Maandalizi ya Hijra ya Mtume na Mafunzo tunayoyapata kutoka katika hijra hii

Maandalizi ya Hijra ya Mtume (s.

Maandalizi ya Hijra ya Mtume na Mafunzo tunayoyapata kutoka katika hijra hii

Maandalizi ya Hijra ya Mtume na Mafunzo tunayoyapata kutoka katika hijra hii

Maandalizi ya Hijra ya Mtume (s.a.w) na Waislamu kuhamia Madinah.
Mtume (s.a.w) hakuhama mpaka alipoletewa amri ya kuhama, na aliindaa safari yake kistretejia akiwa sahibu wake Abubakar (r.a).



Mikakati na Maandalizi ya Kistretejia aliyofanya Mtume (s.a.w) na Abubakar (r.a) kabla ya kuanza safari ya kuhama kwenda Yathrib (Madina);



i.Walipanga kuwa watajificha katika pango Thaur kwa siku tatu kabla ya kuanza safari ya kuelekea Yathrib (Madinah).



ii.Walipanga kutumia njia ya uficho isijulikana na mtu ya kuelekea kusini badala ya njia ya kawaida ya kuelekea kaskazini.



iii.Walimkodi bedui mweledi wa njia ile atakayewaongoza mpaka Yathrib kwa dinari 300.



iv.Abubakar (r.a) alinunua ngamia wawili kwa ajili ya safari yake na Mtume (s.a.w).



v.Abubakar (r.a) alimchukua bint yake Asma kwa siri ili kumuonyesha pango lilipo na awe anawaletea chakula muda watakapo kuwa pangoni.



vi.Pia Abubakar (r.a) alimwagiza mchunga mbuzi wake awe anachungia karibu na pango ili awapatie maziwa.



vii.Abubakar (r.a) pia alimpa jukumu kijana wake Abdullah kuwaletea taarifa za mjini kwa yatakayojitokeza baada ya wao kuondoka.



Maquraish baada ya kubaini kuwa waislamu wameshahamia Yathrib, na Mtume (s.a.w) anajiandaa naye ahame, walipanga njama ya kumuua kabla hajahama.



Maquraish walichagua vijana shupavu kutoka kila ukoo wa kiquraish na kuwapa mapanga makali ili wajewamvamie kwake akiwa amelala usiku kwa pamoja ili lawama ya kumuua isiangukie ukoo mmoja.



Kabla ya kuondoka, Mtume (s.a.w) alimkabidhi Ali (r.a) amana zote za watu ili kuwarejeshea na akamwamuru alale katika kitanda chake.



Allah (s.w) alimnusu na kabla ya Alfajir, Mtume (s.a.w) aliondoka pamoja na Abubakar (r.a) kuelekea pangoni akawaacha ‘wauaji’ nje ya nyumba yake wamelala fofofo.



Kufeli kwa zoezi la kumuua Mtume (s.a.w), Maquraish walitangaza zawadi ya ngamia 100 kwa atakaye mleta Muhammad au Abubakar yuko hai au amekufa.



Maquraish kwa kumkodi bedui mjuzi wa kufuatilia nyayo, akiwaongoza mpaka pangoni lakini Allah (s.w) aliwanusu. Rejea Qur’an (9:40).



Mwishowe baada ya siku tatu, Mtume (s.a.w) na sahibu wake, Abubakar (r.a) waliondoka kuelekea Madinah na walifika salama kabisa.



Kwa heshima ya Mtume (s.a.w), mji wa Madinah ukawa unaitwa ‘Madinatul-Munwwarah’ (mji ung’aao).



Baada ya kufariki (kutawafu) Mtume (s.a.w), Waislamu walikubaliana kuanzisha Kalenda ya mwaka wa Kiislamu ‘Al-Hijrah’ (A.H) ianzie siku ile aliyohama (hijra ya) Mtume (s.a.w) kwenda Madinah.



Mafunzo yatokanayo na Hijrah ya Mtume (s.a.w) na Maswahaba wake.
i.Hatuna budi kutunza na kurejesha amana za watu kwa wenyewe bila kujali uadui wao kwetu.



ii.Waislamu hawanabudi kuweka mipango na mikakati madhubuti juu ya namna ya kutekeleza mambo yao kabla ya utekelezaji wake.



iii.Waislamu hawana budi kuchukua tahadhari katika kuendesha harakati za kidini kwa kuzingatia kuwa dini ya Uislamu ina maadui wengi.



iv.Nusura ya Allah (s.w) na Ushindi hupatikana tu baada ya kufanyika jitihada za dhati katika kuusimamisha Uislamu katika jamii na kumtegemea yeye pia.



v.Waislamu wanalazimika kufanya jitihada ya dhati ya kumuabudu Allah (s.w) ipasavyo kwa kila kipengele cha maisha yao, kama mazingira yatakuwa ndio kikwazo hawanabudi kuhama (kuhajiri) kwenda sehemu (ardhi) yenye wasaa.
Rejea Qur’an (4:97-99).



                   



Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 228


Download our Apps
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

HISTORIA NA MAISHA YA MTUME IDRISA (A.S)
Mtume aliyemfuatia Nabii Adam(a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA KUUMBWA KWA NABII ADAMU (A.S)NA HADHI YAKE NA HADHI YA WANAADAMU DUNIANI
Adam(a. Soma Zaidi...

Khalifa na Utungaji Sheria, na utiifu juu ya sheria na usimamiaji wa haki
Soma Zaidi...

Vita vya uhudi
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mikataba ya aqabah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

NUHU(A.S) NA WATU WAKE NA UOVU WALIOKUWA WAKIUFANYA WATU WAKE
Mtume aliyemfuatia Nabii Idrisa(a. Soma Zaidi...

Maswali kuhusu hali ya bara arabu zama za jahiliyyah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kibri cha Ibilis na Uadui Wake Dhidi ya Binadamu
Ibilis ni katika jamii ya majini aliyekuwa pamoja na Malaika wakati amri ya kumsujudia Adam inatolewa. Soma Zaidi...

HISTORIA YA MAISHA YA UTOTONI YA MTUME MUHAMMAD (S.A.W)
MAISHA YA UTOTONI YA MTUME S. Soma Zaidi...

Imam Abu Daud na Sunan Abi Daud
Soma Zaidi...

MTUME MUHAMMAD (S.A.W) KULELEWA NA BABA YAKE MDOGO MTUME (ABU TALIB)
KULELEWA NA BABA YAKE MDOGOBaada ya kufariki kwa mzee huyu, kiongozi mkubwa wa maquraysh na makkah, kiongozi ambaye jeshi la Abrah liliangamizwa ndani ya utawala wake. Soma Zaidi...

Historia ya kujengwa kwa Alkabah (Maka)
Kama tulivyoona katika maisha ya Mtume Ibrahim(a. Soma Zaidi...