Menu



KAULI ZA WATU MASHUHURI KUHUSU AFYA

KAULI ZA WATU MASHUHURI KUHUSU AFYA

wajua



KAULI ZA WATAALAMU WA AFYA
Hizi ni nukuu kutoka kwa watu mbalimbali na mashuhuri kuhusu Afya. Tumeamua kuleta nukuu hizi kwa lugha ya kiswahili ili kuwapa wasomaji wetu matumaini wakijua nini wamesema watu mashuhuri duniani kuhusu Afya. Tumeweka nukuu hizi pamoja na kuonesha nani amesema mwishoni mwa nukuu. Somo hili litakuwa endelevu pia hivyo tunawataka wasomaji wetu waendelee kuwa nasi. Pia tunapenda kuwajulisha kuwa App yetu nyingine iitwayo Darasa la Afya ipo karibuni kuja hii imesheheni mambo mengi zaidi. Na kwa sasa App yetu iitwayo AFYA 100 ipo hewana. Hii imekusanya dondoo 100 kuhusu afya.


Kauli za watu Mashuhuri kuhusu afya.
1.”Watu hawapaswi kuangalia wengine na kufikiri maisha ni kipande kimoja cha kupendeza. Hiyo ni masoko, na mizunguko. Maisha ni changamoto. Lakini nina ujasiri, nguvu, na afya nzuri yatosha ili kufikia maengo chanya.” Carmen Dell'Orefice


2.”Akili iliyotulia huleta uwezo wa ndani wa kujiamini na nguvu , na ni muhimu sana kwa afya nzuri”. Dalai Lama


3.”Ili kufurahia afya njema, kuleta furaha ya kweli kwa familia ya mtu, kuleta amani kwa wote, mtu lazima awe na nidhamu kwanza na kudhibiti akili yake mwenyewe. Ikiwa mtu anaweza kudhibiti akili yake anaweza kupata njia ya Kuangazia, na hekima na uzuri wote utakuja kwa kawaida.” Buddha


4.”Ili kufurahia mwanga mzuri wa afya njema, unapaswa kufanya mazoezi”. Gene Tunne


5.”Afya nzuri na akili nzuri ni mambo mawili na ni baraka kubwa zaidi za maisha”. Publilius Syrus


6.”Kuweka mwili kuwa na afya njema ni wajibu ... vinginevyo hatutaweza kuweka akili zetu kuwa njema”. Buddha


7.”Nimekuwa na baraka sana katika maisha yangu kwa kuwa na marafiki wazuri na afya njema. Ninashukuru na furaha kwa kuwa na uwezo wa kushiriki wazo hili”. .Eric Idle


8.”Hakuna kitu muhimu zaidi kuliko afya yetu nzuri - hiyo ndiyo mali yetu kuu katika mali zetu”. Arlen Specter


9.”Afya njema sio kitu tunachoweza kununua. Hata hivyo, inaweza kuwa akaunti muhimu sana ya akiba”. Anne Wilson Schaef


10.”Furaha yetu kubwa haipatikani kwa kutegemeana na hali ya maisha ambayo nafasi imetuweka, lakini daima ni matokeo ya dhamiri njema, afya njema, kazi, na uhuru katika shughuli zote tu”. Thomas Jefferson


UMOJA WA MATAIFA (UN) UNAZUNGUMZIAJE AFA?


Umoja wa mataifa una kitengo ambacho kinajihusisha na masuala yote ya afya kitengo hiko nikajulikana kama World_Health_Organization. Kulingana na tafiti za shirika hili la umoja wa mataifa, nimeamua kukuletea dondoo kadhaa za afya. Dondoo hizi zinahusu takwimu mbalimbali za afya duniani kote. Nitaanza kunukuu moja kati ya taarifa hizo hapo chini..


  • Takribani nusu ya wakazi wa dunia bado hawapati huduma za msingi za afya.
  • Takribani watu milioni 100 bado wanasukumwa kwenye ufukara kwa kuwa hawana uwezo wa kulipia huduma zao za afya.
    Zaidi ya watu milioni 800 , sawa na asilimia 12 ya wakazi wote wa dunia, wanatumia asilimia 10 ya kipato cha kaya kugharimia huduma za afya.
  • Mataifa yote 193 wanachama wa Umoja wa Mataifa wamekubaliana kufikia lengo la huduma ya afya kwa wote ifikapo mwaka 2030, ikiwa ni sehemu ya malengo ya maendeleo endelevu, SDGs.

Huu ni ukweli usio pingika kwamba bado vijijini kuna watu wengi sana ambao wanaishi huko hali ya kuwa huduma za afya haipo vizuri ukilinganisha maeneo ya mijini. Mfano mzuri ni ukosekanaji wa baadhi ya vifaa vya kutolea huduma za afya na wakati mwingine hali ya usafiri kuwa mbovu huchangia matatizo ya afya kuendelea kutokea. Elimu ya afya pia maeneo ya vijijini haipatikani ipasavyo, na ndio maana hata hali ya unyanyasaji kwa wenye HIV imekuwa kubwa vijijini kuliko mijini.


Sambamba na kuwa utoaji wa huduma bora za afya maeneo mengi duniani haupo vizuri, na hii ni kutokana na kipato cha wananchi wenyewe. Atahitajika kununua dawa ama kulipia vipimo. Serikali mbalimbali zimeweka utaratibu wa kulipia bima ili kuboresha huduma za afya, hii ni nzuri lakini bado wananchi wengi hawajaweza kuchangia huduma hio. Huenda ni kulingana na kipato chao ni kidogo ama kutokana na kutokuwa na elimu ya kutosha juu ya umuhimu wa kulipia bima ya afya .


Elimu ya afya inahitajika zaidi ili kuweza kuhakikisha maeneo mengi yanapata huduma hizi za afya. Kwa nini elimu ya afya? hii ni kwa sababu endapo wananchi wataelimishwa wataweza kuboresha huduma za afya kwa nguvu zao na raslimali zao. Serikali nazo pia kwa upande mwingine zihakikishe kuwa uboreshwaji wa afya unafikia mpaka maeneo ya vijijini, na wananchi wanashiriki kwa umakini maswala yote ya afya.





                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Post File: Download PDF Views 1315

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zinazofanana:

Umuhimu wa kupiga push up kiafya

Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa kupiga push up kiafya, ni mambo au faida zipatikanazo ki afya kwa wapigaji wa push up kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
VIZAZI

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
ZIJUWE FIGO, KAZI ZA FIGO NA NAMNA YA KULINDA FIGO DHIDI YA MARADHI

Je unatambuwa namna fgo inavyofanya kazi, unazijuwa kazikuu za fogo mwilini, na je unajuwa namna ya kujilinda dhidi ya maradhi ya figo?. Basi makala hii itakujuza kuhusu masomo haya1

Soma Zaidi...
darasa la lishe

Jifunze mengi kuhusu afya na lishe, ujuwe utaratibu wa lishe

Soma Zaidi...
KITABU HA MATUNDA

Jifunze sifa na aina za matunda, vijuwe viruturubisho

Soma Zaidi...
MAZINGIRA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Madhara ya kutumia tissue au toilet paper

Post hii inahusu zaidi madhara ambayo tunaweza kuyapata katika matumizi ya toilet paper au tisu kwenye sehemu za siri.

Soma Zaidi...
dondoo 100 za Afya

Basi tambua haya;- 21.

Soma Zaidi...
Kujiepusha na Vishawishi vya Zinaa

Kujiepusha na Vishawishi vya ZinaaKatika macho ya sheria kitendo cha zinaa kinahesabiwa pale wanapokutana kimwili mwanamume na mwanamke nje ya ndoa.

Soma Zaidi...