WAQFU WAL-IBTIDAAI

WAQFU WAL-IBTIDAAI

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

WAQFU WAL-IBTIDAAI

SURA YATISA
HUKUMU ZA WAQFU AL-IBTIDAI

l-Waqfu Wal-Ibtidaai – Kisimamo Na Kianzio
Msomaji si kwamba muda wote atakuwa anasoma bali, wakati mwingine anapumzika, au anasimama kidogo kumeza mate au kupumua ana atakata kabisa kusoma. Hivyo hapa kuna kauli tatu ambazo inatupasa tuzijue kabla ya kuenddelea. Kauli hizo ni;-
1.Al-waqfu: maana yake ni kisimamo nako ni kukata kusoma kwa muda wa kawaida kwa ajili ya kuvuta pumzi huku msomaji akiwa na nia ya kuendelea kusoma.
2.Al-sakt:maana yake ni kipumziko nako ni kupumzika kwa muda kwa kiasi cha haraka mbili huku msomaji akiwa na nia ya kuendelea kusoma.
3.Al-qatw’u;maana yake ni ukataji nako ni kusimama kusoma kwa lengo la kumaliza kusoma. Hapa inabidi mtu amalize kusoma kwake mwishoni mwa aya au sura. Na inatakikana pindi anapotaka kuendelea kusoma aanze na isti’adha

ALAMA ZA WAQFU KATIKA QURAN:
1.aAlama hii(صلي) inamaanisha inajuzu kuunganisha.
Yaani pindi msomaji anapokuta alama hii anaweza kuunganisha maneno hayo, yaani neno la nyuma na maneno yanayofata. Hivyo hapa msomaji ana hiyari ima kuunganisha au kusimama (kufanya waqfu).

2.Alama hii (قلي) inamaanisha inajuzu kusimama.
Yaani pindi msomaji anapokuta alama hii atakuwa na hiyari ya kusimama.

3.Alama hii (ج) inamaanisha inajuzu kusimama ila kwa ufupi. Yaani msomaji anapokutana na alama hii ataweza kusimama hapa, ila usimamaji wake usiwe mrefu.
4.Alama hii (م) inamaanisha kusimama kwa lazima. Yaani msomaji anapokutana na alama hii kusimama kwake ni kwa lazima.
Alama hii (لا) inamaanisha hairuhusiwi kusimama sehemu hii. Hii inamaanisha msomaji hatakiwi kusimama pindi anapokutana na alama hii.


                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 2396

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Tofauti kati ya sura za makkah na madinah
Tofauti kati ya sura za makkah na madinah

Quran (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Maana ya qalqala na aina zake katika usomaji wa Quran tajwid
Maana ya qalqala na aina zake katika usomaji wa Quran tajwid

Qalqala imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Qalqalatul qubra yaani qalqala kubwa na qalqalat as shughura yaani qalqala ndogo.

Soma Zaidi...
Kitabu Cha  Darsa za Quran
Kitabu Cha Darsa za Quran

Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA MADD YAANI KUVUTA HERUFI KWENYE USOMAJI WA QURAN
HUKUMU ZA MADD YAANI KUVUTA HERUFI KWENYE USOMAJI WA QURAN

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Faida za kujuwa Quran tajwid
Faida za kujuwa Quran tajwid

Hapa nitakufindisha faida za kusoma quran kwa Tajwid.

Soma Zaidi...
As-Sab nuzul
As-Sab nuzul

Sababu za kuteremshwa baadhi ya sura Katika darsa hii tutaangalia sababu za kushuka kwa aya na sura ndani ya quran.

Soma Zaidi...
hukumu za kujifunza tajwid
hukumu za kujifunza tajwid

Kujifunza tajwid ni katika mambo muhimu wakati wa kusoma Quran

Soma Zaidi...
Sababu za kushuka sural Masad (tabat haraka)
Sababu za kushuka sural Masad (tabat haraka)

Sura hii inazungumzia kuhusu hali ya Abulahab namke wake wakiwa kama Watu waovu. Ni moja katika sura ambazo zilishuka mwanzoni toka Mtume alipoamrishwa kulingana dini kwa uwazi.

Soma Zaidi...