Tofauti kati ya sura za makkah na madinah
Quran (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)
- Tofauti kati ya Sura za Makkah na Madinah
|
Sura za Makkah |
Sura za Madinah |
|
1. Walengwa. Walengwa walikuwa waumini waliosimu mwanzo wa Utume. |
Zililenga Maadui wa Dola ya Kiislamu Madinah wakiwemo; Wanafiq, Washirikina, Wayahudi na Wakristo. |
|
2. Ujumbe. Sehemu kubwa ya ujumbe ni kujenga imani juu ya Mwenyezi Mungu (s.w), Malaika, Vitabu, Mitume, Siku ya Mwisho na Qudra yake. |
Ujumbe ulilenga ujenzi wa Dola na jamii ya Kiislamu Madinah kupitia sheria na hukumu mbali mbali. |
|
3. Muundo wa sura. Sura nyingi ni fupi na zina aya fupi fupi zenye lengo moja. |
Sura nyingi ni ndefu na zina aya ndefu zenye ufafanuzi zenye lengo la utekelezaji wa sheria.. |
|
4. Mbinu Zimetumia lugha fupi ya mchomo kwa walengwa kwa kutumia viapo, historia ya watu waliopita, kuwahofisha na kuwakatisha tamaa maadui wa Uislamu na kuwatia moyo na kuwaliwaza waumini katika kutekeleza ujumbe wa Qur’an. |
Zimetumia lugha ya sheria na ufafanuzi katika ujenzi wa Dola ya Kiislamu Madinah, kwa kutumia historia ya Mitume ili kuwaliwaza waumini kupigania Dini na kuwakatisha tamaa maadui wao wakiwemo; makafiri, washirikina, wanafiq na Wakristo. |
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 ai web app 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Sababu za kushuka kwa surat al qariah
Surat Al qariah, ni moja katika sura zilizochuka miaka ya mwanzoni mwa utume.
Soma Zaidi...Sababu za kushuka surat al-Falaq na surat an-Nas na fadhila za kusoma sura hizi
SURAT AL-MUAWIDHATAYN (SURAT AL-FALAQ NA SURATUN-NAS) Inaelezwa kuwa sura mbili hizi zilishuka pamoja, na maulamaa wanaelezea kuwa Mtume (s.
Soma Zaidi...Sababu za kushuka surat Ikhlas
Surat Ikhlas ni katika sura za kitawhid ambazo zilishuka miaka siku za mwanzoni mwa utume. Sura hii imekuja kujibu maswali mengi kuhusu Allah ikiwemo, Allah ni nani?
Soma Zaidi...