PHP - somo la 20 : Jinsi ya kufuta na ku update data kwenye database kwa kutumia PHP
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku update na kufuta data kwenye database kwa kutumia PHP
Ili ku update data tunatumia UDATE na kufuta tunatumia DELETE. Ni muhimu sana kujuwa kufuta na ku update taarifa kwa sababu mbalimbali. Hatahivyo unatakiwa pia uwe makini wakati wa kufuta taarifa, kwani usipoangalia makini command zako unaweza kujikuta unafuta data zote ama table ama database, ama ukafuta row tofauti na uliokusudia.
-
ku update taarifa kwenye database.
Mfano tunataka kubadili price kwenye ugali kutoka 1500 kuwa 1000. hivyo hapa tutatakiwa ku update taarifa hizi. Kitu cha kwanza unachotakiwa kujuwa ni id ya ugali ni ngapi kwenye table yako. Kulingana na table yetu ya menu ad ya ugali ni 1.
Jinsi yakuandaa SQL ya kuweza ku update taarifa
Utaandika UPTADE kisha ikifuatiwa na jina la table mfano UPDATE menu kisha utaandika SET ili kuweza kuset hizo data mpya. mfano UPDATE menu SET itafuatiwa na column unayotaka kui update ikifuatiwa na alama ya =, kwakuwa sisi tunataka ku update column ya price itakuwa hivi UPDATE menu SET price baada ya hapo ni kuweka VALUE au thamani ya hizo data unazotaka ziwe, hakikisha ziwe ndani ya ‘’ kama string (rejea mafunzo ya php kuhusu string). hivyo itakuwa UPDATE menu SET price = ‘1000’ hapa itafuatiwa na WHERE kisha utaweka id ya hiyo row yako. hiyo itakuwa hivi UPDATE menu SET price = ‘1000’ WHERE id = 1
kinachofuata ni kuandaa variable zako kwa ajili ya ku connect na database kama tulivyoona katika masomo yaliopita. Variable ya ku update sasa itasomeka hivi
$sql = "UPDATE menu SET price='1000' WHERE id=1";
Sehemu zilizobakia kila kitu hakuna mabadiliko mengi. Hivyo code nzima za ku update ugali zitasomeka kama hivi
<?php
$servername = "localhost";
$username = "root";
$password = "";
$dbname = "hotel";
// Create connection
$conn = mysqli_connect($servername, $username, $password, $dbname);
// Check connection
if (!$conn) {
die("Connection failed: " . mysqli_connect_error());
}
$sql = "UPDAT...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 web hosting 👉4 Simulizi za Hadithi Audio 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
PHP - somo la 40: Jinsi ya kutumia htaccess file kubadilisha muonekano wa link
Katika somo hili uatakwenda kujifunza jinsi ya kutumia htaccess ili kubadili muonekano wa link ya website ama blog ili kuifanya iwe rafiki zaidi.
Soma Zaidi...PHP - somo la 11: Jinsi ya kutuma tarifa zilizojazwa kwenye form
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kukusanya taarifa za watumiaji kwa kutumia html form.
Soma Zaidi...PHP BLOG - somo la 4: Jinsi ya kutengeneza ukurasa kwa ajili ya kupost
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya kutengeneza ukurasa wa kupost kwa kutumia html form
Soma Zaidi...PHP - somo la 22: Kutafuta jumla, wastani na idani ya vitu kwenye database kw akutumia PHP
Katika somo hili utakwenda jifunza jinsi ya kuhesabu row kwenye database, kutafuta wastani wa taarifa kwenye database na kutafuta idadi yake.
Soma Zaidi...PHP somo la 79: Custom header
Katika somo hili utakwenda kuhifunza kuhusu Custom header na aina zake
Soma Zaidi...PHP - somo la 16: Jinsi ya kufuta tabale na database kwa kutumia php
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kufuta table ya databse kwa kutumia PHP. Pia utajifunza jinsi ya kututa database yeto
Soma Zaidi...