Tambuwa kiungulia, sababu zake, dawa za kiungulia na namna ya kupambana na kiungulia
NJIA ZA KUZUIA KIUNGULIA
Kiungulia hutokea pale tindikali zilizopo tumboni zinapanda juu na kufikia koo sehemu ambayo inaunganisha tumbo na koo la chakula. Kiungulia sio shida sana kiafya kwani huwa kiaondoka chenyewe. Hata hivyo kuna watu wapo hatari kupata kiungulia cha mara kwa mara.
Je na wewe ni mmoja katika wanaopata kiungulia mara kwa mara. Je kiungulia ni kikali kiasi cha kuharibu ratiba na uhuru wako? Makala hii ni kwa ajili yako. Hapa nitakuletea njia ambazo zitakusaidia kuzuia kiungulia cha mara kwa mara.
Njia za kuzuia kiungulia
1.Usile chakula kingi kupitiliza
2.Punguza uzito ulio nao
3.Punguza unywaji wa pombe
4.Usinywe sana chai ya majani ya chai yenye caffein kwa wingi
5.Tafuna bigjii zisizo na sukari nyingi
6.Wacha kutumia kitunguu kisichopikwa kama kwenye kachumbari
7.Epuka vinywaji vyenye carbonate. Soma lebo ya kinywaji chako kama ni soda ama maji kama kuna carbonate
8.Usinywe kwa wingi juisi zilizotokana na vitu vya uchachu kama limao
9.Punguza kula chokoleti kwa wingi
10.Unapolala inuka kichwa chako kwa mfano tumia mto
11.Usilale ndani ya masaa matatu baada ya kula
12.Ukilala lalia upande wa kushoto usilalie upande wa kulia.
Dawa za kutibu kiungulia
Unaweza kutibu kiungulia kwa kutumia antacid kama vile Tums, Rolaids na Maalox. Dawa ambazo zimetengenezwa kwa madini ya calcium carbonate au magnesium ni nzuri pia. Magnesium si nzuri kama ujauzito upo mwishoni.
Madaktari wengi wanakataza kwa wajawazito matumizi ya antacid ambazo zimechanganywa na sodium, ama zila lebo ya aluminium carbonate kwani zinawza kupelekea kukosa choo. Pia dawa hizi za kiungulia zinakatazwa kwa wajawazito Alka-Seltzer.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Saratani ya Koo inarejelea Vivimbe vya Saratani vinavyotokea kwenye koo lako (koromeo), sanduku la sauti (larynx) au tonsils.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi tatizo la fizi kuachana, ni tatizo ambalo uwakumba watu wengi kwa wakati mwingine unakuta fizi zimeachana kutoka sehemu moja kwa nyingine kwa hiyo tunaweza kuona sababu kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi maambukizi kwenye epididimisi, ni maambukizi ambayo hutokea kwenye epididimisi na kusababisha matatizo mengi.
Soma Zaidi...Post hii inazungumzia kuhusiana na Sababu zinazopelekea kuvimba kwa kope, kawaida huhusisha sehemu ya kope ambapo kope hukua na kuathiri kope zote mbili. Pia hutokea wakati tezi ndogo za mafuta ziko karibu na msingi wa kope huziba. Hii inasababisha kuw
Soma Zaidi...Je na wewe unasumbukiwa na kunggoka jwa kucha. Tatizo limekunaza una muda gani nalo?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu dalili za ukosefu wa misuli. ukosefu wa udhibiti wa misuli wakati wa harakati za hiari, kama vile kutembea au kuokota vitu. Ishara ya hali ya msingi, Ataxia inaweza kuathiri harakati, hotuba, harakati za jicho na kumeza.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kuharisha, kuharisha ni kitendo Cha kupitia kinyesi chenye maji inawezekana kina damu au kisichokuwa na damu.
Soma Zaidi...Nimonia ni Hali ya kuvimba pafu inayoathiri hasa vifuko vya hewa viitwavyo Alveoli, husababishwa na Maambukizi ya virusi
Soma Zaidi...