Ratiba ya chanjo ya kifua kikuu
Posti hii inahusu zaidi ratiba ya chanjo ya kuzuia kifua kikuu, hiii ni ratiba ambayo chanjo hii utolewa na ushauri mbalimbali utolewa ili kuweza kufanikisha kazi ya chanjo hii
Ratiba ya chanjo ya kuzuia kifua kikuu.
1.Tunajua wazi kuwa ugonjwa wa kifua kikuu ni ugonjwa ambao unaleta matatizo sana kwenye jamii hasa ikishambulia watoto uweza kuleta madhara makubwa kama vile kudumaa, kuokoa na mambo ya ukuaji kwa mtoto urudi nyuma kwa hiyo tunapaswa kupambana na ugonjwa huu ili kuweza kuwafanya watoto wakue kwa afya njema.
2.Chanjo hii utolewa mara moja tu pale mtoto anapozaliwa na kiwango cha kutoa chanjo huu ni kidogo sana kuliko chanjo nyingine ambacho ni sifuri nukta sufuri, sifuri tano na utolewa kwenye bega la kulia kwenye ngozi nya juu na Chanjo hii inapotolewa kovu lazima lionekane lisipoonekana chanjo urudiwa upya.
3.Wakati wa kutoa chanjo hii kuna maudhi madogo madogo yanaweza kutokea kama vile homa kali lakini homa hii isizidi masaa ishirini na manne na yakizidi na homa bado ipo mtoto anapaswa kupelekwa hospitalini kwa uangalizi zaidi .Na wakati mwingine mtoto anaweza kupata kipu kwenye bega yaani sehemu alipopatiwa chanjo kwa hiyo hilo jipya halipaswi kupasuliwa na ukiona sio la kawaida mpeleke mtoto hospitalini kwa uangalizi zaidi.
4.Kwa hiyo tunaona kwamba chanjo hii ina faida kubwa tunapaswa kuwapeleka watoto ili waweze kupata ili kuepuka kuwepo kwa kifua kikuu kwenye jamii na wale ambao hawaelewi wanapaswa kupewa elimu ili waweze kuacha imani potovu juu ya chanjo hizi zenye manufaa na umuhimu mkubwa kwenye jamii
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 ai web app 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Namna ya kuzuia maambukizi kwenye milija na ovari
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia maambukizi kwenye milija na ovari, ni njia ambazo usaidia kuzuia maambukizi kwenye milija na ovari
Soma Zaidi...Njia za kuzuia kiungulia
Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kuzuia kiungulia
Soma Zaidi...HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYEPATA JOTO LA JUU ZAIDI (HEAT STROKE)
Hii ni hali inayotokea ambapo wili unakuwa na joto la juu sana tofauti na kawaida.
Soma Zaidi...Upungufu wa vitamin
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu madhara ya upungufu wa vitamin
Soma Zaidi...Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na joto kubwa mwilini
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyepatwa na joto kubwa mwilini
Soma Zaidi...