Sababu za mdomo kuwa mchungu

Hapa utajifunza sababu zinzopelekea mdomo kubadilika ladha na kuwa mchungu, ama mchachu.

Sababu za mdomo kuwa mchungu

KWA NINI MDOMO UNAKUWA MCHUNGU?
Umeshawahi kuamka asubuhi ukiwa na ladha chungu sana ya mdomo, na je hali hii ulishawahi kudumu nayo kwa muda wa masaa kadhaa?. bila shaka ungependa kujuwa sababu inayopelekea kutkea hali hii. Makala hii ni kwa ajili yako. Hapa nitakujuza sababu kuu za kuwa na ladha chungu ya mdomo, na nini kifanyike. Endelea kusoma makala hii hadi mwisho. Ila ningependa utambuwe kuwa mdomo kuwa mchungu mara nyingi sio shida sana ya kiafya kiasi cha kuhitaji dawa ama kumuona daktari. Endapo shida itaendelea hapo fanya maamuzi ya kuonana na daktari



Mdomo kuwa mchungu mara nyingi sio maradhi. Hali hii hutokea na kuondoka yenyewe ndani ya masaa machache. Mara nyingi hutokea wakati wa asubuhi ama unapotoka kulala. Hali hii pia huwapata wagonjwa. Hali hii wakati mwingine inakuwa ni dalili ya maradhi. Kama utaona mdomo wako unaendelea kuwa mchungu kwa muda mrefu onana na daktari kwa uchunguzi zaidi.



Ni nini husababisha mdomo kuwa mchungu?
1.Mdomo kutokuwa msafi. Hii ni kawaida wakati umelala mdomo bakteria waliokuwa wapo mdomoni wanaendelea kufanya kazi yao, kula mabaki ya chakula na kuendelea kuzaliana. Kumbuka mate yana kazi ya kusafisha mdomo,lakini wakati umelala mate hayawezi kufanya kazi hii kwani huwezi kuyatoa. Hivyo uchafu huendelea kujizalisha bila ya kutolewa. Hali hii inaweza kusababisha mdomo kuwa mchungu unapoamka.



Vyema usile kitu muda huu, kabla ya kupiga msaki. Safisha kinywa vyema ladha ya mdomo itarudi sawa ndani ya muda mchache. Pia kama ulitoka kulala baada ya kutema mate kwa muda mchache yaani baada ya mdomo kujisafisha hali hii inaweza kuondoka bila ya wasi wala hakuna ulazima wa kupiga mswaki, kwani mdomo una sifa ya kujisafish awenyewe kwa kutumia mate.




2.Matumizi ya madawa ya antibiotics au antidepressants. Dawa hizi pindi mdu anapozitumia hufyonzwa ndani ya mwili na kutolewa kwa kupitia mate na kusababisha mate kuwa machungu. Mfano wa dawa hizi ni:-
A. Tetracycline
B.Gout medication kama allopurinol na lithium
C.Madawa yanayotumika kutibu maradhi ya moyo.

Baada ya kuacha kutumia dawa hizi ladha ya mdomo itarudi sawa ndani ya siku chache. Pia unaweza kunywa juisi ya vitu vichachu kama hali itaendelea kukusumbuwa.



3.Ujauzito, hali ya mdomo kuwa mchungu ama kuwa na ladha ya chuma kwa wajawazito ni kawaida na hali hii kutaalamu hufahamika kama dysgeusia ama metallic taste. Hutokea kwa uda wa siku kadhaa kisha huondoka. Baadhi ya wajawazito wanapata ladha ya pesa, yaani kama ulishawahi kuweka mdomon hela ya sarafu, ile ladha unayoipata ndio ambayo huwapata baadhi ya wajawazito.



4.Kama unatumia dawa za kuongeza vitamini, unaweza kupata ladha hii. Kuna baadhi ya dawa za vitamini zina madini mengi ya metali. Madini hayokama zinc, shaba, chuma na chromium. Kama dawa hiyo ina madini haya inaweza kubadili ladha ya mdomo na kuwa chungu



5.Ni dalili ya maradhi ya ini. Kama ini lako halifanyi kazi vyema ama lina matatzo, mwili utakuwa na kiasikikubwa cha ammonia ambayo ni sumu. Hatimaye kubadili ladha ya mdomo.



6.Mashambulizi ya kwenye mfumo wa upumuaji. Wakati mfumo wa upumuaji unapokuwa katika mashambulizi ya bakteria ama virusi au fangasi, inaweza kuathiri ladha ya mdomo.



7.Kama umecheuwa, hali hii inaweza kupelekea kubadilika kwa ladha ya mdomo



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 20502

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰2 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰3 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰4 web hosting    πŸ‘‰5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    πŸ‘‰6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Fahamu Ugonjwa wa Brucellosis

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa Brucellosis ni maambukizi ya bakteria ambayo huenea kutoka kwa wanyama hadi kwa watu mara nyingi kupitia maziwa ambayo hayajasafishwa au kuchemshwa vizuri na bidhaa zingine za maziwa. Mara chache zaidi, ba

Soma Zaidi...
Madhara ya ugonjwa wa ukimwi kwenye jamii.

Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea ikiwa Ugonjwa huu wa ukimwi ukishasmbaa kutoka sehemu moja kwenda nyingine na kuleta madhara makubwa kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Fahamu Dalili zinazotokana na kuzama kwenye majj kwa watoto.

Kuzama hufafanuliwa kama mchakato unaosababisha upungufu mkubwa wa kupumua kutokana na kuzamishwa kwenye chombo cha kuogelea (kioevu). Kuzama hurejelea tukio ambalo njia ya hewa ya mtoto huzamishwa kwenye kioevu, na kusababisha kuharibika kwa kupumua.

Soma Zaidi...
Virusi vinavyopelekea Kuharisha Sana na Kutapika Sana(norovirus)

Maambukizi ya Norovirus yanaweza kusababisha kutapika sana na Kuhara. Virusi huambukiza sana na kwa kawaida huenea kupitia chakula au maji ambayo yamechafuliwa na kinyesi wakati wa kutayarisha. Unaweza pia kuambukizwa kwa kuwasiliana kwa karibu na mtu

Soma Zaidi...
Sababu za ugonjwa wa pumu, dalili zake na jinsi ya kujilinda na pumu.

Ugonjwa wa pumu ni ugonjwa unaoshambulia mfumo wa hewa ambapo mgonjwa hushindwa kupumua vizuri na hupelekea matatizo ya kudumu kama haujatibiwa mapema.

Soma Zaidi...
Dalili za maumivu ya uti wa Mgongo

Posti hii inahusu zaidi dalili za uti wa mgongo ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye tatizo la uti wa Mgongo.

Soma Zaidi...
Samahan naomb kujua staili za tendo la ndoa

Post hii inakwenda kujibu swali la muulizaji. Kuhusu syyle za tendo la ndoa

Soma Zaidi...
Dalili za mtu mwenye ugonjwa wa kuishiwa damu

Posti hii inahusu zaidi dalili za mtu mwenye ugonjwa wa kupungukiwadamu, ni dalili zinazoonekana kwa mtu Mwenye tatizo la upungufu wa damu.

Soma Zaidi...
Je utambuzi wa maambukizi ya ukimwi hupatikana mda gani pale mtu anapoambukizwa

Kuna ukimwi na HIV na kila kimoja kina dalili zake na muda wa kuonyesha hizo dalili.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa coma

Coma ni hali ya kupoteza fahamu kwa muda mrefu ambayo inaweza kusababishwa na matatizo mbalimbali Jeraha la Kichwa, Kiharusi, Uvimbe kwenye ubongo, ulevi wa dawa za kulevya au pombe, au hata ugonjwa wa msingi,

Soma Zaidi...