image

nini maana ya Unafiki na sifa za unafiki katika quran na sunnah

Mnafiki ni yule anayeukubali Uislamu mdomoni (kwa kauli tu) lakini moyoni mwake na katika matendo yake anaukanusha.

nini maana ya Unafiki na sifa za unafiki katika quran na sunnah

  1. Kuepuka Unafiki 

Mnafiki ni yule anayeukubali Uislamu mdomoni (kwa kauli tu) lakini moyoni mwake na katika matendo yake anaukanusha. Wanafiki wanaainishwa vema katika aya zifuatayo:-

“Na katika watu wako wasemao: Tumemuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho; na hali ya kuwa wao si wenye kuamini. Wanataka kumdanganya Allah na wale w alioamini, lakini hawadanganyi ila nafsi zao, nao hawatambui.” (2:8-9)

Wanafiki pamoja na kuonyesha imani ya uwongo, ni maadui wakubwa wa Allah (s.w) na Mtume wake. Hushirikiana na Makafiri na Washirikina katika kuupiga vita Uislamu. Wao ni maadui wabaya zaidi kuliko makafiri na washirikina kwa sababu wao hutoa siri za ndani za Waislamu na kuwapelekea maadui wa Uislamu ili wapate kuuhilikisha Uislamu. Hivyo Allah (s.w) amewaahidi wanafiki kuwa watapata adhabu kali kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo:



Bila shaka wanafiki watakuwa katika tabaka la chini kabisa katika moto. Hutamkuta kwa ajili yao msaidizi’. (4:145)

Hakuna alama au nembo maalum zinazoonekana katika sura au viwili wili vya wanafiki, bali wanafiki wanatambulika kwa matendo



yao au mienendo yao. Mwenendo wa kinafiki au sifa za wanafiki zimebainishwa kwa uwazi katika Qur-an na Hadith Sahihi. Katika Qur’an Allah (s.w) amewaelelezea wanafiki katika aya zifuatazo:

(2:8-20), (3:167-168), (4:60-63), (4 :138-145), (9:43-68), (33:12-20), (57:13), (59:11-1 7), (63:1-8).



aya hizi tunajifunza kuwa wanafiki wamesifika kwa sifa

Maneno ya wanafiki siku zote ni kinyume na matendo yao.

Wanafiki hujaribu kumdanganya Allah pamoja na Waislamu wakidhani kuwa yaliyo vifuani mwao h ayaju likan i.



    Sifa za wanafiki:

  1. Siku zote wanafiki hufanya ufisadi huku wakidai kuwa wanatenda wema (wanatengeneza).
  2. Huwaona waumini wa kweli kuwa ni wajinga kwa kufuatakwao Uislamu inavyotakikana.
  3. Huwacheza shere Waislamu.
  4. Wanafiki huyapendazaidi maisha ya dunia kuliko ya
  5. Hawapendi kuhukumiwa na sheria ya Allah (s.w).
  6. Hutumia viapo kama kifuniko cha maovu yao.
  7. Huwafanya makafiri na washirikina kuwa ndio marafiki zao wa ndani badala ya Allah na Mtume wake na waislamu.
  8. Hujaribu kushika njia ya katikati baina ya Uislamu na Ukafiri, hivyo huyumbayumba baina ya Uislamu na Ukafiri.
  9. Huenda kuswali kwa uvivu.
  10. Hawamkumbuki Allah(s.w) ila kwa kidogo
  11. Huwafitinisha Waislamu.
  12. Huchukia Waislamu wanapofikwa na kheri na hufurahi wanapofikwa na msiba.
  13. Hawako tayari kutoa mali zao katika njia ya Allah na wakitoa chochote hutoa kwa ria.
  14. Mara nyingi huzifanyia shere aya za Qur-an.
  15. Huamrisha maovu na kukataza mema.
  16. Ni wenye kutapatapa wakati wa matatizo na humdhania vibaya Allah na Mtume wake.
  17. Husema uongo na hawatekelezi ahadi.
  18. Hujitahidi kuwavunja moyo Waislamu wa kweli ili wabakie katika ukafiri sawa na wao.
  19. Hufanya hiyana katika mambo ya kheri na huchagua mambo mepesi mepesi yenye kuwafurahisha.
  20. Wanawaogopa na hukaa upande mmoja na maadui wa Uislamu na Waislamu.
  21. Hupenda kusifiwa kwa kazi nzuri zilizofanywa na wengine.
  22. Huchochea fitna baina ya Waislamu, n.k.


Hizi ndizo sifa za wanafiki kama zilivyobainishwa katika Qur-an. Kwa muhtasari, Mtume (s.a.w) anatufahamisha sifa za wanafiki kama tunavyojifunza katika Hadith ifuatazo:

Mtume (s.a.w) amesema: Mambo manne akiwanayo mtu humfanya awe mnafiki wa wazi hata kama anaswali, anafunga na anadai kuwa ni Muumini,. Anayesema uw ongo kila anapoongea, anayevunja ahadi kila anapo ahidi, anayehini amana kila anapoaminiwa, na anayechupa mipaka kila unapotokea ugomvi. (Bukhari)

Muislamu wa kweli hana budi kujiepusha na unafiki kwa kujinasua na tabia za wanafiki.



                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1036


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Madrasa kiganjani    

Post zifazofanana:-

(xvi)Huepuka ugomvi na mabishano
Waumini wa kweli huepuka kabisa tabia ya ugomvi na mabishano. Soma Zaidi...

quran na sayansi
Soma Zaidi...

Nini maana ya Kibri, madhara yake na kujiepusha na kibri
17. Soma Zaidi...

quran na sayansi
2; mbegu ya uhai uliyo changanyikaUmbile la mwanadamu limepitia hatua nyingi sana kama tutakavyoendelea mbele kuonalakini ukiachilia mbali na hatua zote alizopitia mwanadamu wakati wa kuumbwa lakiniumbile la mwanadamu bado limebakia kuwa dhalili kama ALLA Soma Zaidi...

Kitabu Cha Darsa za Funga
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet. Soma Zaidi...

Nani Muadilifu na zipi sifa za mtu muadilifu kwenye uislamu
Uadilifu ni usimamizi wa ukweli na kutoa haki kwa kila anayestahiki kulingana na ukweli. Soma Zaidi...

Aina za hadithi
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

quran na sayansi
2:UUMBWAJI KWA MAJI YA UZAZIUumbwaji wa mwanadamu umepitia hatua mbalimbali na haya yote yamefanywa kwa sababumaalumu ili tipate mazingatio. Soma Zaidi...

Kuepuka mabishano na madhara ya kugombana
16. Soma Zaidi...

Fadhila za kujenga msikiti
Kuna malipo makubwa kwa ambaye amejenga msikiti kwa ajili ya kuoatavradhi za Allah. Soma Zaidi...

nini maana ya Unafiki na sifa za unafiki katika quran na sunnah
Mnafiki ni yule anayeukubali Uislamu mdomoni (kwa kauli tu) lakini moyoni mwake na katika matendo yake anaukanusha. Soma Zaidi...

tawhid
Soma Zaidi...