Ugonjwa wa macho
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa macho, ni ugonjwa ambao ushambulia zaidi sehemu za nje za macho ambazo kwa kawaida uitwa conjunctiva na cornea hizi sehemu zikipata maambukizi zisipotibiwa mapema uweza kusababisha upofu kwa mgonjwa.
Ugonjwa wa macho.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kujua ni mdudu yupi anayesababisha ugonjwa huu, kwa jina la kitaalamu huitwa Chlamydia trachomatis ndiye anayesababisha ugonjwa huu, kwa hiyo Kuna baadhi ya viashiria ambavyo usababisha kuenea kwa ugonjwa huu na vyo ni .
2. Mazingira yaliyo makavu na yenye vumbi .
Kwa kawaida mazingira haya ndipo wadudu upenda kukaa na kuzaliana kwa hiyo ni vizuri sana iwapo ugonjwa huu ukitokea watu wanaoishi kwenye mazingira haya kuwa na tahadhari Ili kuweza kuepukana na ugonjwa huu ambao ni hatari kwa macho.
3. Sehemu yenye uchafu na inzi.
Kwa kawaida tunajua kuwa inzi ndo usababisha kuenea kwa ugonjwa huu kutoka kwa mgonjwa mmoja kwenda kwa mwingine kwa sababu ikitokea nzi akagusa jicho lililo na maambukizi na akabeba wadudu hao na kutua kwenye jicho la mtu mzima hao wadudu uanza kushambulia jicho na hatimaye maambukizi uenea sana na kusababisha madhara makubwa kama matibabu hayajafanyika.
4. Sehemu zenye mkusanyiko mkubwa wa watu.
Kwa kawaida kwenye mikusanyiko huwa Kuna matatizo na milipuka mingi ya magonjwa kwa hiyo na ugonjwa huu uonekana zaidi kwenye mikusanyiko ya watu kama vile kwa wakimbizi na wafungwa, hii ni kwa sababu ya kutokuwepo kwa uangalizi wa kutosha na usafi ni kidogo kwa hiyo ugonjwa huu ukitokea mazingira hayo ni vigumu kupona haraka.
5. Sehemu zenye uhaba wa maji.
Kweli ugonjwa huu ujitokeza kwenye sehemu zenye uhaba wa maji kwa sababu Kuna sehemu zina ukosefu wa maji ambapo watu utumia masaa kama matano kutafuta maji na ni vigumu kwenye mazingira hayo kukosekana ugonjwa huu kwa sababu uchafu utakuwepo watu watashindwa kupata maji ya kutosha ya kunawa na kufua nguo zao.
6. Kwa hiyo tunapaswa kuelewa kuwa ugonjwa huu upo kwenye jamii na una dawa ila uzembe ukifanyika Kuna hatari ya kupata upofu kwa hiyo ni vizuri kabisa kuwatibu wagonjwa wetu na kuzingatia usafi Ili kuepuka maambukizi
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 web hosting 👉5 ai web app 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Dalili za miguu kufa ganzi
Posti hii inahusu zaidi dalili mbalimbali ambazo Uweza kujitokeza na kuona kwamba ni Dalili za miguu kufa ganzi, pengine utokea kwa watu wote na pengine huwa ni kwa ghafla
Soma Zaidi...Typhoid husabisha mwili kuchoka na maumivu ya kichwa pamoja na joint za miguu kuchoka
Dalili za typhid zinapasa kuangaliwa kwa umakini. Bila vipimo mtu asitumie dawa za tyohod, kwanu dalili za tyohid hufanana na daliki za maradhi mengi.
Soma Zaidi...Upele wa kuambukiza ukeni (BV): Tiba na kinga.
Bacterial Vaginosis (BV) ni hali inayotokea pale uwiano wa bakteria wazuri (wanaolinda uke) unapoathirika na bakteria wabaya kuzaliana kwa wingi. Hili si ugonjwa wa zinaa (STI), ingawa shughuli za kingono zinaweza kuongeza hatari ya kuupata. BV husababisha usumbufu mkubwa na ni muhimu kutibiwa ili kuepuka maambukizi ya mfumo wa uzazi. Makala haya yanakupa uelewa wa dalili, tiba, na mbinu za kuzuia hali hii isijirudie.
Soma Zaidi...Sababu za maumivu ya matiti na chuchu
Maumivu ya matiti yanaweza kuanzia kidogo hadi makali. Inaweza kukuathiri siku chache tu kwa mwezi, kwa mfano kabla tu ya kipindi chako, au inaweza kudumu kwa siku saba au zaidi kila mwezi. Maumivu ya matiti yanaweza kukuathiri kabla tu ya kipindi chako
Soma Zaidi...NI WATU GANI WALIO HATARINI ZAIDI KUPATA UKIMWI?
Post hii itakwena kukufundisha kuhusu historia fupi ya Ukimwi na matibabu yake. Ni wapi wapo hatarini kupata maambukizi na ni kitu gani wafanye?
Soma Zaidi...Aina ya kisukari inayojulikana kama Diabety type 1
Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kisukari Aina ya kwanza ambapo kwa kitaalamu huitwa Diabetes type 1, ni hali ambayo utokea ambapo mwili ushindwa kutengeneza insulini ambayo uweka sukari kwenye hali ya usawa.
Soma Zaidi...