Huduma za msingi kwa mama mjamzito na mtoto.


image


Posti hii inahusu zaidi huduma muhimu anazopaswa kupewa mama mjamzito wakati akiwa na mimba, wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua yaani ndani ya masaa ishirini na manne, tunajua wazi kuwa Mama akiwa mjamzito anaweza kupata matatizo mbalimbali kwa hiyo anapaswa kupewa huduma muhimu kama ifuatavyo.


Huduma za msingi kwa mama mjamzito na mtoto.

1. Uzazi wa mpango.

Hivi ni huduma ya msingi kabisa ambayo Mama anapaswa kujua kabisa namba ya watoto anaowahitaji na ni namna gani wanapaswa kuachana kwa miaka, hali huu umsaidia Mama kupumzika kutoka kwenye nzao moja kwenda nyingine na kuwasaidia watoto kupata mda mzuri wa kukua, kupendwa, kupata malezi ya kutosha kwa mda mwafaka na kupata elimu ya kutosha. Kwa hiyo Mama anapaswa kuchagua njia ya uzazi wa mpango ambayo ni ya maana na faida kwake.

 

2. Usafi wakati wa ujauzito , kujifungua na wakati wa malezi ya mtoto.

Mama anapaswa kuwa msafi mda wote anapokuwa na mimba na kuandaa vifaa vyake kwa hali ya usafi wa hali ya juu kwa kufanya hivyo anazuia maambukizi bambayo yanaweza kuleta maendeleo kwa mtoto na kwa Mama mwenyewe, hali huu utokea kwa akina mama hasa wale wanojifungulia vijijini utumia viwembe vyenye kutu kukata kitovu na hatimaye kusababisha maambukizi kwa mtoto na hatimaye madhara makubwa yanayoweza kujitokeza. Kwa hiyo tunapaswa kuwahimiza akina  mama kujiandaa na kuwa na vifaa vizuri wakati wa kujifungua.

 

3. Kuzuia maambukizi kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto.

Hivi ni njia ambayo umsaidia mtoto kutopata maambukizi ya HIV au AIDS na kaswende kwa hiyo Mama anapoanza mahudhurio ya kwanza anapaswa kuja na mme wake ili kupima Maambukizi na kabla ya Mama kujifungua anapaswa kuja kupima maambukizi ili kama wazazi wana Maambukizi waweze kumkinga mtoto ili hasipatwe na wakati wa kujifungua kuwa makini ili kumzuia mtoto hasipatwe na Maambukizi, na pia huwasaidia wazazi wote way kujua afya zao endapo walikutwa na Maambukizi wanaanza dawa mara moja.

 

4. Pia wakati wa  ujauzito mama anapaswa kukingwa na Dalili za hatari.

Hizi ni Dalili ambazo ujionyesha kwa mama wakati akiwa na mimba na zisipotibiwa au kushughulikiwa mapema zinaweza kufanya mimba kutoka , Dalili hizo ni pamoja na kuvimba miguu kwa mama, kutokwa damu ukeni na uchafu ukeni, mtoto kushindwa kucheza akiwa tumboni, maumivu makali ya kichwa kwa mama mjamzito, Mama akisikia Dalili kama hizi anapaswa kuwahi mapema hospitali kwa ajili ya huduma zaidi, kwa hiyo mama anapaswa kujua wazi dalili za hatari na kuweza kuepukakana nazo au kwenda hospitali mara moja.

 

5. Kumtunza mama na Mtoto, baada ya Mama kumaliza kujifungua,

Hii ni huduma ambayo utolewa kwa Mama na mtoto ndani ya Masaa ishirini na nne, katika kipindi hiki Mama na mtoto upewa nafasi ya kupumzika ili kuweza kuangalia maendeleo yao au kuangalia kama kuna kitu chochote kinachoweza kubadilika lakini elimu utolewa kwa Mama namna ya kumlisha na kumtunza mtoto na chanjo mbalimbali utolewa kwa mtoto ili kumkinga na Magonjwa nyemelezi kwa mtoto, kama mtoto na Mama wanaendelea vizuri wanaweza kuruhusiwa kwenda nyumbani.

 

6. Kwa hiyo tunajua wazi ,Mama akiwa na mimba kuna mabadiliko mengi ambayo utokea kwa hiyo tunapaswa kuwapa kipau mbele na kuwasikiliza wajawazito na kuwapa chakula na dawa zinazofaa kwa hiyo tuachane na mila potofu na imani zisizofaa kwa akina Mama wajawazito.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    2 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    3 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    4 Download App zetu hapa ujifunze zaidi    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Upungufu wa vyakula vya madini
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa vyakula vya madini Soma Zaidi...

image Dalili za saratani ya mapafu
Saratani ya Mapafu ni aina ya Kansa inayoanzia kwenye mapafu. Mapafu yako ni viungo viwili vya sponji kwenye kifua chako ambavyo huchukua oksijeni unapovuta na kutoa kaboni dioksidi unapotoa nje. Soma Zaidi...

image Zijue hasara za magonjwa ya ngono
Posti hii inahusu zaidi hasara za magonjwa ya ngono, ni magonjwa yanayoambukizwa kwa kujamiiana bila kutumia kinga. Soma Zaidi...

image Huduma ya Kwanza kwa mtu aloanguka kifafa
Somo hili linakwenda kukueleza jinsi ya kumfanyia huduma ya Kwanza kwa mtu aloanguka kifafa Soma Zaidi...

image Dalili za mtu Mwenye tatizo la mkojo kushindwa kutoka kwenye kibofu Cha mkojo
Post hii inahusu zaidi dalili za mtu Mwenye tatizo la mkojo kushindwa kutoka kwenye kibofu Cha mkojo.ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye tatizo la mkojo kushindwa kutoka kwenye kibofu Cha mkojo. Soma Zaidi...

image Dalili za PID
Posti hii inahusu zaidi dalili za PID maana yake ni maambukizi kwenye pelvic kwa kitaalamu huitwa pelvic infection disease, ni ugonjwa unaoshambulia sana wanawake na wasichana Soma Zaidi...

image Mbinu za kupunguza Magonjwa ya kuambukiza.
Posti hii inahusu zaidi mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kupunguza kiwango cha kuwepo kwa magonjwa ya kuambukiza, kwa hiyo zifuatazo ni mbinu ambazo zinapaswa kutumika ili kupunguza kiwango cha magonjwa ya kuambukiza. Soma Zaidi...

image Namna ya kuongeza na mjamzito ili kupata taarifa zake na kutoa msaada
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuongea na Mama mjamzito ili kuweza kugundua tatizo lake na kutoa msaada pale penye uhitaji. Soma Zaidi...

image Dalili za upotevu wa kusikia
posti hii inazungumzia kuhusiana na Upotevu wa kusikia unaotokea hatua kwa hatua kadri umri unavyozeeka (presbycusis) ni jambo la kawaida. T Kwa wale walio na umri wa zaidi ya miaka 75, idadi ya watu walio na  upotezaji wa kusikia inakaribia 1 kati ya 2. Soma Zaidi...

image Huduma kwa wanaopata hedhi zaidi ya mara moja kwa mwezi
Posti hii inahusu zaidi huduma kwa wanaoingia kwenye siku zao zaidi ya mara moja kwa mwezi. Soma Zaidi...