Uandishi wa hadithi wakati wa tabii tabiina
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Uandishi wa Hadith Wakati wa Tabi’i Tabi’ina (wafuasi wa wafuasi wa
maswahaba, 201 – 300 A.H).
- Pamoja na uandishi wa Hadith katika karne ya pili, bado kulikuwa na hitajio kubwa la mafunzo ya hadith katika kuendeshea maisha ya kila siku.
- Uandishi wa Hadith karne ya tatu, ulihusika na ukusanyaji wa Hadith kuhusu nyanja zote za maisha ya jamii.
- Wanachuoni pamoja na kukusanya Hadith nyingi muda huo, walikuwa makini mno katika kuchambua usahihi wa Hadith kwa kuzingatia;
- Tabia na mwenendo wa kila msimulizi (mpokezi) wa Hadith hiyo.
- Usahihi wa Matin ya Hadith hiyo.
- Ni kipindi hiki wanazuoni sita walijitokeza waliokusanya na kuchambua kwa umakini mkubwa Hadith sahihi na kuziandika katika vitabu sita mashuhuri kama, “Sahihu Sitta” ambavyo ni;
- Sahihi Al-Bukhari.
- Ni kitabu cha Muhammad bin Ismail Abu Abdallah Al-Ju’fi – mashuhuri
kama Imam Bukhari wa mji wa Bukhara, Urusi (194 A.H/810 A.D – 256
A.H/870 A.D).
- Alikusanya Hadith 600,000 na kuhifadhi 200,000 na alihakiki na kuandika
Hadith 7,275 tu katika kitabu chake.
- Kitabu chake ndio namba moja kwa usahihi wa Hadith, mashuhuri kwa jina
la “Al-Jami’u Al-Sahihi” au “Sahihi Bukhari”.
- Sahihi Muslim.
- Ni kitabu cha Abu Husain Muslim bin Al-Hajjaj mashuhuri – Imam Muslim
wa mji wa Misabur, (202 A.H/818A.D – 261 A.H/875 A.D).
- Alikusanya Hadith 300,000 na alizohakiki na kuziandika katika kitabu chake
ni 9,200 tu.
- Kitabu chake ni namba mbili kwa usahihi wa Hadith, mashuhuri kwa jina la
“Sahihi Muslim”
- Sunan Abu Daud.
- Ni kitabu cha hadith cha Imam Abu Daud (203 – 275 A.H).
- Alikusanya Hadith 500,000 na alizohakiki na kuziandika ni 4,800 katika
kitabu chake kiitwacho, “Sunan Abi Daud”.
- Jami’u at-Tirmidh.
- Ni kitabu cha Hadith cha Abu Isa Muhammad bin Issa bin Sarwa bin
Shaddad, mashuhuri kama Imam At-Tirmidh (209 – 279 A.H).
- Aliandika kitabu cha Hadith mashuhuri kwa jina la, “Jami’u”.
- Sunnah (Sunan) Ibn Majah.
- Ni kitabu cha Hadith cha Muhammad bin Yazid – mashuhuri kwa jina la
Imam Ibn Majah (209 A.H – 295 A.H).
- Aliandika cha Hadith mashuhuri kama, “Sunanu Ibn Majah” au “Sunnah
Ibn Majah”.
- Sunnah (Sunan) An-Nasai.
- Ni kitabu cha Hadith cha Abu Abdur-Rahman Ahmad bin An-Nasai –
mashuhuri kwa jina la, Imam An-Nasai (214 – 303 A.H).
- Aliandika kitabu cha Hadith mashuhuri kama, “Sunan An-Nasai” au
“Sunnah An-Nasai”.
- Hadith za Bukhari na Muslim ndio daraja la kwanza kwa usahihi na za
Maimam Abu Daud, Tirmidh, Ibn Majah na An-Nasai ni daraja la pili kwa
usahihi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 web hosting 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
jamii somo la 35
Hutekeleza ahadi zao wanapoahidiana na wanaadamu wenziwao maadamu ni katika mipaka ya Allah (s.
Soma Zaidi...