Dalili za gonorrhea - gonoria

Dalili za gonorrhea - gonoria

Jifunze dalili za gonorrhea na namna inavyoambukiza, zipi athari za gonori kwa wanawae na wanaume

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Dalili za gonorrhea - gonoria

Dalilii za gonorrhea



Gonorrhea au gonoria ni moja kati ya magonjwa yanayoenezwa kupitia ngono. Huweza kusababishwa na bakteria na kuathiri wanaume na wanawake. Kuweza kuathiri mdomo, koo, mkundu na sehemu za siri kwa wanaume na wanawake. Huweza kuambukizwa kwa kupitia ngono ya mdomo, ngono ya ukeni ama kwenye mkundu. Kwa watoto huweza kuathiri macho. Gonorrhea (gonoria) huambukizwa kutoka kwa mama kuja kwa mtoto wakati wa kujifunguwa.



Dalili za gonoria (gonorrhea) zinaweza kuchelewa kuonekana kwa wanawake kuliko kwa wanaume. Wapo wengine hawaonyeshi dalili yeyote ile hadi hali itakapokuwa ni mbaya zaidi. Kwa mara nyingi dalili za gonoria (gonorrhea) huonekana kuanzia siku 2 mpaka 7 baada ya kuambukizwa. Na kwa wanawake inaweza kuchelewa zaidi hadi mwezi.



Ni zipi dalili za gonoria (gonorrhea)?
Dalili za gonoria (gonorrhea) unaweza kuwa na dalili tofautitofauti kulingana na jinsia. Dalili kwa wanawae na kwa wanaume zinaweza kutofautiana kulingana na maumbile ya jinsia hizi. Muda wa kutokea dalili hizi pia hutofautiana. Pia huweza kuahiri maeneo mengi mwilini.



Dalili za gonorrhea kwa wanaume:-
1.Maumivu wakati wa kukojoa
2.Kutokwa na majimaji kama usaha kwenye uume.
3.Kuvimba pamoja na maumivu ya korodani.



Dalili za gonorrhea kwa wanawake
1.Kutokwa na uchafu sehemu za siri
2.Maumivu makali ya maeneo ya nyonga
3.Maumivu makali wakati wa kukojoa
4.Kutokwa na damu kabla ya hedhi na baada ya hedhi



Dalili za gonoria (gonorrhea) katika maeneo mengine ya mwili:
1.Maumivu ya mkundu, na kutokwa na kama kinyesi pamoja na maumivu ya tumbo na mvurugiko.
2.Maumivu ya macho, kushindwa kuvumilia mwanga mkali, na macho kutoa kama usaha
3.Vidonga vya koo na kuvimba kwa tezi na lumph kwenye shingo
4.Maumivu ya viungio pamoja na kuwa na joto.



Ni nini chanzo na sababu ya gonoria (gonorrhea)
Kama nilivyotangulia kukuambia hapo juu kuwa gonoria huambukizwa na bakteria. Bakteria hawa hufahamika kwa jina la bacterium Neisseria gonorrhoeae. Na huenezwa kwa njia ya kufanya ngono ya mdomo, mkundu ama ukeni.



Waliohatarini kupata gonorrhea (gonoria)
Watu wa umri wowote wanaweza kupata ugonjwa huu. Hata hivyo kuna ambao wapo hatarini zaidi. Kwa wanawake walio zaidi ya miaka 25 wapo hatarini zaidi. Na wanaume ambao wanashiriki ngono ya mkundu wapo hatarini zaidi. Pia wafuatao wanaweza kuwa hatarini kupata gonorrhea:-




1.Kuanza mahusiano na mpenzi mpya
2.Kuwa na wapenzi zaidi ya mmoja (michepuko)
3.Kuwa na penzi ambayo ana wapenzi wengine (michepuko zaidi)
4.Kuwa na maambukizi ya goniria hapo nyuma ama kuwa na maambukizi mengine ya magonjwa ya ngono.



MADHARA YA GONORIA (GONORRHEA) ENDAPO HAITATIBIWA
Endapo gonoria itachelewa kutibiwa inaweza kuleta madhaya mengi ndani ya mwili kuanzia ugumba, kudhoofu mwili, maumivu na mengineye. Yafuatayo ni madhara ya kuchelewa kutibu gonoria:-



1.Ugumba kwa wanawake. Ugonjwa huu kwa mwanamke unakula via vya uzazi kwa fujo sana. Unaathiri mirija ya falopia ambayo nduo inayohusika kubeba yai na utungaji mzima wa mimba na kusababisha PID yaani Pelvic Inflamatory Deseases. Hivyo mwanamke anahitajika atibiwe mapema kabla madhara hayajakuwa makubwa.

2.Ugumba kwa wanaume. Kwa wanaume gonoria huathiri vimirija vijidogo vilivyopo kwenye korodani. Mirija hii hujulikana kama epididymis. Hali hii hupelekea kuharibika kwa mirija hii hivyo kushindwa kubeba mbegu za kiume kuzitoa nje. Ugonjwa unaosababishwa na uharibifu huu hujullukana kama epididymitis.

3.Mashambukizi ya viungo vingine vya mwili na kuleta homa, upele, vidonda, maimivu ya viungo, kukaza na kuvimba kwa viungio.

4.Huongeza hatari zaidi kwa mwenye VVU na UKIMWI. Watu wenye VVU na UKIMWI ni rahisi kueneza gonoria kwenda kwa mwingine.

5.Kwa watoto waliop[ata gonoria wakati wa lujifunguwa wanaweza kupata upofu na madhara mengine kati afya zao.



NJIA ZA KUPAMBANA NA KUKABILIANA NA GONORIA (GONORRHEA)
1.Kuwa mwaminifu katika mahusiano wacha kuchepuka
2.Hakikisha mwenza wako yupo salama
3.Usishiriki ngono na mtu aliyeathiriwa na magonjwa ya ngono bila kinga
4.Tumia kondomu
5.Pima mara kwa mara gonoria.



.





                   



Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 1801

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

MATIBABU YA VIDONDA VYA TUMBO
MATIBABU YA VIDONDA VYA TUMBO

MWISHO Vidonda vya tumbo vinatibika bila ya shaka.

Soma Zaidi...
 Ugonjwa wa Saratani ya ini.
Ugonjwa wa Saratani ya ini.

Saratani ya ini ni Saratani inayoanzia kwenye seli za ini lako.

Soma Zaidi...
Vipimo vya VVU
Vipimo vya VVU

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vipimo mbalimbali vinavyotumika kupima VVU

Soma Zaidi...
Dalili, chanzo, sababu na vmambo hatari kuhusu kifua kikuu
Dalili, chanzo, sababu na vmambo hatari kuhusu kifua kikuu

Katika makala hii utajifunza kuhusu kifua kikuu, dalili zake, sababu zake, chanzo chake na mambo hatari kwa mgonjwa.

Soma Zaidi...
Dalili za ukimwi, unavyoenezwa na njia za kujikinga
Dalili za ukimwi, unavyoenezwa na njia za kujikinga

Ukimwi ni upungufu wa kinga mwilini.unasababishwa na virusi ambavyo hutokea kwa mtu mwingine kwa njia mbalimbali

Soma Zaidi...
Namna Maambukizi kwenye milija na ovari yanavyotokea
Namna Maambukizi kwenye milija na ovari yanavyotokea

Post hii inahusu zaidi namna Maambukizi kwenye milija na ovari ambayo yanatokea,Mara nyingi usababisha na bakteria wanaoweza kuingia kupitia sehemu mbalimbali.

Soma Zaidi...
Jifunze zaidi mzunguko wa mfumo wa damu kwa binadamu
Jifunze zaidi mzunguko wa mfumo wa damu kwa binadamu

Posti hii inahusu zaidi mfumo wa mwili ambao huhusika na kusafirisha damu ,virutubisho na takamwili.mfumo huu unajumuisha damu,mishipa ya damu na moyo.moyo husukuma damu kupitia mishipa ya damu na kufika maeneo yote ya mwili.

Soma Zaidi...
Yajue maambukizi kwenye epididimisi kwa kitaalamu huitwa (Epididymitis)
Yajue maambukizi kwenye epididimisi kwa kitaalamu huitwa (Epididymitis)

Post hii inahusu zaidi maambukizi kwenye epididimisi, ni maambukizi ambayo hutokea kwenye epididimisi na kusababisha matatizo mengi.

Soma Zaidi...
Ulemavu wa ubongo na mfumo wa fahamu -multiple sclerosis
Ulemavu wa ubongo na mfumo wa fahamu -multiple sclerosis

Posti hii inazungumzia kuhusiana na dadili na sababu zinazopelekea Ugonjwa wa ulemavu wa ubongo na mfumo wa fahamu ambao kitaalamu hujulikana Kama multiple sclerosis.

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa uvimbe na mashambulizi ya bacteria kwenye korodani
Dalili za ugonjwa wa uvimbe na mashambulizi ya bacteria kwenye korodani

Posti hii inaonyesha dalili,Sababu,na namna ya kujikinga na ugonjwa wa uvimbe na mashambulizi ya bacteria kwenye korodani ambao kitaalamu hujulikana Kama orchitis.

Soma Zaidi...