picha

Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyeng'atwa na nyoka

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyeng'atwa na nyoka

HUDUMA YA KWANZA KWA ALIYENG’ATWA NA NYOKA

Nyoka wapo katka makundi makuu mawili, kuna wenye sumu na wasio na sumu. Ni vigumu kuwatofautisha wenye sumu na wasio na sumu kwani wakati mwengine wanafanana sifa. Wataalamu wameweka njia kadhaa za kuweza kuwajuwa weenye sumu. Nyoka mwenye sumu ana sifa zifuatazo

1.kichwa chake kipo katika pembe tatu

2.Rangi zake zinameremeta sana

3.Mboni ya Macho yao yamefanana na macho ya paka

4.Wanapoogelea kwenye maji miili yao inaelea juu

 

Tmbua kuwa sifa hizi hata nyoka wasio na sumu wamaweza kuwa nazo. Kuwa makini na kaa mbali na nyoka wa aina yeyote kama huna ujuzi na utambuzi huu. Mtu aliyengatwa na nyka mwenye sumu ataonyesha dalili zifuatazo:-

1.Uchovu

2.Kizunguzungu

3.Anaweza kuzimia

4.Kichefuchefu

5.Kuharisha

6.Kutapika

7.Mapigo ya moyo kuongezeka kwa kasi

8.Misuli kukosa uweze wa kutanuka na kusinyaa

9.Kuvimba eneo alipong’atwa.

 

Ukiona mtu ameng’atwa na nyoka na akaonyesha dalili hizi, wahi kuomba msaada ili awahishwe ituo cha afya kwa haraka. Hakikisha unampatia huduma ya kwanza ili kupunguza athari za kusambaa kwa sumu mwilini. Huduma ya kwanza kwa mtu aliyeng’atwa na nyoka inaweza kuwa kwa nama zifuata zo:-

1.mtulize mgonjwa nafsi yake, mpe maneno matamu na ya kutuliza. Hii itasaidia moyo kupunguza kazi ya kusambaza damu mwilini, hivyo sumu haita sambaa kwa kasi.

2.Muweke mgonjwa chini, na katu usimtembeze, mlaze chini kwa namna ambayo sehemu alipong’atwa itakuwa chini. Kwa mfano kama ameng’atwa mguuni, unaweza kumuwekea kitu kichwani akaegemea kwa mto ili sehemu ya mguuni iwe chini.

3.Ondoa mengo ya nyoka kwa uangalifu na katu usimishe eneo alilongatwa na nyoka.

4.Kama mgonjwa ana kizunguzungu, ama baridi mfunike kwa nguo ili kumuongezea joto

5.Chukuwa maelezo kuhusu aina ya nyoka, hii itasaidia wataalamu wa afya kujuwa tiba sahihi.

6.Osha eneo kwa kupitishia maji kwa juu na katu usisugue ama kuminya jeraha.

 

Usifanye vitu hivi:

1.Usinyonye sumu kwa mdomo wako

2.Usimpe mgonjwa chakula wala maji

3.Usimtembeze mgojwa

4.Usitumie barafu sehemu yenye jeraha

5.Usifunge kwenye jeraha eti kuzuia mzunguo wa damu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Huduma Main: Post File: Download PDF Views 2374

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 ai web app     👉4 web hosting     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Nna swali mimi nimefanya Romance na mtu ambaye sijampima kbsa sasa naogopa anaeza kuwa mgonjwa na mm nkaupata

Muulizaji anauliza he kula denda, ama kumbusu ama kufanya romance na muathirika was HIV na wewe uta ambukizwa?

Soma Zaidi...
Fahamu kuhsu vitamini E na kazi zake mwilini

Je unazijuwa faida za kuwa na vitamini E mwilini mwako.Unahani utapata matatizo yapi ya kiafya endapo utakuwa na upungufu wa vitamini E mwilini? Makala hii ni kwa ajili yako.

Soma Zaidi...
Upungufu wa damu mwilini

Post inaenda kuzungumzia kuhusiana na upungufu wa damu mwilini ambapo tutaona SABABU na dalili zake lakin upungufu wa damu mwilini hujulikana Kama ANEMIA.

Soma Zaidi...
Huduma ya Kwanza kwa aliyekazwa na misuli

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyekazwa na misuli

Soma Zaidi...
Huwezi kuambukizwa Ukimwi kwa mambo yafuatayo

Posti hii inahusu zaidi au inapinga Imani potofu ambayo utokea kwenye jamii kwamba unaweza kuambukizwa Ukimwi kwa vitu ambavyo haviusiani na namna mtu anavyoweza kuambukizwa Ukimwi,Ila mapendekezo kuwa watu wanapaswa kujua kuwa huwezi kuambukizwa Ukimwi k

Soma Zaidi...