Mnafiki ni yule anayeukubali Uislamu mdomoni (kwa kauli tu) lakini moyoni mwake na katika matendo yake anaukanusha.
Mnafiki ni yule anayeukubali Uislamu mdomoni (kwa kauli tu) lakini moyoni mwake na katika matendo yake anaukanusha. Wanafiki wanaainishwa vema katika aya zifuatayo:-
“Na katika watu wako wasemao: Tumemuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho; na hali ya kuwa wao si wenye kuamini. Wanataka kumdanganya Allah na wale w alioamini, lakini hawadanganyi ila nafsi zao, nao hawatambui.” (2:8-9)
Wanafiki pamoja na kuonyesha imani ya uwongo, ni maadui wakubwa wa Allah (s.w) na Mtume wake. Hushirikiana na Makafiri na Washirikina katika kuupiga vita Uislamu. Wao ni maadui wabaya zaidi kuliko makafiri na washirikina kwa sababu wao hutoa siri za ndani za Waislamu na kuwapelekea maadui wa Uislamu ili wapate kuuhilikisha Uislamu. Hivyo Allah (s.w) amewaahidi wanafiki kuwa watapata adhabu kali kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo:
Bila shaka wanafiki watakuwa katika tabaka la chini kabisa katika moto. Hutamkuta kwa ajili yao msaidizi’. (4:145)
Hakuna alama au nembo maalum zinazoonekana katika sura au viwili wili vya wanafiki, bali wanafiki wanatambulika kwa matendo
yao au mienendo yao. Mwenendo wa kinafiki au sifa za wanafiki zimebainishwa kwa uwazi katika Qur-an na Hadith Sahihi. Katika Qur’an Allah (s.w) amewaelelezea wanafiki katika aya zifuatazo:
(2:8-20), (3:167-168), (4:60-63), (4 :138-145), (9:43-68), (33:12-20), (57:13), (59:11-1 7), (63:1-8).
aya hizi tunajifunza kuwa wanafiki wamesifika kwa sifa
Maneno ya wanafiki siku zote ni kinyume na matendo yao.
Wanafiki hujaribu kumdanganya Allah pamoja na Waislamu wakidhani kuwa yaliyo vifuani mwao h ayaju likan i.
Hizi ndizo sifa za wanafiki kama zilivyobainishwa katika Qur-an. Kwa muhtasari, Mtume (s.a.w) anatufahamisha sifa za wanafiki kama tunavyojifunza katika Hadith ifuatazo:
Mtume (s.a.w) amesema: Mambo manne akiwanayo mtu humfanya awe mnafiki wa wazi hata kama anaswali, anafunga na anadai kuwa ni Muumini,. Anayesema uw ongo kila anapoongea, anayevunja ahadi kila anapo ahidi, anayehini amana kila anapoaminiwa, na anayechupa mipaka kila unapotokea ugomvi. (Bukhari)
Muislamu wa kweli hana budi kujiepusha na unafiki kwa kujinasua na tabia za wanafiki.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Waumini wa kweli waliofuzu hutoa Zakat wakiwa na mali na hutoa misaada na huduma waziwezazo kwa wanaadamu wenziwe kwa kadiri ya haja ilivyojitokeza.
Soma Zaidi...Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Ni ipi haki ya mwanamke kwenye mirathi endapo atafiwa na mume wake, ilihali yeye ni mke wa pili?
Soma Zaidi...Haya ni matukio ya kihistoria yanayoamiika kutokea ndani ya masiku 10 ya Mfunguo tatu.
Soma Zaidi...Kuna malipo makubwa kwa ambaye amejenga msikiti kwa ajili ya kuoatavradhi za Allah.
Soma Zaidi...Kipengele hichi kina maswali mbalimbali kuhusiana na dini na mitazamo mbalimbali.
Soma Zaidi...