picha

Huduma za msingi kwa mama mjamzito na mtoto.

Posti hii inahusu zaidi huduma muhimu anazopaswa kupewa mama mjamzito wakati akiwa na mimba, wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua yaani ndani ya masaa ishirini na manne, tunajua wazi kuwa Mama akiwa mjamzito anaweza kupata matatizo mbalimbali kwa h

Huduma za msingi kwa mama mjamzito na mtoto.

1. Uzazi wa mpango.

Hivi ni huduma ya msingi kabisa ambayo Mama anapaswa kujua kabisa namba ya watoto anaowahitaji na ni namna gani wanapaswa kuachana kwa miaka, hali huu umsaidia Mama kupumzika kutoka kwenye nzao moja kwenda nyingine na kuwasaidia watoto kupata mda mzuri wa kukua, kupendwa, kupata malezi ya kutosha kwa mda mwafaka na kupata elimu ya kutosha. Kwa hiyo Mama anapaswa kuchagua njia ya uzazi wa mpango ambayo ni ya maana na faida kwake.

 

2. Usafi wakati wa ujauzito , kujifungua na wakati wa malezi ya mtoto.

Mama anapaswa kuwa msafi mda wote anapokuwa na mimba na kuandaa vifaa vyake kwa hali ya usafi wa hali ya juu kwa kufanya hivyo anazuia maambukizi bambayo yanaweza kuleta maendeleo kwa mtoto na kwa Mama mwenyewe, hali huu utokea kwa akina mama hasa wale wanojifungulia vijijini utumia viwembe vyenye kutu kukata kitovu na hatimaye kusababisha maambukizi kwa mtoto na hatimaye madhara makubwa yanayoweza kujitokeza. Kwa hiyo tunapaswa kuwahimiza akina  mama kujiandaa na kuwa na vifaa vizuri wakati wa kujifungua.

 

3. Kuzuia maambukizi kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto.

Hivi ni njia ambayo umsaidia mtoto kutopata maambukizi ya HIV au AIDS na kaswende kwa hiyo Mama anapoanza mahudhurio ya kwanza anapaswa kuja na mme wake ili kupima Maambukizi na kabla ya Mama kujifungua anapaswa kuja kupima maambukizi ili kama wazazi wana Maambukizi waweze kumkinga mtoto ili hasipatwe na wakati wa kujifungua kuwa makini ili kumzuia mtoto hasipatwe na Maambukizi, na pia huwasaidia wazazi wote way kujua afya zao endapo walikutwa na Maambukizi wanaanza dawa mara moja.

 

4. Pia wakati wa  ujauzito mama anapaswa kukingwa na Dalili za hatari.

Hizi ni Dalili ambazo ujionyesha kwa mama wakati akiwa na mimba na zisipotibiwa au kushughulikiwa mapema zinaweza kufanya mimba kutoka , Dalili hizo ni pamoja na kuvimba miguu kwa mama, kutokwa damu ukeni na uchafu ukeni, mtoto kushindwa kucheza akiwa tumboni, maumivu makali ya kichwa kwa mama mjamzito, Mama akisikia Dalili kama hizi anapaswa kuwahi mapema hospitali kwa ajili ya huduma zaidi, kwa hiyo mama anapaswa kujua wazi dalili za hatari na kuweza kuepukakana nazo au kwenda hospitali mara moja.

 

5. Kumtunza mama na Mtoto, baada ya Mama kumaliza kujifungua,

Hii ni huduma ambayo utolewa kwa Mama na mtoto ndani ya Masaa ishirini na nne, katika kipindi hiki Mama na mtoto upewa nafasi ya kupumzika ili kuweza kuangalia maendeleo yao au kuangalia kama kuna kitu chochote kinachoweza kubadilika lakini elimu utolewa kwa Mama namna ya kumlisha na kumtunza mtoto na chanjo mbalimbali utolewa kwa mtoto ili kumkinga na Magonjwa nyemelezi kwa mtoto, kama mtoto na Mama wanaendelea vizuri wanaweza kuruhusiwa kwenda nyumbani.

 

6. Kwa hiyo tunajua wazi ,Mama akiwa na mimba kuna mabadiliko mengi ambayo utokea kwa hiyo tunapaswa kuwapa kipau mbele na kuwasikiliza wajawazito na kuwapa chakula na dawa zinazofaa kwa hiyo tuachane na mila potofu na imani zisizofaa kwa akina Mama wajawazito.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2022/01/10/Monday - 10:32:26 pm Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 2611

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 web hosting    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 ai web app    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Sababu za Mayai kushindwa kuzalishwa kwa mwanamke

Posti hii inahusu zaidi sababu za kushindwa kuzalishwa mayai kwa mwanamke, ni tatizo ambalo utokea kwa mwanamke ambapo mwanamke anashindwa kuzalisha mayai.

Soma Zaidi...
Mama mjamzito anapo hisi uchungu je mtoto huendelea kucheza tumboni?

Swali langi ni hiliMama mjamzito anapo hisi uchungu je mtoto huendelea kucheza tumboni?

Soma Zaidi...
Umuhimu wa kumpeleka mtoto kliniki

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kumpeleka mtoto kliniki, kliniki nisehemu ambayo mtoto hupelekwa Ili kujua maendeleo ya mtoto akiwa chini ya umri wa miaka mitano

Soma Zaidi...
Ujue Ute kwenye uke

Post hii inahusu zaidi Ute ambao umo kwenye uke, Ute huu utofautiana kulingana na hali ya mama aliyonayo, kama mama ana mimba uke utakuwa tofauti na yule ambaye hana mimba au kama Ute una una magonjwa na hivyo utakuwa tofauti.

Soma Zaidi...
Faida za uzazi wa mpango kwa watoto.

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa uzazi wa mpango kwa watoto, sio akina Mama peke yao wanaofaidika na uzazi wa mpango vile vile na watoto wanafaidika na uzazi wa mpango kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Faida na hasara za Kufunga kizazi kwa Wanaume

Posti hii inazungumzia Faida, hasara, na madhara ya Kufunga kizazi kwa Wanaume.

Soma Zaidi...
Mambo ya kuzingatia kwa mtoto mara tu anapozaliwa

Posti hii inahusu zaidi mambo ya kuzingatia kwa mtoto pindi anapozaliwa,tunajua wazi kuwa mtoto anapoanza kutokeza kichwa tu ndio mwanzo wa kuanza kumtunza mtoto na kuhakikisha anafanyiwa huduma zote za muhimu na zinazohitajika.

Soma Zaidi...
Uume ukiwa unaingia na ukiwa ndani nahic maumivu Kama uke unawaka Moto tafadhali nishauri

Je unasumbuliwa namaumivi wakati wa nlishiriki tendo la ndoa ama baada. Huwenda post hii ikakusaidia.

Soma Zaidi...
Aina za uvimbe kwenye kizazi.

Posti hii inahusu zaidi aina mbalimbali za uvimbe kwenye kizazi, uvimbe unatokea kwenye kizazi ila utofautiana kulingana na sehemu ambazo uvimbe huo umepata.

Soma Zaidi...