nini maana ya Unafiki na sifa za unafiki katika quran na sunnah

Mnafiki ni yule anayeukubaliย Uislamu mdomoni (kwa kauli tu) lakini moyoni mwake na katika matendo yake anaukanusha.

nini maana ya Unafiki na sifa za unafiki katika quran na sunnah

  1. Kuepuka Unafiki 

Mnafiki ni yule anayeukubali Uislamu mdomoni (kwa kauli tu) lakini moyoni mwake na katika matendo yake anaukanusha. Wanafiki wanaainishwa vema katika aya zifuatayo:-

“Na katika watu wako wasemao: Tumemuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho; na hali ya kuwa wao si wenye kuamini. Wanataka kumdanganya Allah na wale w alioamini, lakini hawadanganyi ila nafsi zao, nao hawatambui.” (2:8-9)

Wanafiki pamoja na kuonyesha imani ya uwongo, ni maadui wakubwa wa Allah (s.w) na Mtume wake. Hushirikiana na Makafiri na Washirikina katika kuupiga vita Uislamu. Wao ni maadui wabaya zaidi kuliko makafiri na washirikina kwa sababu wao hutoa siri za ndani za Waislamu na kuwapelekea maadui wa Uislamu ili wapate kuuhilikisha Uislamu. Hivyo Allah (s.w) amewaahidi wanafiki kuwa watapata adhabu kali kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo:



Bila shaka wanafiki watakuwa katika tabaka la chini kabisa katika moto. Hutamkuta kwa ajili yao msaidizi’. (4:145)

Hakuna alama au nembo maalum zinazoonekana katika sura au viwili wili vya wanafiki, bali wanafiki wanatambulika kwa matendo



yao au mienendo yao. Mwenendo wa kinafiki au sifa za wanafiki zimebainishwa kwa uwazi katika Qur-an na Hadith Sahihi. Katika Qur’an Allah (s.w) amewaelelezea wanafiki katika aya zifuatazo:

(2:8-20), (3:167-168), (4:60-63), (4 :138-145), (9:43-68), (33:12-20), (57:13), (59:11-1 7), (63:1-8).



aya hizi tunajifunza kuwa wanafiki wamesifika kwa sifa

Maneno ya wanafiki siku zote ni kinyume na matendo yao.

Wanafiki hujaribu kumdanganya Allah pamoja na Waislamu wakidhani kuwa yaliyo vifuani mwao h ayaju likan i.



    Sifa za wanafiki:

  1. Siku zote wanafiki hufanya ufisadi huku wakidai kuwa wanatenda wema (wanatengeneza).
  2. Huwaona waumini wa kweli kuwa ni wajinga kwa kufuatakwao Uislamu inavyotakikana.
  3. Huwacheza shere Waislamu.
  4. Wanafiki huyapendazaidi maisha ya dunia kuliko ya
  5. Hawapendi kuhukumiwa na sheria ya Allah (s.w).
  6. Hutumia viapo kama kifuniko cha maovu yao.
  7. Huwafanya makafiri na washirikina kuwa ndio marafiki zao wa ndani badala ya Allah na Mtume wake na waislamu.
  8. Hujaribu kushika njia ya katikati baina ya Uislamu na Ukafiri, hivyo huyumbayumba baina ya Uislamu na Ukafiri.
  9. Huenda kuswali kwa uvivu.
  10. Hawamkumbuki Allah(s.w) ila kwa kidogo
  11. Huwafitinisha Waislamu.
  12. Huchukia Waislamu wanapofikwa na kheri na hufurahi wanapofikwa na msiba.
  13. Hawako tayari kutoa mali zao katika njia ya Allah na wakitoa chochote hutoa kwa ria.
  14. Mara nyingi huzifanyia shere aya za Qur-an.
  15. Huamrisha maovu na kukataza mema.
  16. Ni wenye kutapatapa wakati wa matatizo na humdhania vibaya Allah na Mtume wake.
  17. Husema uongo na hawatekelezi ahadi.
  18. Hujitahidi kuwavunja moyo Waislamu wa kweli ili wabakie katika ukafiri sawa na wao.
  19. Hufanya hiyana katika mambo ya kheri na huchagua mambo mepesi mepesi yenye kuwafurahisha.
  20. Wanawaogopa na hukaa upande mmoja na maadui wa Uislamu na Waislamu.
  21. Hupenda kusifiwa kwa kazi nzuri zilizofanywa na wengine.
  22. Huchochea fitna baina ya Waislamu, n.k.


Hizi ndizo sifa za wanafiki kama zilivyobainishwa katika Qur-an. Kwa muhtasari, Mtume (s.a.w) anatufahamisha sifa za wanafiki kama tunavyojifunza katika Hadith ifuatazo:

Mtume (s.a.w) amesema: Mambo manne akiwanayo mtu humfanya awe mnafiki wa wazi hata kama anaswali, anafunga na anadai kuwa ni Muumini,. Anayesema uw ongo kila anapoongea, anayevunja ahadi kila anapo ahidi, anayehini amana kila anapoaminiwa, na anayechupa mipaka kila unapotokea ugomvi. (Bukhari)

Muislamu wa kweli hana budi kujiepusha na unafiki kwa kujinasua na tabia za wanafiki.



                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Dini File: Download PDF Views 2286

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰2 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰3 Kitau cha Fiqh    ๐Ÿ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Zoezi la 3

Kipengele hichi kina maswali mbalimbali kuhusiana na dini na mitazamo mbalimbali.

Soma Zaidi...
Kushika mwenendo wa kati "Na ushike mwenendo wa katiโ€ฆ." (31:19)

Mwenendo wa kati ni mwenendo ulioepukana na kibri na majivuno kwa upande mmoja na ulioepukkana na udhalili na unyonge kwa upande mwingine.

Soma Zaidi...
jamii somo la 26

(vii)Hufanya bias hara na Allah (s.

Soma Zaidi...
Mawaidha Kutokwa kwa Shekhe

Karibu kwenye Darsa za mawaidha na Mafundisho ya dini.

Soma Zaidi...
quran na sayansi

2; mbegu ya uhai uliyo changanyikaUmbile la mwanadamu limepitia hatua nyingi sana kama tutakavyoendelea mbele kuonalakini ukiachilia mbali na hatua zote alizopitia mwanadamu wakati wa kuumbwa lakiniumbile la mwanadamu bado limebakia kuwa dhalili kama ALLA

Soma Zaidi...
Uandishi wa hadithi wakati wa maswahaba wa mtume (s.a.w)

Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Aina za hadithi

Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
HUYU NDIYE MUUMINI WA KWELI KATIKA UISLAMU

ุนูŽู†ู’ ุฃูŽุจููŠ ุญูŽู…ู’ุฒูŽุฉูŽ ุฃูŽู†ูŽุณู ุจู’ู†ู ู…ูŽุงู„ููƒู ุฑูŽุถููŠูŽ ุงู„ู„ู‡ู ุนูŽู†ู’ู‡ู ุฎูŽุงุฏูู…ู ุฑูŽุณููˆู„ู ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆ ุณู„ู… ุนูŽู†ู’ ุงู„ู†ูŽู‘ุจููŠูู‘ ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ?...

Soma Zaidi...
(ix)Wenye kuhifadhi swala

Waumini wa kweli waliofuzu huhifadhi swala kwa kutekeleza kwa ukamilifu shuruti zote za swala nguzo zote za swala na huswali kama alivyoswali Mtume (s.

Soma Zaidi...