Ujuwe mlo sahihi kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo

Post hii itakwenda kuangalia mlo sahihi wa mwenye vidonda vya tumbo. Hata utajifunza ni vyakula vipi hapaswi kula na vipi ana paswa kula.

VYAKULA VYA KUVIEPUKA KWA MGONJWA WA VIDONDA VYA TUMBO

Vidonda vya tumbo ni nini?

Vidonda vya tumbo ni aina za vidonda ambavyo hutokea kwenye mfumo wa mmeng’enyo wa chakula. Vidonda vivi vinaweza kutokea kwenye tumbo ama utumbo. Hata hivyo koo la chakula linaweza kuathirika kupata vidonda, jambo hatuviiti vidonda vya tumbo. Vidonda vya tumbo vinaweza kuleta maumivu makali sana ya tumbo na mara nyingi hutokea wakati mtu ana njaa.

 

Nini husababisha vidonda vya tumbo?

Sababu kuu ya kutokea kwa vidonda vya tumbo ni mashambulizi ya bakteria wanaojulikana kama Helicobacter pylor (H.pylor). bakteria hawa wanaishi kwenye tumbo. Mtu anaweza kuishi na bakteria hawa kwa miaka kwa miaka mingi bila ya kusabbabisha madhara yeyote yale. Lakini si mara zote, bakteria hawa wanaweza kusababisha kuvimba (inflamation) kwenye kuta za tumbo, na kupelekea kutokea kwa michubuko na hatimaye vidonda vya tumbo. Vingine vinavyosababisha vidonda vya tumbo ni kama:-

  1. Misongo ya mawazo
  2. Ongezeko la uzalishwaji wa tindikali tumboni
  3. Matumizi mabaya ya dawa
  4. Saratani ya tumbo

 

Dalili za vidonda vya tumbo

Maumivu ya vidonda vya tumbo ni makali, pia mgonjwa wa vidonda vya tumbo anaweza kupatwa na changamoto nyingine ambazo ni katika dalili za vidonda vya tumbo. Kwa mfano kutapika, kiungulia cha mara kwa mara, tumbo kujaa gesi, maumivu ya kifua, kupungua kwa damu na uzito. Endapo vidonda vya tumbo vitadumu kwa muda mrefu bila ya kupatiwa matibabu afya ya mgonjwa inaweza kuwa mbaya ijapokuwa vidonda vya tumbo havisababishi kifo.

 

Vipi nitatuliza maumivu?

Unaweza kutuliza maumivu ya vidonda vya tumbo kwa kutumia dawa za hospitali. Pia kwa kutumia dawa za kienyeji pia. Lakini unaweza kutuliza maumivu haya kwa kutumia vyakula. Wapo baadhi ya wagonjwa wa vidonda vya tumbo hutumia baadhi ya vyakula kutuliza maumivu. Mfano wa vyakula hivyo ni maziwa. Endelea na makala hii hapo chini utajifunza vyakula hivi vilivyo vizuri kwa vidonda vya tumbo.

 

 

 

Nini husabaabisha maumivu?

Maumivu ya vidonda vya tumbo pia yanaweza kusababishwa na matumizi ya madawa na vyakula ama vinywaji fulani. Pia kukaa kwa njaa kwa muda mrefu kunaweza kuleta maumivu kwa mgonjwa. Hutokea pia misongo ya mawazo ikawa pia ni vichochezi vya maumivu haya. Huenda mgonjwa anatumia hivi bila ya yeye kujua ama anatumia kwa sababu hana namna nyingine ya kufanya. Kwa mfano ijapokuwa maziwa hutuliza maumivu lakini kitaalamu sio mazuri sana kwa mgonjwa. Endelea na makala hii hapo chini utajifunza vyakula hatari kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo.

 

Vyakula anavyopasa kula mgonjwa wa vidonda vya tumbo.

Ni ngumu sana hapa kuanza kukuorodheshea orodha ya vyakula vyote anavyotakiwa kula mgonjwa wa vidonda vya tumbo. Hata hivyo kila jamii ina aina ya vyakula vyao ambavyo ni ngumu kujulikana kwa watu wa jamii nyingine. Hapa nitakuletea tu kanuni ambazo utaziangatia pindi unapochaguwa chakula kwa ajili ya kutumiwa na mgonjwa wa vidonda vya tumbo. Angalia vyakula vyenye sifa hizi:-

  1. Vyakula ambavyo havina gesi
  2. Vyakula ambavyo havina uchachu sana
  3. Vyakula ambavyo havina chumvi nyingi sana
  4. Vyakula ambavyo havina mafuta mengi
  5. Pia vyema ukatumia na vyakula vifuatavyo kwa namna ambayo unaona itafaa kwa upande wako:-

 

  1. kabichi
  2. matunda aina ya maepo
  3. karoti
  4. mboga za majani za kijani
  5. asali
  6. kitunguu thaumu

Vyakula hatari kwa vidonda vya tumbo:

Kama nilivyokueleza hapo juu kuhusu kanuni za kuzishikili unapochaguwa vyakula basi hapa pia utaendelea na kanuni zile zile pindi unapotaka kuepuka vyakula ukiwa kama mgonjwa wa vidonda vya tumbo. Epuka vyakula hivi:-

  1. vyenye gesi kama maharagwe
  2. vyenye uchachu sana
  3. vyenye pilipili kwa wingi
  4. vyenye mafuta mengi
  5. vyenye chumvi nyingi

Pia punguza matumizi ya vifuatavyo ama wacha kabisa iwezekanapo:-

  1. sigara
  2. pombe
  3. kahawa
  4. maziwa unaweza kupunguza tu matumizi
  5. pilipili kwa wingi

 

Vipi nitajilinda na vidonda vya tumbo?

Ni ngumu sana kwa sababu mpaka leo bado haijajulikana sababu ya kupata bakteria wa vidonda vya tumbo. Hivyo kujikinga na vidonda vya tumbo vinavyosababishwa na mashambulizi ya bakteria ni ngumu. Ila kwa kuwa sababu za kutokea kwa vidonda vya tumbo ni nyingi, unaweza kujikinga na vidonda vya tumbo vinavyosababishwa na sababu nyingine. Njkia hizo ni kama:-

  1. Punguza misongo ya mawazo
  2. Wacha ama punguza kutumia kilevi
  3. Punguza ama wacha kabisa kuvuta sigara
  4. Wacha kutumia dawa kiholela

 

Je vidonda vya tumbo vinaweza kupona kabisa?

Tambuwa kuwa vidonda vya tumbo vinatibika bila ya wasi wowote ule. Unaweza kutibiwa na ukapona kabisa. Hakuna muda maalumu wa kupona lakini haiwezi kumaliza miezi hata sita utapona kabisa. Tukutane makala inayofata ttakapojifunza kuhusu matibabu na dawa za vidonda vya tumbo.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 5362

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Dalili na ishara za kuvimba kope.

Posti hii inaonyesha Dalili na ishara za kuvimba kope ambayo kitaalamu hujulikana Kama blepharitis.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kisonono, sababu zake nanjia za kujilinda.

Kisonono husababishwa na bakteria. Bakteria ya kisonono mara nyingi hupitishwa kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine wakati wa kujamiiana, ikiwa ni pamoja na kujamiiana kwa mdomo, mkundu au uke.

Soma Zaidi...
Dalili za VVU

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za VVU

Soma Zaidi...
Sababu za kuwepo kwa saratani ya inni.

Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali za kuwepo kwa saratani ya ini, saratani hii imekuwa tishio kwa wengi ila ni vizuri kujua baadhi ya sababu ambazo uchangia sana kuwepo kwa tatizo hili la saratani ya inni.

Soma Zaidi...
MARADHI MENGINE 10 YANAYOTOKANA NA MBU ( matende, ngirimaji, homa ya manjano, n.k

Tofauti na maradhi yaliyotajwa hapo juu pia tafiti za kisayansi zimethibitisha kuwepo kwa maradhi mengine hatari yanayosambazwa na mbu, kama vile ngirimaji pamoja na matende.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa UTI

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu ugonjwa wa UTI

Soma Zaidi...
vidonda vya tumbo, dalili zake, chanzo chake na tiba yake

Makala hii itakwenda kukupa elimu juu ya vidonda vya tumbo, nini hasa chanzo chake, vipi vinatokea ni zipi dalili zake, ni zipi njia za kujilinda dhidi ya vidonda vya tumbo. Pia tutaangalia matibabu ya kutibi vidonda vya tumbo.

Soma Zaidi...
Nini kinasababisha kizunguzungu?

Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili za kizunguzungu zinazotekea katika mwili wa binadamu

Soma Zaidi...
Njia za kugundua tatizo la kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu

Post hii inahusu Zaidi njia mbali mbali ambazo uweza kitumiwa na wataalamu ili kuweza kugundua tatizo la kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu.

Soma Zaidi...
Je wiki 1 dalili zinaonyesha za maambukizi ya ukimwi na wiki 3 vipimo vinaweza kuonyesha Kama umeasilika

Muda ambao maambukizi ya virusi vya ukimwi kuonyesha dalili unaweza kutofautiana kutika mtu hadi mwingine.

Soma Zaidi...