picha

Huduma za msingi kwa mama mjamzito na mtoto.

Posti hii inahusu zaidi huduma muhimu anazopaswa kupewa mama mjamzito wakati akiwa na mimba, wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua yaani ndani ya masaa ishirini na manne, tunajua wazi kuwa Mama akiwa mjamzito anaweza kupata matatizo mbalimbali kwa h

Huduma za msingi kwa mama mjamzito na mtoto.

1. Uzazi wa mpango.

Hivi ni huduma ya msingi kabisa ambayo Mama anapaswa kujua kabisa namba ya watoto anaowahitaji na ni namna gani wanapaswa kuachana kwa miaka, hali huu umsaidia Mama kupumzika kutoka kwenye nzao moja kwenda nyingine na kuwasaidia watoto kupata mda mzuri wa kukua, kupendwa, kupata malezi ya kutosha kwa mda mwafaka na kupata elimu ya kutosha. Kwa hiyo Mama anapaswa kuchagua njia ya uzazi wa mpango ambayo ni ya maana na faida kwake.

 

2. Usafi wakati wa ujauzito , kujifungua na wakati wa malezi ya mtoto.

Mama anapaswa kuwa msafi mda wote anapokuwa na mimba na kuandaa vifaa vyake kwa hali ya usafi wa hali ya juu kwa kufanya hivyo anazuia maambukizi bambayo yanaweza kuleta maendeleo kwa mtoto na kwa Mama mwenyewe, hali huu utokea kwa akina mama hasa wale wanojifungulia vijijini utumia viwembe vyenye kutu kukata kitovu na hatimaye kusababisha maambukizi kwa mtoto na hatimaye madhara makubwa yanayoweza kujitokeza. Kwa hiyo tunapaswa kuwahimiza akina  mama kujiandaa na kuwa na vifaa vizuri wakati wa kujifungua.

 

3. Kuzuia maambukizi kutoka kwa Mama kwenda kwa mtoto.

Hivi ni njia ambayo umsaidia mtoto kutopata maambukizi ya HIV au AIDS na kaswende kwa hiyo Mama anapoanza mahudhurio ya kwanza anapaswa kuja na mme wake ili kupima Maambukizi na kabla ya Mama kujifungua anapaswa kuja kupima maambukizi ili kama wazazi wana Maambukizi waweze kumkinga mtoto ili hasipatwe na wakati wa kujifungua kuwa makini ili kumzuia mtoto hasipatwe na Maambukizi, na pia huwasaidia wazazi wote way kujua afya zao endapo walikutwa na Maambukizi wanaanza dawa mara moja.

 

4. Pia wakati wa  ujauzito mama anapaswa kukingwa na Dalili za hatari.

Hizi ni Dalili ambazo ujionyesha kwa mama wakati akiwa na mimba na zisipotibiwa au kushughulikiwa mapema zinaweza kufanya mimba kutoka , Dalili hizo ni pamoja na kuvimba miguu kwa mama, kutokwa damu ukeni na uchafu ukeni, mtoto kushindwa kucheza akiwa tumboni, maumivu makali ya kichwa kwa mama mjamzito, Mama akisikia Dalili kama hizi anapaswa kuwahi mapema hospitali kwa ajili ya huduma zaidi, kwa hiyo mama anapaswa kujua wazi dalili za hatari na kuweza kuepukakana nazo au kwenda hospitali mara moja.

 

5. Kumtunza mama na Mtoto, baada ya Mama kumaliza kujifungua,

Hii ni huduma ambayo utolewa kwa Mama na mtoto ndani ya Masaa ishirini na nne, katika kipindi hiki Mama na mtoto upewa nafasi ya kupumzika ili kuweza kuangalia maendeleo yao au kuangalia kama kuna kitu chochote kinachoweza kubadilika lakini elimu utolewa kwa Mama namna ya kumlisha na kumtunza mtoto na chanjo mbalimbali utolewa kwa mtoto ili kumkinga na Magonjwa nyemelezi kwa mtoto, kama mtoto na Mama wanaendelea vizuri wanaweza kuruhusiwa kwenda nyumbani.

 

6. Kwa hiyo tunajua wazi ,Mama akiwa na mimba kuna mabadiliko mengi ambayo utokea kwa hiyo tunapaswa kuwapa kipau mbele na kuwasikiliza wajawazito na kuwapa chakula na dawa zinazofaa kwa hiyo tuachane na mila potofu na imani zisizofaa kwa akina Mama wajawazito.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 2375

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Dalili za kuvimba kwa ovari.

  Posti hii inazungumzia kuhusiana na kuvimba kwa ovari kunakosababishwa na maambukizo ya bakteria na kawaida huweza kusababishwa na magonjwa sugu katika Maambukizi ya mfumo wa Uzazi wa mwanamke.

Soma Zaidi...
Maandalizi ya mama mjamzito kwa ajili ya kujifungulia.

Postii inafundisha maandalizi ya mama kwa ajili ya kujifungulia hii Ni muhimu Sana kwa wale ambao hawajawahi kujingua Ni mara yao ya kwanza wanatakiwa kujua na kuelewa vifaa na mahitaji kujifungulia na kwa wale wanaohudhuria clinic huwa wanafundisha.

Soma Zaidi...
Dalili za Ujauzito mchanga Siku Saba Baada ya Ovulation

Unaweza kujiuliza ikiwa inawezekana kupata dalili za ujauzito mchanga kama siku 7 baada ya kudondoshwa kwa yai (DPO yaani Days Past Ovulation).

Soma Zaidi...
Je kukosa hedhi kwa mwanmke anayenyonyesha ni dalili ya mimba

Kipimo cha mimba cha mkojo hakiwezi kyonyesha mimva changa sana. Hivyo kama ni mimba baada ya wikibpima tena itaweza kuonekana. Dalili hizobulizotaja pekee haziashirii mimba tu huwenda ni homoni zimebadilika kidogo, ama una uti.

Soma Zaidi...
Kutoka kwa mimba, sababu za kutoka kwa mimba, dalili za kutoka mimba na kuzuia mimba kuoka

Mimba inapotoka ina dalili, na zipo sababu kadhaa za kutoka kwa mimba. Je utazuiaje mimba kutoka. Soma makala hii

Soma Zaidi...
Njia za kufanya ili kuepukana na tatizo la kutokwa na majimaji kwenye uume

Posti hii inahusu zaidi njia ambazo mtu anapaswa kutumia ili kuweza kupunguza tatizo hili kisiweze kutokea na pia kama jamii ikishirikiana kwa pamoja tunaweza kuepusha kwa kufanya yafuatayo.

Soma Zaidi...
Imani potofu kwa mwanamke mwenye mimba

Posti hii inahusu zaidi imani potofu kwa mwanamke mwenye mimba, ni Imani ambazo zimekuwepo kwenye jamii kuhusu wanawake wenye mimba.

Soma Zaidi...
siku za hatari

Hizi ni siku za hatari kupata ujauzito.Siku hizi ndio siku za kupata mimba kwa urahisi

Soma Zaidi...
Je siku ya kwanza kabisa ya ovulation mimba inakuwa ni uhakika kupata mimba?

Watu wengi wanadhania kuwa kufanya tendo la ndoa katika siku hatari ni lazima kuwa utapata ujauzito. Hili sio sahihi kabisa. Post hii itakwenda kuangalia jambo hili zaidi.

Soma Zaidi...
Unakuta siku imefka ya hedhi kabla haijaanza kutoka hedhi yanatoka maji meupe clean kabisa hii Ina naamisha nini?

Kutoka na majimaji ka uchache kwa mwanamke sio jambo lakishangaa sana. Damu hii inawezapiabkikbatana damu na maumivu makali.

Soma Zaidi...