Jinsi ya kumuandaa maiti baada ya kufa


image


Haya ni maandalizi ya kumuandaa maiti baada ya kufariki.


Mambo Anayofanyiwa Mtu mara tu baada ya Kufa

Baada ya kushuhudia kuwa ndugu yetu ameshakata roho vyema tuseme na kuzingatia maneno yafuatayo kama alivyotufahamisha Allah (s.w)
“... Hakika sisi ni wa Allah na kwake tutarejea ...” (2:156).

 


Maneno haya ni ya msingi sana katika hali hii ya kufiwa, kwani yanawaliwaza wafiwa na kuwaepusha na fadhaa zinazoweza kutokea juu ya kifo cha marehemu. Ukizingatia maneno ya aya hii utaona kuwa kwa vyovyote iwavyo, kurejea kwa Allah ni jambo lisilozuilika. Hivyo, chochote kile kitakachokuwa ndio sababu ya kifo cha marehemu kitakuwa ni sababu tu ya kifo hicho aliyoiweka Allah (s.w)

 


Baada ya maliwazo haya maiti ile yapasa kufanyiwa yafuatayo:

 

1. Kwa taratibu rudishia mdomo usibakie wazi kwa kufunga kidevu kwa kitambaa na kukizungushia kichwani.

 


2. Funga macho ya marehemu kwa taratibu na huku ukisoma:

 


“Kwa jina la Allah na kwa kufuata mila ya Mjumbe wa Allah. Ewe Mola wetu mrahisishie mambo yake ya sasa na msahilishie mambo yake baadaye. Na jaalia atakayokutana nayo yawe bora kuliko aliyoachana nayo”.

 


3. Lainisha viungo vya maiti kwa kukunja na kukunjua pole pole sehemu zote zenye viungo katika mikono na miguu. Kama patakuwa na ugumu wowote katika kumnyoosha viungo hivyo, maji ya moto au mafuta yanaweza kutumika ili kulainisha. Baada ya kulainisha viungo, miguu na mikono inyooshwe na alazwe huku uso ukielekea Qibla kwenye kitanda kisichokuwa na godoro.

 


4. Maiti avuliwe nguo zote alizokufa nazo kisha kumgubikwa kwa shuka kubwa, pia ni vyema afungwe kitambaa tumboni au kuwekewa kitu chenye uzito kidogo juu ya tumbo ili lisifutuke sana.

 


5. Marashi na ubani vitumike sana mahali alipo maiti ili kuzima harufu ya uvundo itokayo kwa maiti.Mwanaadamu ni msafi sana anapokuwa hai. Lakini muda mfupi tu baada ya kufa huanza kutoa harufu kali ya uozo.

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    2 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    3 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    4 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Mambo ya kuzingatia kabla ya kugawa mirathi
Haya ni mamno muhimu yanayozingatiwa kabla ya kuanza zoezi la kugawa mirathi ya marehemu. Soma Zaidi...

image Nini maana ya kusimamisha swala
Post hii inakwenda kukufundisha maana ya kusimamisha swala kama inavyotumika kisheria. Soma Zaidi...

image Hii ndio hutuba ya ndoa ya kiislamu
Hapa utajifunza utaratibu wa hutuba ya ndoa ya kiislamu. Sharti za jutuba ya ndoa na jinsibya kuozesha Soma Zaidi...

image Utaratibu wa kuzuru makaburi na dua zinazosomwa wakati wa kuzuru kaburi
Post hii itakufundisha taratibu zinazofanyika katika kuzuru kaburi la muislamu. Soma Zaidi...

image Maandalizi kwa ajili ya kifo
Mwanadamu anatakiwa aishi huku akikumbuka kuwa ipo siki atakufa. Hivyo basi inatupata lujiandaa mapema kwa ajili ya kifo. Soma Zaidi...

image Sifa za kuwa maamuma kwenye swala na namna ya kumfuata imamu
Post hii inakwenda kukuelezea sifa za kuwa maamuma na taratibu za kumfuata imamu. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kushona sanda ya maiti na kumvisha yaani kumkafini
Hapa utajifunza taratibu za kumkafini maiti wa kiislamu. Yaani kushona sanda yake na kumvisha. Soma Zaidi...

image Faida na umuhimu wa nfoa katika jamii
Hapa utajifunza faida za ndoa katika Jamii na kwa wanadamu kiafya, kiroho, kiuchumi Soma Zaidi...

image Jinsi ya kufanya suluhu kati ya mume na mke.
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kufanya suluhu katika ndoa. Soma Zaidi...

image Siku ambazo haziruhusiwi kufunga
Ni haramu kufunga katika masiku haya. Na endapo utafunga basi funga haitakuwa na malipo. Soma Zaidi...