PHP - somo la 20 : Jinsi ya kufuta na ku update data kwenye database kwa kutumia PHP
Katika somo hili utakwenda kujifunza jinsi ya ku update na kufuta data kwenye database kwa kutumia PHP
Ili ku update data tunatumia UDATE na kufuta tunatumia DELETE. Ni muhimu sana kujuwa kufuta na ku update taarifa kwa sababu mbalimbali. Hatahivyo unatakiwa pia uwe makini wakati wa kufuta taarifa, kwani usipoangalia makini command zako unaweza kujikuta unafuta data zote ama table ama database, ama ukafuta row tofauti na uliokusudia.
-
ku update taarifa kwenye database.
Mfano tunataka kubadili price kwenye ugali kutoka 1500 kuwa 1000. hivyo hapa tutatakiwa ku update taarifa hizi. Kitu cha kwanza unachotakiwa kujuwa ni id ya ugali ni ngapi kwenye table yako. Kulingana na table yetu ya menu ad ya ugali ni 1.
Jinsi yakuandaa SQL ya kuweza ku update taarifa
Utaandika UPTADE kisha ikifuatiwa na jina la table mfano UPDATE menu kisha utaandika SET ili kuweza kuset hizo data mpya. mfano UPDATE menu SET itafuatiwa na column unayotaka kui update ikifuatiwa na alama ya =, kwakuwa sisi tunataka ku update column ya price itakuwa hivi UPDATE menu SET price baada ya hapo ni kuweka VALUE au thamani ya hizo data unazotaka ziwe, hakikisha ziwe ndani ya ‘’ kama string (rejea mafunzo ya php kuhusu string). hivyo itakuwa UPDATE menu SET price = ‘1000’ hapa itafuatiwa na WHERE kisha utaweka id ya hiyo row yako. hiyo itakuwa hivi UPDATE menu SET price = ‘1000’ WHERE id = 1
kinachofuata ni kuandaa variable zako kwa ajili ya ku connect na database kama tulivyoona katika masomo yaliopita. Variable ya ku update sasa itasomeka hivi
$sql = "UPDATE menu SET price='1000' WHERE id=1";
Sehemu zilizobakia kila kitu hakuna mabadiliko mengi. Hivyo code nzima za ku update ugali zitasomeka kama hivi
<?php
$servername = "localhost";
$username = "root";
$password = "";
$dbname = "hotel";
// Create connection
$conn = mysqli_connect($servername, $username, $password, $dbname);
// Check connection
if (!$conn) {
die("Connection failed: " . mysqli_connect_error());
}
$sql = "UPDAT...
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 web hosting 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
PHP BLOG - somo la 1: Utangulizi na jinsi ya kuandaa kwa ajili ya somo
Katika course hii utakwenda kujifundisha jinsi ya lutengeneza blog kutoka mwanzo hadi mwisho.
Soma Zaidi...PHP somola 63: Jinsi ya ku connect database kwa kutumia PDO na faida zake
Katika soo hili utakwenda kujifunza umuhmu wa kutumia PDO kwenye PHP kwa ajili ya kutumia database.
Soma Zaidi...PHP somo la 75: Content-Type Header
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu content-type header.
Soma Zaidi...PHP - somo la 25: Jinsi ya kukusanya taarifa kutoka kwenye html form kwa kutumia php
Katika somo hili utajifunza jinsi ya kukusanya taarifa ambazo watu wamezijaza kwa kutumia fomu ya html. Kisha utajifunza jinsi ya kuzisoma hizo taarifa.
Soma Zaidi...PHP somo la 58: static method kwenye PHP
Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu static method na inavtotumika kwenye OOP
Soma Zaidi...PHP somo la 49: utangulizi wa Object Oriented Programming katika PHP
Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya PHP na hapa tunaaza rasmi advanced PHP. tutakwenda kuingia ndani zaidi kwenye PHP. Ni vyema kabla ya kuanza course hii ya advanced PHP uwe una uelewa wa kutosha kuhusu mafunzo yetu ya PHP.
Soma Zaidi...