picha

Uandishi wa hadithi wakati wa tabii tabiina

Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Uandishi wa Hadith Wakati wa Tabi’i Tabi’ina (wafuasi wa wafuasi wa   

       maswahaba, 201 – 300 A.H).

 

 

 

  1. Tabia na mwenendo wa kila msimulizi (mpokezi) wa Hadith hiyo.
  2. Usahihi wa Matin ya Hadith hiyo.

 

      -    Ni kipindi hiki wanazuoni sita walijitokeza waliokusanya na kuchambua kwa umakini mkubwa Hadith sahihi na kuziandika katika vitabu sita mashuhuri kama, “Sahihu Sitta” ambavyo ni;

 

  1.   Sahihi Al-Bukhari.

          -  Ni kitabu cha Muhammad bin Ismail Abu Abdallah Al-Ju’fi – mashuhuri  

              kama Imam Bukhari wa mji wa Bukhara, Urusi (194 A.H/810 A.D – 256

              A.H/870 A.D).

 

          -  Alikusanya Hadith 600,000 na kuhifadhi 200,000 na alihakiki na kuandika

              Hadith 7,275 tu katika kitabu chake. 

           

          -  Kitabu chake ndio namba moja kwa usahihi wa Hadith, mashuhuri kwa jina 

              la “Al-Jami’u Al-Sahihi” au “Sahihi Bukhari”. 

 

  1.   Sahihi Muslim.

-  Ni kitabu cha Abu Husain Muslim bin Al-Hajjaj mashuhuri – Imam Muslim 

    wa mji wa Misabur, (202 A.H/818A.D – 261 A.H/875 A.D).

 

          -  Alikusanya Hadith 300,000 na alizohakiki na kuziandika katika kitabu chake 

              ni 9,200 tu.

 

          -  Kitabu chake ni namba mbili kwa usahihi wa Hadith, mashuhuri kwa jina la 

            “Sahihi Muslim”

 

  1.   Sunan Abu Daud.

          -  Ni kitabu cha hadith cha Imam Abu Daud (203 – 275 A.H).

          -  Alikusanya Hadith 500,000 na alizohakiki na kuziandika ni 4,800 katika 

                                 kitabu chake kiitwacho, “Sunan Abi Daud”.    

 

  1.   Jami’u at-Tirmidh.

-  Ni kitabu cha Hadith cha Abu Isa Muhammad bin Issa bin Sarwa bin 

    Shaddad, mashuhuri kama Imam At-Tirmidh (209 – 279 A.H).

-  Aliandika kitabu cha Hadith mashuhuri kwa jina la, “Jami’u”.

 

  1.   Sunnah (Sunan) Ibn Majah.

-  Ni kitabu cha Hadith cha Muhammad bin Yazid – mashuhuri kwa jina la 

    Imam Ibn Majah (209 A.H – 295 A.H).

-  Aliandika cha Hadith mashuhuri kama, “Sunanu Ibn Majah” au “Sunnah 

    Ibn Majah”.

 

  1.   Sunnah (Sunan) An-Nasai.

-  Ni kitabu cha Hadith cha Abu Abdur-Rahman Ahmad bin An-Nasai – 

   mashuhuri kwa jina la, Imam An-Nasai (214 – 303 A.H). 

-  Aliandika kitabu cha Hadith mashuhuri kama, “Sunan An-Nasai” au 

   “Sunnah An-Nasai”.

 

        -  Hadith za Bukhari na Muslim ndio daraja la kwanza kwa usahihi na za 

            Maimam Abu Daud, Tirmidh, Ibn Majah na An-Nasai ni daraja la pili kwa 

                             usahihi.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Jifunze Main: Post File: Download PDF Views 2890

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Uandishi wa hadithi wakati wa tabiina (wafuasi wa maswahaba)

Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
NENO LA AWALI

Darasa la elimu inayohusu ujauzito na namna ya kulea mimba

Soma Zaidi...
Umbwaji wa mwanadamu kutoka Nutfa (tone la mbegu za uzazi), alaqah (tone la damu, mudgha (pande la nyama) na kuwa mtu kamili

عَنْ أَبِي عَبْدِ الرَّحْمَنِ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ مَسْعُودٍ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: حَدَّثَنَا رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم ...

Soma Zaidi...
UANDISHI WA HADITHI WAKATI WA TABI'INA

Wakati wa Wafuasi wa masahaba (Tabi'ina)101-200 A.

Soma Zaidi...