Uandishi wa hadithi wakati wa tabii tabiina


image


Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)


Uandishi wa Hadith Wakati wa Tabi’i Tabi’ina (wafuasi wa wafuasi wa   

       maswahaba, 201 – 300 A.H).

  • Pamoja na uandishi wa Hadith katika karne ya pili, bado kulikuwa na hitajio kubwa la mafunzo ya hadith katika kuendeshea maisha ya kila siku.

 

  • Uandishi wa Hadith karne ya tatu, ulihusika na ukusanyaji wa Hadith kuhusu nyanja zote za maisha ya jamii.

 

  • Wanachuoni pamoja na kukusanya Hadith nyingi muda huo, walikuwa makini mno katika kuchambua usahihi wa Hadith kwa kuzingatia;

 

  1. Tabia na mwenendo wa kila msimulizi (mpokezi) wa Hadith hiyo.
  2. Usahihi wa Matin ya Hadith hiyo.

 

      -    Ni kipindi hiki wanazuoni sita walijitokeza waliokusanya na kuchambua kwa umakini mkubwa Hadith sahihi na kuziandika katika vitabu sita mashuhuri kama, “Sahihu Sitta” ambavyo ni;

 

  1.   Sahihi Al-Bukhari.

          -  Ni kitabu cha Muhammad bin Ismail Abu Abdallah Al-Ju’fi – mashuhuri  

              kama Imam Bukhari wa mji wa Bukhara, Urusi (194 A.H/810 A.D – 256

              A.H/870 A.D).

 

          -  Alikusanya Hadith 600,000 na kuhifadhi 200,000 na alihakiki na kuandika

              Hadith 7,275 tu katika kitabu chake. 

           

          -  Kitabu chake ndio namba moja kwa usahihi wa Hadith, mashuhuri kwa jina 

              la “Al-Jami’u Al-Sahihi” au “Sahihi Bukhari”. 

 

  1.   Sahihi Muslim.

-  Ni kitabu cha Abu Husain Muslim bin Al-Hajjaj mashuhuri – Imam Muslim 

    wa mji wa Misabur, (202 A.H/818A.D – 261 A.H/875 A.D).

 

          -  Alikusanya Hadith 300,000 na alizohakiki na kuziandika katika kitabu chake 

              ni 9,200 tu.

 

          -  Kitabu chake ni namba mbili kwa usahihi wa Hadith, mashuhuri kwa jina la 

            “Sahihi Muslim”

 

  1.   Sunan Abu Daud.

          -  Ni kitabu cha hadith cha Imam Abu Daud (203 – 275 A.H).

          -  Alikusanya Hadith 500,000 na alizohakiki na kuziandika ni 4,800 katika 

                                 kitabu chake kiitwacho, “Sunan Abi Daud”.    

 

  1.   Jami’u at-Tirmidh.

-  Ni kitabu cha Hadith cha Abu Isa Muhammad bin Issa bin Sarwa bin 

    Shaddad, mashuhuri kama Imam At-Tirmidh (209 – 279 A.H).

-  Aliandika kitabu cha Hadith mashuhuri kwa jina la, “Jami’u”.

 

  1.   Sunnah (Sunan) Ibn Majah.

-  Ni kitabu cha Hadith cha Muhammad bin Yazid – mashuhuri kwa jina la 

    Imam Ibn Majah (209 A.H – 295 A.H).

-  Aliandika cha Hadith mashuhuri kama, “Sunanu Ibn Majah” au “Sunnah 

    Ibn Majah”.

 

  1.   Sunnah (Sunan) An-Nasai.

-  Ni kitabu cha Hadith cha Abu Abdur-Rahman Ahmad bin An-Nasai – 

   mashuhuri kwa jina la, Imam An-Nasai (214 – 303 A.H). 

-  Aliandika kitabu cha Hadith mashuhuri kama, “Sunan An-Nasai” au 

   “Sunnah An-Nasai”.

 

        -  Hadith za Bukhari na Muslim ndio daraja la kwanza kwa usahihi na za 

            Maimam Abu Daud, Tirmidh, Ibn Majah na An-Nasai ni daraja la pili kwa 

                             usahihi.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    2 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    3 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    4 Madrasa kiganjani offline    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Kumuamini malaika wa mwenyezi Mungu
Nguzo za Imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kwanini lengo la funga halifikiwi na wafungaji wengi
Nguzo za uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kumuamini malaika wa mwenyezi Mungu...
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Mgawanyiko wa elimu usiokubalika katika uislamu
Ni mgawanyo upi wa elimu haukubaliki. Ni ipi elimul akhera na elimu dunia? (Edk form 1 Dhana ya elimu) Soma Zaidi...

image Maswali kuhusu Quran
Quran (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Mafunzo kutokana na vita vya badri
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Sababu za Quran kuwa mwongozo sahihi wa maisha ya mwanadamu
Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Mtazamo wa uislamh juu ya ibada
Katika kipengele hich tutajifunza dhana ya ibada katika uislamu,maana ua ibada Soma Zaidi...

image Sanda ya mtoto
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Sanda ya mwanamke na namna ya kumkafini
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...