Uandishi wa hadithi wakati wa tabiina (wafuasi wa maswahaba)


image


Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)


Uandishi wa Hadith Wakati wa Tabi’ina (wafuasi wa maswahaba), 

      (101 A.H – 200 A.H).

  • Ni karne ya pili ambapo wanazuoni wengi walijitokeza waliojizatiti katika kazi ya ukusanyaji wa Hadith kutoka vituo mbali mbali vya elimu.

 

  • Vituo mashuhuri vya elimu kipindi hicho vilikuwa; Madinah, Makkah, Baghdad, Basra, Khurasan na Kufa.

 

  • Pia ni kipindi hiki ambapo walitokea maimamu wanne mashuhuri wa Fiqh ambao ni;
  1.   Imamu Abu Hanifa Al-Nu’man bin Thabit (80 – 150A.H).

        -  Mwanachuoni wa Qur’an na Hadith katika mji wa Kufa, Iraq.

        -  Alitoa Fat’wa za kifiq kwa kutumia Qur’an, Hadith na Ijmaa.

        -  Hakuandika kitabu chochote.

 

  1.   Imam Malik bin Anas (95 – 179 A.H).

          -  Mwanachuoni mcha-Mungu wa mji wa Madinah.

          -    Aliandika kitabu mashuhuri cha Hadith kiitwacho, “Al-Muwatta”   kilichotegemewa na umma wa waislamu katika ibada maalum tu.

-  Alifutu mas’ala ya Uislamu kwa mujibu wa Qur’an na Sunnah tu.

   

  1.   Imam Muhammad bin Idris Al-Shafii (150 – 204 A.H).

-  Mwanachuoni mkubwa wa sheria za Kiislamu aliyezaliwa Gaza, Palestina.

-  Imam Malik bin Anas ni miongoni mwa walimu wake.

-  Alitoa fat’wa kwa mujibu wa Qur’an,  Hadith na Ijmaa (na Qiyaas pia).

-  Hakuandika kitabu chochote cha Hadith. 

 

  1.   Imam Ahmad bin Muhammad bin Hambal (164 – 241 A.H).

-  Mwanachuoni mkubwa wa Fiqh na elimu ya Hadith aliyezaliwa mji wa

    Baghdad, Iraq.

 -  Imam Shafii alikuwa mwalimu wake.

 -  Imam Ahmad alitoa fat’wa tofauti na mwalimu wake, Imam Shafii lakini

     waliheshimiana sana.

 -  Aliandika kitabu cha Hadith kiitwacho, “Isnad ya Ibn Hambal”

     kilichokusanya zaidi ya Hadith 30,000.    

 

  • Pamoja na jitihada kubwa za ukusanyaji wa Hadith, wanazuoni hawa waliandika vitabu mashuhuri viwili tu;
  1. Al-Muwatta cha Imam Malik bin Anas.
  2. Isnad ya Ibn Hambal (Musnad Ahmad) cha Imam Ahmad bin Hambal.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    2 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    3 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    4 Download App zetu hapa ujifunze zaidi    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Maadui wakubwa wa dola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Taasisi za kisiasa za msingi alizotumia mtume (s.a.w) katika kuanzisha dola ya kiislamu madinah
Dola ya kiislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Sababu za Quran kuwa mwongozo sahihi wa maisha ya mwanadamu
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Maana ya shahada
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kuamini mitume wa mwenyezi Mungu
Nguzo za Imani (EDK form 2:. Dhana ya elimu ya uislamu Soma Zaidi...

image Kwanini funga imefaradhishwa mwezi wa ramadhani
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kumuamini mwenyezi Mungu (S.W)
Nguzo za imani (EDK form 2: elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Uandishi wa hadithi wakati wa maswahaba wa mtume (s.a.w)
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kina Cha uovu wa shirk
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Maswali juu ya mtazamo wa uislamu kuhusu dini
Mtazamo wa uislamu kuhusu dini (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...