Dalili za gonorrhea - gonoria

Jifunze dalili za gonorrhea na namna inavyoambukiza, zipi athari za gonori kwa wanawae na wanaume

Dalili za gonorrhea - gonoria

Dalilii za gonorrhea



Gonorrhea au gonoria ni moja kati ya magonjwa yanayoenezwa kupitia ngono. Huweza kusababishwa na bakteria na kuathiri wanaume na wanawake. Kuweza kuathiri mdomo, koo, mkundu na sehemu za siri kwa wanaume na wanawake. Huweza kuambukizwa kwa kupitia ngono ya mdomo, ngono ya ukeni ama kwenye mkundu. Kwa watoto huweza kuathiri macho. Gonorrhea (gonoria) huambukizwa kutoka kwa mama kuja kwa mtoto wakati wa kujifunguwa.



Dalili za gonoria (gonorrhea) zinaweza kuchelewa kuonekana kwa wanawake kuliko kwa wanaume. Wapo wengine hawaonyeshi dalili yeyote ile hadi hali itakapokuwa ni mbaya zaidi. Kwa mara nyingi dalili za gonoria (gonorrhea) huonekana kuanzia siku 2 mpaka 7 baada ya kuambukizwa. Na kwa wanawake inaweza kuchelewa zaidi hadi mwezi.



Ni zipi dalili za gonoria (gonorrhea)?
Dalili za gonoria (gonorrhea) unaweza kuwa na dalili tofautitofauti kulingana na jinsia. Dalili kwa wanawae na kwa wanaume zinaweza kutofautiana kulingana na maumbile ya jinsia hizi. Muda wa kutokea dalili hizi pia hutofautiana. Pia huweza kuahiri maeneo mengi mwilini.



Dalili za gonorrhea kwa wanaume:-
1.Maumivu wakati wa kukojoa
2.Kutokwa na majimaji kama usaha kwenye uume.
3.Kuvimba pamoja na maumivu ya korodani.



Dalili za gonorrhea kwa wanawake
1.Kutokwa na uchafu sehemu za siri
2.Maumivu makali ya maeneo ya nyonga
3.Maumivu makali wakati wa kukojoa
4.Kutokwa na damu kabla ya hedhi na baada ya hedhi



Dalili za gonoria (gonorrhea) katika maeneo mengine ya mwili:
1.Maumivu ya mkundu, na kutokwa na kama kinyesi pamoja na maumivu ya tumbo na mvurugiko.
2.Maumivu ya macho, kushindwa kuvumilia mwanga mkali, na macho kutoa kama usaha
3.Vidonga vya koo na kuvimba kwa tezi na lumph kwenye shingo
4.Maumivu ya viungio pamoja na kuwa na joto.



Ni nini chanzo na sababu ya gonoria (gonorrhea)
Kama nilivyotangulia kukuambia hapo juu kuwa gonoria huambukizwa na bakteria. Bakteria hawa hufahamika kwa jina la bacterium Neisseria gonorrhoeae. Na huenezwa kwa njia ya kufanya ngono ya mdomo, mkundu ama ukeni.



Waliohatarini kupata gonorrhea (gonoria)
Watu wa umri wowote wanaweza kupata ugonjwa huu. Hata hivyo kuna ambao wapo hatarini zaidi. Kwa wanawake walio zaidi ya miaka 25 wapo hatarini zaidi. Na wanaume ambao wanashiriki ngono ya mkundu wapo hatarini zaidi. Pia wafuatao wanaweza kuwa hatarini kupata gonorrhea:-




1.Kuanza mahusiano na mpenzi mpya
2.Kuwa na wapenzi zaidi ya mmoja (michepuko)
3.Kuwa na penzi ambayo ana wapenzi wengine (michepuko zaidi)
4.Kuwa na maambukizi ya goniria hapo nyuma ama kuwa na maambukizi mengine ya magonjwa ya ngono.



MADHARA YA GONORIA (GONORRHEA) ENDAPO HAITATIBIWA
Endapo gonoria itachelewa kutibiwa inaweza kuleta madhaya mengi ndani ya mwili kuanzia ugumba, kudhoofu mwili, maumivu na mengineye. Yafuatayo ni madhara ya kuchelewa kutibu gonoria:-



1.Ugumba kwa wanawake. Ugonjwa huu kwa mwanamke unakula via vya uzazi kwa fujo sana. Unaathiri mirija ya falopia ambayo nduo inayohusika kubeba yai na utungaji mzima wa mimba na kusababisha PID yaani Pelvic Inflamatory Deseases. Hivyo mwanamke anahitajika atibiwe mapema kabla madhara hayajakuwa makubwa.

2.Ugumba kwa wanaume. Kwa wanaume gonoria huathiri vimirija vijidogo vilivyopo kwenye korodani. Mirija hii hujulikana kama epididymis. Hali hii hupelekea kuharibika kwa mirija hii hivyo kushindwa kubeba mbegu za kiume kuzitoa nje. Ugonjwa unaosababishwa na uharibifu huu hujullukana kama epididymitis.

3.Mashambukizi ya viungo vingine vya mwili na kuleta homa, upele, vidonda, maimivu ya viungo, kukaza na kuvimba kwa viungio.

4.Huongeza hatari zaidi kwa mwenye VVU na UKIMWI. Watu wenye VVU na UKIMWI ni rahisi kueneza gonoria kwenda kwa mwingine.

5.Kwa watoto waliop[ata gonoria wakati wa lujifunguwa wanaweza kupata upofu na madhara mengine kati afya zao.



NJIA ZA KUPAMBANA NA KUKABILIANA NA GONORIA (GONORRHEA)
1.Kuwa mwaminifu katika mahusiano wacha kuchepuka
2.Hakikisha mwenza wako yupo salama
3.Usishiriki ngono na mtu aliyeathiriwa na magonjwa ya ngono bila kinga
4.Tumia kondomu
5.Pima mara kwa mara gonoria.



.





                   



Kama unahitaji kuuliza maswali Bofya hapa

Mwandhishi Tarehe 2018-08-01     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 261

Post zifazofanana:-

Ni watu gani wanaopewa Zaka
Soma Zaidi...

Dawa ya fangasi ukeni
Usisumbuliwe tene na fangasi ukeni, zijuwe hapa dalili za fangasi ukeni, tiba yake na njia za kukabiliana na fangasi ukeni Soma Zaidi...

Kwa nini lengo la kutoa zaka halifikiwi na watoaji zaka?
Kwa nini Lengo la Zakat na Sadaqat Halijafikiwa katika Jamii yetu? Soma Zaidi...

HUKUMU ZA MADD
Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa Soma Zaidi...

Mafunzo ya Sura Zilizochaguliwa
Soma Zaidi...

KUWAHI KUMALIZA TENDO LA NDOA MAPEMA: kumwaga mbegu mapema
Hii ni hali inayowapata sana wanaume huwa wanamaliza hamu ya tendo la ndoa mapema kabla ya mwenza kuridhika. Soma Zaidi...

hizi ndio nguzo za swala, swala za faradhi na suna
Soma Zaidi...

Fahamu Vitamini E na nz kazi zake, vyakula vya vitamini E na athari za upungufu wake
Katika makala hii nitakwenda kukupa somo linalohusu vitamini E, kazi zake, chanzo chake na madhara ya upungufu wake Soma Zaidi...

UGENI WA DHATI
Soma Zaidi...

Namna ya kulipa swaumu ya ramadhani na ni nani anatakiwa alipe
Soma Zaidi...

Chemsha bongo namba 03
Tatua mzozo wa NI NANI MUUAJI? Soma Zaidi...

Vyakula vya vitamini C na faida zake
Soma Zaidi...