hili ni somo la pili katika mfululizo wa mafunzo haya ya php level 1 na hapa utajifunza namna ya kuandika faili klako la kwanza la php.
SOMO LA PILI:
Tulishaona katika somo lililopita namna ya kuandaa kompyuta yako na simu yako kwa ajili ya kufunguwa php. Kwa maelezo yaliotangulia katika somo la kwanza uliweza kuandaa simu ama kompyuta yako kuwa server. Katika somo hili tutakwenda kujifunza tag za php na jinsi zinavyofanya kazi.
Php ni tofauti sana na html huwenda ni kwa sababu ni lugha mbili tofauti. Hata hivyo html ina mamia ya tag kama tulivyojifunza katika mafunzo ya html level ya kwanza na pili. Php ina tag chache. Katika mafunzo ya HTML pia tulijifunza kuwa kuna tag za kufungulia na kufungia.
TAG ZA PHP
Php hufunguliwa na tag . huwenda hizi ndio tag pekee za php zinazotumika katika kucode php. Tag hizi pia unaweza kuzifupisha kwa mfano
?>
Au
?>
ECHO na PRINT
Ili kuweza kuandika kitu na kionekane kama tulivyotumia kwenye html, basi php inatumia echo na print. Hizi ni statement mbili za php ambazo hutumika ili kuweza kuleta matokeo kwenye browser. Yaani unapoandika code za php zinachakatwa kwenye server, kisha matokeo yake hutolewa kwenye browser kama plain teext (maandishi ya kawaida) kisha html hufanya kazi yake ya kupangilia. Sasa ili kupata haya matokeo ya code za php ambapo mtumiaji wa mtandao ataona ndipo tunatumia hizi echo na print.
Mfano katika html unapotaka kuandika neno “hallo” ili lionekane na mtumiaji wa ukurasa huo utatumia tag mfano
. sasa katika php utaanza tag za php ya kufunga na kufunguwa ambazo ni
echo “hello”;
?>
Kwa kutumia print
print “hello”;
?>
Echo na print sio tag, katika php hizi zinaitwa statement. Tutajifunza zaidi kuhusu statement katika masomo mengine. Kwa ufupi ni kuwa echo na print zinafanya kazi sawa ijapokuwa utofauti wao ni mdogo. Kwa mfano echo ipo fasta katika kuleta matokeo kuliko print. Echo pia inatumika katika kuleta matokeo kutoka katika parameta zaidi ya moja. Hivyo ijapokuwa zote zinafanana ila zina utofauti mdogo.kama huna uhakika ipi utumie vyema kutumia echo.tutajifunza utofauti wao zaidi katika masomo yajayo.
HTML NA PHP
Php na html zote hutumika katika kutengeneza ukurasa wa wavuti. Katika faili ya html unaweza kutumia php na katika faili la php pia unaweza kutumia html. Ipo hivi browser yako inapokutana na tag za html itachakata na kuleta matokeo na ikikutana na tag ya php inapeleka mchakato kwenye server kisha server ikirudisha text ndipo inatoa matokeo. Mfano:-
Html ndani ya php
echo “
?>
Au unaweza kutumia hii:-
print “
Pia unaweza kuandika code za html nje ya tag za php katika faili la php mfano
echo “hello”
?>
hello
PHP NDANI YA HTML
Kama ilivyo ndani ya php file unaweza kuandika html hivyo hivyo unaweza kuandika php ndabi ya faili la html. Unaweza kueka code za php kwenye html tag ama nje ya html tag. Mfano
Kwa mfano huu code zote za php zilizopo ndani ya
NAMNA YA KUWEKA COMMENT KWENYE PHP
Tumejifunza kwenye html kuwa kukoment ni kwamba unaandika kumbukumbu zako katika code kwamba ili uweze kukumbuka amba mtu mwingine aweze kujuwa kwa urahisi kuwa msitari huo wa code unahusu nini. Komenti hazionekani kwa mtumiaji ijapokuwa zipo kwenye code.
Katika html tulujifunza kuwa ukitaka kukoment unatumia
Ila katika php utatumia // kisha utakomeny. Ama utatumia # kisha itakoment. Namna hii ya kukoment ni pale unapokoment kwa maneno yasiozidi msitari mmoja. Na kama unataka kukoment sana utatumia /* kisha utakomenta halafu utafunga kwa */ mfano:
//hallo
#hallo
?>
Au kama unataka kukoment misitari mingi
/* hello
Hii ni
Koment
*/
?>
Endelea kufanyika kazi zaidi somo hili, kwani somo linalofata litakuhitaji uwe umeweza angalau kujuwa tag za php.
Somo linalokuja tutakuja kuangalia namna ya kutumia variable, na kuonyesha matokeo.
Mafunzo haya yanakujia kwa ihsani ya bongoclass
Web: www.bongoclass.com
Email:mafunzo@bongoclass.com
Phone: 0774069753 unaweza kunicheki wasap kwa link hii https://wa.me/message/7CTQP5BSWBR5I1
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya hapa chini kuipakua sasa!
Umeionaje Makala hii.. ?
katika somo hili la tano kwenye mafunzo ya HTML level 1 utajifunza jinsi ya 1.Kuweka picha 2.Kuweka rangi 3.Kuweka linki 4.Kupangilia position na alignment ya maandishi 5.Kuongeza ukubwa wa herufi 6.Kukoment
Soma Zaidi...Somo la pili katika mafunzo ya HTML level 2. Katika somo hili utajifunza maana ya HTML pamoja na historia yake fupi.
Soma Zaidi...Huu ni mwendelezo wa mafunzo ya database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la nne katika mlolongo wa masomo haya. Katika somo hili utajifuza jinsi ya kubadili jina la database na kufuta database. Pia tutajifunza kutumia SQL kufanya hayo.
Soma Zaidi...Katika somo hili la 6 mafunzo ya HTML level 2, tutajfunza namna ya kugawa ukurasa wa wavuti wa html.
Soma Zaidi...Hili ni somo la Tatu katika mfululizo wetu wa mafunzo ya HTML kwa basic level kwa wanaoanza kujifunza. Hapa tutakwenda kujifunza tag za html ambazo huwa zinatumika katika uandishi.
Soma Zaidi...hili ni somo la tatu katika masomo ya php level 1. Hapa utajifunza zaidi kuhusu variable na namna ya kuitengeneza.
Soma Zaidi...Hili ni somo la mwisho mafunzo ya HTML level 2 (html full course for beginners)
Soma Zaidi...Huu ni utangalizi wa mafunzo ya HTML kwa wenye kuanza level ya kwanza kwa lugha ya kiswahili. Haapa utapata msingi wa kuweza kutengeneza tovuti na blog.
Soma Zaidi...Huu ni muendelezo wa mafunzo ya Database kwa kutumia MySQL na hili ni somo la 10. katika somo hili tutakwenda kuendelea namna ya kupangilia muonekano wa data zako kwenye database.
Soma Zaidi...Hili ni somo la saba, mafunzo ya php level 1. Katika somo hili utajifunza jinsi ya kuandika function yako mwenyewe.
Soma Zaidi...