picha

Uandishi wa hadithi wakati wa tabii tabiina

Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Uandishi wa Hadith Wakati wa Tabi’i Tabi’ina (wafuasi wa wafuasi wa   

       maswahaba, 201 – 300 A.H).

 

 

 

  1. Tabia na mwenendo wa kila msimulizi (mpokezi) wa Hadith hiyo.
  2. Usahihi wa Matin ya Hadith hiyo.

 

      -    Ni kipindi hiki wanazuoni sita walijitokeza waliokusanya na kuchambua kwa umakini mkubwa Hadith sahihi na kuziandika katika vitabu sita mashuhuri kama, “Sahihu Sitta” ambavyo ni;

 

  1.   Sahihi Al-Bukhari.

          -  Ni kitabu cha Muhammad bin Ismail Abu Abdallah Al-Ju’fi – mashuhuri  

              kama Imam Bukhari wa mji wa Bukhara, Urusi (194 A.H/810 A.D – 256

              A.H/870 A.D).

 

          -  Alikusanya Hadith 600,000 na kuhifadhi 200,000 na alihakiki na kuandika

              Hadith 7,275 tu katika kitabu chake. 

           

          -  Kitabu chake ndio namba moja kwa usahihi wa Hadith, mashuhuri kwa jina 

              la “Al-Jami’u Al-Sahihi” au “Sahihi Bukhari”. 

 

  1.   Sahihi Muslim.

-  Ni kitabu cha Abu Husain Muslim bin Al-Hajjaj mashuhuri – Imam Muslim 

    wa mji wa Misabur, (202 A.H/818A.D – 261 A.H/875 A.D).

 

          -  Alikusanya Hadith 300,000 na alizohakiki na kuziandika katika kitabu chake 

              ni 9,200 tu.

 

          -  Kitabu chake ni namba mbili kwa usahihi wa Hadith, mashuhuri kwa jina la 

            “Sahihi Muslim”

 

  1.   Sunan Abu Daud.

          -  Ni kitabu cha hadith cha Imam Abu Daud (203 – 275 A.H).

          -  Alikusanya Hadith 500,000 na alizohakiki na kuziandika ni 4,800 katika 

                                 kitabu chake kiitwacho, “Sunan Abi Daud”.    

 

  1.   Jami’u at-Tirmidh.

-  Ni kitabu cha Hadith cha Abu Isa Muhammad bin Issa bin Sarwa bin 

    Shaddad, mashuhuri kama Imam At-Tirmidh (209 – 279 A.H).

-  Aliandika kitabu cha Hadith mashuhuri kwa jina la, “Jami’u”.

 

  1.   Sunnah (Sunan) Ibn Majah.

-  Ni kitabu cha Hadith cha Muhammad bin Yazid – mashuhuri kwa jina la 

    Imam Ibn Majah (209 A.H – 295 A.H).

-  Aliandika cha Hadith mashuhuri kama, “Sunanu Ibn Majah” au “Sunnah 

    Ibn Majah”.

 

  1.   Sunnah (Sunan) An-Nasai.

-  Ni kitabu cha Hadith cha Abu Abdur-Rahman Ahmad bin An-Nasai – 

   mashuhuri kwa jina la, Imam An-Nasai (214 – 303 A.H). 

-  Aliandika kitabu cha Hadith mashuhuri kama, “Sunan An-Nasai” au 

   “Sunnah An-Nasai”.

 

        -  Hadith za Bukhari na Muslim ndio daraja la kwanza kwa usahihi na za 

            Maimam Abu Daud, Tirmidh, Ibn Majah na An-Nasai ni daraja la pili kwa 

                             usahihi.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Jifunze Main: Post File: Download PDF Views 2798

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Dua za Mitume na Manabii     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Husimamisha swala

Husimamisha swala katika maisha yao yote.

Soma Zaidi...
jamii somo la 26

(vii)Hufanya bias hara na Allah (s.

Soma Zaidi...