PHP somo la 73: Maana ya http header

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu http header, maana yake na jinsi ya kusoma taarifa zilizopo kwenye http header.

Karibu kwenye course mpya ya PHP mabayo itakwenda kuzungumzia kuhusu HTTP header na jinsiambavyo inavyofanya kazi. Course hii ni moja ya misingi ya course zinazofuata.

 

Nini utakwenda kujifunza?

  1. Maana ya http header

  2. Jinsi ya kupata header information

  3. Jinsi ya kuweka header information Yako mwenyewe.

  4. Jinsi ya kulinda usalama wa header information

  5. Matumizi ya header information



  1. Http header ni Nini?

Haoa tunazungumzia zile taarifa ambazo zinahusu request inayotokea kwneye server na inayoingia.

 

Request ni like ombi linalofanywa browser ya mtumiaji hii tunaita client request. Mfano wewe umeandika link https://bongoclass.com. Sasa browser Yako itaomba server ambayo inamaudhui yaink husika kuletabmaudhui hayo. Kisha server itajibu kwa kukupa maudhui hayo kama ni habari, hadithi, audio n k. Haya majibu ambayo server inatia yanaitwa server response.

 

Sasa wakati wewe unatumia client request kwa kuandika hiyo link Yako, hiyo link inapokwenda kuomba maudhui kwenye server husika, inakwenda na baadhi ya taarifa maalumu zinazohusu hiyo link.

 

Mfano link hiyo itabeba taarifa inayoonyesha kabla ya kubofya link hiyo unetojea kwenye link Gani, pia taarifa nyingine kama IP address, jina la domain, n k

 

Taarifa hizi huwezi kuziona kwenye link yenyewe mpaka uziombe kwenye server. Sasa njia ambazo taarifa hizi hulitishwa ni kwa kupitia http header.



Http header ni sehemu muhimu ya data ambayo inatumiwa katika mawasiliano ya mtandao kati ya mtandao wa mteja na mtandao wa seva. Ina maelezo yanayoelezea ombi la HTTP au jibu, kama vile aina ya data inayotumwa au kupokelewa, lugha inayotumiwa, kuki za mtumiaji, na maelezo mengineyo muhimu.

 

Baadhi ya yaarifa kwenye httpheader::

Hapa nakuletea tu orodha ya taarifa zinazoweza kupatikana kwenye http header. Katika somo linalofuata tutakwenda kuziangalia taarifa hizi kwa undani zaidi.:-

 

1.Host: Jina la seva inayotakiwa kushughulikia ombi.

 

2.User-Agent: Maelezo kuhusu programu ya mteja inayofanya ombi.

 

3.Accept: Aina za media zinazotakiwa kukubaliwa na mteja.

 

4.Content-Type: Aina ya data inayotumwa kwa seva au inayopokelewa kutoka kwa seva.

 

5.Content-Length: Urefu wa data inayotumwa kwa seva au inayopokelewa kutoka kwa seva.

 

6.Authorization: Msimbo wa uthibitishaji wa mteja.

 

7.Cookie: Habari za kuki za mtumiaji zinazotumwa kwenye seva.

 

8.Location: Anwani ya URL ya kuelekeza kwa mteja (hasa katika majibu ya kuelekeza).

 

9.Cache-Control: Maelezo kuhusu jinsi ya kushughulikia caching ya data.

 

10.Server: Maelezo kuhusu seva inayojibu ombi.

 

11.Date: Tarehe na saa ambayo ombi au jibu lilifanyika.Connection: Hali ya uhusiano wa mtandao, kama vile "close" au "keep-alive".

 

12.Content-Encoding: Aina ya kubadilisha iliyoitumika kwa data iliyotumwa au kupokelewa.

 

13.Referer: URL ya rasilimali iliyosababisha ombi la sasa.

 

14.Accept-Language: Lugha za makala zinazopendelewa na mteja.

 

14.ETag: Alama ya utambulisho wa kipekee kwa rasilimali, kutumika kwa udhibiti wa caching.

 

15.If-Modified-Since: Tarehe ya mwisho ya mabadiliko ya rasilimali, kutumiwa katika udhibiti wa caching.

 

Zipo tarifa nyinginezo ambazo tutaziona huko mbeleni kadiri somo linavyoendelea. Kwa sasa unachotakiw akujuwa ni kuwa ndani ya http header kuna taarifa nyingi sana.



Jinsi ya kusoma taarifa za http header:

Kuna njia kadhaa ambazo tutakwenda kuzitumia ili kusoma data kwenye http header. Njia hizo ni kama:-

  1. Kwa kutumia global variable $_SERVER   

<?php

echo $_SERVER['REQUEST_METHOD']; // Outputs the request method (GET, POST, etc.)

echo "<br>";

 

echo $_SERVER['REMOTE_ADDR']; // Outputs the IP address of the client

echo "<br>";

 

echo $_SERVER['HTTP_USER_AGENT']; // Outputs the user agent string of the client's browser

echo "<br>";

 

echo $_SERVER['SCRIPT_FILENAME']; // Outputs the absolute pathname of the currently executing script

echo "<br>";

 

echo $_SERVER['SERVER_ADDR']; // Outputs the IP address of the server

echo "<br>";

 

echo $_SERVER['SERVER_PORT']; // Outputs the port number to which the request was sent

echo "<br>";

 

echo $_SERVER['DOCUMENT_ROOT']; // Outputs the document root directory under which the current script is executing

echo "<br>";

 

echo $_SERVER['HTTP_ACCEPT_LANGUAGE']; // Outputs the languages the client can accept, based on the Accept-Language HTTP header

echo "<br>";

echo $_SERVER['PHP_SELF'];

echo "<br>";

echo $_SERVER['SERVER_NAME'];

echo "<br>";

echo $_SERVER['HTTP_HOST'];

echo "<br>";

echo $_SERVER['HTTP_REFERER'];

 

...

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: PHP Main: ICT File: Download PDF Views 506

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

PHP - somo la 43: Jinsi ya kutuma email kwa kutumia PHP

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kutuma email kwa kutumia email() function ya PHP. Hii ni njia rahisi zaidi ya kutuma email. Ila hufanya kazi kwenye hosting.

Soma Zaidi...
PHP - somo la 46: Nini maana ya cronjob na matumizi yake

Katika somo hili utajifunza kuhusu cronjob na matumizi yake kwenye PHP

Soma Zaidi...
PHP somo la 49: utangulizi wa Object Oriented Programming katika PHP

Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya PHP na hapa tunaaza rasmi advanced PHP. tutakwenda kuingia ndani zaidi kwenye PHP. Ni vyema kabla ya kuanza course hii ya advanced PHP uwe una uelewa wa kutosha kuhusu mafunzo yetu ya PHP.

Soma Zaidi...
PHP -somo la 31: Matumizi ya include() na require() function kwenye php

Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kuandika function za PHP kama require() na iclude()

Soma Zaidi...
PHP - somo la 17: Jinsi ya kuingiza data kwenye database kwa kutumia PHP

Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuingiza data kwenye dtabase kwa kutumia PHP.

Soma Zaidi...
PHP somola 63: Jinsi ya ku connect database kwa kutumia PDO na faida zake

Katika soo hili utakwenda kujifunza umuhmu wa kutumia PDO kwenye PHP kwa ajili ya kutumia database.

Soma Zaidi...
PHP - somo la 21: Jinsi ya kutafuta kitu kwenye database kwa mutumia PHP

Katika somo hili utakwenda kujifundisha jinsi ya kutafuta taarifa maalumu kwenye database kwa kutumia PHP

Soma Zaidi...
PHP BLOG - somo la 7: Jinsi ya kutengeneza ukurasa wa kusoma post kwenye blog

HApa utakwenda kujifunza sasa namna ya kuzisoma post kutoka kwenye blog

Soma Zaidi...
PHP somo la 102: Cron job

atika somo hli tutakwenda kujifunza kuhusu kitu kinachitwa cron job. ni moja ya teknolojia zinazotumika kufanya kazi zinazofanyika automatic

Soma Zaidi...
PHP somo la 95: Jinsi ya kutengeneza customer ORM

Katika somo hili uttakwend akujifunz ajinsi ambavyo utaweza kutengeneza simple ORM yakwako mwenyewe

Soma Zaidi...