Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Maana ya JSON na sheria za kuandika faili la json
JSON (JavaScript Object Notation) ni format ya kuhifadhi na kubadilishana data ambayo ni rahisi kusoma na kuandika na binadamu, na pia rahisi kwa mashine kuzichakata. Data kwenye JSON huandikwa kwenye jozi yaani key na value . key ni jina la hiyo data yaani name na value ni thamani ya hiyo data. Mfano naweza kusema umri : 30 hii ina maana umri ni key na value yae n 30
Json ni lugha kikompyuta ambayo ni format ya kubadilishana data. Json ni rahisi kuandikwa na binadamu na kusomwa. Yani data zilizopo kwneye JSON unaweza ukazisoma na kuelewa kilichiandikwa hata bila ya kuhitaji msaada wa mashine
Mfano:
{
"jina": "John",
"umri": 30,
"ndoa": true,
"watoto": ["Anna", "Ella"],
"anwani": {
"mtaa": "Kigonzi",
"mji": "Mpanda",
"post": "30"
}
}
Katika mfano huu:
- `jina` ni "key" yenye thamani (`value`) ya "John".
- `umri` ni "key" yenye thamani (`value`) ya 30.
- `ndoa` ni "key" yenye thamani (`value`) ya true.
- `watoto` ni "key" yenye thamani (`value`) ya orodha (`array`) inayojumuisha "Anna" na "Ella".
- `anwani` ni "key" yenye thamani (`value`) ya kitu (`object`) chenye jozi kadhaa za "key" na "value".
Ukiangalia hapo hizo data kwa haraka TU unaweza kuelewa hapo hizo data zinamuhusi John,mwenye umri wa miaa 30 na yupo kwneye ndoa, an watoto wawili ambayo ni Ana na Ella. John anaishi Mtaa wa Kigonzi huko mjini Mpanda na anaweza kupatikana kwa address ya 30.
Matumizi ya JSON
Json imekuwa na matumizi makubwa na hata imefikia kuwa mbadala wa xml kwa baadhi ya maeneo. Miongoni mwa matumizi ya json ni kama:-
Kubadilishana data kwenye network
Hutumika ye API
Hutuma uhifadhi data
Pia hutumika kwenye setting za program
Sheria za uandishi wa JSON:
1.Json huandikwa kwenye jozi yaan key na value kama nilivyo onyesha hapo awali. Key inatakiwa iwe ndani ya double quotation mark yaani alama za funga semi. Na endapo value ni string pia itakuwa na alama hizo. Ila ikiwa value ni sio string hatutatumia alam hizo. Baada ya kuandika key itafuatiwa na nykta pacha (:). Endapo value ni zaidi ya moja utatenganisha kwa alama ya koma (,)
Mfano:
"name": "John Doe",
"age": 30,
"isStudent": false
2.Data za json huandikwa ndani ya mabano ambayo ni curly braces {}
Mfano:
{
"jina": "John",
"umri": 30,
"ndoa": true,
"watoto": ["Anna", "Ella"],
"anwani": {
"mtaa": "Kigonzi",
"mji": "Mpanda",
"post": "30"
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
atika somo hli tutakwenda kujifunza kuhusu kitu kinachitwa cron job. ni moja ya teknolojia zinazotumika kufanya kazi zinazofanyika automatic
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutumia PDO kutengeneza database, kuteneneza table na kuingiza data moja na zaidi ya moja.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunzo kuhusu teknolojia ya ORM na inavyotumika kulinda usalama wa database
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Aina za cache header
Soma Zaidi...Katika soko hili takwenda kujufunza jinsi ya kutuma sms kwa kutumia PHP. Hii itasaidia kama unataka kutuma OTP yaqni Onetime password
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku generate PDF automatik kutoka kwenye php code , html, javascript na css.
Soma Zaidi...Katika somo hii utakwenda kujifunza aina za http header na server variable. Hapa tutakwenda kuchambuwa mgawanyiko wa httpheader na kazi zake.
Soma Zaidi...Katika somo hili unakwenda kujifunza jinsi y kutengeneza database na kuungansha kwenye blog yetu.
Soma Zaidi...Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya PHP na hapa tunaaza rasmi advanced PHP. tutakwenda kuingia ndani zaidi kwenye PHP. Ni vyema kabla ya kuanza course hii ya advanced PHP uwe una uelewa wa kutosha kuhusu mafunzo yetu ya PHP.
Soma Zaidi...Katika somo hili utajifunza jinsi ambavyo unaweza kutengeneza blog ambayo utaweza ku upload faili na kuandika makala kwa kutumia PHP
Soma Zaidi...