula mgonjwa wa vidonda vya tumbo.

Ni ngumu sana hapa kuanza kukuorodheshea orodha ya vyakula vyote anavyotakiwa kula mgonjwa wa vidonda vya tumbo. Hata hivyo kila jamii ina aina ya vyakula vyao ambavyo ni ngumu kujulikana kwa watu wa jamii nyingine. Hapa nitakuletea tu kanuni ambazo utaziangatia pindi unapochaguwa chakula kwa ajili ya kutumiwa na mgonjwa wa vidonda vya tumbo. Angalia vyakula vyenye sifa hizi:-

  1. Vyakula ambavyo havina gesi
  2. Vyakula ambavyo havina uchachu sana
  3. Vyakula ambavyo havina chumvi nyingi sana
  4. Vyakula ambavyo havina mafuta mengi
  5. Pia vyema ukatumia na vyakula vifuatavyo kwa namna ambayo unaona itafaa kwa upande wako:-

 

  1. kabichi
  2. matunda aina ya maepo
  3. karoti
  4. mboga za majani za kijani
  5. asali
  6. kitunguu thaumu

Vyakula hatari kwa vidonda vya tumbo:

Kama nilivyokueleza hapo juu kuhusu kanuni za kuzishikili unapochaguwa vyakula basi hapa pia utaendelea na kanuni zile zile pindi unapotaka kuepuka vyakula ukiwa kama mgonjwa wa vidonda vya tumbo. Epuka vyakula hivi:-

  1. vyenye gesi kama maharagwe
  2. vyenye uchachu sana
  3. vyenye pilipili kwa wingi
  4. vyenye mafuta mengi
  5. vyenye chumvi nyingi

Pia punguza matumizi ya vifuatavyo ama wacha kabisa iwezekanapo:-

  1. sigara
  2. pombe
  3. kahawa
  4. maziwa unaweza kupunguza tu matumizi
  5. pilipili kwa wingi

 

Vipi nitajilinda na vidonda vya tumbo?

Ni ngumu sana kwa sababu mpaka leo bado haijajulikana sababu ya kupata bakteria wa vidonda vya tumbo. Hivyo kujikinga na vidonda vya tumbo vinavyosababishwa na mashambulizi ya bakteria ni ngumu. Ila kwa kuwa sababu za kutokea kwa vidonda vya tumbo ni nyingi, unaweza kujikinga na vidonda vya tumbo vinavyosababishwa na sababu nyingine. Njkia hizo ni kama:-

  1. Punguza misongo ya mawazo
  2. Wacha ama punguza kutumia kilevi
  3. Punguza ama wacha kabisa kuvuta sigara
  4. Wacha kutumia dawa kiholela

 

Je vidonda vya tumbo vinaweza kupona kabisa?

Tambuwa kuwa vidonda vya tumbo vinatibika bila ya wasi wowote ule. Unaweza kutibiwa na ukapona kabisa. Hakuna muda maalumu wa kupona lakini haiwezi kumaliza miezi hata sita utapona kabisa. Tukutane makala inayofata ttakapojifunza kuhusu matibabu na dawa za vidonda vya tumbo.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 5869

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰2 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰3 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰4 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰5 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

UGONJWA WA HOMA YA VIRUSI VYA ZIKA (ZIKV) VINAVYO SABABISHWA NA KUNG'ATWA NA MBU

Mnamo mwaka 2016 World Health Organization (WHO) iliitisha kikao cha dharura mnamo mwezi tarehe 1 mwezi wa pili mpaka tarehe 13 mwezi wa nne.

Soma Zaidi...
Fahamu Ugonjwa wa kifaduro kwa watoto chini ya miaka mitano

post hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa kifaduro ambao hujulikana Kama Pertussis pia inajulikana kama kifaduro ni maambukizi ya bakteria ambayo huingia kwenye pua yako na koo.

Soma Zaidi...
Dalili za macho makavu.

Posti hii inahusu zaidi njia za kutambua Dalili za macho makavu, kama tulivyotangulia kuona kubwa macho kuwa makavu Usababishwa na sehemu ya kuzalisha maji kwenye jicho kushindwa kufanya kazi na jicho hilo huwa kavu na Dalili zake ni kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
YAMINYOO NA ATHARI ZAO KIAF

Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.

Soma Zaidi...
Dalili za Pua iliyovunjika

posti hii inahusu dalili za Pua iliyovunjika, pia inaitwa fracture ya pua, ni kuvunjika au kupasuka kwa mfupa katika pua yako

Soma Zaidi...
Dalili za kuvimbiwa kwa watoto.

Kuvimbiwa kwa watoto ni shida ya kawaida. Kuvimbiwa kwa watoto mara nyingi huonyeshwa na kinyesi kisicho kawaida au kinyesi ngumu na kavu.

Soma Zaidi...
Dalili zinazonesha kuungua kwa Mdomo (burning mouth)

Ugonjwa wa mdomo unaoungua ni neno la kimatibabu kwa ajili ya kuungua kinywani kwa mara kwa mara (kwa muda mrefu) bila sababu dhahiri. Usumbufu huo unaweza kuathiri ulimi wako, ufizi, midomo, ndani ya mashavu yako, paa la mdomo wako au maeneo yaliyoenea

Soma Zaidi...
Yajue magonjwa ya jicho

Posti hii inahusu zaidi Magonjwa ya jicho,ni Magonjwa ambayo ushambulia sehemu mbalimbali za jicho kwa mfano kwenye retina,kuaribu mishipa ya retina ,macho kuwa makavu na pia mtoto wa jicho, hali hii ya magonjwa ya macho Usababisha madhara mbalimbali kama

Soma Zaidi...
Kuharisha choo cha marenda renda ni dalili gani?

Hivi huwa unachunguza choo chako? ivi huwa kinazama kwenye maji ama kinaelea? Kila damu ama malendalenda, je ni cheusi sana na kina harufu kali sana.

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu ya matiti na chuchu

Maumivu ya matiti yanaweza kuanzia kidogo hadi makali. Inaweza kukuathiri siku chache tu kwa mwezi, kwa mfano kabla tu ya kipindi chako, au inaweza kudumu kwa siku saba au zaidi kila mwezi. Maumivu ya matiti yanaweza kukuathiri kabla tu ya kipindi chako

Soma Zaidi...