Post hii itakufundishabkuhusu mirathi ya kiislamu, maana yake.
Maana ya Mirathi
Mirathi katika Uislamu ni kanuni na taratibu alizoziweka Allah (Sw) katika kuwagawawia na kuwarithisha familia na jamaa, mali aliyoiacha marehemu. Qur'an inabainisha kuwa, mtu anapofariki dunia, mali yote aliyochuma hurithiwa na Allah (Sw), kisha Yeye huigawa na kuwarithisha watu wanaostahiki, katika uwiano wa haki na uadilifu.ombeni msaada kwa Mwenyezi Mungu na subirini. Ardhi ni ya Mwenyezi Mungu, anamrithisha amtakaye katika waja wake; na mwisho (mwema) ni kwa wamchao. (7:128)
na urithi wa mbingu na ardhi ni wa Mwenyezi Mungu (5 7:10) Ukweli huu unajitokeza pia katika dua ya nabii Zakaria alipomuamba Allah (Sw) amjaalie mtoto. Nabii Zakaria alimwomba Mola wake akasema: Mola wangu! Usiniache peke yangu na Wewe ndiwe mbora wa wanaorithi (21:89)
Mwanamke ana haki ya kurithi
Katika kugawanya na kuirithisha mali kwa wahusika, Allah (Sw) hakumnyima mwanamke haki ya kurithi akiwa mtoto, mke au mama. Wote wanawake na wanaume wanamafungu maalumu Ia kurithi katika mali aliyoiacha marehemu.
"Wanaume wana sehemu katika mali wanayoyachuma wazazi na jamaa walio karibu. Na wanawake (pia) wanayo sehemu katika yale waliyoyaacha wazazi na jamaa walio karibu. Yakiwa kidogo au mengi. (Hizi) ni sehemu zilizofaradhishwa (na Allah (s.w))" (4:7)
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Uchumi wa uislamu umeweka taratibu mbalimbali katika kuchuma mali.
Soma Zaidi...Haki ya KutalikiKatika jamii nyingi za kjahili haki ya kutoa talaka iko kwa mwanamume tu na mwanamke hana haki yoyote ya kumtaliki mumee.
Soma Zaidi...Swala ya Dhuha ni swala ya sunna inayosaliwa wakati wa asubuhi baada ya jua kuchomoza na kupanda angalau kiasi cha mkuki (takribani dakika 15 baada ya jua kuchomoza) mpaka kabla ya adhuhuri. Ingawa hakuna sura maalum zilizowekwa kisheria, Mtume ï·º alisoma baadhi ya sura zenye maana ya kuhimiza kheri na shukrani.
Soma Zaidi...Uchumi wa kiislamu unatofautiana sana na uchumi wa kikafiri. Hapa utajifunza tofauti hizo.
Soma Zaidi...- Je, Ukeweza, (ndoa ya mke zaidi ya mmoja) humdhalilisha mwanamke?
Soma Zaidi...Vipi lengo la funga litafikiwa na kumfanya mfungaji awe mchamungu.
Soma Zaidi...