Makala hii itakufundisha maradho makuu ya macho, matibabu yake na tiba zake
MARADHI YA MACHO
Matatizo ya macho yapo mengi katika jamii, lakini mara nyingi matatizo ya macho yanatibika iwapo mgonjwa ataonana na daktari mara atakapoona dalili. Miongoni mwa matatizo ya macho ni kupoteza uwezo wa kuona.
1.Kutoona karibu (long sightedness)
Tatizo hili mara nyingi huwatokea watu wenye umri wa miaka 40 na kuendelea.
Dalili
A.Katika mazingira ya kawaida anaona sawa sawa
B.Kushindwa kusoma herufi ndogo ndogo
C.Kushindwa kufanya kazi za sehemu ndogo ndogo mfano kutunga sindano.
Matibabu: Kutumia miwani ya kusomea.
2.Kutoona Mbali (short sightedness)
A.Hayana umri maalum
B.Myopia – haoni mbali vizuri
C.Hyperopia – haoni mbali na kichwa kinauma akikosa kuvaa miwani yenye namba ndogo kusaidia lense.
NB: Mgonjwa anasoma karibu bila miwani
Matibabu: Kutumia miwani ya kuonea mbali
3.Mtoto wa Jicho (cataract)
Dalili
A.Kidoto cheupe katikati ya kioo cheusi cha jicho (kinafunika mboni ya jicho)
B.Kidoto cheupe kisichobadilika kwa mwangaza
C.Kupunguza nuru ya macho
NB - Mtu anaweza kuzaliwa nacho au kupata ukubwani, inaweza kuwa kwenye jicho moja au yote. Mgonjwa huona mchanganyiko wa rangi anapoangalia mwangaza kama taa za umeme au gari.
Matibabu
Mtoto wa Jicho huwa anatibika kwa upasuaji mdogo na kumuwezesha mgonjwa kuona tena.
4.Presha ya macho (glaucoma)
Tatizo hili husababishwa na kuongezeka presha ya jicho (intraocular pressure) kutokana na kukosekana uwiano wa mzunguko wa majimaji ndani ya jicho (aqueous fluid) kinachotoka kidogo kuliko kinachoingia.
Matokeo
Glaucoma hukandamiza na kuuharibu mshipa wa fahamu ya jicho na kusababisha kupungua kwa nuru na baadae kupoteza nuru ya macho.
Matibabu: Kuonana na daktari kwa ushauri na dawa
5.Macho tongo
Hutokea ama kwa mtu mmoja mmoja, makundi au kwa msimu.
Sababu:
Vimelea ambavyo huzaliwa kwenye sehemu za uchafu Wakati wa msimu huambukiza kwa kukosa elimu ya afya, kwa mfano kutokuosha mikono baada ya kuamkiana na mgonjwa mwenye maradhi haya au kutumia vifaa vya macho kwa zaidi ya mtu mmoja kama vile miwani.
Dalili
A.Kuhisi kama kuna mchanga ndani ya jicho
B.Kuvimba mifuniko ya macho bila kupoteza nuru.
C.Macho kuwa mekundu sana (conjuctivitis)
D.Kutoka tongo kila mara
Matibabu
Mgonjwa atumie dawa alizoandikiwa na daktari tu, kwani dawa za matone za macho ni nyingi na zina kazi tofauti.
6.Matatizo ya sehemu nyeusi ya jicho (cornea)
Kuna matatizo manne makubwa
1. Kovu - kidoto/kibaka cheupe
2. Kidonda - kidoto kijivujivu
3. Kuingiwa na kitu - kemikali,mdudu, vumbi n.k
4. Kutoboka na kutoa maji.
Indhari: hali ya pili mpaka ya nne zikitokea mgonjwa akimbizwe
hospital wakati jicho limefunikwa baada ya huduma ya kwanza
Dalili
KOVU
1.Haina maumivu
2.Jicho haliwi jekundu
3.Jicho halivimbi
4.kupungua nuru jicho
KIDONDA
A.Kinayo maumivu
B.Jicho lililoathirika huwa
C.jekundu
D.Jicho kupunguka nuru
E.Kuuma jicho kwenye
F.mwangaza
G.Kutoka machozi
H.Jicho kuvimba
Kidonda kinaweza kusababishwa na bakteria, fangas, ukosefu wa vitamin A au kwa kuumia mfano; kujichoma na kitu chenye ncha au kitu kigumu, kuingiwa na kitu jichoni, kuungua au kuingia kemikali jichon.
Indhari: Iwapo jicho litaumia lifunike jicho lisipate mwangaza kisha mpeleke mgonjwa hospitali.
7. Kemikali na kuungua
Kama mgonjwa ameingia kemikali kama vile acid, alkali, saruji, chokaa mtie maji ya mchuruziko kwa takriban dakika 15 mfululizo na baadae mpeleke hospitali
8.Macho kuwasha na kutokwa na machozi (conjuctivitis)
Huwakumba zaidi watoto wa umri kati ya miaka 5 -15 ambao hupendelea kucheza sehemu za vumbi au kwenye muangaza mkali (pwani yenye mchanga mweupe sana)
Watu wazima wenye kufanya kazi kwenye viwanda vinavozalisha vumbi, na wenye pumu ya muda mrefu.
Dalili
A.Macho kuwasha (Nuru ya macho haipungui)
B.Macho kubadilika rangi (kahawia)
C.Kutokwa na machozi mengi (sana)
D.Kushindwa kuangalia kwenye muangaza mkali
Matibabu
Kusafisha macho mara kwa mara kwa maji safi.
Kutumia dawa kwa maelekezo ya daktari
9.Kinundu katika mfuniko wa juu au chini wa jicho
DALILI
A.Kinundu kisichouma
B.Mara nyingi hupona wenyewe au unaweza kukikanda kwa maji ya uvuguvugu.
C.Kisipopona au kitakapokuwa kikubwa huhitaji upasuaji mdogo.
10.Uvimbe katika mfuniko wa jicho (cellulitis)
A.uvimbe kwenye mifuniko ya jicho
B.inaweza kuzuwia jicho kucheza (kutembea tembea)
C.mara nyingi hutokea baada ya kusambaa kwa maambukizo
D.ya socket ya jicho kutoka pembezoni kwa saines (sinusitis) za pua
E.husababisha kupoteza nuru za macho
Matibabu: Mpeleke mgonjwa kwa daktari wa masikio, pua na koo (ENT).
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowAnemia ya upungufu wa vitamini ni ukosefu wa seli nyekundu za damu zenye afya unaosababishwa na kiasi kidogo cha vitamini fulani kuliko kawaida.
Soma Zaidi...Uvimbe kwenye mfuko wa uzazi hukua kutoka kwenye tishu laini za misuli ya uterasi. Fibroids nyingi ambazo zimekuwepo wakati wa ujauzito hupungua au kutoweka baada ya ujauzito, kwani uterasi inarudi kwenye ukubwa wa kawaida.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi hatua au mbinu za kupambana na ugonjwa wa UTI kwa sababu ugonjwa huu umekuwa tishio kubwa kwa sasa kwa hiyo tunapaswa kutumia njia mbalimbali ili kuweza kupambana na Ugonjwa huu.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi watu walio kwenye liski ya kupata magonjwa ya ngono, ni watu wanaofanya mambo yanayosababisha kupata magonjwa ya ngono.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu visababishi vya vidonda vya tumbo
Soma Zaidi...Homa ni moka ya dalili inayohusiana na maradhi mengi sana. Unaweza kuwa na homa ikawa pia si maradhi kumbe ni stress tu. Je unasumbuliwa na homa za mara kwamara, Makala hii ni kwa ajili yako
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vipimo mbalimbali vinavyotumika kupima VVU
Soma Zaidi...Posti hii inaelezea kuhusiana na Magonjwa mbalimbali ambayo watoto chini ya miaka wanaweza kuyapata kiurahi.
Soma Zaidi...Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu baadhi ya athari zinazoweza kutokea endapo minyoo haitotibiwa
Soma Zaidi...