Ukweli ni uhakika wa jambo.
Ukweli ni uhakika wa jambo. Muislamu wa kweli hana budi kuwa mkweli na kusimamia ukweli. Allah (s.w) anatuamrisha tuwe wakweli katika kuendesha shughuli zetu zote.
“Enyi mlioamini Mcheni Mwenyezi Mungu na kuweni pamoja na wakweli.” (9:119).
Msema kweli ni mpenzi wa Allah (s.w) . Naye Allah (s.w) amewaandalia wakweli ujira mzuri kabisa kwa hapa duniani na huko akhera kama tunavyobainishiwa katika Qur-an” kuwa Allah (s.w) atasema katika hiyo siku ya hisabu:-
“Hii ndiyo siku ambayo wakweli utawafaa ukweli wao. Wao watapata bustani zipitazo mbele yake mito. Humo watakaa milele. Allah amewawia radhi nao wanaradhi naye. Huku ndiko kufaulu kukubwa. (5:119)
“... Na wanaume wasemao kweli na wanawake wasemao kweli... Allah amewaandalia msamaha na ujira mkubwa”. (33:35).
Msisitizo wa Muislamu kujipamba na tabia ya kuwa mkweli pia tunaupata katika Hadith ifuatayo:
‘Abdullah bin Mas ’ud (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Utaongea ukweli kwa sababu ukweli unaongoza kwenye Ucha-Mungu na Ucha-Mungu unaongoza kw enye Pepo. Mja ataendelea kusema kweli na kubakia katika ukweli mpaka aorodheshwe mbele ya Allah kuwa ni miongoni mwa wakweli wakubwa.Tahadharini na uwongo! Uwongo unaongoza kwenye uasi na uasi unaongoza kwenye Moto.Mja ataendelea kusema uwongo na kubakia katika uwongo mpaka aorodheshwe mbele ya Allah kuwa ni miongoni mwa waongo wakubwa”.
(Bukhari na Muslim).
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Muislamu anapoingia Msikitini kabla hajakaa anatakiwa aswali rakaa mbili za maamkizi ya msikiti, Tahiyyatul-Masjid.
Soma Zaidi...