Haya ni maandalizi ya kumuandaa maiti baada ya kufariki.
Mambo Anayofanyiwa Mtu mara tu baada ya Kufa
Baada ya kushuhudia kuwa ndugu yetu ameshakata roho vyema tuseme na kuzingatia maneno yafuatayo kama alivyotufahamisha Allah (s.w)
“... Hakika sisi ni wa Allah na kwake tutarejea ...” (2:156).
Maneno haya ni ya msingi sana katika hali hii ya kufiwa, kwani yanawaliwaza wafiwa na kuwaepusha na fadhaa zinazoweza kutokea juu ya kifo cha marehemu. Ukizingatia maneno ya aya hii utaona kuwa kwa vyovyote iwavyo, kurejea kwa Allah ni jambo lisilozuilika. Hivyo, chochote kile kitakachokuwa ndio sababu ya kifo cha marehemu kitakuwa ni sababu tu ya kifo hicho aliyoiweka Allah (s.w)
Baada ya maliwazo haya maiti ile yapasa kufanyiwa yafuatayo:
1. Kwa taratibu rudishia mdomo usibakie wazi kwa kufunga kidevu kwa kitambaa na kukizungushia kichwani.
2. Funga macho ya marehemu kwa taratibu na huku ukisoma:
“Kwa jina la Allah na kwa kufuata mila ya Mjumbe wa Allah. Ewe Mola wetu mrahisishie mambo yake ya sasa na msahilishie mambo yake baadaye. Na jaalia atakayokutana nayo yawe bora kuliko aliyoachana nayo”.
3. Lainisha viungo vya maiti kwa kukunja na kukunjua pole pole sehemu zote zenye viungo katika mikono na miguu. Kama patakuwa na ugumu wowote katika kumnyoosha viungo hivyo, maji ya moto au mafuta yanaweza kutumika ili kulainisha. Baada ya kulainisha viungo, miguu na mikono inyooshwe na alazwe huku uso ukielekea Qibla kwenye kitanda kisichokuwa na godoro.
4. Maiti avuliwe nguo zote alizokufa nazo kisha kumgubikwa kwa shuka kubwa, pia ni vyema afungwe kitambaa tumboni au kuwekewa kitu chenye uzito kidogo juu ya tumbo ili lisifutuke sana.
5. Marashi na ubani vitumike sana mahali alipo maiti ili kuzima harufu ya uvundo itokayo kwa maiti.Mwanaadamu ni msafi sana anapokuwa hai. Lakini muda mfupi tu baada ya kufa huanza kutoa harufu kali ya uozo.
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Fiqh Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1187
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya
👉2 kitabu cha Simulizi
👉3 Simulizi za Hadithi Audio
👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉5 Madrasa kiganjani
👉6 Kitau cha Fiqh
haki na wajibu kwa wakubwa
Soma Zaidi...
Haya ndio yanayobatilisha Hija
Soma Zaidi...
Hawa ndio wanaoruhusiwa kurithi
Hii ni orodha ya watu ambao wanaweza kurithi malibya marehrmu. Soma Zaidi...
NAMNA YA KUSWALI
13. Soma Zaidi...
Ni zipi sifa za imamu wa swala?
Soma Zaidi...
Usawa na uhuru wa kuchuma mali katika uislamu
Uchumi wa uislamu umeweka taratibu mbalimbali katika kuchuma mali. Soma Zaidi...
Kuandama kwa Mwezi na Kufunga ama kufungua ramadhani, sheria na hukumu za kuangalia mwezi
Soma Zaidi...
Ni mambo gani yanaharibu na kutengua udhu?
Soma Zaidi...
mambo gani ni haramu kwa mwenye damu ya Hedhi na nifasi (damu ya uzazi)
Soma Zaidi...
Nini maana ya kusimamisha swala?
Je kusimamisha swala kuna maana gani kwenye uislamu? Soma Zaidi...
Aina au migawanyo mbalimbali ya haki katika uislamu
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Sifa za uchumi wa kiislamu na njia halali za uchumi na umiliki mali katika uislamu
Soma Zaidi...