Mafunzo yz database MySQL database somo la 12 (final)

Huu ni muendelezowa mafunzo ya database kwa kutumia MySQl na hili ni somo la 12. katika somo hili tutajifunza namna ya kufanya mahesabu kwa kutumia SQl katika database

Katika somo ka 10 na 11 tumejifunza namna ya kupangilia data zetu. Sasa hapa tutakwenda kujifunza mambo makuu 3 mabayo nu kuhesabu idadi ya row, kuhesamu jumla ya item na kuhesabu wastani. Hili ndio somo la mwisho ambalo linakwenda kutufungia mafunzo yetu ya database level 1.

 

1. Kuhesabu idadi ya row.

Lamda hujaelewa row ni nini? Unapoweka data kwenye database kila moja inakaa kwenye row, mmmh, lamda bado lugha ni ngumu, yaani hapa ninachomaanishwa ni data ngapi umeweka. Mfano kwenye table yetu tunatocheza nayo kuna idadi ya menu 10 yaani kuna row 10. sasa fikiria database ni kubwa sana na unataka kujuwa ina row ngapi njia rahisi sio kuhesabu ni kutumia SQL.

 

Kanuni yetu ni ni kutumia COUNT() function (rejea kuhusu function kwenye mafunzo ya php). utaanza kuselect kisha count ndani ya mabano ya function utaweka jina la column mfano name kisha from ikifuatiwa na jina la table. Unaweza pia kuweka na condition kwa kutumia where . mfano

SELECT COUNT(price) FROM menu 

 

Kwa mfano huu itakuletea 10 kwani idadi ya row hapo ni 10. lakini kama ninataka kuhesabu idadi ta row ambazo price ni zaidi ya 1000 hapo itatubidu tutumie condition. Hivyo itakuwa hivi:-

SELECT COUNT(price) FROM menu WHERE price >1000

Hapo itakuletea 7 yaani jumala ya row zote ambazo price yake ni zaidi ya 1000 ni 7 yaani menu ambazo gharama yake ni zaidi ya 1000 zipo 7.

 

2. Kutafuta average au wastani

Kufanya hivi tutatumia AVG() function. Mpangilio wake ni sawa na huo uliotangulia hapo juu. Kwa mfano tunataka kujuwa menu zote hapo wastani wake ni kiasi gani. Kumbuka kuna toauti ya wastani na jumla, Wastani ji jumla gawanya kwa idani. (rejea kanuni za hesabu darasa la tano). hivyo itakuwa hivi:-

SELECT AVG(price) FROM menu

 

Hapo itakupa jibu 4920 yaani wastani wa gharama kwa kila menu ni 4920. kama unataka kuhakiki tumia kanuni huu ya darasa la tano (wastani = jumla/idadi). unaweza pia kutumia WHERE condition kama tulivyoona hapo juu.

 

3. Kutafuta jumla 

Sasa tunataka kujuwa jumala ya menu zote zinagharimu kiasi gani. Ili kufanya hivi tutatumia SUM () function. Hii itatuletea jumala ya item kwenye column. Kama ulivyoona hapo kwenye menu yetu kila kitu na gharama zake saja jumla yake itakuwaje. Mpangilio wa fomula hii ni sawa na hizi mifano miwili iliyotangulia hapo juu. Hivyo itakuwa hivi

SELECT SUM(price) FROM menu

 

Hiyo itakupa jibu la 49200 yaani kama utajumlisha gharama zote hapo utapata 49200. sasa kama unataka kuthibitisha kanuni hizi kwa hesabu ya darasa la 5 unaweza.

 

Unaweza pia kutumia condition. Kwa mfano tunataka kujuwa jumla ya menu zote ambazo price ni chini ya 3000. hii itakuwa SELECT SUM(price) FROM menu WHERE price <3000 ambapo tutapata jibu la 6700.

 

4. Maximum na minimun

Tunataka kujuwa menu yenye gharama ndogo kuliko zote amba kubwa kuliko zote. Kufanya hivi tutatumia MAX() na MIN(). mifano mimngine ni kama ilivyotangulia. Hivyo kama ukipanga vyema itakuwa hivi:-

A. SELECT MAX(PRICE) FROM menu 

Hapa itakupa jibu 25000 kwani ndio price kubwa kuliko zote.

B. SELECT MIN(PRICE) FROM menu

Hapo itakupa jibu 300 kwani ndio price ndogo kuliko zote

 

Na huu ndio mwisho wa mafunzo haya ya database level 1. tukutane level 2 tutakapojifunza mabo mengi zaidi katika database. Usikose mapunzo yetu mengine ya php level 2 na html level 3.

 

Mafunzo haya yamekujia kwa Ihsani ya bongoclass

Web: www.bongoclass.com

Email: mafunzo@bongoclass.com

 

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tehama Main: Jifunze File: Download PDF Views 1770

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 6 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 6)

Katika somo hili la 6 mafunzo ya HTML level 2, tutajfunza namna ya kugawa ukurasa wa wavuti wa html.

Soma Zaidi...
PHP level 1 somo la tano (5)

Haya ni mafunzo ya php na hili ni somo la tano. Katika somovhili utajifunza namna ya kutengeneza functions.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya php level 1 somo la tatu (3)

hili ni somo la tatu katika masomo ya php level 1. Hapa utajifunza zaidi kuhusu variable na namna ya kuitengeneza.

Soma Zaidi...
Php level 1 somo la saba (7)

Hili ni somo la saba, mafunzo ya php level 1. Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika function yako mwenyewe.

Soma Zaidi...
Matumizi ya AI yanaathiri uwezo wa ubongo

Hii ni tafiti ambayo itakushangaza, kwa namna ambavyo matumizi ya AI yalivyo na athari kwenye uwezo wa kufikiri

Soma Zaidi...
Utangulizi wa Android App Development

Haya ni mafunzo ya muda mfupi katika kujifunza hasa ujuzi wa kutengeneza Android App hata kama haujui kitu kuhusiana na Android Development

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 3 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 3)

Hili n somo la tatu katka muendelezo wa mafunzo ya HTML LEVEL 2 kwa lugha ya kiswahili. Mafunzo haya yanakujia kwa Ihsani ya bongoclass

Soma Zaidi...
PHP level 11 somo la kumi na moja (11)

Katika somo hilivutajifunza namna ya kutumia HTML form. Namna ya kuookea taarifa kutoka kwenye madodoso ya html form.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya DATABASE MYSQL na SQL somo la 1

Karibu tena katika mafunzo yetu, na huu ni mwanzo wa mafunzoya DATABASE kwa kutumia MYSQL kwa lugha ya kiswahili. Na hili ni somo la kwanza, katka somo hili utajifunza jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya mafunzo.

Soma Zaidi...
Mafunzo ya HTML Level 2 somo la 1 (HTML FULL COURSE FOR BEGINNERS LESSON 1)

hili ni somo la pili katika mafunzo ya HTML level 2 html full course for beginners. Katika somo hili tutaangalia utangulizi juu ya HTML na pia utajifunza faida za HTML.

Soma Zaidi...