image

HISTORIA YA UANDISHI WA HADITHI

Historia fupi ya uandishi wa Hadith za Mtume (s.

HISTORIA YA UANDISHI WA HADITHI

Historia fupi ya uandishi wa Hadith za Mtume (s.a.w)
Tofauti na Qur-an, ambayo iliandikwa mara tu baada ya kushushwa chini ya malekezo na usimamizi wa Mtume (s.a.w) mwenyewe, Hadith za Mtume (s.a.w) ambamo ndani yake ndio tunapata sunnah yake, zimeandikwa na watu kulingana na walivyomuona, au walivyomsikia. Historia ya uandishi wa Hadith za Mtume (s.a.w) katika vitabu vya Hadith , imechukua takriban muda wa karne tatu. Kwa kurahisisha tutaigawa historia ya kuhifadhiwa Hadith katika maandishi katika hatua nne zifuatazo:  - Wakati wa Mtume (s.a.w).
- Wakati wa Maswahaba wa Mtume (s.a.w).
- Wakati wa Tabi'iina.
- Wakati wa Tabii Tabi'iina.

Wakati wa Mtume (s.a.w)
Wakati wa Mtume (s.a.w), hapakuwa na uandishi mkubwa wa Hadith kwa sababu:

Kwanza, Mtume mwenyewe alikuwepo, hivyo kilichokuwa muhimu kwa Masahaba ni kufuata mafundisho ya Mtume(s.a.w) na kuigiza mwenendo wake,kila walipokwama katika utendaji au kila walipotatizwa na tatizo lolote, walimwendea Mtume(s.a.w) na aliwakwamua au kuwatatulia tatizo lolote walilokuwa nalo.

Pili, Masahaba katika kipindi hiki walijishughulisha sana na kuandika, kusoma na kuhifadhi Qur-an moyoni na kuitekeleza katika maisha yao ya kila siku.

Tatu, kwa kuwa mwanzoni Mtume (s.a.w) aliwakataza Masahaba wake kuandika Hadith, walizoea kutoandika Hadith hata wakati waliporuhusiwa kuandika na walipendelea kutoandika kuliko kuandika Hadith.

Nne, katika wakati huu wa Mtume (s.a.w) Masahaba walishughulika sana katika harakati za kuuhami Uislamu ambao ulikuwa umesongwa sana na maadui wake ambao walipania sana kumuua Mtume, Uislamu na Waislamu.

Kutokana na sababu hizi nne na nyinginezo, uandishi wa Hadith haukupewa nafasi nzito katika kipindi hiki cha Mtume (s.a.w). Hivyo, Hadith nyingi zilibakia katika matendo na vifua vya Masahaba. Masahaba waliokuwa karibu sana na Mtume (s.a.w) kwa muda mrefu wa maisha yao, walihifadhi Hadith nyingi zaidi kuliko wale waliokaa mbali na Mtume (s.a.w). 

Miongoni mwa Masahaba waliofahamika kuwa mashuhuri kwa kuhifadhi Hadith nyingi ni Abu Hurairah, bibi Aysha (mkewe Mtume (s.a.w)) 'Abdullah bin 'Umar, 'Abdullah bin 'Abbas, na Abdullah bin 'Amr na Abdallah bin Masu'ud (r.a)


                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 251


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

quran na sayansi
Soma Zaidi...

Namna ya kutufu, na masharti ya mwenye kutufu
3. Soma Zaidi...

Swala ya kupatwa kwa jua na mwezi na namna ya kuiswali
11. Soma Zaidi...

MAANA YA HADITHI SUNNAH
Maana ya SunnahKilugha: Neno sunnah katika lugha ya Kiarabu lina maana ya mwenendo au mila. Soma Zaidi...

kusai yaani kukimbia kati ya mlima swafa na marwa mara saba
4. Soma Zaidi...

Hadithi aliyoisimulia Kijakazi kwa sultan
Soma Zaidi...

Historia ya kuhifadhiwa na kuandikwa kwa quran toka wakati wa Mtume (s.a.w)
Soma Zaidi...

MAKATAZO DHIDI YA KUISAHAU QURAN BAADA YA KUIHIFADHI
Soma Zaidi...

Je mahari inashusha hadhi ya mwanamke?
Je, Mahari inashusha hadhi ya mwanamke? Soma Zaidi...

Kuamini Mwenyezi Mungu sio suala la Kibubusa au Kufuata Mkumbo
Kuamini Mwenyezi Mungu sio suala la Kibubusa au Kufuata Mkumbo. Soma Zaidi...

Muda wa kuhiji na mwenendo wa mwenye kuhiji
Soma Zaidi...

Hutuba ya ndoa wakati wa kuoa
Soma Zaidi...