Mafunzo yz database MySQL database somo la 12 (final)


image


Huu ni muendelezowa mafunzo ya database kwa kutumia MySQl na hili ni somo la 12. katika somo hili tutajifunza namna ya kufanya mahesabu kwa kutumia SQl katika database


Katika somo ka 10 na 11 tumejifunza namna ya kupangilia data zetu. Sasa hapa tutakwenda kujifunza mambo makuu 3 mabayo nu kuhesabu idadi ya row, kuhesamu jumla ya item na kuhesabu wastani. Hili ndio somo la mwisho ambalo linakwenda kutufungia mafunzo yetu ya database level 1.

 

1. Kuhesabu idadi ya row.

Lamda hujaelewa row ni nini? Unapoweka data kwenye database kila moja inakaa kwenye row, mmmh, lamda bado lugha ni ngumu, yaani hapa ninachomaanishwa ni data ngapi umeweka. Mfano kwenye table yetu tunatocheza nayo kuna idadi ya menu 10 yaani kuna row 10. sasa fikiria database ni kubwa sana na unataka kujuwa ina row ngapi njia rahisi sio kuhesabu ni kutumia SQL.

 

Kanuni yetu ni ni kutumia COUNT() function (rejea kuhusu function kwenye mafunzo ya php). utaanza kuselect kisha count ndani ya mabano ya function utaweka jina la column mfano name kisha from ikifuatiwa na jina la table. Unaweza pia kuweka na condition kwa kutumia where . mfano

SELECT COUNT(price) FROM menu 

 

Kwa mfano huu itakuletea 10 kwani idadi ya row hapo ni 10. lakini kama ninataka kuhesabu idadi ta row ambazo price ni zaidi ya 1000 hapo itatubidu tutumie condition. Hivyo itakuwa hivi:-

SELECT COUNT(price) FROM menu WHERE price >1000

Hapo itakuletea 7 yaani jumala ya row zote ambazo price yake ni zaidi ya 1000 ni 7 yaani menu ambazo gharama yake ni zaidi ya 1000 zipo 7.

 

2. Kutafuta average au wastani

Kufanya hivi tutatumia AVG() function. Mpangilio wake ni sawa na huo uliotangulia hapo juu. Kwa mfano tunataka kujuwa menu zote hapo wastani wake ni kiasi gani. Kumbuka kuna toauti ya wastani na jumla, Wastani ji jumla gawanya kwa idani. (rejea kanuni za hesabu darasa la tano). hivyo itakuwa hivi:-

SELECT AVG(price) FROM menu

 

Hapo itakupa jibu 4920 yaani wastani wa gharama kwa kila menu ni 4920. kama unataka kuhakiki tumia kanuni huu ya darasa la tano (wastani = jumla/idadi). unaweza pia kutumia WHERE condition kama tulivyoona hapo juu.

 

3. Kutafuta jumla 

Sasa tunataka kujuwa jumala ya menu zote zinagharimu kiasi gani. Ili kufanya hivi tutatumia SUM () function. Hii itatuletea jumala ya item kwenye column. Kama ulivyoona hapo kwenye menu yetu kila kitu na gharama zake saja jumla yake itakuwaje. Mpangilio wa fomula hii ni sawa na hizi mifano miwili iliyotangulia hapo juu. Hivyo itakuwa hivi

SELECT SUM(price) FROM menu

 

Hiyo itakupa jibu la 49200 yaani kama utajumlisha gharama zote hapo utapata 49200. sasa kama unataka kuthibitisha kanuni hizi kwa hesabu ya darasa la 5 unaweza.

 

Unaweza pia kutumia condition. Kwa mfano tunataka kujuwa jumla ya menu zote ambazo price ni chini ya 3000. hii itakuwa SELECT SUM(price) FROM menu WHERE price <3000 ambapo tutapata jibu la 6700.

 

4. Maximum na minimun

Tunataka kujuwa menu yenye gharama ndogo kuliko zote amba kubwa kuliko zote. Kufanya hivi tutatumia MAX() na MIN(). mifano mimngine ni kama ilivyotangulia. Hivyo kama ukipanga vyema itakuwa hivi:-

A. SELECT MAX(PRICE) FROM menu 

Hapa itakupa jibu 25000 kwani ndio price kubwa kuliko zote.

B. SELECT MIN(PRICE) FROM menu

Hapo itakupa jibu 300 kwani ndio price ndogo kuliko zote

 

Na huu ndio mwisho wa mafunzo haya ya database level 1. tukutane level 2 tutakapojifunza mabo mengi zaidi katika database. Usikose mapunzo yetu mengine ya php level 2 na html level 3.

 

Mafunzo haya yamekujia kwa Ihsani ya bongoclass

Web: www.bongoclass.com

Email: [email protected]

 



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    2 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    3 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    4 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Mafunzo ya database mySQl database somo la 11
huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database klwa kutumia MySQL na hili ni somo la 11. katika somo hili tutaendelea kujifunza mpangilio wa muonekano wa data kwenye database. Soma Zaidi...

image Mafunzo ya database MySQL somo la 3
Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database na jinsi ya kutengeneza bloga na website na hili ni somo la tatu. hapa utajifunza jinsiya kutengeneza database yako kwa mara ya kwanza. Soma Zaidi...

image Mafunzo ya DATABASE kwa kutumia MySQL DATABASE kwa kiswahili somo la 4
Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la nne katika mlolongo wa masomo haya. Katika somo hili utajifuza jinsi ya kubadili jina la database na kufuta database. Pia tutajifunza kutumia SQL kufanya hayo. Soma Zaidi...

image Mafunzo ya DATABASE - MySQL database somo la 8
Huuu ni muendeleo wa mafunzo ya database kwa lugha ya kiswahili, na hili ni somo la nane. Katika somo hli utajifunza namna ya kuweka taarifa kwenye database, kuzfuta na kuziediti yaani kuzifanyia marekebisho. Soma Zaidi...

image Mafunzo ya database MySQL database somo la 9
haya ni mafunzo ya database kwa kutumia MySQl na hili ni somo la 9. katika soo hili utajifunza namna ya kusoma ama kutumia taarifa zilizomo kwenye DATABASE. Soma Zaidi...

image Mafunzo ya DATABASE - MySQL database somo la 5
Huu ni muendelezo wa mafunzo ya DATABASE kwa kutumia software ya MySQL na hili ni somo la tano. katika somo hili utajifunza type of data yaani aina ya taarifa ambazo unaweza kuzihifadhi kwenye database yako. Soma Zaidi...

image Mafunzo ya DATABASE - MySQL somo la 7
Mafunzo ya database kwa utumia software ya MySQL kwa lugha ya kiswahili na hili ni somo la 7. Soma Zaidi...

image Mafunzo yz database MySQL database somo la 12 (final)
Huu ni muendelezowa mafunzo ya database kwa kutumia MySQl na hili ni somo la 12. katika somo hili tutajifunza namna ya kufanya mahesabu kwa kutumia SQl katika database Soma Zaidi...

image Mafunzo ya DATABASE MYSQL na SQL somo la 1
Karibu tena katika mafunzo yetu, na huu ni mwanzo wa mafunzoya DATABASE kwa kutumia MYSQL kwa lugha ya kiswahili. Na hili ni somo la kwanza, katka somo hili utajifunza jinsi ya kuandaa kifaa chako kwa ajili ya mafunzo. Soma Zaidi...

image Mafunzo ya database MySQL - DATABASE somo la 6
Huu ni muendelezo wa mafunzo ya database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la 6. Katika somo hili tutakwenda kuona jinsi ya kutengeneza table kwa kutumia MySQL na kwa kutuma SQL. Soma Zaidi...