Uandishi wa hadithi wakati wa tabiina (wafuasi wa maswahaba)
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Uandishi wa Hadith Wakati wa Tabi’ina (wafuasi wa maswahaba),
(101 A.H – 200 A.H).
- Ni karne ya pili ambapo wanazuoni wengi walijitokeza waliojizatiti katika kazi ya ukusanyaji wa Hadith kutoka vituo mbali mbali vya elimu.
- Vituo mashuhuri vya elimu kipindi hicho vilikuwa; Madinah, Makkah, Baghdad, Basra, Khurasan na Kufa.
- Pia ni kipindi hiki ambapo walitokea maimamu wanne mashuhuri wa Fiqh ambao ni;
- Imamu Abu Hanifa Al-Nu’man bin Thabit (80 – 150A.H).
- Mwanachuoni wa Qur’an na Hadith katika mji wa Kufa, Iraq.
- Alitoa Fat’wa za kifiq kwa kutumia Qur’an, Hadith na Ijmaa.
- Hakuandika kitabu chochote.
- Imam Malik bin Anas (95 – 179 A.H).
- Mwanachuoni mcha-Mungu wa mji wa Madinah.
- Aliandika kitabu mashuhuri cha Hadith kiitwacho, “Al-Muwatta” kilichotegemewa na umma wa waislamu katika ibada maalum tu.
- Alifutu mas’ala ya Uislamu kwa mujibu wa Qur’an na Sunnah tu.
- Imam Muhammad bin Idris Al-Shafii (150 – 204 A.H).
- Mwanachuoni mkubwa wa sheria za Kiislamu aliyezaliwa Gaza, Palestina.
- Imam Malik bin Anas ni miongoni mwa walimu wake.
- Alitoa fat’wa kwa mujibu wa Qur’an, Hadith na Ijmaa (na Qiyaas pia).
- Hakuandika kitabu chochote cha Hadith.
- Imam Ahmad bin Muhammad bin Hambal (164 – 241 A.H).
- Mwanachuoni mkubwa wa Fiqh na elimu ya Hadith aliyezaliwa mji wa
Baghdad, Iraq.
- Imam Shafii alikuwa mwalimu wake.
- Imam Ahmad alitoa fat’wa tofauti na mwalimu wake, Imam Shafii lakini
waliheshimiana sana.
- Aliandika kitabu cha Hadith kiitwacho, “Isnad ya Ibn Hambal”
kilichokusanya zaidi ya Hadith 30,000.
- Pamoja na jitihada kubwa za ukusanyaji wa Hadith, wanazuoni hawa waliandika vitabu mashuhuri viwili tu;
- Al-Muwatta cha Imam Malik bin Anas.
- Isnad ya Ibn Hambal (Musnad Ahmad) cha Imam Ahmad bin Hambal.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 ai web app 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 Dua za Mitume na Manabii 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Kitabu cha Afya
Post zinazofanana:
Iv shekh haifai kufunga kwa nia utimize jambo labda kuna kitu unakitaka kwhy unaamua kugunga ili kama kuzidisha maombi kwa mungu jambo lifanikiwe
Ibada yavfubga ni katika ibadavanbazo hufanya nakaribia dini zote kubwa. Ibada hii imekuwaikikabiliw na naswlo mengi.
Soma Zaidi...Matukio ya kihistoria katika masiku 10 ya Dhul Hija -Mfunguo tatu
Haya ni matukio ya kihistoria yanayoamiika kutokea ndani ya masiku 10 ya Mfunguo tatu.
Soma Zaidi...