Dalili za ugonjwa wa upele
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa upele, ni dalili au mwonekano wa mgonjwa wa upele.
Dalili za ugonjwa wa upele.
1. Kwanza kabisa tunafahamu kabisa mdudu anayesababisha ugonjwa huu kwa kitaalamu huitwa mites sarcoptes scabies, huyu mdudu kwa kawaida akishakomaa utaga mayai kwenye vishimo vidogo vya mwili na kuanza kuishi Humo na kusababisha maumivu makali sana kwa mwathirika hasa kama ugonjwa huu haukutibiwa mapema kwa kuwepo kwa mayai kwenye ngozi usababisha na dalili nyingine kama vile
2. Kuwashwa wakati wa usiku.
Tunajua wazi kuwa wakati wa usiku ni mda ambao unakuwa umetulia sana na mwili pia unakuwa kwenye utulivu Fulani hakuna jua Wala kitu chochote cha kukusumbua mwili kwa hiyo ndipo wadudu Hawa uwa active na kuanza kushambulia na kusababisha kuwepo kwa miwasho na mgonjwa uanza kujikuna mara nyingi na kukosa kusinzia.
3. Hali ya kukosa kusinzia usababisha watoto kusinzia wakati wa mchana au kama wamefikia hatua ya kwenda shule usinzia darasani na kusababisha kupoteza mda wa masomo kwa hiyo ni vizuri kuwatibu watoto kwa tiba Sahihi na kuwafanya watoto waweze kuhudhulia masomo ipasavyo kwa hiyo wazazi wawe mstari wa mbele Ili kulinda na kuwatunza vizuri watoto Ili waweze kuepuka magonjwa kama haya.
4. Kuwepo kwa mikwaluzo kwenye ngozi.
Kwa sababu ya kujikuna sana mara nyingi kunakuwepo na mikwaluzo kwenye sehemu za ngozi na wakati mwingine mikwaluzo uandamana na kutokwa na damu ,hali hii uwanyima Raha watoto kwa sababu mda mwingi wanaendelea na kujikuna sana na pengine wanaweza kuleta maambukizi kwa watoto wenzao na wale wanaoishi nao.
5. Kuwepo kwa vidonda kwenye sehemu mbalimbali za mwili, pindi maambukizi yanapozidi yanasababisha kuwepo kwa vidonda kwenye sehemu mbalimbali za mwili kama vile kwenye vidole, kwenye kiwiko, kwenye tumbo, kwenye kiuno, kwenye chuchu za matiti na sehemu mbalimbali za mwili kwa ujumla, kwa hiyo ni vizuri kutibu kwa sababu hizi dalili zikitokea kwa mtu mmoja kwenda familia ni lazima atawaambukiza na wengine
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 web hosting 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Dalili za ugonjwa wa macho.
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa macho, ugonjwa huu kwa kawaida una dalili kuu tano kadri ya maambukizi yanavyoongezeka na madhara yake kwa hiyo tunapaswa kujua dalili hizo Kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces
Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces, hawa ni fangasi wanaosababisha maradhi yajulikanayo kama blastomycosis.
Soma Zaidi...Fahamu ugonjwa wa kaswende wakati wa ujauzito.
Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kaswende wakati wa ujauzito, kaswende inaweza kukaa kwa mtu zaidi ya miaka mingi bila kuleta madhara ya moja kwa moja lakini kadiri ya siku zinavyokwenda madhara utokea hasa wakati wa ujauzito, madhara hayo umwadhiri mtot
Soma Zaidi...Fahamu kuhusu magonjwa yasiyoambukizwa
Post hii inahusu magonjwa yasiyo ya kuambukizwa,haya ni magonjwa ambayo hayawezi kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda mwingine
Soma Zaidi...Fangasi wanaosababisha mapunye dalili zao na jinsi ya kupambana nao
Fangasi hawa ni maarufu sana kwa mapunye ya kichwani ama kwenye ngozi mikononi ama miguuni.
Soma Zaidi...Dalilili za Ngozi kuwa kavu
Posti hii inazungumzia kuhusiana na Ngozi kuwa kavu si mbaya, lakini inaweza kusumbua na isipendeze, ikitengeneza mistari laini na Mikunjo.
Soma Zaidi...