Ugonjwa wa macho
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa macho, ni ugonjwa ambao ushambulia zaidi sehemu za nje za macho ambazo kwa kawaida uitwa conjunctiva na cornea hizi sehemu zikipata maambukizi zisipotibiwa mapema uweza kusababisha upofu kwa mgonjwa.
Ugonjwa wa macho.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kujua ni mdudu yupi anayesababisha ugonjwa huu, kwa jina la kitaalamu huitwa Chlamydia trachomatis ndiye anayesababisha ugonjwa huu, kwa hiyo Kuna baadhi ya viashiria ambavyo usababisha kuenea kwa ugonjwa huu na vyo ni .
2. Mazingira yaliyo makavu na yenye vumbi .
Kwa kawaida mazingira haya ndipo wadudu upenda kukaa na kuzaliana kwa hiyo ni vizuri sana iwapo ugonjwa huu ukitokea watu wanaoishi kwenye mazingira haya kuwa na tahadhari Ili kuweza kuepukana na ugonjwa huu ambao ni hatari kwa macho.
3. Sehemu yenye uchafu na inzi.
Kwa kawaida tunajua kuwa inzi ndo usababisha kuenea kwa ugonjwa huu kutoka kwa mgonjwa mmoja kwenda kwa mwingine kwa sababu ikitokea nzi akagusa jicho lililo na maambukizi na akabeba wadudu hao na kutua kwenye jicho la mtu mzima hao wadudu uanza kushambulia jicho na hatimaye maambukizi uenea sana na kusababisha madhara makubwa kama matibabu hayajafanyika.
4. Sehemu zenye mkusanyiko mkubwa wa watu.
Kwa kawaida kwenye mikusanyiko huwa Kuna matatizo na milipuka mingi ya magonjwa kwa hiyo na ugonjwa huu uonekana zaidi kwenye mikusanyiko ya watu kama vile kwa wakimbizi na wafungwa, hii ni kwa sababu ya kutokuwepo kwa uangalizi wa kutosha na usafi ni kidogo kwa hiyo ugonjwa huu ukitokea mazingira hayo ni vigumu kupona haraka.
5. Sehemu zenye uhaba wa maji.
Kweli ugonjwa huu ujitokeza kwenye sehemu zenye uhaba wa maji kwa sababu Kuna sehemu zina ukosefu wa maji ambapo watu utumia masaa kama matano kutafuta maji na ni vigumu kwenye mazingira hayo kukosekana ugonjwa huu kwa sababu uchafu utakuwepo watu watashindwa kupata maji ya kutosha ya kunawa na kufua nguo zao.
6. Kwa hiyo tunapaswa kuelewa kuwa ugonjwa huu upo kwenye jamii na una dawa ila uzembe ukifanyika Kuna hatari ya kupata upofu kwa hiyo ni vizuri kabisa kuwatibu wagonjwa wetu na kuzingatia usafi Ili kuepuka maambukizi
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 web hosting π2 Madrasa kiganjani π3 Simulizi za Hadithi Audio π4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) π5 Dua za Mitume na Manabii π6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Dalili za Maambukizi kwa Wanaume
βMakala haya yanatoa mwongozo muhimu kuhusu dalili za maambukizi ya mfumo wa mkojo na uzazi kwa wanaume. Tunasisitiza umuhimu wa utambuzi wa mapema na kutafuta ushauri wa kitaalamu wa kitabibu ili kuepuka matatizo ya muda mrefu ya kiafya.
Soma Zaidi...Dalili za tezi dume ambayo hazijashuka (cryptorchidism)
Tezi dume ambayo haijashuka si ya kawaida kwa ujumla, lakini ni ya kawaida kwa wavulana waliozaliwa kabla ya wakati.na muda mwingine zikipanda tumboni huwa hazishuki kabisa kwenye korodani.
Soma Zaidi...Ujue ugonjwa wa kuishiwa na damu
post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kuishiwa damu kwa kitaalamu huitwa(Anemia) ni ugonjwa wa kuishiwa na damu mwilini na kusababisha maisha ya mtu kuwa hatarini
Soma Zaidi...Madhara ya fangasi.
Posti hii inahusu zaidi madhara ya fangasi za ukeni kwa kawaida tunajua kubwa fangasi zikiingia kwenye uke usababisha madhara mbalimbali ambayo mengine yanaweza ya kudumu na mengine ya mda kama yametibiwa mapema.
Soma Zaidi...nahis miguu pamoja na mikono kuishiwa nguvu ni mgongo kuuma ni dalili za ugonjwa gan ?
mm nahis miguu pamoja na mikono kuishiwa nguvu ni mgongo kuuma ni dalili za ugonjwa gan ?
Soma Zaidi...Fahamu Ugonjwa wa mshtuko wa sumu.
Ugonjwa wa Mshtuko wa Sumu ni matatizo ya nadra, yanayotishia maisha ya aina fulani za maambukizi ya bakteria. Mara nyingi ugonjwa wa mshtuko wenye sumu hutokana na sumu zinazozalishwa na bakteria.
Soma Zaidi...