image

NI UPI MKATABA WA AL-FUDHUL NA ASILI YAKE, ATHARI ZAKE NA WALOHUSIKA

MKATABA WA AL-FUDHULBaada ya vita hivi viongozi wa pande mbili hizi waliamuwa wakae chini na wakubaliane kuweka kanun i na utaratibu utakaozuia kutotokea uonevu kama huuu tena.

NI UPI MKATABA WA AL-FUDHUL NA ASILI YAKE, ATHARI ZAKE NA WALOHUSIKA


MKATABA WA AL-FUDHUL
Baada ya vita hivi viongozi wa pande mbili hizi waliamuwa wakae chini na wakubaliane kuweka kanun i na utaratibu utakaozuia kutotokea uonevu kama huuu tena. Na hii ni kuwa maeneo mengi ya waarabu enzi hizo yalikuwa na utaratibu kama huu wa kuweza kusaidiana na kuzuia uonezu na unyanganyi wa haki. Makataba huu ulikuwa na lengo la kuwasaidia watu wanyonge ambao hawana urafiki na mahusiano na watu wenyenguvu, madaraka ama uwezo wa kipesa.

Hivyo lengo kuu la kiapo au mkataba huu ilikuwa kulinda haki za wanyonge, kuzuia dhulma na uonevu. Kuwapa haki watu wanaostahiki kupewa haki bila ya kujali wapi wametoka, ni nani ndugu zao au wanauwezo gani. Makataba huu ulifanyika kwenye nyumba ya mzee mwenye heshima,na mwenye umri aliyefahamika kwa jina la Abdallah bin Jad’an. Walohudhuria kwenye mkutano huu ni wawakilishi kutoka kabila la Banu hashim, Banu Al-Muttalib, Asad bin Abdul ‘Uzza, Zahran bin Kilab pamoja na Taim bin Murra.

Baada ya makubaliano yao ya kujenga amani kati yao wenyewe na wageni wao wanaokuja Makkah walikwenda kwenye Al-Ka’abah na kufanya kiapo. Kiapo chao ni kuyatekeleza walokubaliana kuwa watampa kila mtu haki yake na watapigana na yeyote ambaye atadhulumu na kumsaidia atakaye dhulumiwa. Watapigana na yeyote atakayevunja makubaliano haya mpaka haki ipatuikane. Walifanya kiapo ndani ya al-ka’aba mbele ya kiwe jeusi.

Miongoni mwa walohudhuria mkutano huu kutoka upande wa maquraysh ni Mtume s.a.w. na baada ya kupewa utume Mtume (a.s.w) alisema: “nilishuhudia (mkutano, makubaliano mkataba) kwenye nyumba ya Abdallah bin Jad’an, mkutano ninaoupenda kuliko ngamia mwekundu, na lau ningeliitwa tena kwenye mkutano kama huu hakika ningehudhuri”. Maneno haya yanathibitisha kuwa mkutano huu uliridhiwa na Allah. Hizi pia zilikuwa ni katika vitangulizi vya kuja kwa mtume wa mwisho.

Na inasemekana kuwa jimbuko na wao kukutana ni kuwa alitokea mfanyabiashara mmoja kutoka katika kabila la Zubaid alikuja Makkah kufanya biashara. Hivyo akamuuzia Al-‘As bin Wa’il As-Sahmy baadhi ya bidhaa zake. Baadaye Al-As akakataa kumlipa mtu huyu. Hivyo mfanyabiashara akawa anaomba msaada kwa Maquraysh waweze kumsaidia ili apate haki yake, lakini hakuna ambaye alimjali.


                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 400


Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitau cha Fiqh    

Post zifazofanana:-

Hawa ndio waaasi wakwanza wa Dola ya kiislamu wakati wa makhalifa
Soma Zaidi...

Imam Muhammad Idris al-Shafii
Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII AYYUUB(A.S)
Ayyuub(a. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII YUSUFU(A.S.): Ndoto ya nabii Yusufu
Mtume Yusufu(a. Soma Zaidi...

Madhumuni ya dola ya uislamu
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII ADAM
Soma Zaidi...

Kuandaliwa kwa Muhammad kabla ya kupewa utume
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

HISTORIA YA MTUME DHUL-KIFL(A.S)
Mtume Dhul-kifl ananasibishwa na Ezekiel anayetajwa ndani ya Biblia. Soma Zaidi...

Maandalizi ya Hijra ya Mtume na Mafunzo tunayoyapata kutoka katika hijra hii
Maandalizi ya Hijra ya Mtume (s. Soma Zaidi...

Upinzani Dhidi ya Ujumbe wa Mtume(s.a.w)
Mtume(s. Soma Zaidi...

Uteuzi wa Uthman bin Al-'Afan khalifa wa Tatu baada ya Mtume
Soma Zaidi...

Darsa za Sira historia ya Mtume (s.a.w) Jaribio la 04
Soma Zaidi...