Tofauti kati ya sura za makkah na madinah

Quran (EDK form 3:dhana ya elimu ya uislamu)

Sura za Makkah

Sura za Madinah

 

1. Walengwa. 

Walengwa walikuwa waumini waliosimu mwanzo wa Utume.

 

Zililenga Maadui wa Dola ya Kiislamu Madinah wakiwemo; Wanafiq, Washirikina, Wayahudi na Wakristo.

 

2. Ujumbe.

Sehemu kubwa ya ujumbe ni kujenga imani juu ya Mwenyezi Mungu (s.w), Malaika, Vitabu, Mitume, Siku ya Mwisho na Qudra yake.

 

Ujumbe ulilenga ujenzi wa Dola na jamii ya Kiislamu Madinah kupitia sheria na hukumu mbali mbali.

 

3. Muundo wa sura.

Sura nyingi ni fupi na zina aya fupi fupi zenye lengo moja.

 

Sura nyingi ni ndefu na zina aya ndefu zenye ufafanuzi zenye lengo la utekelezaji wa sheria..

 

4. Mbinu 

Zimetumia lugha fupi ya mchomo kwa walengwa kwa kutumia viapo, historia ya watu waliopita, kuwahofisha na kuwakatisha tamaa maadui wa Uislamu na kuwatia moyo na kuwaliwaza waumini katika kutekeleza ujumbe wa Qur’an.

 

Zimetumia lugha ya sheria na ufafanuzi katika ujenzi wa Dola ya Kiislamu Madinah, kwa kutumia historia ya Mitume ili kuwaliwaza waumini kupigania Dini na kuwakatisha tamaa maadui wao wakiwemo; makafiri, washirikina, wanafiq na Wakristo.  

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Quran Main: Dini File: Download PDF Views 6161

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

fadhila za sura kwenye quran

FADHILA ZA BAADHI YA SURA Umuhimu na ubora wa baadhi ya sura na aya.

Soma Zaidi...
Ni zipi hukumu za nuni yenye sakina au tanwin?

Hapa utajifunza usomaji wa Quran pindi utakapokuta nuni yenyebsakina au tanwin

Soma Zaidi...
HUKUMU ZA QALQALA

Jifunze namna ya kusoma quran, pata mafunzo ya tajwid hapa

Soma Zaidi...
Tofauti kat ya sura za Maka na Madina

Sura za Makka na Madina Kutokana na historia ya kushuka kwake sura za Qur-an zimegawanywa katika makundi mawili - sura za Makka na sura za Madina.

Soma Zaidi...
Nini maana ya Iqlab katika hukumu za tajwid

Hapa utajifunza maana ya iqlab katika usomaji wa Quran kwa tajwid

Soma Zaidi...
Uthibitisho kuwa Qur-an ni neno la Allah (s.w)

Uthibitisho kuwa Qur-an ni neno la Allah (s.

Soma Zaidi...