Uandishi wa hadithi wakati wa tabii tabiina

Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Uandishi wa Hadith Wakati wa Tabi’i Tabi’ina (wafuasi wa wafuasi wa   

       maswahaba, 201 – 300 A.H).

 

 

 

  1. Tabia na mwenendo wa kila msimulizi (mpokezi) wa Hadith hiyo.
  2. Usahihi wa Matin ya Hadith hiyo.

 

      -    Ni kipindi hiki wanazuoni sita walijitokeza waliokusanya na kuchambua kwa umakini mkubwa Hadith sahihi na kuziandika katika vitabu sita mashuhuri kama, “Sahihu Sitta” ambavyo ni;

 

  1.   Sahihi Al-Bukhari.

          -  Ni kitabu cha Muhammad bin Ismail Abu Abdallah Al-Ju’fi – mashuhuri  

              kama Imam Bukhari wa mji wa Bukhara, Urusi (194 A.H/810 A.D – 256

              A.H/870 A.D).

 

          -  Alikusanya Hadith 600,000 na kuhifadhi 200,000 na alihakiki na kuandika

              Hadith 7,275 tu katika kitabu chake. 

           

          -  Kitabu chake ndio namba moja kwa usahihi wa Hadith, mashuhuri kwa jina 

              la “Al-Jami’u Al-Sahihi” au “Sahihi Bukhari”. 

 

  1.   Sahihi Muslim.

-  Ni kitabu cha Abu Husain Muslim bin Al-Hajjaj mashuhuri – Imam Muslim 

    wa mji wa Misabur, (202 A.H/818A.D – 261 A.H/875 A.D).

 

          -  Alikusanya Hadith 300,000 na alizohakiki na kuziandika katika kitabu chake 

              ni 9,200 tu.

 

          -  Kitabu chake ni namba mbili kwa usahihi wa Hadith, mashuhuri kwa jina la 

            “Sahihi Muslim”

 

  1.   Sunan Abu Daud.

          -  Ni kitabu cha hadith cha Imam Abu Daud (203 – 275 A.H).

          -  Alikusanya Hadith 500,000 na alizohakiki na kuziandika ni 4,800 katika 

                                 kitabu chake kiitwacho, “Sunan Abi Daud”.    

 

  1.   Jami’u at-Tirmidh.

-  Ni kitabu cha Hadith cha Abu Isa Muhammad bin Issa bin Sarwa bin 

    Shaddad, mashuhuri kama Imam At-Tirmidh (209 – 279 A.H).

-  Aliandika kitabu cha Hadith mashuhuri kwa jina la, “Jami’u”.

 

  1.   Sunnah (Sunan) Ibn Majah.

-  Ni kitabu cha Hadith cha Muhammad bin Yazid – mashuhuri kwa jina la 

    Imam Ibn Majah (209 A.H – 295 A.H).

-  Aliandika cha Hadith mashuhuri kama, “Sunanu Ibn Majah” au “Sunnah 

    Ibn Majah”.

 

  1.   Sunnah (Sunan) An-Nasai.

-  Ni kitabu cha Hadith cha Abu Abdur-Rahman Ahmad bin An-Nasai – 

   mashuhuri kwa jina la, Imam An-Nasai (214 – 303 A.H). 

-  Aliandika kitabu cha Hadith mashuhuri kama, “Sunan An-Nasai” au 

   “Sunnah An-Nasai”.

 

        -  Hadith za Bukhari na Muslim ndio daraja la kwanza kwa usahihi na za 

            Maimam Abu Daud, Tirmidh, Ibn Majah na An-Nasai ni daraja la pili kwa 

                             usahihi.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Dini File: Download PDF Views 2550

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 web hosting    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Nani Muadilifu na zipi sifa za mtu muadilifu kwenye uislamu

Uadilifu ni usimamizi wa ukweli na kutoa haki kwa kila anayestahiki kulingana na ukweli.

Soma Zaidi...
Je wajuwa kuwa jua hujizungurusha kwenye mhimili wake?

Tulipokuwa shule tulisoma kuwa jua halizunguruki, ila dunia ndio huzunguka jua.

Soma Zaidi...
Aina za hadithi

Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Zoezi la 5

Maswali mbalimbali kuhusu fiqih

Soma Zaidi...
sura ya 02

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Neno la awali

Asalaamu alykum warahmatullah wabarakaatuh Sifanjema zinamstahikia Allah Mola wa viumbe, muumba wa mbingu na ardhi na vilivyomo.

Soma Zaidi...