Huu ni muendelezowa mafunzo ya database kwa kutumia MySQl na hili ni somo la 12. katika somo hili tutajifunza namna ya kufanya mahesabu kwa kutumia SQl katika database
Katika somo ka 10 na 11 tumejifunza namna ya kupangilia data zetu. Sasa hapa tutakwenda kujifunza mambo makuu 3 mabayo nu kuhesabu idadi ya row, kuhesamu jumla ya item na kuhesabu wastani. Hili ndio somo la mwisho ambalo linakwenda kutufungia mafunzo yetu ya database level 1.
1. Kuhesabu idadi ya row.
Lamda hujaelewa row ni nini? Unapoweka data kwenye database kila moja inakaa kwenye row, mmmh, lamda bado lugha ni ngumu, yaani hapa ninachomaanishwa ni data ngapi umeweka. Mfano kwenye table yetu tunatocheza nayo kuna idadi ya menu 10 yaani kuna row 10. sasa fikiria database ni kubwa sana na unataka kujuwa ina row ngapi njia rahisi sio kuhesabu ni kutumia SQL.
Kanuni yetu ni ni kutumia COUNT() function (rejea kuhusu function kwenye mafunzo ya php). utaanza kuselect kisha count ndani ya mabano ya function utaweka jina la column mfano name kisha from ikifuatiwa na jina la table. Unaweza pia kuweka na condition kwa kutumia where . mfano
SELECT COUNT(price) FROM menu
Kwa mfano huu itakuletea 10 kwani idadi ya row hapo ni 10. lakini kama ninataka kuhesabu idadi ta row ambazo price ni zaidi ya 1000 hapo itatubidu tutumie condition. Hivyo itakuwa hivi:-
SELECT COUNT(price) FROM menu WHERE price >1000
Hapo itakuletea 7 yaani jumala ya row zote ambazo price yake ni zaidi ya 1000 ni 7 yaani menu ambazo gharama yake ni zaidi ya 1000 zipo 7.
2. Kutafuta average au wastani
Kufanya hivi tutatumia AVG() function. Mpangilio wake ni sawa na huo uliotangulia hapo juu. Kwa mfano tunataka kujuwa menu zote hapo wastani wake ni kiasi gani. Kumbuka kuna toauti ya wastani na jumla, Wastani ji jumla gawanya kwa idani. (rejea kanuni za hesabu darasa la tano). hivyo itakuwa hivi:-
SELECT AVG(price) FROM menu
Hapo itakupa jibu 4920 yaani wastani wa gharama kwa kila menu ni 4920. kama unataka kuhakiki tumia kanuni huu ya darasa la tano (wastani = jumla/idadi). unaweza pia kutumia WHERE condition kama tulivyoona hapo juu.
3. Kutafuta jumla
Sasa tunataka kujuwa jumala ya menu zote zinagharimu kiasi gani. Ili kufanya hivi tutatumia SUM () function. Hii itatuletea jumala ya item kwenye column. Kama ulivyoona hapo kwenye menu yetu kila kitu na gharama zake saja jumla yake itakuwaje. Mpangilio wa fomula hii ni sawa na hizi mifano miwili iliyotangulia hapo juu. Hivyo itakuwa hivi
SELECT SUM(price) FROM menu
Hiyo itakupa jibu la 49200 yaani kama utajumlisha gharama zote hapo utapata 49200. sasa kama unataka kuthibitisha kanuni hizi kwa hesabu ya darasa la 5 unaweza.
Unaweza pia kutumia condition. Kwa mfano tunataka kujuwa jumla ya menu zote ambazo price ni chini ya 3000. hii itakuwa SELECT SUM(price) FROM menu WHERE price <3000 ambapo tutapata jibu la 6700.
4. Maximum na minimun
Tunataka kujuwa menu yenye gharama ndogo kuliko zote amba kubwa kuliko zote. Kufanya hivi tutatumia MAX() na MIN(). mifano mimngine ni kama ilivyotangulia. Hivyo kama ukipanga vyema itakuwa hivi:-
A. SELECT MAX(PRICE) FROM menu
Hapa itakupa jibu 25000 kwani ndio price kubwa kuliko zote.
B. SELECT MIN(PRICE) FROM menu
Hapo itakupa jibu 300 kwani ndio price ndogo kuliko zote
Na huu ndio mwisho wa mafunzo haya ya database level 1. tukutane level 2 tutakapojifunza mabo mengi zaidi katika database. Usikose mapunzo yetu mengine ya php level 2 na html level 3.
Mafunzo haya yamekujia kwa Ihsani ya bongoclass
Web: www.bongoclass.com
Email: mafunzo@bongoclass.com
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Tehama Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 1380
Sponsored links
👉1
kitabu cha Simulizi
👉2
Madrasa kiganjani
👉3
Simulizi za Hadithi Audio
👉4
Kitabu cha Afya
👉5
Kitau cha Fiqh
👉6
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Mafunzo ya HTML Level 1 somo la 2 for beginner (html full course for beginners)
Somo la pili katika mafunzo ya HTML level 2. Katika somo hili utajifunza maana ya HTML pamoja na historia yake fupi. Soma Zaidi...
Mafunzo ya Database MySQL database somo la 10
Huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la 10. katika somo hili tutakwenda kuendelea namna ya kupangilia muonekano wa data zako kwenye database. Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML level 1 somo la 2 (HTML basic level FOR BEGINNERS)
Hili ni somo la pili katika mfululizo wa mafunzo ya html level ya 1 na hapa tutakwenda sasa kunanza somo letu rasmi, kwani katika somo la kwanza umejifunza jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya mafunzo. Soma Zaidi...
PHP level 1 somo la tano (5)
Haya ni mafunzo ya php na hili ni somo la tano. Katika somovhili utajifunza namna ya kutengeneza functions. Soma Zaidi...
Mafunzo ya database MySQL somo la 3
Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database na jinsi ya kutengeneza bloga na website na hili ni somo la tatu. hapa utajifunza jinsiya kutengeneza database yako kwa mara ya kwanza. Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML kwa wenye kuanza (basic level)
Huu ni utangalizi wa mafunzo ya HTML kwa wenye kuanza level ya kwanza kwa lugha ya kiswahili. Haapa utapata msingi wa kuweza kutengeneza tovuti na blog. Soma Zaidi...
Mafunzo ya database mySQl database somo la 11
huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database klwa kutumia MySQL na hili ni somo la 11. katika somo hili tutaendelea kujifunza mpangilio wa muonekano wa data kwenye database. Soma Zaidi...
Mafunzo ya php level 1 somo la tatu (3)
hili ni somo la tatu katika masomo ya php level 1. Hapa utajifunza zaidi kuhusu variable na namna ya kuitengeneza. Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 6 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 6)
Katika somo hili la 6 mafunzo ya HTML level 2, tutajfunza namna ya kugawa ukurasa wa wavuti wa html. Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 3 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 3)
Hili n somo la tatu katka muendelezo wa mafunzo ya HTML LEVEL 2 kwa lugha ya kiswahili. Mafunzo haya yanakujia kwa Ihsani ya bongoclass Soma Zaidi...