Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu http header, maana yake na jinsi ya kusoma taarifa zilizopo kwenye http header.
Karibu kwenye course mpya ya PHP mabayo itakwenda kuzungumzia kuhusu HTTP header na jinsiambavyo inavyofanya kazi. Course hii ni moja ya misingi ya course zinazofuata.
Nini utakwenda kujifunza?
Maana ya http header
Jinsi ya kupata header information
Jinsi ya kuweka header information Yako mwenyewe.
Jinsi ya kulinda usalama wa header information
Matumizi ya header information
Http header ni Nini?
Haoa tunazungumzia zile taarifa ambazo zinahusu request inayotokea kwneye server na inayoingia.
Request ni like ombi linalofanywa browser ya mtumiaji hii tunaita client request. Mfano wewe umeandika link https://bongoclass.com. Sasa browser Yako itaomba server ambayo inamaudhui yaink husika kuletabmaudhui hayo. Kisha server itajibu kwa kukupa maudhui hayo kama ni habari, hadithi, audio n k. Haya majibu ambayo server inatia yanaitwa server response.
Sasa wakati wewe unatumia client request kwa kuandika hiyo link Yako, hiyo link inapokwenda kuomba maudhui kwenye server husika, inakwenda na baadhi ya taarifa maalumu zinazohusu hiyo link.
Mfano link hiyo itabeba taarifa inayoonyesha kabla ya kubofya link hiyo unetojea kwenye link Gani, pia taarifa nyingine kama IP address, jina la domain, n k
Taarifa hizi huwezi kuziona kwenye link yenyewe mpaka uziombe kwenye server. Sasa njia ambazo taarifa hizi hulitishwa ni kwa kupitia http header.
Http header ni sehemu muhimu ya data ambayo inatumiwa katika mawasiliano ya mtandao kati ya mtandao wa mteja na mtandao wa seva. Ina maelezo yanayoelezea ombi la HTTP au jibu, kama vile aina ya data inayotumwa au kupokelewa, lugha inayotumiwa, kuki za mtumiaji, na maelezo mengineyo muhimu.
Baadhi ya yaarifa kwenye httpheader::
Hapa nakuletea tu orodha ya taarifa zinazoweza kupatikana kwenye http header. Katika somo linalofuata tutakwenda kuziangalia taarifa hizi kwa undani zaidi.:-
1.Host: Jina la seva inayotakiwa kushughulikia ombi.
2.User-Agent: Maelezo kuhusu programu ya mteja inayofanya ombi.
3.Accept: Aina za media zinazotakiwa kukubaliwa na mteja.
4.Content-Type: Aina ya data inayotumwa kwa seva au inayopokelewa kutoka kwa seva.
5.Content-Length: Urefu wa data inayotumwa kwa seva au inayopokelewa kutoka kwa seva.
6.Authorization: Msimbo wa uthibitishaji wa mteja.
7.Cookie: Habari za kuki za mtumiaji zinazotumwa kwenye seva.
8.Location: Anwani ya URL ya kuelekeza kwa mteja (hasa katika majibu ya kuelekeza).
9.Cache-Control: Maelezo kuhusu jinsi ya kushughulikia caching ya data.
10.Server: Maelezo kuhusu seva inayojibu ombi.
11.Date: Tarehe na saa ambayo ombi au jibu lilifanyika.Connection: Hali ya uhusiano wa mtandao, kama vile "close" au "keep-alive".
12.Content-Enc...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Katika somo hili utakwenda kujifunza jisniya kutuma email kwa kutumia PHPMailer kwenye project ya PHP. Katika somo hili tutakwend akutuma email kwa kutumia localhost.
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza jisni ya kudhibiti error ambazo zinaweza kutokea wakati wa ku encode na ku decoe json data
Soma Zaidi...Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu aina za loop DO, FOR, FOREACH LOOPS kwenye PHP
Soma Zaidi...Katika somo hili tutakwenda kutumia prepared ststement kwenye ku fetch data kutoka kwenye database.
Soma Zaidi...katika post hii utajifunza jinsi ya kufuta post kwenye database. pia utajifunza jinsi ya kufuta picha kwenye server
Soma Zaidi...Katika somo hili uttakwend akujifunz ajinsi ambavyo utaweza kutengeneza simple ORM yakwako mwenyewe
Soma Zaidi...