Maandalizi ya Hijra ya Mtume na Mafunzo tunayoyapata kutoka katika hijra hii

Maandalizi ya Hijra ya Mtume (s.

Maandalizi ya Hijra ya Mtume na Mafunzo tunayoyapata kutoka katika hijra hii

Maandalizi ya Hijra ya Mtume na Mafunzo tunayoyapata kutoka katika hijra hii

Maandalizi ya Hijra ya Mtume (s.a.w) na Waislamu kuhamia Madinah.
Mtume (s.a.w) hakuhama mpaka alipoletewa amri ya kuhama, na aliindaa safari yake kistretejia akiwa sahibu wake Abubakar (r.a).



Mikakati na Maandalizi ya Kistretejia aliyofanya Mtume (s.a.w) na Abubakar (r.a) kabla ya kuanza safari ya kuhama kwenda Yathrib (Madina);



i.Walipanga kuwa watajificha katika pango Thaur kwa siku tatu kabla ya kuanza safari ya kuelekea Yathrib (Madinah).



ii.Walipanga kutumia njia ya uficho isijulikana na mtu ya kuelekea kusini badala ya njia ya kawaida ya kuelekea kaskazini.



iii.Walimkodi bedui mweledi wa njia ile atakayewaongoza mpaka Yathrib kwa dinari 300.



iv.Abubakar (r.a) alinunua ngamia wawili kwa ajili ya safari yake na Mtume (s.a.w).



v.Abubakar (r.a) alimchukua bint yake Asma kwa siri ili kumuonyesha pango lilipo na awe anawaletea chakula muda watakapo kuwa pangoni.



vi.Pia Abubakar (r.a) alimwagiza mchunga mbuzi wake awe anachungia karibu na pango ili awapatie maziwa.



vii.Abubakar (r.a) pia alimpa jukumu kijana wake Abdullah kuwaletea taarifa za mjini kwa yatakayojitokeza baada ya wao kuondoka.



Maquraish baada ya kubaini kuwa waislamu wameshahamia Yathrib, na Mtume (s.a.w) anajiandaa naye ahame, walipanga njama ya kumuua kabla hajahama.



Maquraish walichagua vijana shupavu kutoka kila ukoo wa kiquraish na kuwapa mapanga makali ili wajewamvamie kwake akiwa amelala usiku kwa pamoja ili lawama ya kumuua isiangukie ukoo mmoja.



Kabla ya kuondoka, Mtume (s.a.w) alimkabidhi Ali (r.a) amana zote za watu ili kuwarejeshea na akamwamuru alale katika kitanda chake.



Allah (s.w) alimnusu na kabla ya Alfajir, Mtume (s.a.w) aliondoka pamoja na Abubakar (r.a) kuelekea pangoni akawaacha ‘wauaji’ nje ya nyumba yake wamelala fofofo.



Kufeli kwa zoezi la kumuua Mtume (s.a.w), Maquraish walitangaza zawadi ya ngamia 100 kwa atakaye mleta Muhammad au Abubakar yuko hai au amekufa.



Maquraish kwa kumkodi bedui mjuzi wa kufuatilia nyayo, akiwaongoza mpaka pangoni lakini Allah (s.w) aliwanusu. Rejea Qur’an (9:40).



Mwishowe baada ya siku tatu, Mtume (s.a.w) na sahibu wake, Abubakar (r.a) waliondoka kuelekea Madinah na walifika salama kabisa.



Kwa heshima ya Mtume (s.a.w), mji wa Madinah ukawa unaitwa ‘Madinatul-Munwwarah’ (mji ung’aao).



Baada ya kufariki (kutawafu) Mtume (s.a.w), Waislamu walikubaliana kuanzisha Kalenda ya mwaka wa Kiislamu ‘Al-Hijrah’ (A.H) ianzie siku ile aliyohama (hijra ya) Mtume (s.a.w) kwenda Madinah.



Mafunzo yatokanayo na Hijrah ya Mtume (s.a.w) na Maswahaba wake.
i.Hatuna budi kutunza na kurejesha amana za watu kwa wenyewe bila kujali uadui wao kwetu.



ii.Waislamu hawanabudi kuweka mipango na mikakati madhubuti juu ya namna ya kutekeleza mambo yao kabla ya utekelezaji wake.



iii.Waislamu hawana budi kuchukua tahadhari katika kuendesha harakati za kidini kwa kuzingatia kuwa dini ya Uislamu ina maadui wengi.



iv.Nusura ya Allah (s.w) na Ushindi hupatikana tu baada ya kufanyika jitihada za dhati katika kuusimamisha Uislamu katika jamii na kumtegemea yeye pia.



v.Waislamu wanalazimika kufanya jitihada ya dhati ya kumuabudu Allah (s.w) ipasavyo kwa kila kipengele cha maisha yao, kama mazingira yatakuwa ndio kikwazo hawanabudi kuhama (kuhajiri) kwenda sehemu (ardhi) yenye wasaa.
Rejea Qur’an (4:97-99).



                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1243

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

tarekh 01

NASABA YA MTUME (S.

Soma Zaidi...
Historia ya Al-Khidhri

Jina Al-Khidhri halikutajwa mahali popote katika Qur’an.

Soma Zaidi...
MJADALA JUU YA NDOA YA MTUME S.A.W NA BI KHADIJA (HADIJA)

LAKINI UMRI WANGU MKUBWABaada ya kuwaza na kufikiri muda mrefu, bibi Khadija (Radhiya Llahu anha) akafikia uamuzi wa kutaka kuolewa na Muhammad (Swalla Laahu alayhi wa sallam).

Soma Zaidi...
Mafunzo Yatokanayo na mambo Aliyofanya Mtume (s.a.w) Katika Kuanzisha Dola ya Kiislamu

Kwanza, ili tuweze kusimamisha Uislamu katika jamii hatunabudi kuanzisha na kuendeleza vituo vya harakati, misikiti ikiwa ndio vitovu.

Soma Zaidi...
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Lut (a.s)

(i) Tujitahidi kwa kadiri ya uwezo wetu kuondoa maovu katika jamii kwa mikono yetu na ikiwa hatuwezi tuyakemee kama alivyofanya Nabii Lut(a.

Soma Zaidi...
Kazi alizokuwa akizifanya Mtume Muhammad s.a.w kabla ya utume.

Historia na sifa ya Mtume Muhammad s.a.w , sehemu ya 14. Hapa utajifunza kuhusu kazi alizozifanya Mtume s.a.w Enzo za ujana wake kabla ya utume.

Soma Zaidi...