Vidonda vya tumbo chanzo chake na dalili zake

Vidonda vya tumbo chanzo chake na dalili zake

Katika post hii utajifunz akuhusu vidonda vya tumbo na jinsi vinavyotokea. Utajifunza pia tahadhari anazopasa mtu achukuwe na vyakula salama anavyopaswa kula.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

VIDONDA VYA TUMBO, CHANZO CHAKE NA DALILI ZAKE.

Vidonda vya tumbo ni katika matatizo ya kiafya ambayo yamekuwa yakiathiri watu wengi leo. Si wanawake tu lakini hata wanaume, wazee kwa watoto. Kumekuwa na fikra nyingi potofu kuhusu vidonda vya tumbo nini hasa sababu zake, dalili zake na kwa namna gani vidonda vya tumbo hutokea. Je na wewe ni katika watu wahawa?. makala hii ni kwa ajili yako. Lengo la makala hii ni kukujuza dalili za vidonda vya tumbo.

 

Vidonda vya tumbo ni vidonda ambavyo hutokea kwenye mfumo wa mmeng’enyo wa chakula. Vinaweza kutokea kuanzia eneo la juu la tumbo la chakula, kuelekea kwenye tumbo, utumbo mdogo hadi utumbo mkubwa. Vidonda hivi pia vinaweza kuathiri koo la chakula. Mara nyingi watu wamekuwa wakidhani vidonda vya tumbo vipo kwenye tumbo la chakula tu. Hii sio sahihi kabisa. Lamda tuone aina za vidonda vya tumbo.

 

Vidonda vya tumbo vimegawanyika katika aina zisizopunguwa tatu. Miongoni mwazo ni  vidonda vya tumbo vinavyotokea kwenye tumbo la chakula, vidonda vya tumbo vinavyotokea kwenye sehemu inayounganisha koo la chakula na tumbo la chakula na vidonda vya tumbo vinavyotokea kwenye sehemu ya juu ya utumbo mdogo.

 

Nini chanzo cha vidonda vya tumbo?

Watu wengi wamekuwa wakidhania kuwa chanzo cha vidonda vya tumbo ni kukaa na njaa muda mrefu. Kwa namna moja wapo sahihi. Lakni ukweli ni kuwa hiki sio chanzo kikuu. Na wanaopata vidonda vya tumbo kwa sababu hii ni wachache sana. Chanzo kikuu cha vidonda vya tumbo ni mashambulizi ya bakteria wanaojulikana kama Helicobacter pylori (.pylori) hawa ni bakteria ambao wanakwenda kushambullia tumbo na utumbo hatimaye kusababisha vidonda.

 

Vyanzo vingine vya vidonda vya tumbo ni kama matumizi ya aina flani za dawa kwa muda mrefu. Mfano mzuri ni dawa za kutuliza maumivu zinazofahamika kama NSAIDs kirefu chake ni kusema nonesteroidal anti-inflamatory drugs mfano wa dawa hizi ni kama advil na aleve. Chanzo kingine cha vidonda ni misongo ya mawazo kwa muda mrefu, na chanzo kingine ni uzalishwaji wa tindikali kuongezeka ndani ya mwili.

 

Je ni kivipi vidonda hutokea?

Kwa ufupi vidond hutokea baada ya utando mlaini kwenye tumbo na utumbo kulika na kubakisha tumbo ama utumbo kuwa wazi hivyo kuruhusu shughuli za tindikali kuathiri tumb na utumbo. Hii husababisha michubuko na hatimaye kuleta vidonda vya tumbo. Bila shaka huwenda hujaelewa hapa. Wacha nikujuze zaidi

 

Katika tumbo na utumbo kuna tindikali (acid) ambazo huzalishwa mwilini kwa ajili ya kuuwa bakteria kwenye vyakula. Zipo kazi nyingine pia. Tindikali hizi zina nguvu kiasi hata kuraruwa bati. Sasa kwa nguvu hii hata ngozi inaweza kuchubuka na kusababisha vidonda. Sasa kwa kuwa kwenye tumbo na utumbo kuna utando wa utelezi huu husaidia kuzuia athari ya bakteria haiathiri utumbo na tumbo.

 

Sasa endapo utandu huu utaathirika na hautakuwepo tena ama utakuwepo kwa uchache hali hii itaruhusu tindikali zinazozalishwa kwenye tumbo na utumbo kuchubuwa kuta za utumbo na utumbo na hatimaye kusababisha vidonda.

Kuhusu bakteria wanavyosababisha vidonda inaweza kuwa tofauti kidogo. Wao bakteria kwanza mara nyingi hawana shida wanweza kuishi mika mingi bila ya kusababisha vidonda. Sasa wakati mwingine wanaweza kusababisha kuta laini za utumbo na tumbo kuvimba. Hii mivimbo baadaye kusababisha vidonda.

 

Hutokea pia tindikali zikaunguza utando laini huu unaokinga ngozi ya tumbo na utumbo. Hii hutokea endapo uzalishwaji wa tindikali utaongezeka. Hii inaweza kusababishwa na vyakula, misongo ya mawazo ama matumizi ya dawa kama ilivyoelezwa hapo juu.

 

Ni zipi dalili za vidonda vya tumbo?

Dalili za vidonda vya tumbo zinaweza kuwa tofauti kutokana na mtu mwenyewe, mahali vilipo na mengineyo lakini zipo ambazo hutokea kwa watu karibia wote. Dalili hizo ni kama:-

  1. Tumbo kujaa gesi
  2. Kiungulia cha mara kwa mara
  3. Maumivu ya tumbo hasa unapokuwa na njaa
  4. Uchovu wa mra kwa mara
  5. Kupata choo cheusi ama chenye damu
  6. Huwenda ukatapika damu
  7. Inaweza tokea ukapunguwa uzito
  8. Kukosa hamu ya kula

 

Mgonjwa anaweza kupata nafuu ya maumivu baada ya kula na kshiba. Pia kuna wengine wanapata nafuu baada ya kunywa maziwa. Lakini tambuwa kuwa ijapokuwa maziwa yanaweza kukupa nafuu lakini sio mazuri huwenda yakaja kukuletea madhara huko siku za mbele.

 

Je vidonda vya tumbo vinatibika?

Jibu fupi ndio, vidonda vya tumbo hutibika tena bila ya ugumu wowote. Vindonda vya tumbo vinaweza kutibika kwa dawa za asili kama bamia, kabichi, kitunguu thaumu, asaili na nyinginezo. Lakini pia ni vyema kutumiadawa za hoospitali kwa sababu zina vipimo maalumu.

 

Vidonda vya tumbo vinaweza kuwa sugu. Na hii hutokea endapo utumiaji wa dozi hautafata masharti. Lakini pia inawez akutokea bila ya sababu maalumu. Wakati mwingine vidonda vya tumbo huwa sugu kwa sababu tiba yake sio inayotumika. Ili kuweza kutokomeza vidonda vya tumbo kwanza ni kujuwa sababu gani inayosababisha vidonda vya tumbo.

 

Kama sababu ni tindikali kuzaliwa nyingi bai mgonjwa apewe dawa za kuzuia uzalishwaji wa tindikali kutokuwa mwingi zaidi. Na kama sababu ni matumizi ya dawa mgonjwa iangaliwe kama ataweza kubadilishiwa dawa. Na kama sababu ni bakteria mgonjwa atapewa dawa ya kuuwa bakteria hao tumboni.

 

Imanipotofu kuhusu vodona vya tumbo

Kama nilivyokueleza mwanzoni mwa makala hii kuwa kuna imani nyingi potofu na hazina ushahidi wa kitaalamu. Inaweza kuwa watu ndivyo wanavuyoamini kutokana na jamii zaoama kutokana na tafiti za zamani ambazo kwa sasa zimekosolewa kutokanana tafiti mpya. Imani hizo ni kama:-

  1. Vyakula vyenye pilipili husababisha vidonda vya tumbo, hii si kweli
  2. Kukaa na njaa ndio sababu kubwa ya kutokea vidonda vya tumbo, hii si kweli
  3. Vidonda vya tumbo havitibiki, hii ia si kweli.

 

Tukutane makala ijayo tutakapoona vyakula vizuri na vibaya kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 1571

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

 Zifahmu Dalili za homa ya ini Kali ya pombe.
Zifahmu Dalili za homa ya ini Kali ya pombe.

Posti hii inaonyesha dalili na Mambo Hatari yanayosababisha homa ya ini Kali ya pombe.

Soma Zaidi...
Dalili za Dengue.
Dalili za Dengue.

Posti hii inahusu zaidi dalili za Dengue,ni Dalili ambazo huwa kwenye makundi matatu na kuwepo kwa makundi hayautegemea kuongezeka kwa tatizo kwa sababu tatizo likiongezeka bila kutibiwa na dalili uongezeka na kufikia kwenye sehemu isiyo ya kawaida kwa mg

Soma Zaidi...
 DALILI ZA MINYOO: maumivu ya tumbo, kichwa, kuwashwa, kutapika damu, moyo kuumwa, ukuaji hafifu, udhaifu na kuchoka
DALILI ZA MINYOO: maumivu ya tumbo, kichwa, kuwashwa, kutapika damu, moyo kuumwa, ukuaji hafifu, udhaifu na kuchoka

DALILI ZA MINYOO Wakati mwingine ni vigumu sana kujua kama una minyoo, kwani minyoo wanaweza kukaa ndani ya mwili kwa muda mrefu bila ya kuonesha dalili yeyote, ama madhara yeyote.

Soma Zaidi...
Dalili za madonda ya koo
Dalili za madonda ya koo

Posti hii inahusu zaidi magonjwa ya koo, ni ugonjwa unaoshambulia sana sehemu ya koo la hewa, na na huwa na dalili zake kama ifuayavyo.

Soma Zaidi...
Sababu ya maumivu ya magoti.
Sababu ya maumivu ya magoti.

Posti hii inahusu zaidi sababu za maumivu ambayo yanasikika kwenye magoti, huu ni ugonjwa ambao umewapata walio wengi na bado ni kilio kwa walio wengi kwa vijana na kwa wazee, Kuna wataalamu mbalimbali ambao wameweza kugundua sababu za maumivu kwenye mago

Soma Zaidi...
Dalili za anemia ya upungufu wa vitamin.
Dalili za anemia ya upungufu wa vitamin.

Anemia ya upungufu wa vitamini ni ukosefu wa seli nyekundu za damu zenye afya unaosababishwa na kiasi kidogo cha vitamini fulani kuliko kawaida.

Soma Zaidi...
Madhara ya maambukizi kwenye tumbo
Madhara ya maambukizi kwenye tumbo

Posti hii inahusu zaidi madhara ya maambukizi kwenye tumbo,hasa pale ambapo mgonjwa hakutibiwa

Soma Zaidi...
Je mtu anaweza kushiriki mapenzi na mtu mwenye maambukizi ya ukimwi pasipo kuambukizwa?
Je mtu anaweza kushiriki mapenzi na mtu mwenye maambukizi ya ukimwi pasipo kuambukizwa?

Naomba kuuliza swaliJe mtu anaweza kushiriki mapenzi na mtu mwenye maambukizi ya ukimwi pasipo kuambukizwa?

Soma Zaidi...
Je unaweza sex na mwanamke mwenye HIV na ukaenda kupima wiki moja na ukagundurika kwa vipimo vya maabara
Je unaweza sex na mwanamke mwenye HIV na ukaenda kupima wiki moja na ukagundurika kwa vipimo vya maabara

Utakapofanya ngono na aliyeathirika haimaanishi na wewe kuwa lazima utakuwa umeathirika. Kuathirika kuna mambo mengi lazima yafanyike.

Soma Zaidi...
Ni zipi dalili za awali za pumu
Ni zipi dalili za awali za pumu

Kabla ya kubanwa zaidi na pumu, kuna dalili za awali zinzznza kujitokeza, na hapo ndipo utakapoanza kuchukuwa tahadhari. Makala hii itakwenda kukujulisha zaidi kuhusu dalili hizo.

Soma Zaidi...