Menu



Athari na faida za kumuamini Allah katika maisha ya mwanadamu duniani na akhera

Athari za Kumuamini Mwenyezi Mungu (s.

Athari na faida za kumuamini Allah katika maisha ya mwanadamu duniani na akhera

Athari na faida za kumuamini Allah katika maisha ya mwanadamu duniani na akhera

Athari za Kumuamini Mwenyezi Mungu (s.w) katika maisha ya kila siku.
Muumini wa kweli huishi katika kila kipengele cha maisha yake kwa mujibu wa taratibu na kanuni alizoweka Mwenyezi Mungu (s.w), na hii kama ifuatavyo;



(i)Kupata ukombozi kutokana na utumwa wa aina zote;
Huu hupatikana baada ya mtu kuwa huru na kuishi kwa kufuata taratibu na kanuni alizoweka Mwenyezi Mungu (s.w) pekee.
Rejea Qur’an (12:39).



(ii) Mwanaadamu huwa mwadilifu katika utendaji wa maisha yake ya kila siku;
Muumini wa kweli hufanya mema na kuepuka maovu bila hata ya kusimamiwa au kuonekana na watu, kwa kujua kuwa mjuzi pekee ni Mwenyezi Mungu (s.w).
Rejea Qur’an (50:16).



(iii) Humfanya mwanaadamu kuwa mpole, mvumilivu na mwenye huruma;
Mwanaadamu huwa mpole hasa kwa wenye shida na matatizo na pia kuwa na subra anapofikwa na mitihani na kujiepusha na kibri, majivuno na kujiona.
Rejea Qur’an (6:165).



(iv) Humfanya mja kuwa jasiri katika kusimamia haki, uadilifu na usawa katika jamii;
Muumini wa kweli huwa shujaa katika kupambana na dhulma na ukandamizaji wa aina yeyote na kupigania haki bila kumchelea mtu yeyote.
Rejea Qur’an (4:74), (5:45) na (9:111).



(v) Humfanya mja kuwa na mtazamo mpana na sahihi juu ya maisha;
Muumini wa kweli kamwe hawi na fikra na mtazamo finyu katika kuyaendea maisha yake ya kila siku kwa kujua lengo, thamani na nafasi yake juu ya maisha ya Akhera.
Rejea Qur’an (15:9).



(vi) Humuwezesha mja kuwa mwenye kukinai na kutosheka;
Muumini wa kweli hutosheka na kuridhika na kile alichokadiriwa na Mwenyezi Mungu (s.w) iwe kwa kupungukiwa au kuzidishiwa, yote kwake anashukuru.



                   

Download app yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download

Download Now Bongoclass

           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Views 1107


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Kiwango cha mahari katika uislamu
Kiasi gani Kinachojuzu kutolewa Mahari? Soma Zaidi...

Shufaa
Soma Zaidi...

Taratibu za kumuona mchumba
Soma Zaidi...

AMRI YA KUMFUATA MTUME (s.a.w9)
Amri ya Kumfuata Mtume (s. Soma Zaidi...

Umuhimu wa kusimamisha uislamu katika jamii
1. Soma Zaidi...

Namna ya kuswali swala ya kuombea haja
9. Soma Zaidi...

Kwa Nini Mwanaadamu Hawezi Kuunda Dini Sahihi ?
1. Soma Zaidi...

Faida za kiafya za kula Mbegu za maboga
Soma Zaidi...

Zijuwe suna (sunnah) za Udhu ama Kutawadha
Soma Zaidi...

Sifa za mchumba
Soma Zaidi...