Ugonjwa wa macho
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa macho, ni ugonjwa ambao ushambulia zaidi sehemu za nje za macho ambazo kwa kawaida uitwa conjunctiva na cornea hizi sehemu zikipata maambukizi zisipotibiwa mapema uweza kusababisha upofu kwa mgonjwa.
Ugonjwa wa macho.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kujua ni mdudu yupi anayesababisha ugonjwa huu, kwa jina la kitaalamu huitwa Chlamydia trachomatis ndiye anayesababisha ugonjwa huu, kwa hiyo Kuna baadhi ya viashiria ambavyo usababisha kuenea kwa ugonjwa huu na vyo ni .
2. Mazingira yaliyo makavu na yenye vumbi .
Kwa kawaida mazingira haya ndipo wadudu upenda kukaa na kuzaliana kwa hiyo ni vizuri sana iwapo ugonjwa huu ukitokea watu wanaoishi kwenye mazingira haya kuwa na tahadhari Ili kuweza kuepukana na ugonjwa huu ambao ni hatari kwa macho.
3. Sehemu yenye uchafu na inzi.
Kwa kawaida tunajua kuwa inzi ndo usababisha kuenea kwa ugonjwa huu kutoka kwa mgonjwa mmoja kwenda kwa mwingine kwa sababu ikitokea nzi akagusa jicho lililo na maambukizi na akabeba wadudu hao na kutua kwenye jicho la mtu mzima hao wadudu uanza kushambulia jicho na hatimaye maambukizi uenea sana na kusababisha madhara makubwa kama matibabu hayajafanyika.
4. Sehemu zenye mkusanyiko mkubwa wa watu.
Kwa kawaida kwenye mikusanyiko huwa Kuna matatizo na milipuka mingi ya magonjwa kwa hiyo na ugonjwa huu uonekana zaidi kwenye mikusanyiko ya watu kama vile kwa wakimbizi na wafungwa, hii ni kwa sababu ya kutokuwepo kwa uangalizi wa kutosha na usafi ni kidogo kwa hiyo ugonjwa huu ukitokea mazingira hayo ni vigumu kupona haraka.
5. Sehemu zenye uhaba wa maji.
Kweli ugonjwa huu ujitokeza kwenye sehemu zenye uhaba wa maji kwa sababu Kuna sehemu zina ukosefu wa maji ambapo watu utumia masaa kama matano kutafuta maji na ni vigumu kwenye mazingira hayo kukosekana ugonjwa huu kwa sababu uchafu utakuwepo watu watashindwa kupata maji ya kutosha ya kunawa na kufua nguo zao.
6. Kwa hiyo tunapaswa kuelewa kuwa ugonjwa huu upo kwenye jamii na una dawa ila uzembe ukifanyika Kuna hatari ya kupata upofu kwa hiyo ni vizuri kabisa kuwatibu wagonjwa wetu na kuzingatia usafi Ili kuepuka maambukizi
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
π1 kitabu cha Simulizi π2 web hosting π3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina π4 Kitabu cha Afya π5 Kitau cha Fiqh π6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
Je maumivu juu ya kitovu ni miongoni mwa dalili za mimba?
Dalili za mimba zinaweza kuanzia kuonekana mapema ndani ya wiki ya kwanza, japo sio rahisi nabhakuna uthibitishobwa uhakika juu ya kauli hii. Makala hii itakwebda kujibubswali la msingi la muuulizaji kama maumivu ya tumbo ni dalili ya ujauzito.
Soma Zaidi...Namna ya kuzuia virusi vya ukimwi
Posti hii inaelezea kuhusiana na kujikinga au kuzuia virusi vya ukimwi.
Soma Zaidi...Fahamu Ugonjwa wa misuli kuwa dhaifu.
hali ambayo misuli unayotumia kwa hotuba ni dhaifu au unapata shida kuidhibiti mara nyingi inaonyeshwa na usemi wa kufifia au polepole ambao unaweza kuwa mgumu kuelewa. Sababu za kawaida za Ugonjwa huu ni pamoja na matatizo ya mfumo wa neva (neurolojia
Soma Zaidi...Mambo yanayochangia katika makuzi ya mtoto
Post hii inahusu zaidi mambo yanayochangia katika makuzi ya mtoto, mtoto katika makuzi yake anahitaji kutunzwa vizuri Ili akue kwa afya nzuri bila magonjwa
Soma Zaidi...Dawa za kutuliza vvu zinaongeza damu
Hakuna dawa ya UKIMWI ya kutibu kuondoa virusi mwilini, lakini zipo dawa za kuweza kupunguza makali ya virusi hawa. Hivi unesha jiuliza kuwa je zile dawa zinaongeza damu?
Soma Zaidi...Ugonjwa wa kuungua Mdomo (mouth burning syndrome)
Ugonjwa wa mdomo unaounguaΓΒ ni neno la kimatibabu kwa ajili ya kuwaka moto mara kwa mara mdomoni bila sababu dhahiri. Usumbufu huo unaweza kuathiri ulimi wako, ufizi, midomo, ndani ya mashavu yako, paa la mdomo wako au maeneo yaliyoenea ya mdomo wako wot
Soma Zaidi...