Ugonjwa wa macho
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa macho, ni ugonjwa ambao ushambulia zaidi sehemu za nje za macho ambazo kwa kawaida uitwa conjunctiva na cornea hizi sehemu zikipata maambukizi zisipotibiwa mapema uweza kusababisha upofu kwa mgonjwa.
Ugonjwa wa macho.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kujua ni mdudu yupi anayesababisha ugonjwa huu, kwa jina la kitaalamu huitwa Chlamydia trachomatis ndiye anayesababisha ugonjwa huu, kwa hiyo Kuna baadhi ya viashiria ambavyo usababisha kuenea kwa ugonjwa huu na vyo ni .
2. Mazingira yaliyo makavu na yenye vumbi .
Kwa kawaida mazingira haya ndipo wadudu upenda kukaa na kuzaliana kwa hiyo ni vizuri sana iwapo ugonjwa huu ukitokea watu wanaoishi kwenye mazingira haya kuwa na tahadhari Ili kuweza kuepukana na ugonjwa huu ambao ni hatari kwa macho.
3. Sehemu yenye uchafu na inzi.
Kwa kawaida tunajua kuwa inzi ndo usababisha kuenea kwa ugonjwa huu kutoka kwa mgonjwa mmoja kwenda kwa mwingine kwa sababu ikitokea nzi akagusa jicho lililo na maambukizi na akabeba wadudu hao na kutua kwenye jicho la mtu mzima hao wadudu uanza kushambulia jicho na hatimaye maambukizi uenea sana na kusababisha madhara makubwa kama matibabu hayajafanyika.
4. Sehemu zenye mkusanyiko mkubwa wa watu.
Kwa kawaida kwenye mikusanyiko huwa Kuna matatizo na milipuka mingi ya magonjwa kwa hiyo na ugonjwa huu uonekana zaidi kwenye mikusanyiko ya watu kama vile kwa wakimbizi na wafungwa, hii ni kwa sababu ya kutokuwepo kwa uangalizi wa kutosha na usafi ni kidogo kwa hiyo ugonjwa huu ukitokea mazingira hayo ni vigumu kupona haraka.
5. Sehemu zenye uhaba wa maji.
Kweli ugonjwa huu ujitokeza kwenye sehemu zenye uhaba wa maji kwa sababu Kuna sehemu zina ukosefu wa maji ambapo watu utumia masaa kama matano kutafuta maji na ni vigumu kwenye mazingira hayo kukosekana ugonjwa huu kwa sababu uchafu utakuwepo watu watashindwa kupata maji ya kutosha ya kunawa na kufua nguo zao.
6. Kwa hiyo tunapaswa kuelewa kuwa ugonjwa huu upo kwenye jamii na una dawa ila uzembe ukifanyika Kuna hatari ya kupata upofu kwa hiyo ni vizuri kabisa kuwatibu wagonjwa wetu na kuzingatia usafi Ili kuepuka maambukizi
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Simulizi za Hadithi Audio 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Dalili za ugonjwa wa kipindupindu
Post hii inahusu zaidi juu ya ugonjwa wa kipindupindu.Ni dalili zinzojitokeza kwa magonjwa wa kipindupindu.
Soma Zaidi...Maajabu ya damu na mzunguuko wake mwilini.
Ukistaajabu ya Musa utastaajabu ya Firauni. Haya ni maneno ya wahenga. Sasa hebu njoo u staajabu ya damu
Soma Zaidi...Dalilili za maumivu ya kifua
Maumivu ya kifua huja kwa aina nyingi, kuanzia kuchomwa na kisu hadi kuuma kidogo. Baadhi ya Maumivu ya kifua yanafafanuliwa kama kuponda kuungua. Katika baadhi ya matukio, maumivu husafiri juu ya shingo, hadi kwenye taya.
Soma Zaidi...Ugonjwa wa kuporomoka kwa mapafu (pneumothorax)
Posti hii inazungumzia Ugonjwa wa mapafu ambao hujulikana Kama pafu lililoporomoka (Pneumothorax) hutokea wakati hewa inavuja kwenye nafasi kati ya mapafu yako na ukuta wa kifua. Hewa hii hutoka nje ya pafu lako. Ugonjwa huu unaweza kusababishwa na jera
Soma Zaidi...Dalili za moyo kushindwa kufanya kazi (heart failure)
post inaonyesha dalili mbalimbali za Kushindwa kwa moyo, wakati mwingine hujulikana kama kutofaulu kwa moyo, hutokea wakati misuli ya moyo wako haisukuma damu kama inavyopaswa. Hali fulani, kama vile ateri nyembamba katika moyo wako (Ugonjwa wa ateri y
Soma Zaidi...Dalili za Saratani ya utumbo mdogo.
Posti hii inaonyesha ishara na dalili za Saratani ya utumbo mdogo
Soma Zaidi...