image

Haki na wajibu wa mtoto kwa wazazi na katika jamii

Haki na wajibu wa mtoto kwa wazazi na katika jamii

Wajibu wa Watoto kwa Wazazi



Wajibu wa watoto kwa wazazi wao ni kuwatii katika kiwango cha hali ya juu, kuwaheshimu na kuwahurumia hasa wanapokuwa wazee. Kuwatii wazazi ni kitendo kinachochukua nafasi ya juu sana katika Uislamu. Utii kwa wazazi huchukuwa nafasi baada tu ya Kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Msisitizo wa kuwatii wazazi, kuwaonea huruma na kuwafanyia ihsani uko wazi katika Qur-an:


Na Mola wako amehukumu kuwa msimuabudu yeyote ila Yeye tu. Na (ameagiza) kuwafanyia wema (mkubwa) wazazi. Kama mmoja wao akifikia uzee pamoja nawe, au wote wawili, usiwaambie hata A/i! Wala usiwakemee. Na useme nao kwa msemo wa heshima kabisa. Na uwainamishie bawa ?a unyenyekevu kwa (kuwaonea) huruma na useme: 'Mola wangu! Warehemu (wazee wangu) kama walivyonilea katika utoto ". (17:23-24).



Wazazi, hasa mama, wamestahiki kutiiwa kwa kiwango cha hali ya juu, kuwafanyia ihsani na kuhurumiwa na watoto wao hasa wanapokuwa wazee, iii iwe kama malipo ya kazi ngumu ya kuwalea watoto wao. Mtoto hana malipo ya kumlipa mzazi wake kwa kumzaa na kumlea mpaka kufikia utu uzima wake. Malipo anayotakiwa na Mwenyezi Mungu (s.w)


awalipe wazazi wake kwa taabu zote walizochukua katika kumlea ni kumshukuru Mwenyezi Mungu (s.w) na wazazi wake kwa kumtii Mwenyezi Mungu (s.w) na Mtume na kisha kuwatii wazazi wake, kuwafanyia ihsani na kuwahurumia kama tunavyojifunza katika Qur-an:


Na tumemuusia mwanaadamu (kuwafanyia ihsani) wazazi wake - mama yake amechukua mimba yake kwa udhafujuu ya udhafu na kumnyonyesha katika kipindi cha miaka miwili - (tumemuusia) ya kwamba unishukuru Mimi na wazazi wako, marejeo yenu ni kwangu. (31:14)


Na tumemuusia mwanaadamu afanye wema kwa wazazi wake,.Mama yake amechukua mimba yake kwa taabu. Na ku be ha mimba yake hata kumwachisha ziwa, (uchache wake) ni miezi thelathini (46:15). Pia mtoto mwema, pamoja na kuwatii na kuwahurumia wazazi wake kwa kuwapa kila msaada wanaohitajia, huwaombea dua wakiwa hai au wakiwa wametangulia kufa kwa kusema:


Mola wetu! Unighufirie mimi na wazazi wangu wote wawili na wanaoamini Siku ya Hisabu. (14:41). Utii kwa wazazi unatakiwa uendelezwe hata baada ya kufa kwao kama tunavyojifunza katika hadithi: Abu Usaydi as-Said (r.a) amesimulia: Tulikuwa karibu na Mtume (s.a.w) wakati alpomjia mtu wa ukoo wa Salimah na kumuuliza: Ee Mtume wa mwenyezi Mungu! Kuna utii


mwingine uliobakia kwa wazazi baada ya kutawafu kwao? "Ndio" alUibu Mtume. "Kuwaombea dua, kuwaombea msamaha na maghfira kwa Mwenyezi Mungu (s.w), kutekeleza wasia wao, kuwa na uhusiano mwema na wale mliofahamiana kutokana na wao na kuwaheshimu rafiki zao ". (Abu Daud, Ibn Majah)



Pia katika hadithi iliyosimuliwa na Ibn Umar mtume (s.a.w) amesema:
Utii wa hali ya juu kwa wazazi ni mtu kufanya urafiki na marafiki wa baba yake baada ya kufa kwake. (Muslim).
Hata hivyo, kiwango cha utii na huruma ya mtoto kwa wazazi wawili kinatofautiana. Mama anastahiki kupata nafasi ya kwanza ndio baba afuatie kama tunavyojifunza katika hadithi:



Abu Hurairah amesimulia kuwa mtu mmoja aliuliza: Ee Mtume wa Mwenyezi Mungu! Ni nani hasa anayestahiki upendo wangu wa hali ya juu? 'Mama yako ", alijibu Mtume. Kisha akauliza tena: Nani anayefuatia? "Mama yako ", alijibu Mtume. Akauliza tena: Nani anayefuatia? 'Mama yako ' alj/ibu Mtume. Katika maelezo mengine al/ibu Mtume: Mama yako, kisha mama yako, kisha mama yako, kisha baba yako, kisha jamaa zako wa karibu, (Bukhari na Muslim).




                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 956


Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Nguzo za swala.
Kipengele hiki kinaelezea nguzo mbalimbali za kuswali. Soma Zaidi...

Mazao ambayo inapasa kutolewa zaka
Soma Zaidi...

Kuenea kwa dhana ya udhibiti uzazi na uzazi wa mpango
Kustawi kwa Kampeni ya Kudhibiti UzaziMiongoni mwa sababu zilizosaidia kustawi kwa kampeni hii ni matokeo ya mapinduzi ya viwanda (Industrial revolution) ya huko Ulaya. Soma Zaidi...

Swala ya maiti, namna ya kuiswali, nguzo zake, sharti zake na suna zake, hatua kwa hatua
Soma Zaidi...

Ni yapi masharti ya Udhu na kujitwaharisha
Soma Zaidi...

Umuhimu na nafasi za hijjah katika uislamu
Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Jinsi ya kuswali kuswali swala ya maiti
Post hii itakufundisha kuhusu swala ya maiti, nguzo za swala ya maiti, sharti za swwla ya maiti na jinsi ya kuiswali. Soma Zaidi...

Kumswalia maiti, masharti ya swala ya maiti
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Sunnah za siku ya idi na utaratibu wa kusherehekea
Hapa utajifunza utaratibu wa kusherekea ifil fitir. Pia utajifunza sunnah zinazoambatsns na idil fitir Soma Zaidi...

Hili ndio lengo la kufunga.
Ni kwa nini Allah ametutaka tugunge. Je kuna lengo gani hasa katika kufunga. Soma Zaidi...

Kumuosha maiti hatua kwa hatua nguzo zake, na suna zake
Soma Zaidi...

Ndoa ya mke zaidi ya mmoja katika uislamu na taratibu zake, faida zake na namna ya kuitekeleza
- Je, Ukeweza, (ndoa ya mke zaidi ya mmoja) humdhalilisha mwanamke? Soma Zaidi...