picha

Muhutasari wa sifa za wanafiki

Kwa kuzingatia aya zote tulizozipitia juu ya wanafikitunaweza kutoa majumuisho ya sifa za wanafiki kama ifuatavyo:- (1)Hutenda kinyume cha imani wanaodai kuwa nayo.

Muhutasari wa sifa za wanafiki

Muhutasari wa sifa za wanafiki


Kwa kuzingatia aya zote tulizozipitia juu ya wanafikitunaweza kutoa majumuisho ya sifa za wanafiki kama ifuatavyo:-
(1)Hutenda kinyume cha imani wanaodai kuwa nayo.


(2)Hujaribu kumdanganya Mwenyezi Mungu pamoja na waumini wakidhani kuwa yaliyo nyoyoni mwao hayajulikani.


(3)Hufanya maovu katika ardhi huku wakidai kuwa wanatenda mema.


(4)Huwaona waumini wa kweli kuwa ni wajinga kwa kufuata kwao Uislamu inavyotakikana.


(5)Huwacheza shere Waislamu.


(6)Hujiiona kuwa wao ni bora kuliko waumini


(7)Hujikomba kwa viongozi wa kitwaaghuti.


(8)Huwafanya makafiri na Washirikina kuwa marafiki zao wa ndani badala ya Allah(s.w) Mtume wake na waumini.


(9)Huyapenda zadi maslahi ya dunia kuliko ya akhera.


(10)Hukataa kuhukumiwa na sheria za Allah (s.w).


(11)Hutumia viapo kama kifuniko cha maovu yao.


(12)Huchanganya haki na batili, kufuru na Uislamu.


(13)Huendea swala kwa uvivu.


(14)Hawamtaji Allah ila kidogo sana.


(15)Huwafitinisha Waislamu.


(16)Huchukia Waislamu wanapofikwa na kheri na kufurahia wanapofikwa na msiba.


(17)Hawako tayari kutoa mali zao katika njia ya Allah (s.w) na wakitoa chochote hutoa kwa ria


(18)Huwazuia watu kutoka katika njia ya Allah.


(19)Huzifanyia stihizai (shere) aya za Qur-an.


(20)Huamrisha maovu na kukataza mema.


(21)Husema uongo na kuvunja ahadi.


(22)Huwa vunja moyo na kuwakatisha tamaa Waislamu wa kweli ili wabakie katika ukafiri sawa na wao.


(23)Hufanya hiyana katika mambo ya kheri na kuchagua mambo mepesi mepesi.


(24)Wanawaogopa na kuwachelea watu zaidi kuliko Allah (s.w).


(25)Hush irikiana na maadui kuupiga vita Uislamu na Waislamu.



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Views 1335

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Dua za Mitume na Manabii     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 ai web app     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Msimamo wa Nabii Nuhu(a.s) Dhidi ya Makafiri

Pamoja na upinzani mkali alioupata kutoka kwa viongozi wa makafiri, Nabii Nuhu(a.

Soma Zaidi...
Kazi alizokuwa akizifanya Mtume Muhammad s.a.w kabla ya utume.

Historia na sifa ya Mtume Muhammad s.a.w , sehemu ya 14. Hapa utajifunza kuhusu kazi alizozifanya Mtume s.a.w Enzo za ujana wake kabla ya utume.

Soma Zaidi...
Mtume Muhammad s.a. w amelewa na Baba yake mdogo

Historia na sura ya Mtume Muhammad, sehemu ya 10.

Soma Zaidi...