Madai ya makafiri dhidi ya quran na hoja zao

Madai ya makafiri dhidi ya quran na hoja zao

Download Post hii hapa

Madai ya makafiri dhidi ya quran na hoja zao

Madai ya Makafiri dhidi ya Qur-an



Waislamu wanaamini pasi na tone la shaka kuwa Qur-an ni kitabu cha Allah (s.w) neno kwa neno kama mwenyewe anavyothibitisha:


"Hiki ni kitabu kisichokuwa na shaka ndani yake, ni uongozi kwa wamchao Mwenyezi Mungu." (2:2)
Pamoja na uthibitisho huu, makafiri wa zama za kale na za sasa wameibuka na upinzani dhidi ya Qur-an na kudai kuwa kitabu hiki amekitunga mwenyewe Mtume Muhammad (s.a.w):



"Au ndio wanasema kuwa hii Qur-an ameitunga (Muhammad)? Bali wao hawaamini lolote." (52:33)
Dai hili la kumpa Mtume (s.a.w) utunzi wa Qur-an limewakilishwa katika sura mbali mbali na makafiri wa zama mbali mbali. Kwa ujumla makafiri wamedai kuwa Qur-an ni:


1. Mashairi aliyotunga Mtume Muhammad (s.a.w).
2. Zao la njozi za Muhammad (s.a.w) zilizovurugika
3. Zao la mwenye kujidhania kupata ufunuo
4. Zao la mwenye kifafa na aliyepagawa na shetani.
5. Aya za shetani
6. Uandishi wa Muhammad (s.a.w) kwa msaada wa Mayahudi na Wakristo.
7. Utunzi wa Muhammad (s.a.w) ili kuleta umoja na ukombozi wa Waarabu.
8. Utunzi wa Muhammad (s.a.w) ili kurekebisha tabia ya Waarabu.
9. Utunzi wa Muhammad (s.a.w) ili ajinufaishe kiuchumi.
10. Utunzi wa Muhammad (s.a.w) ili kuwania madaraka na ukubwa.



Qur-an yenyewe inakanusha madai haya katika aya mbali mbali kama tunavyojifunza katika aya zifuatazo:


Basi naapa kwa mnavyoviona. Na msivyoviona. Kwa hakika hii ni kauli iliyoletwa na Mjumbe (wa Mwenyezi Mungu) mwenye hishima (kubwa). Wala si kauli ya mtunga mashairi (kama mnavyosema).Ni machache sana mnayoyaamini. Wala si kauli ya mchawi (kama mnavyodai). Ni kidogo kabisa kuwaidhika kwenu. Ni mteremsho utokao kwa Mola wa viumbe vyote. Na kama


(Mtume) angelizua juu yetu baadhi ya maneno tu, bila shaka tungalimshika kwa mkono wa kuume, (wa kulia). Kisha kwa hakika tungalimkata mshipa mkubwa wa moyo (69:38-46).


Na hapana yeyote katika nyie angeweza kutuzuia naye. Kwa hakika hii (Qur-an) ni mawaidha kwa wanaomcha Mwenyezi Mungu. Na kwa yakini tunajua kuwa miongoni mwenu wamo wanaokadhibisha. Na itakuwa ni sikitiko, (m ajut o) juu ya wanaokanusha. Na hakika hii ni haki ya yakini. Basi litukuze jina la Mola wako aliye Mkuu. (69:47-52)
Pamoja na aya hizi na nyingine nyingi zinazokanusha madai ya makafiri dhidi ya utunzi wa Qur-an bado Allah (s.w) ametoa changa moto kwa makafiri wa zama zote tangu ianze kushuka Qur-an hadi leo, kuwa:


"Na ikiwa mna shaka kwa hayo tuliyomteremshia Mtumwa Wetu (kuwa hakuteremshiwa na Mwenyezi Mungu) basi leteni sura moja iliyofanywa na (mtu) aliye mfano wake, na muwaite waungu wenu bighairi ya Mwenyezi Mungu (wakusaidieni), ikiwa mnasema kweli." (2:23)
Pamoja na changamoto hii ya Qur-an, hebu tuangalie kwa undani kidogo udhaifu wa hizi hoja kumi za makafiri dhidi ya Qur-an:




                   


Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 1697

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰2 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰4 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰5 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Sura za makkah na madinah
Sura za makkah na madinah

Quran (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Nini maana ya Iqlab katika hukumu za tajwid
Nini maana ya Iqlab katika hukumu za tajwid

Hapa utajifunza maana ya iqlab katika usomaji wa Quran kwa tajwid

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA MIIM YENYE SAKINA
HUKUMU ZA MIIM YENYE SAKINA

SURA YA NNE HUKUMU ZA MIYM YENYE SAKNA HUKUMU ZA MIYM SAKINA: Mym sakina ni miym ambayo haina i’rab ( Ω…Ω’).

Soma Zaidi...
Maana ya qalqala na aina zake katika usomaji wa Quran tajwid
Maana ya qalqala na aina zake katika usomaji wa Quran tajwid

Qalqala imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Qalqalatul qubra yaani qalqala kubwa na qalqalat as shughura yaani qalqala ndogo.

Soma Zaidi...
fadhila za sura kwenye quran
fadhila za sura kwenye quran

FADHILA ZA BAADHI YA SURA Umuhimu na ubora wa baadhi ya sura na aya.

Soma Zaidi...
sura ya 11
sura ya 11

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA TAFKHIIM NA TARQIQ
HUKUMU ZA TAFKHIIM NA TARQIQ

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Hukumu ya tafkhim na tarqiq katika usomaji wa Quran tajwid
Hukumu ya tafkhim na tarqiq katika usomaji wa Quran tajwid

Tarqiq ni kuisoma herufi kwa kuipa wepesi na tqfkhim ni kuisoma herufi kwa kuipa uzito.

Soma Zaidi...