image

Mifano na namna ya kurithisha

Ugawaji wa mirathi-Mume ana nusu (1/2) = 1/2 -Mama ana sudusi.

Mifano na namna ya kurithisha

Ugawaji wa mirathi
-Mume ana nusu (1/2) = 1/2
-Mama ana sudusi. (1/6) = 1/6
-Ndugu wengine wa kwa mama wana thuluthi (1/3) = 2/6



Hapo utaona kuwa mafungu yote sita yamegawanywa yakaisha na ndugu wa kwa baba na mama hawakupata kitu. Hapa itabidi ile Thuluthi waliyoipata ndugu wa kwa mama wagawane sawa sawa na ndugu wa kwa baba na mama maana nao wanayo haki ya ndugu wa kwa mama kama wao na wala hakoseshwi kwa sababu ya unasaba wake.


Mifano ya namna ya kurithisha
Wakikutana warithi na pakawa hapana amzuiliaye mwenziwe na ikawa wote ni asaba, wataigawanya mali iliyopo sawa sawa kwa kadri ya idadi yao. Kwa mfano: Akifa mtu, akawa ameacha vijana wanamume wanne, mali yote itagawanywa mafungu manne sawa sawa na kila mmoja apewe fungu lake.



Ama wakikutana asaba wanaume na wanawake, bali kila mwanamume atahesabiwa kuwa ni wanawake wawili na mali itapigwa mafungu kila mwanamume mmoja apewe mafungu mawili na kila mwanamke apewe fungu moja. Kwa mfano: Amekufa mtu kaacha watoto sita, wanne wanaume na wawili wanawake. Wanaume wanne watahesabiwa kuwa ni sawa na wanawake wanane. Kwa hiyo mali itagawanywa katika mafungu kumi yaliyo sawa sawa. Wanaume watapata mafungu mawili kila mmoja na wanawake watapata fungu moja moja.



Iwapo warithi ni mchanganyiko wa wenye mafungu maalum na asaba, itabidi kutafuta kigawe kidogo cha shirika (Kigawe kidogo cha shirika - KDS) ili kupata mafungu yatakayogawiwa kwa kila mrithi kwa kadiri ya haki yake anayoistahiki. Hebu tuangalie mifano kadhaa ya mgawanyo wa mirathi.



Mfanol:
Amekufa mke na kuacha
(i)Mume.
(ii)Mtoto mwanamume.
(iii)Baba.



Wenye mafungu maalum kati ya hawa ni: (i)Mume - ana robo (1/4) madhali yupo mtoto.
(ii)Baba - ana sudusi(1/6) madhali yupo mtoto.



Asaba: Mtoto mwanamume na atachukua kitakachobakia. Ugawaj i:
Mafungu yatakayotolewa ni: (1/4), (1/6). Hesabu ndogo ambayo
inaweza kutolewa mafungu ya urithi ni 12 yaani KDS ya 4 na 6. Kwa hiyo mali ya urithi itagawanywa kwenye mafungu 12 yaliyo sawa sawa na ugawaji utakuwa kama ifuatavyo:



(i)Mume atapata 1/4 ya 12 = 114x 12 = 3 Yaani atachukua mafungu 3 katika mafungu 12.
(ii)Baba atapata (1/6) ya 12 = (1/6) x 12 = 2. Yaani atachukua mafungu 2 kati ya mafungu 12.



Mfano 2:
Amekufa mume na kuacha wafuatao:
(i)Mke mmoja.
(ii)Mama.
(iii)Mjukuu mmoja wa kike (binti wa mtoto mwanamume).
(iv)Mtoto mwanamume.
(v)Watoto watatu wanawake.



Kama mali iliyoachwa na marehemu ni shilingi 1,200,000/= utarithisha wahusika kama ifuatavyo:
Wenye mafungu maalum kati ya hawa ni:
(i)Mke ambaye atapata thumuni 1/8 kwa sababu wapo watoto.
(ii)Mama atapata sudusi 1/6 ya mali kwa sababu wapo watoto.
(iii)Mjukuu hapati kitu kwa sababu wapo watoto ambao humzuilia.


(iv)Mtoto mwanamume na watoto wanawakewatagawana mali iliyobakia, wakiwa hao asaba mwanamume achukue sawa na
wanawake wawili (2:1)



Njia mbili zifuatazo zinaweza kutumika katika kurithisha wahusika: (a) Hisabu ndogo inayoweza kutolewa mafungu ni 24. Yaani KDS
ya 8 na 6. Kila fungu litakuwa na thamani ya shilingi 50,000 -(1,200,000/24)
Mke atapata 1/8 ya 24 = 3 yaani atapata 3 x 50,000/=
Mama atapata 1/6 ya 24 (1 x 24) = 4 yaani atapata 4 x 50,000 = 200,000/=
Asaba watarithi mali iliyobakia ambayo ni 1,200,000 - (150,000 ~ 200,000) = 850,000.


Mali hii itagawanywa katika mafungu 5 (kumbuka: Mwanamume atapata sawa na wanawake wawili). Hivyo, kila mtoto wa kike atapata: Shs. 1/5 x 850,000 = 170,000
Mtoto wa kiume atapata shs. 2/5 x 850,000 (au 2 x 170,000) = 340,000



(b)Njia ya pili ni kutafuta sehemu ya mali atakayopata kila mwenye fungu maalum. Kama mali inayorithiwa ni shs. 1,200,000/=
(i)Mke atapata 1/8 ya 1,200,000 = I X 1200000/8 = 150,000/=
(ii)Mama atapata 1/6 ya 1,200,000 = I X 1,200,000/6 = 200,000/
(iii)Asaba watagawana mali iliyobakia ambayo ni 1,200,000 - 350,000 = 850,000.
Kuna mabinti watatu na kijana mmoja ambaye ni sawa na mabinti wawili. Hivyo mali iliyobakia itagawanywa katika mafungu 5 ambapo kila binti atapata: I X 850,000/5 = 170,000/=
Kijana atapata sawa na mabinti wawili sh. 2 x 170,000 = 340,000/=



Kuongeza mafungu (Awl)
Iwapo idadi ya mafungu yatakayogaiwa kwa warithi wenye mafungu maalum ni kubwa kuliko mafungu yaliyopatikana kwa njia ya (KDS), idadi ya mafungu itabidi iongezeke ili kila mmoja apate haki yake. Hebu tuangalie mifano ifuatayo:



Mfano 1:
Amefariki mke na kuacha warithi wafuatao:
(i)Mume.
(ii)Dada wawili wa kwa baba na mama.
Wote hawa wana mafungu maalum:
(i)Mume atapata (1/2) kwa sababu hapana mtoto.
(ii)Dada wawili watapata thuluthi mbili (2/3) kwa sababu wako zaidi ya mmoja.
KDS ya 2 na 3 ni 6, hivyo:
(i) Mume atapata nusu (1/2) ya mafungu 6 = 3.


(ii) Dada wawili watapata thuluthi mbili (2/3) ya mafungu 6 = 4.
Utakuta kuwa jumla ya mafungu yanayohitajika ni 7(3 + 4) badala ya 6.
Hivyo mali ya marehemu itagawanywa katika mafungu yaliyo sawa sawa. Katika hayo mume atapata mafungu 3 na kila dada atapata mafungu 2.



Mfano 2:
Amefariki mke na kuacha warithi wafuatao:
(i)Mume.
(ii)Mama.
(iii)Dada mmoja wa kwa baba na mama.
Wote hawa wana mafungu maalum:
(i)Mume atachukua (1/2) kwa sababu hapana mtoto.
(ii)Mama atachukua (1/3) kwa sababu hapana mtoto na dada aliyopo ni mmoja tu.
(iii)Dada atapata (1/2) yuko peke yake.



Mgawanyo:
KDS ya 2 na 3 ni 6.
(i)Mume atapata (1/2) ya mafungu 6 = mafungu 3.
(ii)Mama atapata (1/3) ya mafungu 6 = mafungu 2.
(iii)Dada atapata (1/2) ya mafungu 6 = mafungu 3
Jumla ya mafungu yanayohitajika ni 8, badala ya 6. Hivyo itabidi mafungu mawili yaongezwe kwenye (KDS) ili kila mrithi apate haki yake.
Sehemu ya maskini na jamaa wa karibu katika mirathi:



Waumini wana usiwa kuwa japo ni wazi kuwa mali ya urithi ni haki ya warithi kwa mujibu wa sheria, hawana budi kuwahurumia mayatima, maskini na jamaa wa karibu kwa kuwapa kitu kutokana na urithi japo kidogo na hasa watakapohudhuria wakati wa kugawanya.


Na wakati wa kugawanya wakihudhuriajamaa na mayatima na maskini, wapeni kitu katika hayo (mali ya urithi) na waambieni kauli njema. (4:8)




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 673


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zifazofanana:-

Jinsi ya kuoga josho la kiislamu ( janaba, hedhi na nifasi)
Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ya kuoga josho kisheria. Soma Zaidi...

Swala ya kuomba mvua swalat istiqaa na jinsi ya kuiswali.
Hapa nitakujulisha kuhusu swala ya kuomba mvia, na taratibu za kuiswali. Soma Zaidi...

Kwa nini lengo la Hija halifikiwi?
Soma Zaidi...

mambo yanayofungua swaumu
post hii ijakwenda kukufundisha mambo yanayoharibu funga Soma Zaidi...

Vituo vya kunuia hijjah au umrah
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Taratibu za eda ya kufiwa katika uislamu
Hapa utajifunza taratibu za kukaa eda kwa mwanamke ambaye amefiwa na mume. Soma Zaidi...

Kumuandaa maiti punde baada ya kufariki dunia
Soma Zaidi...

Utaratibu wa kuzika, hatua kwa hatua, na namna ya kusindikiza jeneza
4. Soma Zaidi...

Swala ya tarawehe jinsi ya kuiswali
Post hii itakwenda kukufundisha kuhusi swala ya tarawehe, faida zake na jinsi ya kuiswali. Soma Zaidi...

Kusimamisha swala za faradh katika nyakati za dharura.
Kipengele hichi tutajifunza namna ya kusimamisha swala ukiwa safarini na vitani na nguzo zake. Soma Zaidi...

Zifahamu njia za kutwaharisha, aina za maji, udongo na Namna ya kujitwaharisha
Soma Zaidi...

Hijja na umrah
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...