Hapa utajifunza sababu zinzopelekea mdomo kubadilika ladha na kuwa mchungu, ama mchachu.
KWA NINI MDOMO UNAKUWA MCHUNGU?
Umeshawahi kuamka asubuhi ukiwa na ladha chungu sana ya mdomo, na je hali hii ulishawahi kudumu nayo kwa muda wa masaa kadhaa?. bila shaka ungependa kujuwa sababu inayopelekea kutkea hali hii. Makala hii ni kwa ajili yako. Hapa nitakujuza sababu kuu za kuwa na ladha chungu ya mdomo, na nini kifanyike. Endelea kusoma makala hii hadi mwisho. Ila ningependa utambuwe kuwa mdomo kuwa mchungu mara nyingi sio shida sana ya kiafya kiasi cha kuhitaji dawa ama kumuona daktari. Endapo shida itaendelea hapo fanya maamuzi ya kuonana na daktari
Mdomo kuwa mchungu mara nyingi sio maradhi. Hali hii hutokea na kuondoka yenyewe ndani ya masaa machache. Mara nyingi hutokea wakati wa asubuhi ama unapotoka kulala. Hali hii pia huwapata wagonjwa. Hali hii wakati mwingine inakuwa ni dalili ya maradhi. Kama utaona mdomo wako unaendelea kuwa mchungu kwa muda mrefu onana na daktari kwa uchunguzi zaidi.
Ni nini husababisha mdomo kuwa mchungu?
1.Mdomo kutokuwa msafi. Hii ni kawaida wakati umelala mdomo bakteria waliokuwa wapo mdomoni wanaendelea kufanya kazi yao, kula mabaki ya chakula na kuendelea kuzaliana. Kumbuka mate yana kazi ya kusafisha mdomo,lakini wakati umelala mate hayawezi kufanya kazi hii kwani huwezi kuyatoa. Hivyo uchafu huendelea kujizalisha bila ya kutolewa. Hali hii inaweza kusababisha mdomo kuwa mchungu unapoamka.
Vyema usile kitu muda huu, kabla ya kupiga msaki. Safisha kinywa vyema ladha ya mdomo itarudi sawa ndani ya muda mchache. Pia kama ulitoka kulala baada ya kutema mate kwa muda mchache yaani baada ya mdomo kujisafisha hali hii inaweza kuondoka bila ya wasi wala hakuna ulazima wa kupiga mswaki, kwani mdomo una sifa ya kujisafish awenyewe kwa kutumia mate.
2.Matumizi ya madawa ya antibiotics au antidepressants. Dawa hizi pindi mdu anapozitumia hufyonzwa ndani ya mwili na kutolewa kwa kupitia mate na kusababisha mate kuwa machungu. Mfano wa dawa hizi ni:-
A. Tetracycline
B.Gout medication kama allopurinol na lithium
C.Madawa yanayotumika kutibu maradhi ya moyo.
Baada ya kuacha kutumia dawa hizi ladha ya mdomo itarudi sawa ndani ya siku chache. Pia unaweza kunywa juisi ya vitu vichachu kama hali itaendelea kukusumbuwa.
3.Ujauzito, hali ya mdomo kuwa mchungu ama kuwa na ladha ya chuma kwa wajawazito ni kawaida na hali hii kutaalamu hufahamika kama dysgeusia ama metallic taste. Hutokea kwa uda wa siku kadhaa kisha huondoka. Baadhi ya wajawazito wanapata ladha ya pesa, yaani kama ulishawahi kuweka mdomon hela ya sarafu, ile ladha unayoipata ndio ambayo huwapata baadhi ya wajawazito.
4.Kama unatumia dawa za kuongeza vitamini, unaweza kupata ladha hii. Kuna baadhi ya dawa za vitamini zina madini mengi ya metali. Madini hayokama zinc, shaba, chuma na chromium. Kama dawa hiyo ina madini haya inaweza kubadili ladha ya mdomo na kuwa chungu
5.Ni dalili ya maradhi ya ini. Kama ini lako halifanyi kazi vyema ama lina matatzo, mwili utakuwa na kiasikikubwa cha ammonia ambayo ni sumu. Hatimaye kubadili ladha ya mdomo.
6.Mashambulizi ya kwenye mfumo wa upumuaji. Wakati mfumo wa upumuaji unapokuwa katika mashambulizi ya bakteria ama virusi au fangasi, inaweza kuathiri ladha ya mdomo.
7.Kama umecheuwa, hali hii inaweza kupelekea kubadilika kwa ladha ya mdomo
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowPost hii inahusu zaidi mkojo kushindwa kutoka kwenye kibofu na kwa kitaalamu huitwa retention of urine.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi madhara ya kutotibu Maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo, ni madhara ambayo yanaweza kutokea iwapo maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo hayatatibiwa kwa wakati.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukuletea baadhi ya maradhi yatokanayo na fangasi
Soma Zaidi...posti inaonyesha dalili mbalimbali za Saratani ya ini. Saratani ya ini ni Saratani inayoanzia kwenye seli za ini lako. Ini lako ni kiungo cha ukubwa wa mpira wa miguu ambacho kinakaa sehemu ya juu ya kulia ya tumbo lako, chini ya diaphr
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi maambukizi kwenye uume, maambukizi hata utokea kwenye kichwa Cha uume kwa kitaalamu huitwa Balanitis, zifuatazo ni sababu za kuwepo kwa ugonjwa huu.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kuharisha, kuharisha ni kitendo Cha kupitisha kinyesi Cha maji chenye damu au kisichokuwa na damu
Soma Zaidi...Pisti hii inahusu zaidi dalili za mtoto mwenye Maambukizi ya ugonjwa wa Dondakoo, tunajua wazi kuwa ugonjwa huu uwashambulia hasa watoto wadogo ambao wako chini ya miaka mitano, kwa hiyo zifuatazo ni baadhi ya Dalili zinazoweza kujitokeza kwa watoto hawa.
Soma Zaidi...Zijuwe sababu kuu zinazokufanya ukahisi maumivu makali ya tumbo kwa chini upande wa kushoto
Soma Zaidi...Minyoo ni katika viume wanyonyaji, wanaoishi katika miili ya viumbe hai na kujipatia chakula humo. Minyoo wanaweza kuishi kwenye maeneo yenye majimaji kama kwenye maji, ndani ya viumembe hai kama mtu, ngombe, ngure na paka. Minyoo pia wanaweza kuishi kwen
Soma Zaidi...Presha ya kushuka ama kitaalamu huitwa hypotension, presha ya kushuka ni hatari kwa afya kama ilivyo presha ya kupanda, maana mwili unakosa nguvu kabisa.
Soma Zaidi...