Uandishi wa hadithi wakati wa tabii tabiina
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Uandishi wa Hadith Wakati wa Tabi’i Tabi’ina (wafuasi wa wafuasi wa
maswahaba, 201 – 300 A.H).
- Pamoja na uandishi wa Hadith katika karne ya pili, bado kulikuwa na hitajio kubwa la mafunzo ya hadith katika kuendeshea maisha ya kila siku.
- Uandishi wa Hadith karne ya tatu, ulihusika na ukusanyaji wa Hadith kuhusu nyanja zote za maisha ya jamii.
- Wanachuoni pamoja na kukusanya Hadith nyingi muda huo, walikuwa makini mno katika kuchambua usahihi wa Hadith kwa kuzingatia;
- Tabia na mwenendo wa kila msimulizi (mpokezi) wa Hadith hiyo.
- Usahihi wa Matin ya Hadith hiyo.
- Ni kipindi hiki wanazuoni sita walijitokeza waliokusanya na kuchambua kwa umakini mkubwa Hadith sahihi na kuziandika katika vitabu sita mashuhuri kama, “Sahihu Sitta” ambavyo ni;
- Sahihi Al-Bukhari.
- Ni kitabu cha Muhammad bin Ismail Abu Abdallah Al-Ju’fi – mashuhuri
kama Imam Bukhari wa mji wa Bukhara, Urusi (194 A.H/810 A.D – 256
A.H/870 A.D).
- Alikusanya Hadith 600,000 na kuhifadhi 200,000 na alihakiki na kuandika
Hadith 7,275 tu katika kitabu chake.
- Kitabu chake ndio namba moja kwa usahihi wa Hadith, mashuhuri kwa jina
la “Al-Jami’u Al-Sahihi” au “Sahihi Bukhari”.
- Sahihi Muslim.
- Ni kitabu cha Abu Husain Muslim bin Al-Hajjaj mashuhuri – Imam Muslim
wa mji wa Misabur, (202 A.H/818A.D – 261 A.H/875 A.D).
- Alikusanya Hadith 300,000 na alizohakiki na kuziandika katika kitabu chake
ni 9,200 tu.
- Kitabu chake ni namba mbili kwa usahihi wa Hadith, mashuhuri kwa jina la
“Sahihi Muslim”
- Sunan Abu Daud.
- Ni kitabu cha hadith cha Imam Abu Daud (203 – 275 A.H).
- Alikusanya Hadith 500,000 na alizohakiki na kuziandika ni 4,800 katika
kitabu chake kiitwacho, “Sunan Abi Daud”.
- Jami’u at-Tirmidh.
- Ni kitabu cha Hadith cha Abu Isa Muhammad bin Issa bin Sarwa bin
Shaddad, mashuhuri kama Imam At-Tirmidh (209 – 279 A.H).
- Aliandika kitabu cha Hadith mashuhuri kwa jina la, “Jami’u”.
- Sunnah (Sunan) Ibn Majah.
- Ni kitabu cha Hadith cha Muhammad bin Yazid – mashuhuri kwa jina la
Imam Ibn Majah (209 A.H – 295 A.H).
- Aliandika cha Hadith mashuhuri kama, “Sunanu Ibn Majah” au “Sunnah
Ibn Majah”.
- Sunnah (Sunan) An-Nasai.
- Ni kitabu cha Hadith cha Abu Abdur-Rahman Ahmad bin An-Nasai –
mashuhuri kwa jina la, Imam An-Nasai (214 – 303 A.H).
- Aliandika kitabu cha Hadith mashuhuri kama, “Sunan An-Nasai” au
“Sunnah An-Nasai”.
- Hadith za Bukhari na Muslim ndio daraja la kwanza kwa usahihi na za
Maimam Abu Daud, Tirmidh, Ibn Majah na An-Nasai ni daraja la pili kwa
usahihi.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 web hosting 👉5 ai web app 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Nani Muadilifu na zipi sifa za mtu muadilifu kwenye uislamu
Uadilifu ni usimamizi wa ukweli na kutoa haki kwa kila anayestahiki kulingana na ukweli.
Soma Zaidi...Matukio ya kihistoria katika masiku 10 ya Dhul Hija -Mfunguo tatu
Haya ni matukio ya kihistoria yanayoamiika kutokea ndani ya masiku 10 ya Mfunguo tatu.
Soma Zaidi...