Kiungulia, dawa yake na namna ya kuzuia kiungulia
Tambuwa kiungulia, sababu zake, dawa za kiungulia na namna ya kupambana na kiungulia
NJIA ZA KUZUIA KIUNGULIA
Kiungulia hutokea pale tindikali zilizopo tumboni zinapanda juu na kufikia koo sehemu ambayo inaunganisha tumbo na koo la chakula. Kiungulia sio shida sana kiafya kwani huwa kiaondoka chenyewe. Hata hivyo kuna watu wapo hatari kupata kiungulia cha mara kwa mara.
Je na wewe ni mmoja katika wanaopata kiungulia mara kwa mara. Je kiungulia ni kikali kiasi cha kuharibu ratiba na uhuru wako? Makala hii ni kwa ajili yako. Hapa nitakuletea njia ambazo zitakusaidia kuzuia kiungulia cha mara kwa mara.
Njia za kuzuia kiungulia
1.Usile chakula kingi kupitiliza
2.Punguza uzito ulio nao
3.Punguza unywaji wa pombe
4.Usinywe sana chai ya majani ya chai yenye caffein kwa wingi
5.Tafuna bigjii zisizo na sukari nyingi
6.Wacha kutumia kitunguu kisichopikwa kama kwenye kachumbari
7.Epuka vinywaji vyenye carbonate. Soma lebo ya kinywaji chako kama ni soda ama maji kama kuna carbonate
8.Usinywe kwa wingi juisi zilizotokana na vitu vya uchachu kama limao
9.Punguza kula chokoleti kwa wingi
10.Unapolala inuka kichwa chako kwa mfano tumia mto
11.Usilale ndani ya masaa matatu baada ya kula
12.Ukilala lalia upande wa kushoto usilalie upande wa kulia.
Dawa za kutibu kiungulia
Unaweza kutibu kiungulia kwa kutumia antacid kama vile Tums, Rolaids na Maalox. Dawa ambazo zimetengenezwa kwa madini ya calcium carbonate au magnesium ni nzuri pia. Magnesium si nzuri kama ujauzito upo mwishoni.
Madaktari wengi wanakataza kwa wajawazito matumizi ya antacid ambazo zimechanganywa na sodium, ama zila lebo ya aluminium carbonate kwani zinawza kupelekea kukosa choo. Pia dawa hizi za kiungulia zinakatazwa kwa wajawazito Alka-Seltzer.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 Kitau cha Fiqh π2 Madrasa kiganjani π3 Kitabu cha Afya π4 kitabu cha Simulizi π5 Bongolite - Game zone - Play free game π6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Madhara ya kaswende kwa wajawazito na watoto wadogo.
Posti inahusu zaidi madhara ya kaswende kwa mama mjamzito na mtoto, Ni ugonjwa unaopatikana hasa kwa njia ya kujamiiana na utoka kwa mwenye Ugonjwa kwenda kwa mtu ambaye hana ugonjwa, kwa hiyo tunapaswa kujua madhara ya ugonjwa huu kwa mama mjamzito na mt
Soma Zaidi...Huduma kwa mtoto mwenye Maambukizi kwenye mifupa
Posti hii inahusu zaidi msaada kwa mtoto mwenye Maambukizi kwenye mifupa, ni huduma anayopewa mtoto mwenye Maambukizi kwenye mifupa.
Soma Zaidi...Habari za leo ndugu zangu mimi Ni dalili zipi hasa za awali zinazoashiria umeambukizwa ukimwi
Anataka kujuwa dalili za awali za kujuwa kuwa umeathirika na UKIMWI
Soma Zaidi...Tofauti kati ya homa ya mapafu (Nimonia) na mafua makali.
βMara nyingi watu huchanganya Nimonia (Pneumonia) na mafua makali kwa sababu yote huathiri mfumo wa upumuaji. Hata hivyo, haya ni magonjwa tofauti kimsingi: mafua husababishwa na virusi na huathiri njia ya juu ya hewa (pua, koo), wakati Nimonia ni maambukizi ya viini (bakteria, virusi, au fangasi) yanayoshambulia mifuko ya hewa ndani ya mapafu (alveoli). Makala hii inaelezea tofauti za kifizikia na umuhimu wa kupata matibabu sahihi.
Soma Zaidi...Madhara ya gonorrhea endapo haitotibiwa
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya gonorrhea endapo haitotibiwa
Soma Zaidi...Saratani ya tezi dume (Prostate Cancer): Dalili za mwanzo kwa wanaume.
Saratani ya tezi dume ndiyo saratani ya kawaida zaidi kwa wanaume duniani kote. Ingawa inaweza kutisha, saratani hii inatibika vyema ikiwa itagunduliwa katika hatua za mwanzo. Makala haya yanalenga kutoa elimu muhimu kuhusu dalili za mwanzo, mambo yanayoongeza hatari, na umuhimu wa wanaume kufanya uchunguzi wa mara kwa mara ili kulinda afya zao.
Soma Zaidi...