Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Maana ya JSON na sheria za kuandika faili la json
JSON (JavaScript Object Notation) ni format ya kuhifadhi na kubadilishana data ambayo ni rahisi kusoma na kuandika na binadamu, na pia rahisi kwa mashine kuzichakata. Data kwenye JSON huandikwa kwenye jozi yaani key na value . key ni jina la hiyo data yaani name na value ni thamani ya hiyo data. Mfano naweza kusema umri : 30 hii ina maana umri ni key na value yae n 30
Json ni lugha kikompyuta ambayo ni format ya kubadilishana data. Json ni rahisi kuandikwa na binadamu na kusomwa. Yani data zilizopo kwneye JSON unaweza ukazisoma na kuelewa kilichiandikwa hata bila ya kuhitaji msaada wa mashine
Mfano:
{
"jina": "John",
"umri": 30,
"ndoa": true,
"watoto": ["Anna", "Ella"],
"anwani": {
"mtaa": "Kigonzi",
"mji": "Mpanda",
"post": "30"
}
}
Katika mfano huu:
- `jina` ni "key" yenye thamani (`value`) ya "John".
- `umri` ni "key" yenye thamani (`value`) ya 30.
- `ndoa` ni "key" yenye thamani (`value`) ya true.
- `watoto` ni "key" yenye thamani (`value`) ya orodha (`array`) inayojumuisha "Anna" na "Ella".
- `anwani` ni "key" yenye thamani (`value`) ya kitu (`object`) chenye jozi kadhaa za "key" na "value".
Ukiangalia hapo hizo data kwa haraka TU unaweza kuelewa hapo hizo data zinamuhusi John,mwenye umri wa miaa 30 na yupo kwneye ndoa, an watoto wawili ambayo ni Ana na Ella. John anaishi Mtaa wa Kigonzi huko mjini Mpanda na anaweza kupatikana kwa address ya 30.
Matumizi ya JSON
Json imekuwa na matumizi makubwa na hata imefikia kuwa mbadala wa xml kwa baadhi ya maeneo. Miongoni mwa matumizi ya json ni kama:-
Kubadilishana data kwenye network
Hutumika ye API
Hutuma uhifadhi data
Pia hutumika kwenye setting za program
Sheria za uandishi wa JSON:
1.Json huandikwa kwenye jozi yaan key na value kama nilivyo onyesha hapo awali. Key inatakiwa iwe ndani ya double quotation mark yaani alama za funga semi. Na endapo value ni string pia itakuwa na alama hizo. Ila ikiwa value ni sio string hatutatumia alam hizo. Baada ya kuandika key itafuatiwa na nykta pacha (:). Endapo value ni zaidi ya moja utatenganisha kwa alama ya koma (,)
Mfano:
"name": "John Doe",
"age": 30,
"isStudent": false
2.Data za json huandikwa ndani ya mabano ambayo ni curly braces {}
Mfano:
{
"jina": "John",
"umri": 30,
"ndoa": true,
"watoto": ["Anna", "Ella"],
"anwani": {
"mtaa": "Kigonzi",
"mji": "Mpanda",
"post": "30"
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu Cookie Headers
Soma Zaidi...Katika course hii utakwenda kujifundisha jinsi ya lutengeneza blog kutoka mwanzo hadi mwisho.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwend akujifunza jinsi ya kubadili json data na kuwaphp array ama php object. Kwa ufupi tunakwend aku decode json data kuwa phparray amaobject
Soma Zaidi...katika post hii utajifunza jinsi ya kufuta post kwenye database. pia utajifunza jinsi ya kufuta picha kwenye server
Soma Zaidi...Katika project hii utakwenda kujifunza jinsi ya kufanya CRUDE operation kwa kutumia PHP OOP na MySQL database.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza aina kuu 3 za variable katika PHP mabzo ni local variable, global variable na static variable.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu class inheritance kwenye object oriented programming.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu http header, maana yake na jinsi ya kusoma taarifa zilizopo kwenye http header.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda Jinsi ya kutengeneza ORM inayofanya CDRUDE operation.
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwenda kutumia prepared ststement kwenye ku fetch data kutoka kwenye database.
Soma Zaidi...