Home Afya Shule ICT Burudani Dini Maktaba Maswali Madrasa Apps Blog Legacy Login

TAASISI ZA KISIASA ZA MSINGI ALIZOTUMIA MTUME (S.A.W) KATIKA KUANZISHA DOLA YA KIISLAMU MADINAH


image


Dola ya kiislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)


  • Hatua na Mambo (Taasisi za Kisiasa) za msingi alizotumia Mtume (s.a.w) katika kuanzisha Dola ya Kiislamu Madinah.

 

  1. Kujenga Msikiti.

-  Msikiti ulikuwa ndio Ikulu, mahakama, kituocha jeshi, ukumbi wa bunge (shura), n.k. Qur’an (3:95), (2:150).

-  Ulikuwa kituo muhimu cha kiharakati katika kusimamisha na kuendeleza Uislamu. Rejea Qur’an (22:40), (2:114), (72:18) na (9:19).

 

  1. Kujenga Ummah wa Kiislamu.

-  Mtume (s.a.w) aliwapatanisha kabila la Aus na Khazraj Madinah waliokuwa na uadui wa muda mrefu baina yao. Qur’an (3:103).

-  Mtume (s.a.w) pia aliwaunganisha udugu imara kati ya Muhajirina wa   

-    Makkah na Answaar wa Madinah na kuwa ummah mmoja. Qur’an (8:75).

-  Pia aliimarisha uchumi kwa kuunganisha ummah wa Kiislamu na kuwa kitu  kimoja. Qur’an (59:8-9).

 

  1. Kuweka Mkataba wa Madinah (Madinah Charter).

-  Mtume (s.a.w) alijieleza katika mkataba huo kuwa yeye ni Mtume wa Mwenyezi Mungu na ndiye kiongozi mkuu wa Dola ya Kiislamu.

-  Mkataba uliainisha vipengele vya amani na wajibu wa kila kundi kati ya makabila ya Mayahudi na Waarabu washirikina wa Madinah na Dola ya Kiislamu Madinah. 

-  Uliainisha nafasi, majukumu na wajibu wa waumini katika Dola.

-  Mkataba uliainisha uhuru wa kila mtu kuabudu kwa mujibu wa imani na dini zao.

           

  1. Kuweka Mikataba ya amani na Makabila ya Mayahudi na mengine yaliyokuwa pembezoni mwa Dola ya Kiislamu Madinah.

-  Makabila na koo tatu za Kiyahudi zenye nguvu zilizokuwa pembezoni mwa mji wa  Madinah yalikuwa;

  • Banu Quraizah
  • Banu Qainuqa na
  • Banu Nadhir

 

  1. Kuunda Shura na Sekretarieti.

-  Mtume (s.a.w) aliteua washauri wake wakuu katika kuendesha Dola ambao Walikuwa Abu Bakr (r.a), Umar bin Khattab (r.a), Uthman bin Affan (r.a), Ally bin Abu Twalib (r.a) na Hamza bin Abdul-Muttalib (r.a).

 

-  Aliteua waandishi maalumu wa kuandika na kutunza mikataba, takwimu, kumbukumbu na nyaraka zote za Dola ya Kiislamu Madinah. 

 

  1. Kuandaa Ummah wa Kiislamu Kijeshi na Kiusalama.

-  Mtume (s.a.w) aliwaanda na kuwahimiza waislamu kuwa wakakamavu na hodari katika shabaha, mieleka na kutumia silaha.

-  Kila Muislam alikuwa mpiganaji na mpelelezi dhidi ya maadui wa waislamu na Dola ya Kiislamu.  Rejea Qur’an (4:71).

-  Aliunda na kuweka vikosi vya doria na ulinzi kuzunguka mipaka ya Dola ya Kiislamu Madinah. Qur’an (8:26).

 

  1. Kuimarisha Uchumi.

-  Mtume (s.a.w) aliwahimiza waislam kufanya kazi kwa bidii ili kujiimarisha Kiuchumi na kuendeleza Dola.

-  Utoaji wa Zaka, Sadaka na mapato mengine yalihimizwa na kukusanywa Kijamii na kuboresha huduma za jamii.

Rejea Qur’an (22:41).



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Jifunze fiqh       ðŸ‘‰    2 Magonjwa na afya       ðŸ‘‰    3 Madrasa kiganjani       ðŸ‘‰    4 Mafunzo ya html kwa kiswahili       ðŸ‘‰    5 Hadiythi za alif lela u lela       ðŸ‘‰    6 Maktaba ya vitabu    


Je! una maswali, mapendekezo ama maoni? tuma ujumbe wa meseji SMS hapo chini ili kuunganishwa na muhusika au bofya hapa

SMS SMS

Imeandikwa na Tags Dini , DARSA , ALL , Tarehe 2022/01/25/Tuesday - 10:20:11 am     Share On facebook or WhatsApp Topic school Zaidi Dini AFYA ICT Burudani Tags Uzazi maswali Afya mengineyo dini HIV Sira vyakula Matunda HTML php Alif Lela 1 Alif Lela 2 FANGASI Dawa SQL Tips Quran Sunnah fiqh DARSA Magonjwa Tajwid tawhid simulizi Dua Academy Wahenga chemshabongo WAJUWA Michezo ICT Imesomwa mara 615



Post Nyingine


image Vita vya uhudi
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Siku zilizoharamishwa kufunga Sunnah
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Maswali juu ya haki na uadilifu katika uislamu
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3:Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Tofauti kati ya hijjah na umrah
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kwa nini Elimu imepewa nafasi ya kwanza katika Uislamu?
Kwa nini katika uislamu elimu imepewa nafasi ya kwanza ( EDK form 1 Dahana ya elimu) Soma Zaidi...

image Maandalizi ya hijrah ya mtume na waislamu kuhamia madinah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Uandishi wa hadithi wakati wa tabii tabiina
Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kumswalia maiti, masharti ya swala ya maiti
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Kwanini funga imefaradhishwa mwezi wa ramadhani
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

image Mafunzo yatokanayo na upinzani wa maquraish dhidi ya uislamu
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...