Uandishi wa hadithi wakati wa tabiina (wafuasi wa maswahaba)
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Uandishi wa Hadith Wakati wa Tabi’ina (wafuasi wa maswahaba),
(101 A.H – 200 A.H).
- Ni karne ya pili ambapo wanazuoni wengi walijitokeza waliojizatiti katika kazi ya ukusanyaji wa Hadith kutoka vituo mbali mbali vya elimu.
- Vituo mashuhuri vya elimu kipindi hicho vilikuwa; Madinah, Makkah, Baghdad, Basra, Khurasan na Kufa.
- Pia ni kipindi hiki ambapo walitokea maimamu wanne mashuhuri wa Fiqh ambao ni;
- Imamu Abu Hanifa Al-Nu’man bin Thabit (80 – 150A.H).
- Mwanachuoni wa Qur’an na Hadith katika mji wa Kufa, Iraq.
- Alitoa Fat’wa za kifiq kwa kutumia Qur’an, Hadith na Ijmaa.
- Hakuandika kitabu chochote.
- Imam Malik bin Anas (95 – 179 A.H).
- Mwanachuoni mcha-Mungu wa mji wa Madinah.
- Aliandika kitabu mashuhuri cha Hadith kiitwacho, “Al-Muwatta” kilichotegemewa na umma wa waislamu katika ibada maalum tu.
- Alifutu mas’ala ya Uislamu kwa mujibu wa Qur’an na Sunnah tu.
- Imam Muhammad bin Idris Al-Shafii (150 – 204 A.H).
- Mwanachuoni mkubwa wa sheria za Kiislamu aliyezaliwa Gaza, Palestina.
- Imam Malik bin Anas ni miongoni mwa walimu wake.
- Alitoa fat’wa kwa mujibu wa Qur’an, Hadith na Ijmaa (na Qiyaas pia).
- Hakuandika kitabu chochote cha Hadith.
- Imam Ahmad bin Muhammad bin Hambal (164 – 241 A.H).
- Mwanachuoni mkubwa wa Fiqh na elimu ya Hadith aliyezaliwa mji wa
Baghdad, Iraq.
- Imam Shafii alikuwa mwalimu wake.
- Imam Ahmad alitoa fat’wa tofauti na mwalimu wake, Imam Shafii lakini
waliheshimiana sana.
- Aliandika kitabu cha Hadith kiitwacho, “Isnad ya Ibn Hambal”
kilichokusanya zaidi ya Hadith 30,000.
- Pamoja na jitihada kubwa za ukusanyaji wa Hadith, wanazuoni hawa waliandika vitabu mashuhuri viwili tu;
- Al-Muwatta cha Imam Malik bin Anas.
- Isnad ya Ibn Hambal (Musnad Ahmad) cha Imam Ahmad bin Hambal.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Dua za Mitume na Manabii π2 ai web app π3 Madrasa kiganjani π4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π5 Kitau cha Fiqh π6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
jamii somo la 35
Hutekeleza ahadi zao wanapoahidiana na wanaadamu wenziwao maadamu ni katika mipaka ya Allah (s.
Soma Zaidi...Kushika mwenendo wa kati "Na ushike mwenendo wa katiβ¦." (31:19)
Mwenendo wa kati ni mwenendo ulioepukana na kibri na majivuno kwa upande mmoja na ulioepukkana na udhalili na unyonge kwa upande mwingine.
Soma Zaidi...