Taasisi za kisiasa za msingi alizotumia mtume (s.a.w) katika kuanzisha dola ya kiislamu madinah

Dola ya kiislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

 

  1. Kujenga Msikiti.

-  Msikiti ulikuwa ndio Ikulu, mahakama, kituocha jeshi, ukumbi wa bunge (shura), n.k. Qur’an (3:95), (2:150).

-  Ulikuwa kituo muhimu cha kiharakati katika kusimamisha na kuendeleza Uislamu. Rejea Qur’an (22:40), (2:114), (72:18) na (9:19).

 

  1. Kujenga Ummah wa Kiislamu.

-  Mtume (s.a.w) aliwapatanisha kabila la Aus na Khazraj Madinah waliokuwa na uadui wa muda mrefu baina yao. Qur’an (3:103).

-  Mtume (s.a.w) pia aliwaunganisha udugu imara kati ya Muhajirina wa   

-    Makkah na Answaar wa Madinah na kuwa ummah mmoja. Qur’an (8:75).

-  Pia aliimarisha uchumi kwa kuunganisha ummah wa Kiislamu na kuwa kitu  kimoja. Qur’an (59:8-9).

 

  1. Kuweka Mkataba wa Madinah (Madinah Charter).

-  Mtume (s.a.w) alijieleza katika mkataba huo kuwa yeye ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na ndiye kiongozi mkuu wa Dola ya Kiislamu.

-  Mkataba uliainisha vipengele vya amani na wajibu wa kila kundi kati ya makabila ya Mayahudi na Waarabu washirikina wa Madinah na Dola ya Kiislamu Madinah. 

-  Uliainisha nafasi, majukumu na wajibu wa waumini katika Dola.

-  Mkataba uliainisha uhuru wa kila mtu kuabudu kwa mujibu wa imani na dini zao.

           

  1. Kuweka Mikataba ya amani na Makabila ya Mayahudi na mengine yaliyokuwa pembezoni mwa Dola ya Kiislamu Madinah.

-  Makabila na koo tatu za Kiyahudi zenye nguvu zilizokuwa pembezoni mwa mji wa  Madinah yalikuwa;

 

  1. Kuunda Shura na Sekretarieti.

-  Mtume (s.a.w) aliteua washauri wake wakuu katika kuendesha Dola ambao Walikuwa Abu Bakr (r.a), Umar bin Khattab (r.a), Uthman bin Affan (r.a), Ally bin Abu Twalib (r.a) na Hamza bin Abdul-Muttalib (r.a).

 

-  Aliteua waandishi maalumu wa kuandika na kutunza mikataba, takwimu, kumbukumbu na nyaraka zote za Dola ya Kiislamu Madinah. 

 

  1. Kuandaa Ummah wa Kiislamu Kijeshi na Kiusalama.

-  Mtume (s.a.w) aliwaanda na kuwahimiza waislamu kuwa wakakamavu na hodari katika shabaha, mieleka na kutumia silaha.

-  Kila Muislam alikuwa mpiganaji na mpelelezi dhidi ya maadui wa waislamu na Dola ya Kiislamu.  Rejea Qur’an (4:71).

-  Aliunda na kuweka vikosi vya doria na ulinzi kuzunguka mipaka ya Dola ya Kiislamu Madinah. Qur’an (8:26).

 

  1. Kuimarisha Uchumi.

-  Mtume (s.a.w) aliwahimiza waislam kufanya kazi kwa bidii ili kujiimarisha Kiuchumi na kuendeleza Dola.

-  Utoaji wa Zaka, Sadaka na mapato mengine yalihimizwa na kukusanywa Kijamii na kuboresha huduma za jamii.

Rejea Qur’an (22:41).

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1181

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰2 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰4 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰5 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana: