picha

Dalili za ugonjwa wa upele

Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa upele, ni dalili au mwonekano wa mgonjwa wa upele.

Dalili za ugonjwa wa upele.

1. Kwanza kabisa tunafahamu kabisa mdudu anayesababisha ugonjwa huu kwa kitaalamu huitwa mites sarcoptes scabies, huyu mdudu kwa kawaida akishakomaa utaga mayai kwenye vishimo vidogo vya mwili na kuanza kuishi Humo na kusababisha maumivu makali sana kwa mwathirika hasa kama ugonjwa huu haukutibiwa mapema kwa kuwepo kwa mayai kwenye ngozi usababisha na dalili nyingine kama vile 

 

2. Kuwashwa wakati wa usiku.

Tunajua wazi kuwa wakati wa usiku ni mda ambao unakuwa umetulia sana na mwili pia unakuwa kwenye utulivu Fulani hakuna jua Wala kitu chochote cha kukusumbua mwili kwa hiyo ndipo wadudu Hawa uwa active na kuanza kushambulia na kusababisha kuwepo kwa miwasho na mgonjwa uanza kujikuna mara nyingi na kukosa kusinzia.

 

3. Hali ya kukosa kusinzia usababisha watoto kusinzia wakati wa mchana au kama wamefikia hatua ya kwenda shule usinzia darasani na kusababisha kupoteza mda wa masomo kwa hiyo ni vizuri kuwatibu watoto kwa tiba Sahihi na kuwafanya watoto waweze kuhudhulia masomo ipasavyo kwa hiyo wazazi wawe mstari wa mbele Ili kulinda na kuwatunza vizuri watoto Ili waweze kuepuka magonjwa kama haya.

 

4. Kuwepo kwa mikwaluzo kwenye ngozi.

Kwa sababu ya kujikuna sana mara nyingi kunakuwepo na mikwaluzo kwenye sehemu za ngozi na wakati mwingine mikwaluzo uandamana na kutokwa na damu ,hali hii uwanyima Raha watoto kwa sababu mda mwingi wanaendelea na kujikuna sana na pengine wanaweza kuleta maambukizi kwa watoto wenzao na wale wanaoishi nao.

 

5.  Kuwepo kwa vidonda kwenye sehemu mbalimbali za mwili, pindi maambukizi yanapozidi yanasababisha kuwepo kwa vidonda kwenye sehemu mbalimbali za mwili kama vile kwenye vidole, kwenye kiwiko, kwenye tumbo, kwenye kiuno, kwenye chuchu za matiti na sehemu mbalimbali za mwili kwa ujumla, kwa hiyo ni vizuri kutibu kwa sababu hizi dalili zikitokea kwa mtu mmoja kwenda familia ni lazima atawaambukiza na wengine

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 4373

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 web hosting     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

Dalili za maambukizi kwenye figo

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Maambukizi kwenye figo (pyelonephritis) ni aina mahususi ya maambukizi ya njia ya mkojo (UTI) ambayo kwa kawaida huanza kwenye urethra au kibofu chako na kusafiri hadi kwenye figo zako.

Soma Zaidi...
Aina za vyakula somo la 13: Faida za bamia

Katika somo hili utakwenda kujifunza kuhusu faida za bamia mwilini

Soma Zaidi...
Kujifungua kwa operesheni (Cesarean Section): Unachotakiwa kujua.

Kujifungua kwa operesheni, maarufu kama Cesarean Section (C-Section), ni utaratibu wa upasuaji unaofanywa ili kumtoa mtoto tumboni kupitia mkato katika tumbo na mji wa mimba wa mama. Ingawa wengi hupendelea uzazi wa kawaida, upasuaji huu ni njia salama na wakati mwingine ya kuokoa maisha ya mama na mtoto pale matatizo ya kiafya yanapojitokeza wakati wa ujauzito au leba. Makala hii inaangazia sababu, utaratibu, na hatua za kupona baada ya operesheni.

Soma Zaidi...
Fahamu matatizo ya ini kuwa na kovu

kovu (Fibrosis) ya ini inayosababishwa na aina nyingi za magonjwa na hali ya ini, kama vile Homa ya Ini na unywaji pombe kupita kiasi. Ini hufanya kazi kadhaa muhimu, ikiwa ni pamoja na kuondoa vitu vyenye madhara katika mwili wako, kusafisha damu yako

Soma Zaidi...
Je unaweza kupata ujauzito bila ya kupata hedhi miezi 9 baada ya kujifunguwa?

Baada ya kujifungua mwili wa mwanamke huwa na mabadiliko tofauti na siku za nyuma. Kwa mfano hatapatavtena hedhi, hatoweza kupata ujauzito kwa muda wa mwezi ama zaidi. Endelea na post hii ujifunze zaidi

Soma Zaidi...
Dalili za tezi dume ambayo hazijashuka (cryptorchidism)

Tezi dume ambayo haijashuka si ya kawaida kwa ujumla, lakini ni ya kawaida kwa wavulana waliozaliwa kabla ya wakati.na muda mwingine zikipanda tumboni huwa hazishuki kabisa kwenye korodani.

Soma Zaidi...