Huu ni muendelezowa mafunzo ya database kwa kutumia MySQl na hili ni somo la 12. katika somo hili tutajifunza namna ya kufanya mahesabu kwa kutumia SQl katika database
Katika somo ka 10 na 11 tumejifunza namna ya kupangilia data zetu. Sasa hapa tutakwenda kujifunza mambo makuu 3 mabayo nu kuhesabu idadi ya row, kuhesamu jumla ya item na kuhesabu wastani. Hili ndio somo la mwisho ambalo linakwenda kutufungia mafunzo yetu ya database level 1.
1. Kuhesabu idadi ya row.
Lamda hujaelewa row ni nini? Unapoweka data kwenye database kila moja inakaa kwenye row, mmmh, lamda bado lugha ni ngumu, yaani hapa ninachomaanishwa ni data ngapi umeweka. Mfano kwenye table yetu tunatocheza nayo kuna idadi ya menu 10 yaani kuna row 10. sasa fikiria database ni kubwa sana na unataka kujuwa ina row ngapi njia rahisi sio kuhesabu ni kutumia SQL.
Kanuni yetu ni ni kutumia COUNT() function (rejea kuhusu function kwenye mafunzo ya php). utaanza kuselect kisha count ndani ya mabano ya function utaweka jina la column mfano name kisha from ikifuatiwa na jina la table. Unaweza pia kuweka na condition kwa kutumia where . mfano
SELECT COUNT(price) FROM menu
Kwa mfano huu itakuletea 10 kwani idadi ya row hapo ni 10. lakini kama ninataka kuhesabu idadi ta row ambazo price ni zaidi ya 1000 hapo itatubidu tutumie condition. Hivyo itakuwa hivi:-
SELECT COUNT(price) FROM menu WHERE price >1000
Hapo itakuletea 7 yaani jumala ya row zote ambazo price yake ni zaidi ya 1000 ni 7 yaani menu ambazo gharama yake ni zaidi ya 1000 zipo 7.
2. Kutafuta average au wastani
Kufanya hivi tutatumia AVG() function. Mpangilio wake ni sawa na huo uliotangulia hapo juu. Kwa mfano tunataka kujuwa menu zote hapo wastani wake ni kiasi gani. Kumbuka kuna toauti ya wastani na jumla, Wastani ji jumla gawanya kwa idani. (rejea kanuni za hesabu darasa la tano). hivyo itakuwa hivi:-
SELECT AVG(price) FROM menu
Hapo itakupa jibu 4920 yaani wastani wa gharama kwa kila menu ni 4920. kama unataka kuhakiki tumia kanuni huu ya darasa la tano (wastani = jumla/idadi). unaweza pia kutumia WHERE condition kama tulivyoona hapo juu.
3. Kutafuta jumla
Sasa tunataka kujuwa jumala ya menu zote zinagharimu kiasi gani. Ili kufanya hivi tutatumia SUM () function. Hii itatuletea jumala ya item kwenye column. Kama ulivyoona hapo kwenye menu yetu kila kitu na gharama zake saja jumla yake itakuwaje. Mpangilio wa fomula hii ni sawa na hizi mifano miwili iliyotangulia hapo juu. Hivyo itakuwa hivi
SELECT SUM(price) FROM menu
Hiyo itakupa jibu la 49200 yaani kama utajumlisha gharama zote hapo utapata 49200. sasa kama unataka kuthibitisha kanuni hizi kwa hesabu ya darasa la 5 unaweza.
Unaweza pia kutumia condition. Kwa mfano tunataka kujuwa jumla ya menu zote ambazo price ni chini ya 3000. hii itakuwa SELECT SUM(price) FROM menu WHERE price <3000 ambapo tutapata jibu la 6700.
4. Maximum na minimun
Tunataka kujuwa menu yenye gharama ndogo kuliko zote amba kubwa kuliko zote. Kufanya hivi tutatumia MAX() na MIN(). mifano mimngine ni kama ilivyotangulia. Hivyo kama ukipanga vyema itakuwa hivi:-
A. SELECT MAX(PRICE) FROM menu
Hapa itakupa jibu 25000 kwani ndio price kubwa kuliko zote.
B. SELECT MIN(PRICE) FROM menu
Hapo itakupa jibu 300 kwani ndio price ndogo kuliko zote
Na huu ndio mwisho wa mafunzo haya ya database level 1. tukutane level 2 tutakapojifunza mabo mengi zaidi katika database. Usikose mapunzo yetu mengine ya php level 2 na html level 3.
Mafunzo haya yamekujia kwa Ihsani ya bongoclass
Web: www.bongoclass.com
Email: mafunzo@bongoclass.com
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Ktika somo hili la 7 utajifunza namna ya kuandaa na kujiandaa kutengeneza website ama blog. Pia utajifunza maandalizi ya kuhost
Soma Zaidi...Mafunzo ya database kwa utumia software ya MySQL kwa lugha ya kiswahili na hili ni somo la 7.
Soma Zaidi...Karibu tena katika mafunzo yetu, na huu ni mwanzo wa mafunzoya DATABASE kwa kutumia MYSQL kwa lugha ya kiswahili. Na hili ni somo la kwanza, katka somo hili utajifunza jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya mafunzo.
Soma Zaidi...Somo la nane mafunzo ya php, katika somo hili utajifunza kuhusu array na jinsi ya kutengeneza array.
Soma Zaidi...Hili n somo la tatu katka muendelezo wa mafunzo ya HTML LEVEL 2 kwa lugha ya kiswahili. Mafunzo haya yanakujia kwa Ihsani ya bongoclass
Soma Zaidi...Huu ni muendelezo wa mafunzo ya DATABASE kwa kutumia software ya MySQL na hili ni somo la tano. katika somo hili utajifunza type of data yaani aina ya taarifa ambazo unaweza kuzihifadhi kwenye database yako.
Soma Zaidi...Hili ni somo la Tatu katika mfululizo wetu wa mafunzo ya HTML kwa basic level kwa wanaoanza kujifunza. Hapa tutakwenda kujifunza tag za html ambazo huwa zinatumika katika uandishi.
Soma Zaidi...hili ni somo la sita katika mfululizo wa mafunzo ya HTML level 1. Katika somo hili tutajifunza mambo makuu matatu ambayo ni kuweka menyu, kuweka background color na kufanya faili lako liwe responsive.
Soma Zaidi...Haya ni mafunzo ya HTML kwa wanaoanza level ya kwanza, na hili ni somo la kwanza katika masomo 8 yatakayokujia katika mtiririko wa course hii.
Soma Zaidi...Huu ni muendelezo wa mafunzo ya database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la 6. Katika somo hili tutakwenda kuona jinsi ya kutengeneza table kwa kutumia MySQL na kwa kutuma SQL.
Soma Zaidi...